Blackcornshman
JF-Expert Member
- Aug 25, 2016
- 6,514
- 15,701
Kunyanyua kwapa.fukuza wote wasio na nidhamu, mchezaji asiye na nidhamu/jua umuhimu wa kuipigania timu yake na taifa lake wa nini?
Kaseja na kuwa bora ila hana nidhamu alisugua benchi iwe hao wahuni.
mambo ya kufeli yapo tu uingeleza hadi leo anafeli kunyanyua kwapa iwe Tanzania.
Fukuza mpaka wawe na akili
Baada ya Kumaliza kusoma hili gazeti.. Nikuulize, Je Aishi Manula yeye alimaliza Mechi saa mbili asubuhi??!! Mbona karipoti na ni mchezaji wa simba??!!Ushindi ni kiwango cha kutandaza kandanda, hayo mengine ni mbwembwe tu. Kuna wachezaji watukutu duniani lakini makocha walienda nao hivyo hivyo kwa kutambua mchango wao. Edmundo, Romario na Baloteli ni mfano tu wa wachezaji wasio na nidhamu ndani na nje ya uwanja, yaani red card ni muda wowote! Lakini hasara ya kuwakosa kikosini ni kubwa kuliko kuwa nao, na ndio maana makocha walikuwa wanawatumia hivyo hivyo kwenye vikosi vyao. Sasa itakuwa hawa waliochelewa kufika kambini, ukizingatia siku waliyotakiwa kuripoti kambini walikuwa na mechi iliyoisha saa 2.00 usiku! Mbona kambi bado inasubiri wachezaji kibao tu, watano waliopo Kigali na Yanga, akina Samata, Msuva, Ulimwengu, Banda, Farid, Chilunda na Mandawa, wote hao wapo nje bado hawajafika, eti unawafukuza wachezaji waliomaliza mechi saa 2 usiku !
Aishi Manula yeye ni mchezaji wa Faru Jeuri au Manzese mbona kafika kambiniTff wamepangua ratiba ya mechi ya Azam, Simba na Yanga..kwasababu Kocha anawahitaji mapema zaidi wachezaji kambini.
Inamaana Tff walikwenda na ratiba sawa na Kanuni hasa kuhusu timu zote za Taifa na Vilabu vya mpira. Sasa yeye anataka akae muda mrefu kinyume ya ilivyozoeleka.
Mchezaji akiitwa timu ya Taifa tayari anajua, ni maelekezo kidogo tu. Hapa tatizo kocha na hasa ukizingatia walimaliza mechi yao mwisho saa ngapi? Na yeye anawahitaji muda gani?
Sent using Jamii Forums mobile app
Kuhusu hili na mm nimejiuliza sana Mkuu! Nahisi kocha amekurupuka kuamua kuwatimua wachezaji hawa. Au Kuna mtu amemshauri vibaya juu ya hili.Pomoja na hivyo mkuu, kumbuka akina Chilunda, Samatta, Mao, Msuva, Banda..Hawajaripoti na wachezaji wa Simba sio kwamba wamegoma wamechelewa tena masaa.
Tuangalie na upande wa pili, hiyo imo
Sent using Jamii Forums mobile app
Katika hili kwa kweli amechemka kabisaKocha anatuchokoza huyu sasa subiri tutaendelea kuzomea taifa stars
Timu ya taifa wachezaji wakiitwa lazima wapewe na posho za kuwafikisha kambini hilo halijazingatiwa kocha anakurupuka tu
Day one failure
NdioAishi Manula yeye ni mchezaji wa Faru Jeuri au Manzese mbona kafika kambini
Akili za viazi mbatata zitajibu ilivyojibu
Mpumbavu lazima ajibiwe hivyoAkili za viazi mbatata zitajibu ilivyojibu
Hao wachezaji wenu wa Simba na Yanga unaowashabikia waliishafanya mini cha maana, kuanzia kwenye vilabu vyao hadi timu ya taifa, hebu tueleze ili tujue aisee, mwacheni mwalimu atengenezi kikosi chake.mpira wa kibongo unatawaliwa na SIMBA na YANGA sasa ngoja tushuhudie maneno baada ya kufungwa hata mechi moja wanao msaport kwa sasa ndo hugeuka mwiba kwenye kibarua chake
Inaonekana kabisa wew siyomushambiki wewe ni mshagiliaji acha watu watoe hoja za manaMkataba wake wa kufuindisha Taifa Star ukiisha anahamia Yanga.
Tushawajua mambo yenu, tumejifunza kwa Kocha Maximo wa Brazili.
Simba hebu tuelekeze nguvu zetu kwenye mechi zetu za ligi na za kimataifa.
Huyo ni kocha wao huyo, ukiona mtu unamfanyia kosa moja tu na anakimbilia adhabu kali kama hatua ya kwanza ujue alishakuwa na kisasi fulani kwako.
Mafunzo ya ukocha yanajumuisha mahusiano mazuri na wachezaji wake, kama mchezaji kafanya kosa flani jambo la kwanza ni kufahamu chanzo cha hilo kosa, na linafuatia suluhisho la kiungwana ikiwa pamoja na kuzungumza na wachezaji au mchezaji husika ili kuweza kupata ufumbuzi unaofaa na wenye Busara
Dunia ya sasa sio ya kufanya maamuzi ya harakaharaka yaliyojaa jazba na visasi.
Karibu The Crane
Sent using Jamii Forums mobile app