Kivuli cha Kwame Nkrumah katika TANU

Kivuli cha Kwame Nkrumah katika TANU

Ongezeo, tumemsoma Kwame, Nelson, Keneth, Ghaddafi, Mugabe, BenBella, Nujoma na wengineo wa nyakati hizi katika contemporary African politics.
Lakini bado kwa sisi wengine tunamuona Nyerere kama aliwazidi wengi ktk uongozi hasa ktk kujenga msingi wa uongozi katika awamu ya kwanza ya uongozi baada ya uhuru.
 
Malcom,
Abdul Sykes alifahamiana na Kenyatta 1950 kabla ya Nyerere.

Ally Sykes alifahamiana na Kenneth Kaunda 1953 kabla ya Nyerere.

Abbas Sykes amesoma darasa moja King's College, Budo na Kabaka Edward Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa Uganda.

Hizi zote ni historia za kusisimua sana.

Nimezieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
ndo Mana na nyerere senior hawakuiva waliiva kiupande upande
 
Malcom,
Abdul Sykes alifahamiana na Kenyatta 1950 kabla ya Nyerere.

Ally Sykes alifahamiana na Kenneth Kaunda 1953 kabla ya Nyerere.

Abbas Sykes amesoma darasa moja King's College, Budo na Kabaka Edward Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa Uganda.

Hizi zote ni historia za kusisimua sana.

Nimezieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Unaulizwa Malealle wewe unadakia Sykes
 
Mzee,
Nimepata shauku, andiko la Nguruvi linatakiwa kudhibitishwa.
Kwa ufahamo wako, ni kweli kuwa Ally Sykes hakuwai toa hutuba yoyote ya kudai uhuru nje ya Mwembe Togwa au nje ya Dar esam Salaam?
James...
Nguruvi haipendi historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika ambayo mimi nimeandika katika kitabu cha Abdul Sykes.

Kabla ya mimi kuandika historia hii historia ya TANU na uhuru ilikuwa ikitamtaja Nyerere peke yake.

Hapo ndipo mimi nikaandika historia ya harakati za uhuru kupitia Nyaraka za Sykes.

Ukifanya rejea nyuma utaona niliyoandika.

Yeye anaemkusudia ni Abdul Sykes si Ally Sykes mdogo wake.

Kleist Sykes baba yao hawa ndugu wawili na Abbas Sykes ndiye aliyeasisi African Association mwaka wa 1929 lakini hakuna popote nilipokuta kuwa alikuwa anahutubia mikutano ya hadhara.

Sababu ni kuwa wakati wa African Association hadi TAA viongozi hawakuwa wanaitisha mikutano ya hadhara.

Mikutano ya hadhara ilianza baada ya TANU kuundwa 1954.

Nguruvi tatizo lake ni kuwa nisingeandika historia ya Abdul Sykes anataka tubakie ni ile historia rasmi ya Chuo Cha CCM Kivukoni ambayo Abdul Sykes na wazalendo wengine hawakutajwa ila Julius Nyerere peke yake
 
Unaulizwa Malealle wewe unadakia Sykes
Kolola,
"Marealle."

Hapana sikudakia.
Hii ni katika kuieleza historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Mangi Mkuu Chief Thomas Marealle alikuwa rafiki mkubwa wa Abdul Sykes na kila akifika Dar es Salaam ilikuwa lazima amtembelee Abdul nyumbani kwake.

Na machifu wote wakifanya hivi.

Nimesoma barua ambazo Thomas Marealle alikuwa akiandikiana na Ally Sykes wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.

Hizi barua zinasisimua sana.
 
Malcom,
Abdul Sykes alifahamiana na Kenyatta 1950 kabla ya Nyerere.

Ally Sykes alifahamiana na Kenneth Kaunda 1953 kabla ya Nyerere.

Abbas Sykes amesoma darasa moja King's College, Budo na Kabaka Edward Mutesa aliyekuja kuwa Rais wa kwanza wa Uganda.

Hizi zote ni historia za kusisimua sana.

Nimezieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
Vipi kuhusu Chief Edward wa UMASSAI, alifahamiana na Nkurumah lini ??
 
Marealle alienda kudai Uhuru wa Wachagga, hakuwa na Chama.
Laki...
Akiwa hana chama cha siasa sasa atatoa au alitoa vitambulisho ''credentials,'' gani UNO?

Ungetusaidia sana kama ungetupa ''source,' ya hizi taarifa zako.
 
Vipi kuhusu Chief Edward wa UMASSAI, alifahamiana na Nkurumah lini ??
Malcom...
Sijapata kumsikia huyu Chief Edward wa Umasai lakini kwa ufupi machifu wote walikuwa upande wa serikali ya kikoloni na ndiyo maana ikawa tabu kwao kujiunga na harakati za kudai uhuru.
 
Malcom...
Sijapata kumsikia huyu Chief Edward wa Umasai lakini kwa ufupi machifu wote walikuw aupande wa serikali ya kikoloni na ndiyo maana ikawa tabu kwao kujiunga na harakati za kudai uhuru.
Mtafute, alikuwa ni moja ya wapambania uhuru wa mapema kabisa nchini Tanganyika. Alishauriwa na baadhi ya viongozi wa dini wenye asili ya Kimarekani kudai uhuru wa maeneo ya wamassai tu. Alikuwa na ushawishi mkubwa sana tu kwenye eneo lake.

Ukipitia baadhi ya nyaraka za Foreign Affairs zinazoelezea kilichotokea kuanzia mwaka 1949-1964 utakutana na majina ya watu ambao walianza kudai uhuru wa maeneo yao husika wakishirikiana na taasisi kubwa za kidini duniani.

Huu ukurasa wa historia haujawekwa wazi,......
 
Malcom...
Chief Edward ni nani na alikuwa chief wa wapi?
Alikuwa ni Chief wa wamassai, alikuwa na ushawishi mkubwa sana akisaidiwa na viongozi wa dini (Catholic Priests) kutoka Marekani ili kudai uhuru wa eneo lake pekee. Huwezi kumkuta kwenye vitabu vya historia, mpaka ufanya jitihada za ziada ndiyo utamfahamu. Nyaraka za historia za Ministry of Foreign Affairs zimewahi kumtaja, fanya kuzitafuta.
 
Ongezeo, tumemsoma Kwame, Nelson, Keneth, Ghaddafi, Mugabe, BenBella, Nujoma na wengineo wa nyakati hizi katika contemporary African politics.
Lakini bado kwa sisi wengine tunamuona Nyerere kama aliwazidi wengi ktk uongozi hasa ktk kujenga msingi wa uongozi katika awamu ya kwanza ya uongozi baada ya uhuru.
James...
Inataka uwe umesoma vitabu vya kutosha.
Historia ya Tanzania ina mengi sana wengi hamyajui.

Labda nikuulize swali moja kisa tuendelee.
Ulikuwa unaijua historia ya Abdul Sykes na TANU?
 
Mtafute, alikuwa ni moja ya wapambania uhuru wa mapema kabisa nchini Tanganyika. Alishauriwa na baadhi ya viongozi wa dini wenye asili ya Kimarekani kudai uhuru wa maeneo ya wamassai tu. Alikuwa na ushawishi mkubwa sana tu kwenye eneo lake.

Ukipitia baadhi ya nyaraka za Foreign Affairs zinazoelezea kilichotokea kuanzia mwaka 1949-1964 utakutana na majina ya watu ambao walianza kudai uhuru wa maeneo yao husika wakishirikiana na taasisi kubwa za kidini duniani.

Huu ukurasa wa historia haujawekwa wazi,......
Malcolm...
Hebu weka hapa rejea tusome.

Mimi nimesoma kila kilichoandikwa kuhusu Tanganyika lakini haya unayosema sijayaona popote.

Hizo Nyaraka za Foreign Affairs ni zipi na ziko katika maktaba gani?
Chief Edward lipi jina lake la pili?

Image result for chief edward of maasai
Maasai society is organised into male age-groups whose members together pass through initiations to become warriors, and then elders. They have no chiefs, although each section has a Laibon, or spiritual leader, at its head.
 
Malcolm...
Hebu weka hapa rejea tusome.

Mimi nimesoma kila kilichoandikwa kuhusu Tanganyika lakini haya unayosema sijayaona popote.

Hizo Nyaraza za Foreign Affairs ni zipi na ziko katika maktaba gani?
Mkuu una maana gani kusema umesoma yote yaliyoandikwa kuhusu Tanganyika ??? Kuna tafiti za wizara ya mambo ya nje ziliandikwa na Earl Seaton na Sosthenes Maliti zimeyaweka haya wazi kabisa. Kuna chapisho lao linaitwa Tanzanian Treaty Practice litafute uzipate hizi taarifa.
 
Mkuu una maana gani kusema umesoma yote yaliyoandikwa kuhusu Tanganyika ??? Kuna tafiti za wizara ya mambo ya nje ziliandikwa na Earl Seaton na Sosthenes Maliti zimeyaweka haya wazi kabisa. Kuna chapisho lao linaitwa Tanzanian Treaty Practice litafute uzipate hizi taarifa.
Malcom,
Mimi sina tatizo na taarifa hizi nauliza ili nipate kujua.

Earle Seaton nimemkuta katika Nyaraka za Sykes na mimi naamini ndiye mwandishi wa kwanza kumuhusisha na harakati za uhuru wa Tanganyika watu wakamsoma.

Ukisoma kitabu cha Abdul Sykes utakuta historia yake humo.
 
Mkuu una maana gani kusema umesoma yote yaliyoandikwa kuhusu Tanganyika ??? Kuna tafiti za wizara ya mambo ya nje ziliandikwa na Earl Seaton na Sosthenes Maliti zimeyaweka haya wazi kabisa. Kuna chapisho lao linaitwa Tanzanian Treaty Practice litafute uzipate hizi taarifa.
Malcom...
Nimeanza kutafuta hizi taarifa:

Sijapata hiyo taarifa lakini naendelea.

Nimeona na hiyo hapo chini:


Bahati mbaya sijaweza kufungua na kusoma kuhusu Wamasai kudai uhuru wao.

Lakini umenisaidia kwa kueleza kuwa "Chief" Edward alishauriwa na watu kutoka Amerika adai uhuru.

Ndiyo kusema yeye mwenyewe hakuwa na fikra ya kuutaka uhuru wake?

Je aliunda chama cha kuwaunganisha watu wake?

Maswali ni mengi.
 


Nguruvi,
Mimi sikejeli wala kukebehi.

Nakueleza historia ya TANU kama ukweli wake ulivyokuwa.

Na nimenyanyua kalamu baada ya kuona hizo historia zilizoandikwa zimepotoshwa.

Nani alikuwa anaijua historia ya African Association, TAA hadi kuundwa kwa TANU kwa kiwango nilichoeleza mimi?

Kadi ya TANU No. 1 Territorial President Julius Kambarage Nyerere, kadi No. 2 Ally Kleist Sykes, kadi No. 3 Abdulwahid Kleist Sykes, kadi No. 4 Waziri Dossa Aziz, kadi No. 5 Denis Phombeah (Mnyasa) Kadi No. 6 Dome Okochi Budohi (Mkenya).

Nani alikuwa anaijua historia hii?

Katika hao wanachama wa TANU sita ambae sikupata kuwajua ni wawili - Nyerere na Phombeah.

Hawa nimewasoma katika Nyaraka za Sykes.

Lakini hao wote sita nimeeleza historia zao katika kitabu cha Abdul Sykes.

Kitabu hiki kimevunja rekodi tunakwenda toleo la tano Kiswahili na Kiingereza.

Kwa nini kitabu hiki kimependwa kiasi hiki?

Sababu ni kuwa hii ndiyo historia ya kweli ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Nikejeli na "Mwembe Togwa," na maneno yote upendayo mimi sirejeshi kejeli narejesha maneno ya kweli katika historia ya kupigania uhuru wa Tanganyika kwa ushahidi wa picha na nyaraka.

Ndiyo maana hapa nimeingia na jina langu halisi.

Wewe unaweza ukatukana, ukakejeli na kukebehi.

Anakujua nani?
Mimi niko hapa kwa picha na sauti.

Hakuna asiyenifahamu.

Mimi nimebeba dhima ya elimu yangu na heshima ya walimu wangu na heshima ya mama yangu aliyenifunza adabu.

Sithubutu kukurejeshea ufedhuli.

Acha kujirudiarudia kila siku wewe Mzee. Wewe si mzima tushang'amua hilo, una ugonjwa wa akili kila mara kujirudiarudia na stories zako na kutafuta mwanya wowote lengo lako kuu likiwa kusifia Sykes kwa namna yoyote. Unajishushia hadhi na maandiko yako hayana credibility ya kuwa historia sababu una upendeleo wa wazi.
 
Unaulizwa swali kuhusu uhusiano wa Marealle na Nkrumah, badala ya kujibu swali kwa vithibitisho, wewe unaanza kuwasifia Sykes eti walifahamiana na Nkrumah hata kabla ya Nyerere. Ni sawa na pale ulipoulizwa swali Sykes kahutubia wapi nje ya Kariakoo, wewe badala ya kujibu swali, unaleta story ya Sykes kumliki Mercedes Benz.
 
Back
Top Bottom