Kiwanda gani naweza fungua/anzisha kwa gharama ya millioni nne?

Hata ukiweka korona ukaanza kukamua miwa ni kiwanda pia mkuu na kwa mtaji huo ni safi
 
Kwa wadogo zetu mnaokua na watu wazima ambao bado akili zinakua tungependa kuwaarifu kuwa sisi tunajua kuandika utani na pumba zaidi yenu lakini tufahamu tuandike wapi na wakati gani, kuna majukwaa mengi ya utani lakini when it comes to business kuweni na adabu tafadhali
 
Pata ushauri kutoka kwa mkulu, atakuja kukifungia mwenyewe.
 
Nimekuwa interested na peanut butter ila changamoto naona iko kwenye bidhaa kuweza kupenyeza sokoni pamoja na vibali kama vya TFDA na TBS. Nahitaji mwanga zaidi.
 
Anzisha kiwanda cha kutengeneza unga wa nazi.unakausha zile nazi halafu unazisaga.halafu unazitia kwenye paketi.hakikisha paketi haiingizi hewa ndani ili huo unga usiharibike.hapo utatafuta kampuni ikutengenezee hizo paketi.halafu uzipige nembo yako. Kuna watu wengi hawana mda wa kukuna nazi hivo utapata wateja wengi tuu hata nje ya tz utauza.na machine unayohitaji kwa kuanzia ni moja tu ya kusaga.
 
Nimekuwa interested na peanut butter ila changamoto naona iko kwenye bidhaa kuweza kupenyeza sokoni pamoja na vibali kama vya TFDA na TBS. Nahitaji mwanga zaidi.
Hakuna ugumu wowote. Kwa kuanzia tbs utaiomba kupitia sido ni mchakato rahisi sana na kulipa fee kidogo sana. Tfda hawana complication unafuata tu masharti yao na kulipa gharama kidogo.

Wengi wanaogopa bila kujaribu
 
Dah.... Angalia hitaji LA soko kwanza..... Usijerudi unalialia hapa[emoji87] [emoji41]
 

Aisee bora hata umesema mkuu, kuna watu wanamambo ya kitoto sana. Tuwe na tabia ata ya kujionea aibu wenyewe haiwezekani mtu anaandika ujinga sehemu kama hii ambayo mtu unaweza ukapata jambo linaloweza kukusahidia.

Id fake na kutokujulikana kusifanye tuwe wapuuzi JF si humu ni watu wazima.

Wanakera sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…