Kocha Pep Guardiola kuondoka Man City mwishoni mwa msimu ujao

Kocha Pep Guardiola kuondoka Man City mwishoni mwa msimu ujao

Jambo la kwanza nahisi kuna tatizo kwenye ueleo wenu wa hilo neno overrated,

Pep ni kocha mzuri sana, mmoja ya makocha bora kwenye modern day game.

Ila hoja yangu ya kuwa overrated ni kutokana na kumwagiwa sifa zilizopindukia huku nyengine zikiwa za uwongo kabisa.
Taja sifa za uongo anazopewa Pep
 
Kubeba mara 4 mfululizo ni kweli kamzidi ila kiubora wa kiushindani hapana. Pep kabeba ubingwa EPL akiwa na washindani dhaifu sana kila msimu ndani ya misimu 6 aliyobeba ni timu moja tu ndio iliyokuwa ikikimbizana nae wakati wengine wote wakiwa hoi.

Chini ya Pep Man United wamemaliza nyuma yake mara 2, Liverpool mara 2 pamoja na Arsenal pia mara 2. Ndani ya hii misimu timu zingine zote zilikuwa zinakuwa nyepesi sana. Kipindi cha Ferguson top 4 zote zilikuwa za moto haikuwa rahisi kuvuka points 90 kirahisi rahisi haikuwa kazi nyepesi kuchukua points 6 kwa wakubwa wenzio.
Liverpool amewahi kuchukua points 6 kwa big four na ubingwa akachukua Man U miaka hiyooo.

Huo ubora wa ligi ya uingereza na timu zake ni wa midomoni tu check hata UEFA miaka unayosema walikuwa bora walichukua mara 1 tu mwaka 2009
 
Matusi ya nini mkuu?

Coach akipigwa kwa game inamaanisha ni kibonde? Mpira ni mchezo wa matokeo matatu na lolote linawezekana ila sio kigezo cha kutumia game 1, 2 ama 3 kuconclude kuhusu ubora wa coach Fulani.

Liverpool alitoka kuwin league Akala 7 mbele ya Astonvilla kwamba Clop alikuwa kibonde?

Lewandowsk aliwanyoosha Madrid 4 kwamba walikuwa vibonde ama coach alikuwa kibonde?

Last season Madrid alikufa 4 kwa City kwamba coach wao ni kibonde?

Unaangalia mpira wa wapi mkuu?


Ndo Leo najua kwamba coach akipoteza mchezo kwa goal nyingi ni kibonde.
Huyo hajui football
 
PUMBA TUPU. yani Laporta aachwe kusikilizwa Laporta ambaye ndio Rais wa Club asikilzwe Cruyff? Be serious dude
Tatizo unaamini uendeshaji wa club kwa wenzetu huko na kama uliopo kwa hapa kwenu Bongo ambapo mtu akiwa na hela tu na cheo basi yeye ndio anakuwa mwenye kauli ya mwisho hata kama hajui mpira na ni mwanasiasa tu....

Huko kwa wenzetu mambo hayako hivyo wewe, huko cheo cha uraisi ni cheo tu cha uongozi tena wa kisiasa tu basi, na wala raisi hawezi kuwa mtu mwenye last say hata kidogo...

Huko mtu aliyefanya makubwa kwanzia ndani mpaka nje ya uwanja kwenye timu ndio huwa anasikilizwa sana, ukienda pale Bayern Munich kuna mtu ambaye kwa sasa ni marehemu anaitwa Franz Beckenbeur, ukienda pale Milan kuna mtu anatwa Paolo Maldin, ukija Barcelona ndio ulikuwa unakutana na Johan Cryuff... hawa ni watu ambao mawazo huwa yana heshimika sana kwenye vilabu husika

Unaongelea raisi?? Raisi si anaweza akawa ni mdau tu wa club karuka vihunzi vyote atimae akawa raisi lakini hajawahi hata kucheza mpira wala kuelewa utamaduni wa club husika...

Ujiulizi ni kwani mashabiki wa United huwa wanamheshimu san Ferguson na kukubaliana na mawazo yake karibu kwenye kila jambo na wanaizomea ile grazer family ambao ndio wamiliki wa club???
 
Kubeba mara 4 mfululizo ni kweli kamzidi ila kiubora wa kiushindani hapana. Pep kabeba ubingwa EPL akiwa na washindani dhaifu sana kila msimu ndani ya misimu 6 aliyobeba ni timu moja tu ndio iliyokuwa ikikimbizana nae wakati wengine wote wakiwa hoi.

Chini ya Pep Man United wamemaliza nyuma yake mara 2, Liverpool mara 2 pamoja na Arsenal pia mara 2. Ndani ya hii misimu timu zingine zote zilikuwa zinakuwa nyepesi sana. Kipindi cha Ferguson top 4 zote zilikuwa za moto haikuwa rahisi kuvuka points 90 kirahisi rahisi haikuwa kazi nyepesi kuchukua points 6 kwa wakubwa wenzio.
Ferguson katika mara 11 zote alizochukua ubingwa wa EPL hakuwahi hata siku moja kufikisha points 90 na wala hata kushida mechi 30 msimu aliowahi kishinda mechi nyingi alishinda 25 ambapo alikusanya points 84 na tena kipindi hicho timu shindani zilikuwa ni New Castle,Liverpool,Arsenal,Leeds United na Man u yenyewe na pia kipindi hicho EPL ilikuw hata sio ligi bora ulaya.

Leo pep anakusanya mpaka points 98 mbele ya timu kama Liverpool ya Jurgen klop,Chelsea ya Tuchel,United ya Olegunner,Arsenal ya Unai Emry, Spurs ya Pochetino hizi zote ni timu zinazotumia pesa za nyingi kwenye usajili..... bila kusahau timu ving'ang'anizi kama New castle,Brighton,Aston Villa,Brentford na pia zaidi ya hapo EPL ikiwa ndio ligi bora duniani

Halafu unasema kuwa Pep anatusmbua kwa sababu sasa hivi hakuna ushindani?? Aloo huwezi kuwa serious wewe... mimi sio shabiki wa city ila Pep alichokifanya anastahili heshima yake.

Binafsi naamini hata Ferguson angekuwa bado yupo pale EPL zama hizi angeishia kuwa permanent runner-up tu kama akina Jurgen na Arteta.

Pep Epl ameifanyia najisi kiasi kwamba sasa hivi zimezuka nadharia kibao ikiwemo hii yako ya kusema eti sasa hivi ushindani hakuna.
 
Mkuu umetisha sana. Umetoa maelezo sahihi kwa faida ya wengi.

Watu wengi mpira hawaufuatilii ama hawaujui vizuri ila wanaendeshwa na stori za vijiweni mwisho wa siku ukiwaambia watoe hoja hawana wanaishia kutukana tu.

Wengi watajifunza, big up 🔥🔥🔥
Wengi wa haters wa Pep kama huyu mshikaji hapa wameanza kumfuatilia kwa ukaribu Pep akiwa Man City na ndio maana hata hoja zao ni nyepesi sana na hazina uhakika hata kidogo.....

Mbaya zaidi hata wachambuzi wetu wa bongo nao wana mawazo haya haya kama ya huyu mshikaji
 
Wengi wa haters wa Pep kama huyu mshikaji hapa wameanza kumfuatilia kwa ukaribu Pep akiwa Man City na ndio maana hata hoja zao ni nyepesi sana na hazina uhakika hata kidogo.....

Mbaya zaidi hata wachambuzi wetu wa bongo nao wana mawazo haya haya kama ya huyu mshikaji
Asipokuelewa kwa maelezo ya hapo juu basi hakuna kitu atakuja kukielewa kwenye maisha yake. Umetoa shule kubwa mno.
 
Tatizo unaamini uendeshaji wa club kwa wenzetu huko na kama uliopo kwa hapa kwenu Bongo ambapo mtu akiwa na hela tu na cheo basi yeye ndio anakuwa mwenye kauli ya mwisho hata kama hajui mpira na ni mwanasiasa tu....

Huko kwa wenzetu mambo hayako hivyo wewe, huko cheo cha uraisi ni cheo tu cha uongozi tena wa kisiasa tu basi, na wala raisi hawezi kuwa mtu mwenye last say hata kidogo...

Huko mtu aliyefanya makubwa kwanzia ndani mpaka nje ya uwanja kwenye timu ndio huwa anasikilizwa sana, ukienda pale Bayern Munich kuna mtu ambaye kwa sasa ni marehemu anaitwa Franz Beckenbeur, ukienda pale Milan kuna mtu anatwa Paolo Maldin, ukija Barcelona ndio ulikuwa unakutana na Johan Cryuff... hawa ni watu ambao mawazo huwa yana heshimika sana kwenye vilabu husika

Unaongelea raisi?? Raisi si anaweza akawa ni mdau tu wa club karuka vihunzi vyote atimae akawa raisi lakini hajawahi hata kucheza mpira wala kuelewa utamaduni wa club husika...

Ujiulizi ni kwani mashabiki wa United huwa wanamheshimu san Ferguson na kukubaliana na mawazo yake karibu kwenye kila jambo na wanaizomea ile grazer family ambao ndio wamiliki wa club???

acheni kukariri, Maldini alikuwa director ndani ya milan kwa hiyo influence kwenye timu alikuwa anayo. Usilinganishe kabisa na Cryff na Frans, wao walikuwa ni maraisi wa heshima tu. Laporta kaingia madarakani kwa uchaguzi, na yeye ndio aliechagua timu yake ya uongozi katika kila postion. Bongo ndio hata mtu ambaye hayumo kwenye nafasi ya uongozi anawezakusikilizwa anachosema ila sio Ulaya mkuu.
 
Back
Top Bottom