James Comey
JF-Expert Member
- May 14, 2017
- 8,759
- 14,831
ndo Mana na nyerere senior hawakuiva waliiva kiupande upandeMalcom,
Abdul Sykes alifahamiana na Kenyatta 1950 kabla ya Nyerere.
Ally Sykes alifahamiana na Kenneth Kaunda 1953 kabla ya Nyerere.
Abbas Sykes amesoma darasa moja King's College, Budo na Kabaka Edward Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa Uganda.
Hizi zote ni historia za kusisimua sana.
Nimezieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Unaulizwa Malealle wewe unadakia SykesMalcom,
Abdul Sykes alifahamiana na Kenyatta 1950 kabla ya Nyerere.
Ally Sykes alifahamiana na Kenneth Kaunda 1953 kabla ya Nyerere.
Abbas Sykes amesoma darasa moja King's College, Budo na Kabaka Edward Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa Uganda.
Hizi zote ni historia za kusisimua sana.
Nimezieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
James...Mzee,
Nimepata shauku, andiko la Nguruvi linatakiwa kudhibitishwa.
Kwa ufahamo wako, ni kweli kuwa Ally Sykes hakuwai toa hutuba yoyote ya kudai uhuru nje ya Mwembe Togwa au nje ya Dar esam Salaam?
Kolola,Unaulizwa Malealle wewe unadakia Sykes
Vipi kuhusu Chief Edward wa UMASSAI, alifahamiana na Nkurumah lini ??Malcom,
Abdul Sykes alifahamiana na Kenyatta 1950 kabla ya Nyerere.
Ally Sykes alifahamiana na Kenneth Kaunda 1953 kabla ya Nyerere.
Abbas Sykes amesoma darasa moja King's College, Budo na Kabaka Edward Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa Uganda.
Hizi zote ni historia za kusisimua sana.
Nimezieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Laki...Marealle alienda kudai Uhuru wa Wachagga, hakuwa na Chama.
Malcom...Vipi kuhusu Chief Edward wa UMASSAI, alifahamiana na Nkurumah lini ??
Malcom...Vipi kuhusu Chief Edward wa UMASSAI, alifahamiana na Nkurumah lini ??
Mtafute, alikuwa ni moja ya wapambania uhuru wa mapema kabisa nchini Tanganyika. Alishauriwa na baadhi ya viongozi wa dini wenye asili ya Kimarekani kudai uhuru wa maeneo ya wamassai tu. Alikuwa na ushawishi mkubwa sana tu kwenye eneo lake.Malcom...
Sijapata kumsikia huyu Chief Edward wa Umasai lakini kwa ufupi machifu wote walikuw aupande wa serikali ya kikoloni na ndiyo maana ikawa tabu kwao kujiunga na harakati za kudai uhuru.
Alikuwa ni Chief wa wamassai, alikuwa na ushawishi mkubwa sana akisaidiwa na viongozi wa dini (Catholic Priests) kutoka Marekani ili kudai uhuru wa eneo lake pekee. Huwezi kumkuta kwenye vitabu vya historia, mpaka ufanya jitihada za ziada ndiyo utamfahamu. Nyaraka za historia za Ministry of Foreign Affairs zimewahi kumtaja, fanya kuzitafuta.Malcom...
Chief Edward ni nani na alikuwa chief wa wapi?
James...Ongezeo, tumemsoma Kwame, Nelson, Keneth, Ghaddafi, Mugabe, BenBella, Nujoma na wengineo wa nyakati hizi katika contemporary African politics.
Lakini bado kwa sisi wengine tunamuona Nyerere kama aliwazidi wengi ktk uongozi hasa ktk kujenga msingi wa uongozi katika awamu ya kwanza ya uongozi baada ya uhuru.
Malcolm...Mtafute, alikuwa ni moja ya wapambania uhuru wa mapema kabisa nchini Tanganyika. Alishauriwa na baadhi ya viongozi wa dini wenye asili ya Kimarekani kudai uhuru wa maeneo ya wamassai tu. Alikuwa na ushawishi mkubwa sana tu kwenye eneo lake.
Ukipitia baadhi ya nyaraka za Foreign Affairs zinazoelezea kilichotokea kuanzia mwaka 1949-1964 utakutana na majina ya watu ambao walianza kudai uhuru wa maeneo yao husika wakishirikiana na taasisi kubwa za kidini duniani.
Huu ukurasa wa historia haujawekwa wazi,......
Mkuu una maana gani kusema umesoma yote yaliyoandikwa kuhusu Tanganyika ??? Kuna tafiti za wizara ya mambo ya nje ziliandikwa na Earl Seaton na Sosthenes Maliti zimeyaweka haya wazi kabisa. Kuna chapisho lao linaitwa Tanzanian Treaty Practice litafute uzipate hizi taarifa.Malcolm...
Hebu weka hapa rejea tusome.
Mimi nimesoma kila kilichoandikwa kuhusu Tanganyika lakini haya unayosema sijayaona popote.
Hizo Nyaraza za Foreign Affairs ni zipi na ziko katika maktaba gani?
Soma iyo barua ya Chief MarealleLaki...
Akiwa hana chama cha siasa sasa atatoa au alitoa vitambulisho ''credentials,'' gani UNO?
Ungetusaidia sana kama ungetupa ''source,' ya hizi taarifa zako.
Malcom,Mkuu una maana gani kusema umesoma yote yaliyoandikwa kuhusu Tanganyika ??? Kuna tafiti za wizara ya mambo ya nje ziliandikwa na Earl Seaton na Sosthenes Maliti zimeyaweka haya wazi kabisa. Kuna chapisho lao linaitwa Tanzanian Treaty Practice litafute uzipate hizi taarifa.
Malcom...Mkuu una maana gani kusema umesoma yote yaliyoandikwa kuhusu Tanganyika ??? Kuna tafiti za wizara ya mambo ya nje ziliandikwa na Earl Seaton na Sosthenes Maliti zimeyaweka haya wazi kabisa. Kuna chapisho lao linaitwa Tanzanian Treaty Practice litafute uzipate hizi taarifa.
Laki,Soma iyo barua ya Chief Marealle
Acha kujirudiarudia kila siku wewe Mzee. Wewe si mzima tushang'amua hilo, una ugonjwa wa akili kila mara kujirudiarudia na stories zako na kutafuta mwanya wowote lengo lako kuu likiwa kusifia Sykes kwa namna yoyote. Unajishushia hadhi na maandiko yako hayana credibility ya kuwa historia sababu una upendeleo wa wazi.https://www.facebook.com/
Nguruvi,
Mimi sikejeli wala kukebehi.
Nakueleza historia ya TANU kama ukweli wake ulivyokuwa.
Na nimenyanyua kalamu baada ya kuona hizo historia zilizoandikwa zimepotoshwa.
Nani alikuwa anaijua historia ya African Association, TAA hadi kuundwa kwa TANU kwa kiwango nilichoeleza mimi?
Kadi ya TANU No. 1 Territorial President Julius Kambarage Nyerere, kadi No. 2 Ally Kleist Sykes, kadi No. 3 Abdulwahid Kleist Sykes, kadi No. 4 Waziri Dossa Aziz, kadi No. 5 Denis Phombeah (Mnyasa) Kadi No. 6 Dome Okochi Budohi (Mkenya).
Nani alikuwa anaijua historia hii?
Katika hao wanachama wa TANU sita ambae sikupata kuwajua ni wawili - Nyerere na Phombeah.
Hawa nimewasoma katika Nyaraka za Sykes.
Lakini hao wote sita nimeeleza historia zao katika kitabu cha Abdul Sykes.
Kitabu hiki kimevunja rekodi tunakwenda toleo la tano Kiswahili na Kiingereza.
Kwa nini kitabu hiki kimependwa kiasi hiki?
Sababu ni kuwa hii ndiyo historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika.
Nikejeli na "Mwembe Togwa," na maneno yote upendayo mimi sirejeshi kejeli narejesha maneno ya kweli katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika kwa ushahidi wa picha na nyaraka.
Ndiyo maana hapa nimeingia na jina langu halisi.
Wewe unaweza ukatukana, ukakejeli na kukebehi.
Anakujua nani?
Mimi niko hapa kwa picha na sauti.
Hakuna asiyenifahamu.
Mimi nimebeba dhima ya elimu yangu na heshima ya walimu wangu na heshima ya mama yangu aliyenifunza adabu.
Sithubutu kukurejeshea ufedhuli.