Kocha Juma Mgunda nakuonya, uchezaji wa Simba bado hauridhishi

Kocha Juma Mgunda nakuonya, uchezaji wa Simba bado hauridhishi

martial jb

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2021
Posts
863
Reaction score
1,462
Habari wakuu.

Kwanza nianze kukupa hongera kocha mkuu wa Simba Juma Mgunda kwa kufuzu kwako makundi kwenye michuano ya CAF Champions League, hakika umepambana kwa kuitoa SIMBA pale ilipokuwa mpaka hapo ulipofikia.

Ila ningependa kukuonya na kukuonya tena, onyo hili ambalo hautalisikia kwa mtu mwingine yeyote bali ni mimi tu. Bado timu inahitaji mikakati na ubora kwa kiasi cha kutosha. Uchezaji unaocheza Simba bado hauridhishi kiukweli kabisa. Kwa uchezaji huu, inawezekana tukaenda kudhalilika hatua ya makundi Ligi ya Mabingwa na hata Ligi Kuu hapo baadae.

Wachezaji hawana kasi, umakini, na wazito tofauti na ilivyo kawaida. Pia pasi hazifiki kwa walengwa, timu hailewani na timu inaonekana kuridhika sana tofauti na ilivyo kawaida.

Nakumbushia Simba ya Aussems na pia nItakumbushia Simba ya Gomes. Simba ambazo zilikuwa na kasi na mashambulizi ya kutosha na pia njaa ya magoli muda wote. kwani kama De Agosto angekutana na Simba zile si ajabu angekula 9-0!

Inawezekana kufuzu makundi na kuondolewa kwa Yanga kukanyima nafasi ya hili kuongelewa, ila mimi ntaliongelea ili isije kukugharimu.

Nakukumbusha pia mashabiki wa Simba hatuchelewi kubadilika pindi utakapo tuzoea sana, na kutuharibia kikosi chetu pendwa.

Zaidi ya hapo nakupa hongera, Mtanzania mwenzangu.
 
Team hazikosi mapungufu, Al hillal kamtahiri utopolo akiwa kamiliki mpira karata ya kufuzu ni mhimu Sana siyo kucheza kwa kufurahisha watazamaji.

Mengine mwalimu kayaona mwenyewe.
Ni kweli ndio maana namwambia mgunda aangalie makosa yake
 
Ila wewe jamaa bana

Hivi uliangalia yale magoli matatu tuliyowafunga Agosto kule kwao? Uliona ile speed ys Okrah kwenye goli la kwanza?

Uliona ile speed ya Mzamiru, Chama, Kanoute na Mwenda kwenye goli la pili?

Uliona speed ya Chama na Phiri kwenye goli la tatu?

Sijui unataka watu wakimbieje. Mpira unachezwa kwa malengo. Hukimbii hovyo kama Moloko au Twisila.
 
Ukweli ni kwamba tuna kaupepo fulani ka michuano ya caf, ila timu bado haichezi vizuri, tutapata tabu ama aibu kabisa huko kwenye makundi.
Mimi naridhika tunavyocheza

Tuncheza kikubwa sana. Huchezi hovyo hovyo. Unacheza kwa discipline. Tulishapata matokeo mechi ya awali, hii mechi ya leo haikuhitaji kucheza hovyo ili yasitukute yaliyotukuta na Jwaneng mwaka jana
 
Mimi naridhika tunavyocheza


Tuncheza kikubwa sana. Huchezi hovyo hovyo. Unacheza kwa discipline. Tulishapata matokeo mechi ya awali, hii mechi ya leo haikuhitaji kucheza hovyo ili yasitukute yaliyotukuta na Jwaneng mwaka jana
Tusubiri muda utasema, hii mbinu yake ipo siku litatusibu jambo.

Sifurahishwi na kumuweka okrah kushoto, kuna vitu anashindwa kuvifanya,
 
Tusubiri muda utasema, hii mbinu yake ipo siku litatusibu jambo.

Sifurahishwi na kumuweka okrah kushoto, kuna vitu anashindwa kuvifanya,
Alipokuwa Ghana alikuwa anacheza huko huko kushoto ndio kulimfanya ang'ae.

Timu yetu ni imara sana. Imekamilika sehemu nyingi kasoro beki 2 na namba 7 wake baada ya Sakho ku drop kiwango.

Kapombe akirejea na Banda/Sakho akicheza namba 7 kwa ufanisi tuna nafasi nzuri sana maana midfield kwa sasa ni imara sana kwa Muzamiru na Putin Kanoute
 
Shida kubwa ipo sehemu ya katikati. Wachezaji wakifika mbele kidogo ya dimba wanashindwa kujua nini cha kufanya, mipira mingi inarudishwa nyuma.

Hawajiamini wakifika eneo lile, wanaogopa kupoteza mpira ndiyo maana wanaamua kurudi nyuma. Leo nimeona mara kadhaa mpira uko kwenye kona karibu na kibendera upande wa Waangola, badala ya kuendelea na pressure, mpira ulirudishwa nyuma hadi kwa Manula.
 
Juma Mgunda ni kocha aliyekamilika kimbinu na kiujuzi........mengine ni ya kibinadamu tu......

Timu imeshapata matokeo Angola hakuna haja ya kupress hali ya kuwa tuna game zingine ngumu mbele ambazo ni za muhimu timu imecheza kikubwa sana, timu imekamilika kasoro zipo ndogo ndogo, ukicheza Kwa kuwafurahisha mashabiki utapata majeruhi na mechi zijazo zitakuwa ngumu.
 
Mimi ni shabiki wa Yanga SC
kiukweli bora huyo wa Simba SC ambae mpira wake sio ila angalau wanapata matokeo katika mechi zile muhimu na tusipoangalia hiyo mechi ya Tarehe 23 Simba sc atampiga Yanga sc coz kwa sasa wana confidence ila pia hawana kinachowapa stress tofauti na Yanga sc ambao kwa sasa baada ya matokeo ya Jana kinachoendelea ni lawama na kumtafuta mchawi ilihali kuna mechi na Simba sc inakuja.
 
Mimi ni shabiki wa Yanga SC
kiukweli bora huyo wa Simba SC ambae mpira wake sio ila angalau wanapata matokeo katika mechi zile muhimu na tusipoangalia hiyo mechi ya Tarehe 23 Simba sc atampiga Yanga sc coz kwa sasa wana confidence ila pia hawana kinachowapa stress tofauti na Yanga sc ambao kwa sasa baada ya matokeo ya Jana kinachoendelea ni lawama na kumtafuta mchawi ilihali kuna mechi na Simba sc inakuja.
Rudi Kulala Simba hawezi mfunga yanga
 
Back
Top Bottom