Kiwanda gani naweza fungua/anzisha kwa gharama ya millioni nne?

Napenda nachokisoma kwenye huu uzi watu bila choyo wanatupa technique za maisha safi sana huu ndio undugu wa Afrika tunatakiwa kuwa nao tutafika mbali sana tukishirikiana hivi hivi bega kwa bega Kesho ni ya kwetu najua kuna wajinga wachache wanajaribu kuharibu uzi siwalaumu maana bado hawajayajua maisha [emoji1490][emoji1490] Jamii Forums idumu "Too much sauce" in here.
 
Unaweza kusaga kwa kutumia food grinder au waambie sido watakupa machine ndogo hivi itakufaa au nunua machine yoyote ya kusaga ambayo ni ndogo.si lazima usage unga uwe laini sana. Tui utapata kwa kuongeza maji moto kwenye huo unga halaf unakamua.
 
 
Jf huwa ni mahala salama sana tukiachana na zile interview za kule kwa kina muosha Rungu,

Idea zilizotolewa hapa ni babkubwa mtu anatoka na kitu cha msingi sana,
 
Umenena! Wengine tunapatia mawazo humu na kuya implement kabisa.
 
Ni wazo zuri, jaribu kuwekeza kwenye Mini grids I mean off-grids electricity hasa katk maeneo ambayo mpango wa usambazaji wa umeme vjjn hayajafikiwa, unaweza ukara hela.
Hii ndio nini mkuu?
 
Wakuu nawashukuru kwa maoni na mapendekezo mazuri sana.
Maoni zaidi yanahitajika.
 
Unaweza kuzisaga kwa mashine gani mkuu,

Pili, ukikausha ule unga tui litapatikana kweli ?
haliwezi patikana,
jamaa anafikiri ile nazi ya unga inapatikana kwa kusaga nyama ya nazi,wakati kinachokaushwa ni tui,baada ya kuchuja machicha
 
haliwezi patikana,
jamaa anafikiri ile nazi ya unga inapatikana kwa kusaga nyama ya nazi,wakati kinachokaushwa ni tui,baada ya kuchuja machicha
Nilijiuliza ivo kama inawezekana kweli baada ya kukausha,
Jamaa anatetea kwamba ukiweka na maji ya moto inapatikana,
Labda nifanye majaribio.
 
baishara ya ku-process na ku-tui au unga wa nazi naona kama itakua ngumu sana. Bakhressa analeta toka Indonesia ila zimekua branded, hata american gardens pia. Bei ya nazi ipo juu, umeme sio rafiki na hata vifungashio ni ghali. Ukiwa mzalishaji mdogo itakusumbua sana kushindana kwenye bei.

Siku hizi mjini watu wanatumia sana tomato paste na nyingi inatoka china au uarabuni. Naona kama nyanya ni nyingi na bei iko chini kama ukiweza kufanya uchunguzi wa kibiashara hii inaweza kukutoa. Kuna kampuni 1 tu ya kitanzania ambayo ikoa arusha ambayo inajihusisha na utengenezaji wa tomato paste.
 
haliwezi patikana,
jamaa anafikiri ile nazi ya unga inapatikana kwa kusaga nyama ya nazi,wakati kinachokaushwa ni tui,baada ya kuchuja machicha
Hio unayoisema wew siijui.mimi niliyonunua na kuitumia haiko laini.unga wake uko katika chembechembe.na nilitia maji moto.kwa hio nipe hio brand uliyowahi kutumia na tuelimishe uliitumiaje.
 

Hili wazo nitalifanyia kazi haki
 
Hupati tui mkuu
Ukikausha unga wa nazi tui huondoka kwa njia ya evaporation na kinacho baki ni mafuta tuu!!!
Kinachoondoka sio tui bali majimaji yalio kwenye tui.tui lina vitu vingi ndani yake.unapokausha unaondoa majimaj tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…