Kocha Matola, Boss wako Pablo na Benchi lenu zima la Ufundi ni kwamba Orlando Pirates FC yenyewe ni ile ya kuanzia dakika ya 70 hadi ya 93 ya Mchezo

Huo ndio ukweli, labda tusubiri miujiza
 
Watu hawachoki na ramli kwanini lakini,kabla ya mechi kunawatu walisema Orando ni moto Simba atapigwa tano,baa da ya mechi kuisha Simba kushinda wanaanza ramli mpya',,eti ngoja mechi ya marudiano Simba ataona cha moto".

Kumbukeni kuna timu zimekosa kabisa ushindi wakiwa nyumbani kwenye haya mashindano.
 
Msiba ushatokea tanzania kule south ni kwenda kuanua matanga tu, na wakirudi ndo wataanza kuhisi yale maumivu ya kuzidiwa alama 10 kwenye ligi wakati huo wakianza process mdogo mdogo za kumfukuza kocha wa madrid ambae kipimo chake cha mwisho ni derby ya kariakoo, kwa sasa wanamlia timing tu wamchinjie baharini!
 
Robo fainali nan utamchapa goli zote hizoooo kilamtu kajipanga sana angalia hata matokeo ya wenzetu
Kwani mlipochapwa na kaizer chiefs kule kwao 4 bila na mkarudi kwa mkapa mkashinda 3 bila yale magoli yalitokea wapi? Kilichowabeba kaizer chief ni ushindi wao mnene nyumbani vinginevyo walikuwa wanatupwa nje, ndo uelewe maana ya goli nyingi nyumbani vinginevyo utegemee muujiza tu kusonga mbele
 
hamchoki na stori zenu hizi ? Mmetoka kwa Mkapa mmeshahamia SA.
 
Natamani kuona vijana wanacheza siku ya marudiano, Banda, Muhilu, wakisaidiwa na Boko au Kagele au Mzamiru Bila kukosa Mugalu.
Wana Kasi na wanakaba. Pia, nataraji kuona mipira mirefu itakayowafanya vijana kukimbiza.
 
Uko sahihi,wale jamaa lile ndio soka lao..sasa mechi ya marudiano ule msako utakua tangia dakika ya kwanza..na jinsi wachezaji wa simba wanavyokabia kwa macho..tutegemee over 1.5 kipindi cha kwanza..

Ingawa mimi ni Simba damu damu Mkurungwa kiukweli umenifanya nicheke peke yangu kwavhiyo statement yako ya wachezaji wa simba wanakabia kwa macho! [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji28]
 
Usijal mkuu ishauri wako nimeupokea
Pale kusini tutaenda na mbinu tuloanza nayo kipindi cha kwanza zaid yan tutawapa nafasi wao wacheze then tutawapiga mashambuliz ya kushtukiza.
Mungu atakuwa nasi tutafunzu

Tuna eksipiriensi ya Kaizer Chifu lazima tutoboe. Simba anaenda kupiga game ya kufunguka na kuwkimbiza full time wataomba pooo
 
Kwa hiyo wao watakuwa wanafanya msako Simba wamesama?

Kama wakiamua hivyo hata Simba wana uwezo wa kufika golini kwao.

Ninawashangaa watanzania kuwa na viroho vidogo kama vya kumbi kumbi halafu unakuta jitu kuubwa! Mnawatisha wachezaji na kuwaambukiza viroho vya senene!
Uko sahihi,wale jamaa lile ndio soka lao..sasa mechi ya marudiano ule msako utakua tangia dakika ya kwanza..na jinsi wachezaji wa simba wanavyokabia kwa macho..tutegemee over 1.5 kipindi cha kwanza..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…