Kocha wa Simba SC, Pablo Franco ni Kocha mzuri ila anahitaji wachezaji

Kocha wa Simba SC, Pablo Franco ni Kocha mzuri ila anahitaji wachezaji

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Kocha wa Simba SC, Pablo Franco Martin ni mwalimu mzuri sana, ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake ili ufanisi wa kazi yake uonekane zaidi Tanzania na Nje.

Kwenye mchezo dhidi ya Orlando Pirates, Simba SC walicheza Football Pass, mbinu ambayo inawafanya wasikae na mpira muda mrefu, huku wakiwa na nidhamu ya kujilinda zaidi.

Kocha Pablo aliingia kwa kuzuia huku akiwa ametengeneza mistari mitatu [5-3-2] wakati ambao Simba hawana mpira Sakho na Mugalu walibaki kwenye mstari kusaidia timu kujilinda, kwa mbinu hii Kocha Pablo alifanikiwa mno ila tatizo likawa kwa mabeki kutokuwa bora kwenye kuanzisha mashambulizi vizuri kutoka chini.

Kwenye mchezo wa Derby ya Kariakoo Kocha Pablo Franco alikuja na mfumo wa [4-2-3-1] kuonyesha kuwa alitaka matokeo ya ushindi lakini Simba hawakuwa bora kwenye idara yake ya ushambuliaji, mipango yote iliishia kushindwa kupiga pasi mpenyezo nyuma ya mabeki wa Yanga.

Kocha Pablo amejipambanua kuwa ni mwalimu mzuri sana ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake kizidi kuwa tishio na imara ili kuweza kutoa upinzani haswa na kuweka sawia mipango yake uwanjani na kufikia lengo la timu.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
 
Kocha wa Simba SC, Pablo Franco Martin ni mwalimu mzuri sana, ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake ili ufanisi wa kazi yake uonekane zaidi Tanzania na Nje.

Kwenye mchezo dhidi ya Orlando Pirates, Simba SC walicheza Football Pass, mbinu ambayo inawafanya wasikae na mpira muda mrefu, huku wakiwa na nidhamu ya kujilinda zaidi.

Kocha Pablo aliingia kwa kuzuia huku akiwa ametengeneza mistari mitatu [5-3-2] wakati ambao Simba hawana mpira Sakho na Mugalu walibaki kwenye mstari kusaidia timu kujilinda, kwa mbinu hii Kocha Pablo alifanikiwa mno ila tatizo likawa kwa mabeki kutokuwa bora kwenye kuanzisha mashambulizi vizuri kutoka chini.

Kwenye mchezo wa Derby ya Kariakoo Kocha Pablo Franco alikuja na mfumo wa [4-2-3-1] kuonyesha kuwa alitaka matokeo ya ushindi lakini Simba hawakuwa bora kwenye idara yake ya ushambuliaji, mipango yote iliishia kushindwa kupiga pasi mpenyezo nyuma ya mabeki wa Yanga.

Kocha Pablo amejipambanua kuwa ni mwalimu mzuri sana ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake kizidi kuwa tishio na imara ili kuweza kutoa upinzani haswa na kuweka sawia mipango yake uwanjani na kufikia lengo la timu.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
Ubaya usajili wa wachezaji hafanyi yy vitengo vya watu hivyo, so kocha awe mpole atakaye letewa ampokee.
 
Kwelii Kabisa,ila ananikera kukosea sub,mfano Leo alishaona Mugalu anaruka2 tu, angemwingiza Boko naye ajaribu hata Dk 10
Kumuingiza bocco acheze dakika nyingi kwenye mechi ya leo bocco ambaye hajacheza mechi zaidi ya 5 ilikuwa ni wrong move

Hizi zilikuwa ni lawama ambazo asingeweza kuziepuka kocha pablo.

Yani hiyo dhana ya kusema ajaribu ilikuwa sio hatua nzuri kabisa hususani ukiangalia namna ambavyo Yanga walikuwa wanalifikia lango la simba kirahisi na wao walikuwa wananyimwa utulivu na mabeki bora ambao simba wanao

Bocco kiwango chake cha mwisho kucheza ambacho wote tulikifurahia nakumbuka ni mechi fulani hivi miezi kadhaa imepita ambayo alikosa header moja ikaenda offtarget halafu akaja kufunga (sijui ndio ile tuwapige wale ruvu)

Lakini baada ya hapo hatujaona kiwango cha kuridhisha kwa john bocco huo ndio ukweli, plus hajacheza mechi nyingi huwenda alikuwa na majeraha au hakuwa katika form work ya kimchezo nk
 
Kocha wa Simba SC, Pablo Franco Martin ni mwalimu mzuri sana, ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake ili ufanisi wa kazi yake uonekane zaidi Tanzania na Nje.

Kwenye mchezo dhidi ya Orlando Pirates, Simba SC walicheza Football Pass, mbinu ambayo inawafanya wasikae na mpira muda mrefu, huku wakiwa na nidhamu ya kujilinda zaidi.

Kocha Pablo aliingia kwa kuzuia huku akiwa ametengeneza mistari mitatu [5-3-2] wakati ambao Simba hawana mpira Sakho na Mugalu walibaki kwenye mstari kusaidia timu kujilinda, kwa mbinu hii Kocha Pablo alifanikiwa mno ila tatizo likawa kwa mabeki kutokuwa bora kwenye kuanzisha mashambulizi vizuri kutoka chini.

Kwenye mchezo wa Derby ya Kariakoo Kocha Pablo Franco alikuja na mfumo wa [4-2-3-1] kuonyesha kuwa alitaka matokeo ya ushindi lakini Simba hawakuwa bora kwenye idara yake ya ushambuliaji, mipango yote iliishia kushindwa kupiga pasi mpenyezo nyuma ya mabeki wa Yanga.

Kocha Pablo amejipambanua kuwa ni mwalimu mzuri sana ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake kizidi kuwa tishio na imara ili kuweza kutoa upinzani haswa na kuweka sawia mipango yake uwanjani na kufikia lengo la timu.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
Nakubaliana na wewe kwa 80% Ila na yeye anashida kwenye selection ya wachezaji unakuta anakuja na formation nzuri Ila anajaribu selection.
Mfano mechi ya Orlando nafasi aliyokuwa akicheza Israel mwenda kwanini hakuwa Gadiel? Maana tunajua Shabalala anaudhaifu kidogo kwenye kukaba?
Na hata kwenda SA bila Bocco ilikuwa ni risk pia.

Pia Leo akaja na formation nzuri Ila akamkosa Peter Banda ama Jimmyson mwanuke hata Benchi
 
Nakubaliana na wewe kwa 80% Ila na yeye anashida kwenye selection ya wachezaji unakuta anakuja na formation nzuri Ila anajaribu selection.
Mfano mechi ya Orlando nafasi aliyokuwa akicheza Israel mwenda kwanini hakuwa Gadiel? Maana tunajua Shabalala anaudhaifu kidogo kwenye kukaba?
Na hata kwenda SA bila Bocco ilikuwa ni risk pia.

Pia Leo akaja na formation nzuri Ila akamkosa Peter Banda ama Jimmyson mwanuke hata Benchi
Asante mkuu, Ila hapo kwa Israel alicheza ile game kwasababu Kapombe alipandishwa juu kama Kiungo Kivuli.

Kwa ambavyo Hussein amejiwekea ni wazi kuwa ubora wake ni mkubwa zaidi kuliko mapungufu yake, kwahivyo hata Kocha asingeeleweka kumuacha Hussein nje halafu acheze Gadiel.
 
Asante mkuu, Ila hapo kwa Israel alicheza ile game kwasababu Kapombe alipandishwa juu kama Kiungo Kivuli.

Kwa ambavyo Hussein amejiwekea ni wazi kuwa ubora wake ni mkubwa zaidi kuliko mapungufu yake, kwahivyo hata Kocha asingeeleweka kumuacha Hussein nje halafu acheze Gadiel.
Nilichomaanisha Gadiel angecheza Kama wingback ya kushoto then Zimbwe acheze juu ili kuupa huo upande Nguvu maana upande wa kulia Kapombe anapata back up ya Wawa
 
Kumuingiza bocco acheze dakika nyingi kwenye mechi ya leo bocco ambaye hajacheza mechi zaidi ya 5 ilikuwa ni wrong move

Hizi zilikuwa ni lawama ambazo asingeweza kuziepuka kocha pablo.

Yani hiyo dhana ya kusema ajaribu ilikuwa sio hatua nzuri kabisa hususani ukiangalia namna ambavyo Yanga walikuwa wanalifikia lango la simba kirahisi na wao walikuwa wananyimwa utulivu na mabeki bora ambao simba wanao

Bocco kiwango chake cha mwisho kucheza ambacho wote tulikifurahia nakumbuka ni mechi fulani hivi miezi kadhaa imepita ambayo alikosa header moja ikaenda offtarget halafu akaja kufunga (sijui ndio ile tuwapige wale ruvu)

Lakini baada ya hapo hatujaona kiwango cha kuridhisha kwa john bocco huo ndio ukweli, plus hajacheza mechi nyingi huwenda alikuwa na majeraha au hakuwa katika form work ya kimchezo nk
Naunga mkono hoja..Labda kidogo angekuwepo Kagere.
 
Mkuu Scars na Proved hebu kujeni hapa kwanza, je kuna la zaidi katika hili?
Kuna siku nilikuwa nafatilia interviews za matukio baada ya mechi.

Kuna mwana yanga mmoja alitoa ushauri ambao binafsi nakubaliana naye kwa % kubwa.

Alisema tanzania tunaweza tukajijenga vizuri kisoka na tukafanya mambo makubwa ya kuwashangaza mataifa mengine endapo tutakubali kuwa wachoyo

Kwamba leo tukicheza na timu kubwa pinzani, wachezaji wetu wataoonesha ubora zaidi na kuwafanya timu hizo pinzani zisifunge basi management ya timu hizo zitataka kuwanunua hao.

Tatizo linapokuja ni baada ya sisi kuwauza hao wachezaji wazuri na kubakisha hawa wenye average ya kati.

Sasa badala ya hizo Pesa tulizopata baada ya kuuza wachezaji wetu kwa Pesa kubwa tuzitumie kununua wachezaji wengine wakubwa wa aina hiyo au zaidi ya hapo ikiwezekana hata katika hiyo Pesa tuongeze na nyingine ili kupata mchezaji mwenye uwezo wa juu kufikia malengo, tunaanza kuhangaika na sajili za laki mbili mbili eti tuwakuze.

Hapa katikati tutatumia muda mwingi mpaka kunijenga wakati wenzetu wahafika mbaliz na kukishajijenga watakuja tena na madau yao kununua wachezaji ambao wao wanawaona ni tishio kwao.

Kwanini tusiwe wachoyo tusikubali kuwauza, au tuwauze kwa bei kubwa afu tununue wa aina hiyo au zaidi ya hao?

Na ndio maana tunaishia kufukuza makocha, lakini sio kweli kuwa kila matokeo mabaya yanayopatikana basi Sababu ni kocha.

Simba inabidi ifahamu kuwa saizi ni muda wa kufanya makubwa zaidi ya kuishia robo, Wafanye sajili kubwa tano za maana.

Mugalu asepe, bocco tunamheshimu lakini hatuna namna, kagere plus na umri hata yeye mwenyewe analijua, wawa hatufai ana vi cross vya hovyo sana, sakho akishindwa kujirekebisha na tabia yake ya kucheza na jukwaa afungashiwa vilago...
 
Back
Top Bottom