Kocha mkuu wa Argentina: Messi alikuwa hazuiliki

Kocha mkuu wa Argentina: Messi alikuwa hazuiliki

Nadhani wewe sio mwanampira, umekariri "old is gold" Messi hata asipofunga unafurahia anavyocheza

Huyo gaucho mbali na kupiga kanzu, kipi kingine cha maana!! Chenga hamfikii hata robo Messi na Maradona

So, acha kukariri
Hao awamfikii Gaucho ata robo
 
  • Thanks
Reactions: K11
Kilichobaki kwa Messi ni kupumzika tu maana amepata kila kitu alichopaswa. King 👑 of football of all the time Lionel Messi. Daima utaishi katika fikra zetu.
 
Hakika umesema hizi ni biashara. Kuna mwaka Adebayor alilalamika, alipewa taarifa yeye ndiye mshindi akasema Kwa bahati mbaya hawezi kufika kwenye tuzo sababu ana mechi muhimu. Kilichotokea wakamwambia kama haendi atachaguliwa mchezaji mwingine, na hakika ndicho kilichotokea. Tuzo za kijanja kijanja.
Kwamba yeye adebayo ndie alistahili mshindi wa ballon 😄 chumvi hizi!
 
kwa hyo wewe kusema hakuna wa kufananishwa na andunje ndo mwanampira siyo, kila anayekuwa na mawazo tofauti na wewe kuhusu andunje siyo mwanampira siyo, mkuu unataka ulimwengu wote uwaze kama wewe? hlo linawezekana kwel

Hujalazimishwa na mtu umkubali
 
Wapo walosema hastahili na wapo walosema anastahili.
Lewandowski alipata mafanikio ya klabu peke yake pamoja na huyo halland na katika mafanikio binafsi Messi alikua juu kitakwimu.
2023 alipata kwa ubora aloonesha kombe la Dunia 2022 na kwa kuwa mchezaji Bora kombe la Dunia na kuweka rekodi duniani kuwa Toka kombe la dunia kuanza yeye ndiye mchezaj pekee kubeba golden ball nyingi wengine wote wamebeba Moja moja.
We ungempa nani??
Kwa Mimi ballon zote 8 ni halali kwa alivyochukua.
Maana hao kina halland na lewandowski Wana mafanikio ya sehem moja hata ukiyalinganisha bado Messi anaonekana yupo juu.

Ndani ya mwaka tu ana world cup, copa amerika, finallisima 😄 aise huyu jamaa ni hatari
 
Aina ya uchezaji Messi anafanana na Maradona so Messi ni second version ya Maradona iliyo focus kwenye mpira wa kisasa wa numbers.
 
Ubora wa wachezaji wa kisasa kuonekana una athiriwa na numbers. Mchezaji akiwa na numbers nzuri ni rahisi sana kuimbwa mpira wa kizamani haukujikita sana huku.
 
Hakika umesema hizi ni biashara. Kuna mwaka Adebayor alilalamika, alipewa taarifa yeye ndiye mshindi akasema Kwa bahati mbaya hawezi kufika kwenye tuzo sababu ana mechi muhimu. Kilichotokea wakamwambia kama haendi atachaguliwa mchezaji mwingine, na hakika ndicho kilichotokea. Tuzo za kijanja kijanja.
Duh! Adebayor na ballon d'or!? Mwaka gani huo chief?

Hii uliipata kijiwe gani? Huyo muuza kahawa siku hiyo nadhani aliwamixia cocaone na kuberi humo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Messi huyu jamaa enzi akiwa kwenye peak pale Barca, alikuwa anaufanya mpira uonekane ni kitu rahisi mno...

Ilikuwa burudani sana kumtazama yeye na kina Iniesta wakitandaza kabumbu moja maridhawa sana...
 
Back
Top Bottom