Klabu Bingwa Africa: Zesco yaichapa Yanga kwa magoli 2 - 1 na kuingia hatua ya makundi; Yanga kucheza mtoano kwenye kombe la Shirikisho

DonDonald

JF-Expert Member
Joined
Feb 14, 2011
Posts
2,533
Reaction score
2,709
Kivumbi kinatarajia kutimka leo saa 10 jioni kwenye uwanja wa Levy Mwanawasa wakati wawakilishi wa Tanzania, Dar es Salaam Young Africans (Yanga) almaarufu kama wakimataifa / timu ya wananchi / mabingwa wa kihistoria watakapokuwa wanapambana na timu ya Zesco kutoka Zambia

Katika mechi ya kwanza iliyofanyika uwanja wa taifa, Dar es Salaam timu hizo zilitoka sare kwa kufungana goli 1 - 1

Yanga leo imedhamiria kupindua meza kibabe kwa kuitoa Zesco kwao, Zesco ambayo inajivunia rekodi yake ya kutofungwa kwenye uwanja wao wa nyumbani

Mungu Ibariki Yanga, Mungu ibariki Tanzania

Kikosi cha Yanga

1. Metacha Mnata
2. Ally Ally
3. Ally Mtoni
4. Lamine Moro
5. Kelvin Yondani
6. AbdulAziz Makame
7. Deus Kaseke
8. Feisal Salum
9. Sadney Khoetage
10. Papy Tshishimbi
11. Patrick Sibomana

Benchi: Shikalo, Abdul Muharami, Ngasa, Kalengo, Balinya, Jafary

UPDATES

Mpira umeanza hapa

"5: Zesco 0 - 0 Yanga

"15: Zesco 0 - 0 Yanga

Goal

"22: Jesse Were anaifungia Zesco goli la kwanza

"25: Zesco 1 - 0 Yanga

Goal

"30: Sadney anawanyanyua hapa wananchi kwa kutupia mpira nyavuni

35": Zesco 1 (Were) - 1 Yanga (Sadney)

"45: Zesco 1- 1 Yanga

Half Time: Mpira ni mapumziko hapa kwa kila timu kufunga goli 1 -1, kumbuka mechi ya kwanza iliisha kwa kila timu kufunga goli 1 - 1

Second Half

"46: Zesco 1 (Were) - 1 Yanga (Sadney)

"55: Zesco 1 (Were) - 1 Yanga (Sadney)

"65: Zesco 1 (Were) - 1 Yanga (Sadney)

Goal

"80: Makame anajifunga hapa na kufanya Zesco kuwa mbele kwa magoli 2 -1

Red Card: Beki wa Yanga Lamine Moro anaonyeshwa kadi nyekundu

"90: Zesco 2 - 1 Yanga

Full Time: Zesco 2 - 1 Yanga..... Zesco wamefanikiwa kuingia hatua ya makundi wakati Yanga wataingia kwenye michuano ya shirikisho kugombea nafasi ya kuingia kwenye makundi ya shirikisho
 
Mnata si ana njano zaidi ya 2 huyu au? Naomba ufafanuzi please
 
Kocha mbona hampangi Balinya?????aarrggg
 
Kila la kheri chama langu.....ila mh iyo beki namba 2 sijui kama atakua amejibadilisha
 
Kila la kheri timu ya Wananchi.

"Daima mbele nyuma mwiko"

Nilitaka kushanga ukose hapa kweli, ingekuwa ni muujiza kabisa na wala uzi usingenoga Wallah.

Hivi huwa wanaku-tag huko au, naona front page kabisa ushatia timu shosty wng.

Najua unacheka tu hapo...!

😍
 
Yanga beki za pemben bado ni tatizo,hyo namba 2 sijawah kuelewa kwa kigezo gani walimsajili?au kwa kuwa alisaidia kupata ushind msimu uliopita
 
Yanga beki za pemben bado ni tatizo,hyo namba 2 sijawah kuelewa kwa kigezo gani walimsajili?au kwa kuwa alisaidia kupata ushind msimu uliopita
Unauliza kwa nini mlemavu anawekwa dukani hata kama hawezi kuhudumia wateja?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…