Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Kutana na moja kati ya nyoka hatari sana duniani.

THE DEADLIEST SNAKE ON THE PLANET!
Anaitwa koboko au, The African Black Mamba!
Anapatikana katika Bara la Africa tuu...
Ndie nyoka hatari kabisa! Anatoa sumu aina mbili na zote ni noooma! Anatoa sumu inayojulikana kama "Neurotoxin hii huathiri mfumo wa neva
Napia anatoa sumu nyingine aina ya Cardiotoxin hii hushambulia mfumo wa moyo.... Nyoka huyu akikuuma unaweza kufa ndani ya dakika 20!

Black Mamba ninyoka mkorofi katili anasumu kali, anasifa ya urefu kama uavyomuona anafika hadi miguu 14 kwa hesabu za kiswahili! Ye huwa hana mwili mkubwa kama kina Python(Chatu) Mungu ni fundi sana huwa hakosei! Huyu nyoka ana roho mbaya sana kwanza amejaaliwa mbio kuliko nyoka wote! Ukikutana nae kuna ishara kuu mbili atakuonyesha kuwa Mimi African Black Mamba... Nyoka niliye jaaliwa sumu kuliko nyoka wote! Ulaya hayupo huyu lkn Wazungu wanamtambua vema wakotaka kuja Afrika kuna viumbe kwanza wanaambiwa mkifika huko mnapaswa kuchukua tahadhari ya hali ya juu na viumbe hivi hatari.. Ktk list huyu nae yumo! So ukipata bahati yakukutana nae kwanza atakutisha! Ata achama kinywa ama mdomo wake wenye rangi nyeusi kwa ndani! Kinywa chake ni cheusi kwa ndani na ndio kimefanya aitwe Black Mamba! Pili utamskia anatoa sauiti kama msela anaita demu! Au kama tairi linalotoa upepo...Tatu utamuona anatanua shingo yake japo c kama ya Cobra!!! Hapo ujue uko mbele ya nyoka hatari kabisa! Uzidishe maombi! Vitu viwili usijethubutu kuvifanya! Moja... Uskimbie.. Maana huyu nyoka anambio zaidi ya Husein Bolt! Mamba anakimbia Maili 12 kwa saa... Na akikumbiza hakubali hadi akugonge sehemu ya mwili wako.. Ye ardhini huwa anateleza! Na ukimkimbia ni lazima tuu atakuunganishia! Na hatakukosa! Pili kuna wale watu akiona tu nyoka ye anakimbilia fimbo au jiwe... Siku ukutana na nyoka huyu jua umekwisha! Wataalam wanakwambia nyoka huyu hapigwi! Kwani hata hilo jiwe huenda usiwahi kulirusha au mfe wote! Kwani Black Mamba anasifika kwa Show za kikatili anashambulia vibaya sana! Ndio maana nilisema Mungu nifundi! Pamoja na kumuumba nyoka huyu na Sumu kali mbio nyingi, hasira na urefu lkn hapo hapo nyoka huyu amejaaliwa huruma ndani yake ukikutana nae akianza kukuonyesha sarakasi zake kuwa mimi ndie nyoka hatari nawe Binaadam ukijishusha uskimbie wala ustupe jiwe ubaki unamuangalia tuu macho kwa macho! Unaambiwa atatuliza mzuka! Na wala hatakugusa ataingia zake mitini! Unaona Muumba alivyo wa ajabu!! Mamba anataga mayai kama kuku tuu kiota chake huwa ardhini...Jike anataga mayai 10-25 akishataga mayai yake huwa yanajiengua yenyewe tuu baada ya miezi mitatu....Joto ni muhimu kwaajili ya lncubation...na vitoto vyake vikisha jitotoa unaambiwa vinaanza mishe saa hiyohiyo hujitegemea kwa kilakitu! Na vinakuwa na sumu kali kama Mama yao tuu yaani haina kuremba!!! Nyoka huyu anaishi hadi miaka 11 porini... Akiwa anafugwa anaeza ishi hadi miaka 12...... Mi nilishawahi muona huyu nyoka michezo alituonyesha imenifanya nisitamani kukutanae tena japo nawapenda wanyama na wadudu!!.

Picha na stori toka kwa Faru Wa Kikwete
d3414b74fd882b09a6c98cd2c5bca8dd.jpg
 
huyu kiumbe mbilinge mbilinge zake nazijua uzuri sana, miaka ya 98-99 tulikuwa na kibarua cha kuwinda nyoka, kuna msouth alikuwa anakula hawa wadudu( momma, chatu na Cobra alikuwa anahitaji sijui huyu cobra alikuwa anahitaji nini maana ilikuwa mkimpeleka bila kichwa hamlipwi,,,sasa kuna siku tulimuona huyo blach mamba, kwa mbaali tuu nilimjua nikawaambia wenzangu leo pori limeingiliwa tuondoke maana huyo ndio m babe wa pori, huyu jamaa anakwepa hata risasi nuksi kweli kweli Cobra asubiri sana hapo, na ukimkuta karibia na mayai yake ndo siku yako imefika...
 
pia kuna nyoka mmoja anarangi ya pink ushawahi kukutana nae?
 
FB_IMG_1480009233710.jpeg


THE DEADLIEST SNAKE ON THE PLANET!

Anaitwa Mamba mweusi wa Africa

The African Black Mamba!
Anapatikana katika Bara la Africa tuu...

Ndie nyoka hatari kabisa! Anatoa sumu aina mbili na zote ni noooma!

Anatoa sumu inayojulikana kama "Neurotoxin hii huathiri mfumo wa neva
Napia anatoa sumu nyingine aina ya Cardiotoxin hii hushambulia mfumo wa moyo.... Nyoka huyu akikuuma unaweza kufa ndani ya dakika 20!

Black Mamba ninyoka mkorofi katili anasumu kali, anasifa ya urefu kama uavyomuona anafika hadi miguu 14 kwa hesabu za kiswahili! Ye huwa hana mwili mkubwa kama kina Python(Chatu) Mungu ni fundi sana huwa hakosei!

Huyu nyoka ana roho mbaya sana kwanza amejaaliwa mbio kuliko nyoka wote! Ukikutana nae kuna ishara kuu mbili atakuonyesha kuwa Mimi African Black Mamba... Nyoka niliye jaaliwa sumu kuliko nyoka wote!

Ulaya hayupo huyu lkn Wazungu wanamtambua vema wakotaka kuja Afrika kuna viumbe kwanza wanaambiwa mkifika huko mnapaswa kuchukua tahadhari ya hali ya juu na viumbe hivi hatari..

Ktk list huyu nae yumo! So ukipata bahati yakukutana nae kwanza atakutisha! Ata achama kinywa ama mdomo wake wenye rangi nyeusi kwa ndani!

Kinywa chake ni cheusi kwa ndani na ndio kimefanya aitwe Black Mamba! Pili utamskia anatoa sauiti kama msela anaita demu! Au kama tairi linalotoa upepo...Tatu utamuona anatanua shingo yake japo c kama ya Cobra!!! Hapo ujue uko mbele ya nyoka hatari kabisa! Uzidishe maombi!

Vitu viwili usijethubutu kuvifanya! Moja... Uskimbie.. Maana huyu nyoka anambio zaidi ya Husein Bolt! Mamba anakimbia Maili 12 kwa saa...

Na akikumbiza hakubali hadi akugonge sehemu ya mwili wako.. Ye ardhini huwa anateleza! Na ukimkimbia ni lazima tuu atakuunganishia! Na hatakukosa!

Pili kuna wale watu akiona tu nyoka ye anakimbilia fimbo au jiwe... Siku ukutana na nyoka huyu jua umekwisha! Wataalam wanakwambia nyoka huyu hapigwi!

Kwani hata hilo jiwe huenda usiwahi kulirusha au mfe wote! Kwani Black Mamba anasifika kwa Show za kikatili anashambulia vibaya sana! Ndio maana nilisema Mungu nifundi!

Pamoja na kumuumba nyoka huyu na Sumu kali mbio nyingi, hasira na urefu lkn hapo hapo nyoka huyu amejaaliwa huruma ndani yake ukikutana nae akianza kukuonyesha sarakasi zake kuwa mimi ndie nyoka hatari nawe Binaadam ukijishusha uskimbie wala ustupe jiwe ubaki unamuangalia tuu macho kwa macho!

Unaambiwa atatuliza mzuka! Na wala hatakugusa ataingia zake mitini! Unaona Muumba alivyo wa ajabu!! Mamba anataga mayai kama kuku tuu kiota chake huwa ardhini...

Jike anataga mayai 10-25 akishataga mayai yake huwa yanajiengua yenyewe tuu baada ya miezi mitatu....

Joto ni muhimu kwaajili ya lncubation...na vitoto vyake vikisha jitotoa unaambiwa vinaanza mishe saa hiyohiyo hujitegemea kwa kilakitu! Na vinakuwa na sumu kali kama Mama yao tuu yaani haina kuremba!!! Nyoka huyu anaishi hadi miaka 11 porini... Akiwa anafugwa anaeza ishi hadi miaka 12......

Mi nilishawahi muona huyu nyoka michezo alituonyesha imenifanya nisitamani kukutanae tena japo nawapenda wanyama na wadudu!!.
 
Huyo Nyoka ni Kifo!Nishamuona Pacha Wake the Green Mamba!
Mkuu,waweza tupia tu video twake tuvili tutatu!?
 
Aisee, niliwahi kumuona huyu nyoka nachunga bt yey alikuwa wa kijan kweli aliniangalia kwa makin kila nilichokifanya had nikaishia na yey akaendelea na mishe zake, mbuzi walianza kumuona alisimama km vile amening'inizwa akiniangalia nafanya nini, Hawa kweli Co nyoka wazuri.
 
Back
Top Bottom