Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Koboko (Black Mamba) - Nyoka hatari zaidi duniani

Mkuu huyo nyoka na mjua vizuri sana nimesoma uko tabora boys wapo wengi tu akisikia binadam anajongea sehem alipo hua anafoka kukujulisha nipo maeneo haya so usimzuru na unaweza pishana nae bila tatizo lolote.sisi tulikua tukiona ana vuka barabara tuna mchezea kwa kumvuta nyuma alipo toka anaishia kufoka tu ila hiyo mashine nyingine ilishawahi kuzingua watu makabulini akuna aliye baki nahisi ata marehem asinge kua ndani ya jeneza angekimbia
hahaaa...daahhh acha basiii marehemu angefanyaje ??!!
 
honey-badger-pin-cushion-wf-wm.jpg
 
Kuna koboko mmoja alikuta roli la madawa limeanguka vidonge vikawa vimesambaa kila mahali kwa njaa zake koboko yule akala Viagra basi alisimama mwezi mzima.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji28] chaii
 
Kinachochekesha ni kwamba pamoja na sumu yake yote akimng'ata nguchiro anazimia tu hafi. Hahahahahaha, nilivyosikia NAT GEO Wild nilicheka kweli, Mamba kajipiga akakang'ata kakalala baada ya muda kakamdaka yeye.
Nakumbuka na mimi niliona kipindi kinacho fanana na hicho ulichoona wewe battle ilikuwa ya haja!! Utofauti ni kuwa Mamba alikang'ata mara nyingi nyingi sana.

Kutokana na Majeraha Mamba alikufa ila alishakaingizia sumu ya kutosha kalizima kwa muda halafu kikaamka tena kikamla Mamba kiroho safi kabisa.

Hivi kuna tofauti kati ya nguchiro na Nyegele? (Honey badger) Kwa sababu ile niliyoona mimi ilikuwa Mamba vs Honey badger.
 
Nyoka wengi hua wana aibu na huwa wa kwanza kuretreat unless wawe cornered, koboko hajui kuretreat, ana accuracy, speed na bado yeye ndiyo ataanzisha ugomvi.

Iwe iwavyo ninachojua hachomoki mbele ya honey badger.
Nilitaka kuuliza hapo kwa honey badger maana huyu jamaa ni mbishi hatari, nyoka wote wanamuogopa hahahha
 
Koboko ni level nyingine kabisaa yaani sio simba,chui,chatu, cobra wote unawajua wewe ni wachumba mbele ya koboko.

Simba au chui mkiwa watu wawili au watatu mmeshika mawe au mna silaha za jadi simba mwenyewe anakimbia mkimbia lakini sio koboko.....

Yaani hata muwe watu 100 na mna silaha za moto na mabomu ya machozi mbele ya koboko ni sawa mnajisumbuaaa buree kwa sababu ana uwezo wa kupambana na jeshi zaidi ya miaa na akawauwa watu woteee na hakuna atayebakia salama

Kwa kifupi tuu koboko ni jeshi la mtu mmoja
Jeshi la nyoka mmoja !!!
 
Unajua huyu mnyama huwa hana staha,kuna wakati huwa anang'atwa na nyuki mpaka anakufa.
Huyo ndiye nguchiro ...daah kama ndiye huyo kweli nimbishi "" halafu mbona kama anafanana nawale waliomkimbiza yule mzungu wa kwenye bush man (the god must be crazy) mpka wakawa wanakula viatu vyake ...wale nao walikuwa wabish mnooo aisee
 
Huu ni moto wa kuotea mbali
Nakumbuka wakati Marehemu Samuel Sita aliomba watumwe kikosi kazi wakawasake hawa viumbe Urambo lakini walitahadharishwa wakaambiwa wanakwepa shaba hao na wana mbio za 12miles/h
Ilibidi waombwe na wanakijiji wasaidie lakini wapi walikuwa wameishaua wanne

Ni kiumbe hatari kuwahi kuishi na wanapatikana maeneo mengi East and southern Africa
Wanatajwa sana kwa hilo jina mimi sijawahi kuambiwa usimtaje
Kiboko ya koboko ni nyegere
 
Huyo ni Badger bird akiona mzinga wa nyuki huwa anaenda alipo Nyegere na kuanza kuimba imba Nyegere akimuona huyo ndege anajua asali imeoatikana bila kujua nyuki wanamsubiri.
aiseee nyegere ndiye nguchiro "" daahh kwahiyo huyo ndege ni mchochezi ...wataka kuniambia ndio tabia ya zito ?? hahaa
 
Back
Top Bottom