KLH Exclusive:Mhe Anne Kilango Malecela Alonga!

KLH Exclusive:Mhe Anne Kilango Malecela Alonga!

Mkuu "Mutu"

Heshima mbele bro, usiwe na wasi wasi ni lazima sometimes kuwekana sawa, lakini watu wanatalkiwa kuelewa haya ni majadiliano tu yas siasa, lakini nilihisi toka Ijumaa ule mwendo kuwa utaishia kuleta madhara, lakini sisi ni watu wazima ni lazima tuwekane sawa ikibidi, na tuheshimiane pia,

Kuhusu Mama Kilango, mimi kama raia wa Tanzania nina imani naye tena sana, na ninamtakia heri ya maisha ili aendelee hivyo hivyo alivyo sasa!
 
Lakini baadhi yetu hatumuongelei Mama AKM kama MKE wa mtu. Hilo moja; la pili, Nchi yetu imeanza kutafunwa kwa nguvu sana baada ya Mwalimu kufariki na huyu Mama ameingia Bungeni kwa KITI MAALUM wakati Nchi inatafunwa kwelikweli! Hakusema kitu wala kuukataa uteuzi wa waliokuwa wakiitafuna Nchi yetu. Ninachokiamini mimi: UZALENDO na UADILIFU mtu HUZALIWA navyo, HAVIZUKI wala KUUNDWA.

nakupa shavu kwa hilo. watu wanadhania uadilifu unakuja tu ghafla leo mzandiki kesho mkweli.
 
Sasa jadilini alichokisema, tusije kuishia kujadili personality halafu huo ukawa mwisho kwani yeyote anayefikiri atakutana na binadamu asiye na "madudu" yake huyo naye yuko njozini. La maana kwangu ni kuona mtu ambaye amejirudi, ametambua makosa yake na kuamua kutengeneza.

Tumechoka na watu waliao "bangusilo" na yakuwa wameonewa. Tusije tukaingia mtego wa kusema tunataka mtu "mkamilifu" ambaye hajawahi kutokea bado, na badala yake mtu mwadilifu ambaye anajua mapungufu yake na yuko tayari kusafisha alipochafua.
 
Mkuu "Mutu"

Heshima mbele bro, usiwe na wasi wasi ni lazima sometimes kuwekana sawa, lakini watu wanatalkiwa kuelewa haya ni majadiliano tu yas siasa, lakini nilihisi toka Ijumaa ule mwendo kuwa utaishia kuleta madhara, lakini sisi ni watu wazima ni lazima tuwekane sawa ikibidi, na tuheshimiane pia,

Kuhusu Mama Kilango, mimi kama raia wa Tanzania nina imani naye tena sana, na ninamtakia heri ya maisha ili aendelee hivyo hivyo alivyo sasa!



Yup,thats whatsup bro! we must keep people in the line when thing goes wrong .Yah mama namuona makini hata mimi.
 
mheshimiwa pale juu kuna mahali panasema "Listen Shows" usiingie hapo kwenye podomatic promotional..
 
Bravo kaka Mwanakijiji, tunasubiri kwa hamu kusikiliza mahojiano yako na Mhe. Anne Kilango Malecela (Mbunge wa CCM - Same Mashariki) ili tuchambue contents na kuelewa mawazo yake yanavyooana na hatima ya nchi yetu katika hizi zama za UFISADI na WIZI ULIOKITHIRI. Mungu Ibariki Tanzania.

Shukrani Mkjj huyu mama miezi michache iliyopita alitoa kauli kwamba hawaogopi mafisadi na yuko tayari kufa katika hii vita dhidi ya mafisadi na kusema kwamba wengine wataendelea pale alipofikia. Huyu mama namuona ni shujaa na nikijaliwa kumuona mahali popote pale duniani nitampa hongera nyingi sana kwa juhudi zake na kumwambia yeye ni mmoja wa mashujaa wetu Tanzania. Tunataka viongozi kama Mama Kilango ambao wanaweka mbele maslahi ya Tanzania badala ya matumbo yao.

Ndio maana nawashangaa watu wanaodai kwamba eti kumjadili fisadi Mkapa ni upuuzi mtupu hatuwezi kumfanya chochote kwa sababu katiba inamlinda!!!!

Nguvu ya umma inapotoa sauti na kusema sasa basi, hakuna katiba wala mama yake katiba inayoweza kuzuia nguvu ya umma, na hapo ndipo viongozi watabadilisha hiyo katiba ili iwapunguzie madaraka viongozi na kutoa uwezo zaidi kwa bunge na wananchi.

Mungu ibariki Tanzania na pia mbariki Mama Anna Kilango
 
Mkuu Bubu tupo wote hapo, yaani ukurasa mmoja ninaisikiliza sasa hii habari safi sana Mkuu MMJ, maana naipata tena very clear! Na ninamsikia akimkoma nyani giladi
 
jamani sometime tuwe appreciative, kusipokuwa na wa kusema tunalalamika, na mtu akiamua kujifunga kibwebwe kusema bado haturidhiki, sasa lipi jema sie, mbona tunakuwa viumbe wazito sana.

Mama, wengine hawana shukrani!!! Kuna tofauti kubwa kati ya binadamu anayetetea ufisadi hata iweje na kuufumbia macho na yule anayesema I can do better than this for my country as well as my people. I need to change and a positive change for that matter. There is BIG DIFFERENCE between those 2 people but some of us don't see any difference!!!!
 
Nimesikiliza mahojiano yote ambayo ni kama dakika 27 hivi kati ya Mkjj na Mama Kilango. Kama CCM ikiamua kumuweka mgombea tofauti na Kikwete 2010 na huyu mama akaamua kuweka jina lake basi hana mshindani si Membe wa Masha wanaoweza kusimama na huyu mama. CCM kama kweli inataka kujisafisha na kurudisha hadhi iliyokuwa nayo miaka ya nyuma basi wanahitaji watu kama Mama Kilango wanaosema ukweli bila kuogopa na wanaosema yale yaliyo moyoni mwao. Siku hizi kusikia kiongozi wa CCM anaongea maneno mazito kama huyu mama ni nadra sana. Wote wamekuwa MASPIN DOCTORS ili kuendelea kuwalinda mafisadi
 
Natoa shukurani nying kwa MKJJ kuturushia hewani hiyo mahojiano na Mheshimiwa Anna Kilango.

Naamini huyu mama/dada ni jasiri sana ktu ambacho Tanzania ya sasa ni kigeni kabisa naweza kusema kuwa huu unakumbusha ujasiri wa mababu zetu kina Mkwawa....big up Anna....(BTW she has a very**** voice)
 
mpiganaji bora ni yule ajuaye kupanga mashambulizi yake.
kuna wakati mpiganaji inabidi arudi nyuma kujipanga upya,
upo wakati inabidi akae kimya na kumsoma adui na ukifika
wakati muafaka mpiganaji hodari hufanya mashambulizi.

mashambulizi ya namna hiyo huleta matunda na hakika
maadui huanguka moja baada ya mwengine. iwe dodoma
au bandarini. mwenye macho haambiwi tazama.
 
Mzee mwanakijiji,

Kwanza nampongeza sana mama Malecela kwa mahojiano uliyofanya naye na hakika ndiye kiongozi pekee ambaye amekuja ukumbini kwako na kusema bila kuficha msimamo wake tofauti na wengi ambao walikuwa wakizunguka mbuyu mara inapotokea swala la kuonyesha msimamo wake.
Binafsi nimechukua baadhi ya point zake dhaifu na nitaziweka hapa kulingana na jinsi nilivyomsikiliza.
Kwanza inaonyesha wazi kuwa yeye mkweli pale alipoonyesha hafahamu ama amepuuza kiini cha Uchaguzi mkuu ndani ya chama, walipovunja sheria za uchaguzi wa chama hicho kuondoa hatua ya tatu ya uchaguzi wa rais...Hii ilikuwa imepangwa haiwezekani kabisa kubadilisha sheria dakika za mwisho..

Mama malecela hakurudi nyuma zaidi ktk kutazama hili swala limeanzia wapi zaidi ya kutazama kura za wananchi asilimia 80 kumchagua Kikwete,ushindi ambao hauna mashaka kwa sababu wananchi wengi bado walikuwa wakikiamini chama CCM kuwa ni chama chenye mrengo bora na pengine viongozi waadilifu...
Tatiuzo langu kubwa na Kikwete ni pale alipochagua baraza la mawaziri ambalo asilimia 80 walikuwa mafisadi na wenye uchu wa mali..mapema kabla alikwisha onywa kuhusu kundi hili lakini bado aliwachagua aidha iwe walipendekezwa kwake ama walikubalika na washauri wake lakini kwa sababu he had the last say.. hapa inanipa shida sana kuamini kwamba alikuwa hana UBIA na MTU...
Msemo huu unazidi kunitia mashaka pale aliposema TUSIJE KULAUMIANA MBELE YA SAFARI...ikiwa na maana vyeo walivyopata ilikuwa ni fadhila ama malipo fulani ambayo yatategemea uwajibikaji wako!..Kama kweli mtu ana deserve nafasi hiyo huwezi kumwambia tusije kulaumiana kama vile unafahamu uzembe wake ambao hutapenda aufanye pale!
Binafsi matumizi ya neno hili hayawezi kuja kama hakuna ushirika ktk mpangilio mzima wa kutawala maanake unapomwambia mtu usije kunilaumu ina maana - I have played my part, kazi kwako...Hilo kwanza..

Pili, ni kwamba hawa jamaa wote walikuwa very relaxed kwa kila walichokuwa wakikifanya na ajabu ni kwamba Kikwete kasubiri hadi maswala haya yamefika kwa wananchi wakati siku zote moja ya ahadi yake kubwa kwa wananchi ilikuwa yeye kuwashitaki watu hawa kwa wananchi.. meaning yeye atakuwa na habari mbaya kuhusu watu hawa na atazipeleka kwa wananchi ambao walikuwa hawafahamu. yet hata baada ya wananchi kuzifahamu mara nyingi amekuwa akitoa hotuba zinazowalinda wahalifu hao hao..
Na mwisho, hao mafisadi wamefikia kujiuzuru ktk hali ambayo inatatanisha sana yaani hawa watu wamechukua mabillioni ya fedha za serikali, kuingia mikataba mibovu ambayo yeye mwenyewe kama rais alitakiwa kuona ubovu wake, haihitaji Phd kuelewa jinsi fedha za serikali zilivyoliwa ovyo..anawaacha huru?... au ndio kutolaumiana kwenyewe huko!
Nne kama rais aliweza kuyaona mabaya yote yaliyotangulia wakati wa Mkapa lakini badala yake akayapa nafasi zaidi kwa kutumia watu wale wale waliokuwa wakiiba wakati wa Mkapa kushika nafasi kubwa zenye madaraka makubwa ktk sehemu nyeti za uchumi wetu.... WHY?..
Hata hivyo, baada ya yote haya viongozi hawa bado wanashika nafasi ndani ya chama, ndani ya Bunge letu bado wanatumikia wakati hawa watu ni sawa kabisa na Molesters ambao bado wanaruhusiwa kuendelea kuwa karibu na watoto ati kwa sababu walichaguliwa na wananchi ambao hawakufahamu kuwa hawa jamaa walikuwa criminals..
Pamoja na yote haya nafikiria Mama Malecela anahitaji muda zaidi kutazama undani wa ufisadi huu, apate muda wa kukuna kichwa vizuri na kujiuliza maswali mengi mazito ambayo hayawezi kuendeleza mapambano kuwaondoa utawala dhalimu..
South Afrika hawakupigana kumwodoa Botha na baadhi viongozi wachache waliokuwa wakiharibu jina la Utawala huo isipokuwa wakipigana vita kuondoa mfumo mzima wa Apartheid na sio watu wachache. Mimi nasema vita yetu Watanzania haitaishia kuwaondoa viongozi wa chafu wa CCM, bali kuondoa mfumo mzima unaotawala uchumi wetu ikiwa ni pamoja na AZIMIO la Zanzibar!..
Hao kina FISADIs watashughulikiwa kama wahalifu lakini kinachotangulia ni mfumo mzima wa CCM ambao ulizaliwa siku ya AZIMIO la ZANZIBAR kuwawezesha wao kugawana mali za serikali katika kujiandaa kwao na UBEPARI..

Hivyo hitimisaho langu ni kwamba yawezekana kabisa kuwa Mama Malecela ni mmoja kati ya viongozi wasiofahamu kinachoendelea jikoni lakini anatakiwa kuwa makini pale mashambulizi yanapotakiwa, kwa sababu Mafisadi ndani ya CCM ni wengi sana kiasi kwamba wengine hula nao sinia moja kila siku...na wamekaa msibani kama vile sio wao wachawi.
 
NAAM SHUKRAN MWK! HUYU MAMA ameonyesha ujasiri mkubwa sana kuongea ukweli!
nina imani kuna watu safi CCM ambao kwa sasa wataanza kuongea ukweli,zile dhana za ndio mzee na uoga zimeanza kutokomea .kwa hali hii huenda kukawa na mabadiliko makubwa katika nchi yetu!
 
Field Marshall ES,
humfahamu mama kilango. ungekuwa unamfahamu usingemtetea hapa. wazee wa kipare tayari wameapa huyu mama ubunge ni miaka 5 tu. mama kilango amewatukana matusi makubwa wazee wa kihurio-jitengeni kutokana na kisasi chake kisichokwisha kwa mzazi mwenzake.

serekali iliamua kutoa fedha kujenga sekondari 2 kihurio-uzambara na kihurio-jitengeni. lakini kwa ubinafsi alionao mama kilango akaamua sekondari ijengwe kihurio-uzambara alikozaliwa yeye.

katika mkutano wa hadhara mama kilango akawaambia wananchi wa kihurio-jitengeni wakiwemo wazee kwamba hataki kusikia habari ya ujenzi wa sekondari jitengeni. mama kilango akasema anayetaka kuongelea suala hilo akazungumzie chumbani na mkewe!!!

wazee na wananchi wa kihurio-jitengeni wakaamua kujenga sekondari kwa nguvu zao wenyewe bila msaada wa serikali na mbunge wao. sekondari ya jitengeni imejengwa wakati sekondari ya mama kilango inasuasua.

wazee wameamua wembe ulomnyoa ndhira 'daniel yona' ndiyo huohuo utakaomnyoa anna kione kilango. hawataki tena kumsikia huyu mama. kama kuna anayempigia debe basi ampe ubunge wa taifa, lakini same mashariki hapati tena.
 
mpiganaji bora ni yule ajuaye kupanga mashambulizi yake.
kuna wakati mpiganaji inabidi arudi nyuma kujipanga upya,
upo wakati inabidi akae kimya na kumsoma adui na ukifika
wakati muafaka mpiganaji hodari hufanya mashambulizi.

mashambulizi ya namna hiyo huleta matunda na hakika
maadui huanguka moja baada ya mwengine. iwe dodoma
au bandarini. mwenye macho haambiwi tazama.


Mkuu Kafara,

Heshima mbele mkuu, maneno mazito sana hayo na ubarikiwe, wabunge wetu wako macho sana, hivi karibuni niliongea sana na Mkulu Zitto akaniambia kwamba hakuna kuangalia nyuma wala pembeni, straight ahead mpaka kieleweke!
 
Nimesikiliza mahojiano yote ambayo ni kama dakika 27 hivi kati ya Mkjj na Mama Kilango. Kama CCM ikiamua kumuweka mgombea tofauti na Kikwete 2010 na huyu mama akaamua kuweka jina lake basi hana mshindani si Membe wa Masha wanaoweza kusimama na huyu mama. CCM kama kweli inataka kujisafisha na kurudisha hadhi iliyokuwa nayo miaka ya nyuma basi wanahitaji watu kama Mama Kilango wanaosema ukweli bila kuogopa na wanaosema yale yaliyo moyoni mwao. Siku hizi kusikia kiongozi wa CCM anaongea maneno mazito kama huyu mama ni nadra sana. Wote wamekuwa MASPIN DOCTORS ili kuendelea kuwalinda mafisadi

Mkuu Bubu,

Maneno mazito sana haya, unajua inatakiwa mwananchi awe na kichwa kikali kuweza kuona namna yako, bravo mkuu!
 
Nimesikiliza mahojiano yote ambayo ni kama dakika 27 hivi kati ya Mkjj na Mama Kilango. Kama CCM ikiamua kumuweka mgombea tofauti na Kikwete 2010 na huyu mama akaamua kuweka jina lake basi hana mshindani si Membe wa Masha wanaoweza kusimama na huyu mama. CCM kama kweli inataka kujisafisha na kurudisha hadhi iliyokuwa nayo miaka ya nyuma basi wanahitaji watu kama Mama Kilango wanaosema ukweli bila kuogopa na wanaosema yale yaliyo moyoni mwao. Siku hizi kusikia kiongozi wa CCM anaongea maneno mazito kama huyu mama ni nadra sana. Wote wamekuwa MASPIN DOCTORS ili kuendelea kuwalinda mafisadi
Ni rahisi kwa Lowassa kupendekezwa kuwa mgombea kwa tiketi ya CCM kuliko Masha, Membe au Mama Kilango. Labda mnaongelea CCM ambayo naijua mimi.
Kwa hiyo Mama Kilango akigombania urais na Mbowe mtampa mama Kilango?
 
"Tulikokuwa tunaenda siko, tumeamua kugeuka" - Mhe. Anne Kilango Malecela

...mambo ambayo anayazungumzia ni pamoja na ... kwanini wabunge wa CCM walikuwa wanaitetea serikali yao hata ilipokuwa inaharibu

... kwanini anaamini Kikwete ni kweli anataka mabadiliko

...Mimi niko impressed na watu mara chache sana.. this is one of those times.

Anna Kilango Malecela (Mb.) ni shujaa kweli kweli. Ni wachache ndani ya CCM, kama wapo, ambao wanamshinda kwa uwazi, juhudi na ari mpya ya kuleta mabadiliko. Hata hivyo, japo ana nia ya dhati ya kufanya kazi za Wananchi, uchambuzi na uelewa wake wa masuala ya Kisiasa una mushkeli nyingi. Aidha anaogopa kusema anachotaka au anashindwa kuwasilisha anachotaka kukisema. Na inawezekana hajui kinachoendelea.

Kuhusu ufisadi, anasema tatizo kubwa lililotufikisha hapa tulipo ni kwamba mali za nchi hazilindwi na viongozi. Ukisema viongozi hawalindi mali za Umma unatenganisha wezi na walinzi. Huu uchambuzi aidha ni wa asiye jua picha halisi ya Ufisadi au wa anae ogopa kusema Viongozi ni wezi wa mali za Umma. Hakuongelea matatizo ya kutokuwepo kwa ufuatiliaji wa Sheria au kutokuwepo kwa Sheria za kuwakamata Mafisadi.

Anasema suluhisho la matatizo yetu ni kubadilisha mfumo wa kiuchumi ambao unaruhusu wachache kumiliki mabilioni ya pesa huku walio wengi hawana kitu. Halafu hapo hapo anasema hayo mapesa yanayomilikiwa na wachache sio yao, bali, ni ya Serikali. Tatizo la kutoelewa au labda kushindwa kujieleza linajitokeza hapa. Kama wachache wanamiliki pesa zisizo kuwa zao basi hilo ni tatizo la ufisadi, tatizo la wizi, na sio tatizo la mfumo wa Uchumi. Utabadilisha mfumo, na hata ukafufua Azimio la Arusha, lakini kama kujapigana na ufisadi, mfumo wako mpya labda ndio utakuongezea matatizo maana utazidi kujichanganya. Sasa hivi Watanzania tumechanganyikwa juu ya mfumo wa Siasa na Uchumi tunaofuata, kati ya Ujamaa na Kujitegemea au Ubepari unaoruhusu njia kuu za uchumi kumilikiwa na wachache. Kubadili mfumo wa Kiuchumi peke yake hakuwezi kutatua ufisadi.

Akitetea jinsi Bunge la CCM lilivyo kuwa limelala usingizi, anasema hata South Africa walitawaliwa na Makaburu mpaka siku moja wakaamua kugeuka, wakaona hawawezi kuongozwa na makaburu wachache. Huu mfano hauhusiki, kwa sababu hakuna siku wa South Africa walikuwa wanaona ni sawa kutawaliwa na Makaburu. Vita vya kwanza dhidi ya Wadachi vilianza siku maharamia wa kampuni ya Dutch East India Co. walipotia mguu kwenye ardhi za wa KhoiKhoi karne ya 17. Tofauti na wapigania Uhuru wa South Africa, hili Bunge la CCM ya Mama Malecela lilikuwa limelala likiota njozi za Alinacha. Ni pale wakina Zitto, Slaa na wengine wawili watatu walipoonekana ndio peke yao wanafanya kazi kati ya mamia ya Wabunge wa Jamhuri ndipo wakina Mama Malecela walipoona soni na kuzinduka kutoka katika usingizi wa Rip Van Winkle!

Uchambuzi wa Siasa za Uchaguzi wa Anne Malecela nao una matatizo makubwa ya kurahisisha rahisisha mambo. Anasema Kikwete alichaguliwa na Mkutano Mkuu wa CCM na baadaye kwa 80% kwenye uchaguzi mkuu. Kwa mtaji huo, anadai, si yeyote bali ni wananchi waliomchagua Kikwete. Sasa hili ni jaribio la wazi wazi la kuficha madhambi ya CCM wakati wa Uchaguzi. Kwamba chaguzi za CCM zimejaa mizengwe na shutuma za rushwa. Ndo maana kabla ya Mkutano Mkuu mgombea tiketi ya CCM, Jakaya Kikwete, ilibidi atoe onyo rasmi kwamba safari hii akifanyiwa mizengwe katika kuchagua jina la tiketi basi hatokubali; Ndo maana kuna vikundi vya "Mtandao" na "wasio Mtandao" ndani ya CCM; Ndo maana mpaka leo Zanzibar kunafukuta moto kufuatia chaguzi za CCM zilizo jaa mushkeli, dhulma, na zahma za mateso dhidi ya wapinzani, na wakati mwingine hata umwagaji damu. Ndo maana waasisi wa CCM, wakina Butiku wamekuwa wakisema wameshuhudia rushwa zikitembea mchana mchana kwenye chaguzi za CCM; Ndo maana Mahakama Kuu ilifutilia mbali ufisadi wa wazi wazi wa uchaguzi uliobatizwa jina la kuficha ficha, takrima. Kwa hiyo, Malecela hawezi kusema eti matokeo ya kura yanaonyesha matakwa ya wananchi. Hawezi kujifanya hajui kwamba wapo wachache fulani wazito waliohusika katika kumchagua Kikwete, zaidi ya kura za Wananchi. Malecela, mbunge wa ngwe ya pili, si mgeni wa Siasa na atakubaliana na mwandishi wa Kimarekani aliyewahi kusema "ukweli haujulikani kwa kura ya wengi."

Mama Malecela pia aliharibu vibaya vibaya aliposema Kikwete ana nia ya kuleta mabadiliko eti kwa sababu katika hotuba yake ya kwanza Bungeni aliahidi kupitia upya mikataba. Malecela pia anamsifu Kikwete kwa kuliambia Bunge kwamba hana ubia na kiongozi na kwamba aliliambia Baraza lake la Mawaziri la kwanza kwamba wasilaumiane mbele ya safari kama wakilega lega kwenye kazi. Tatizo ni kwamba amempasisha Rais kwa maneno ya hotuba aliyo yatoa alipopata Madaraka. Kikwete amemaliza nusu ya Utawala wake sasa hivi, utawezaje kumtathmini kwa kuangalia alichosema siku anachukua madaraka?

Huwezi kutuambia Kikwete ana nia ya kuleta mabadiliko bila kutueleza inakuwaje kuwaje anateua mafisadi kutwa kucha, akidharau nasihi za wananchi kuhusu sifa chafu za teuzi zake. Rais anaefukuza Gavana wa Benki halafu anamrithisha kazi msaidizi wa aliyemfukuza. Rais anaewaambia viongozi wasiogope kuitwa mafisadi, akidharau msingi muhimu wa maadili ya uongozi unaosema Kiongozi yabidi aepuka, sio tu ufisadi dhahiri, bali hata taswira ya ufisadi. Rais anaekalia ripoti za uchunguzi wa ufisadi bila kujali vilio vya wananchi vikiomba azitoe hadharani. Rais anae waambia wananchi kwamba viongozi wastaafu wanaoshutumiwa na Ufisadi kushoto na kulia "waachwe wapumzike." Rais anaevumilia kuona kilindi cha kiza kinagubika mazingira ya kutoweka kwa mashahidi na washutumiwa wa ufisadi wa mabilioni ya fedha za jasho la masikini wa kutupwa!

Ukitetea Rais kama huyo, tunaweza kusema aidha huelewi elewi kinacho endelea au na wewe juhudi zako inawezekana ni changa la macho. Kinacho fadhaisha zaidi na zaidi ni kwamba watu kama Mbunge Anne Malecela ndio tegemeo la nchi, ndio crème de la crème ya uongozi wa nchi yetu, halafu nao hawajui kinachoendelea!
 
jamani sometime tuwe appreciative, kusipokuwa na wa kusema tunalalamika, na mtu akiamua kujifunga kibwebwe kusema bado haturidhiki, sasa lipi jema sie, mbona tunakuwa viumbe wazito sana.

Mama nakubaliana nawe kabisa.

Nimemsikiliza huyu mama kwa kweli nimetokea kuvutiwa naye sana.Anakubali na kukiri pale walipokosea na yuko tayari kufanya mabadiliko. Kwa kweli kuna wakati Watanzania wanaudhi sana na ndo maana huwa nasema tuko mbele sana kulalamika tu na kusubili wengine watutengenezee. Huyu Mama kajitolea hapa na ni hatari hata kwa uhai wake lakini watu hatuoni hilo. Akikaa kimya tunalaumu, akikosoa tunamtafutia sababu, tatizo letu nini!!. Mimi siku zote nasema JK pamoja na kuwa na kashfa, lakini akiamua leo kuwashughulikia maafisafi wote vilivyo na kuwapeleka mahakamani, kuanzia wa mikataba ya mibovu hadi wa wizi BOT na rasili mali za Watanzania sitakuwa na tatizo naye.

Binadamu sie sio malaika, unapogundua umekosa na kukiri na ukajirekebisha ni vizuri zaidi kuliko angeendelea kukaa kimya. Kwa nini kila mbunge anapovalia njuga ufisadi tunamtuhumu kuwa anatafuta uwaziri? Mama Malecela funga kibwebwe twende mbele tuko nyuma yako.
 
Back
Top Bottom