Kocha wa Simba SC, Pablo Franco ni Kocha mzuri ila anahitaji wachezaji

Kocha wa Simba SC, Pablo Franco ni Kocha mzuri ila anahitaji wachezaji

Kuna siku nilikuwa nafatilia interviews za matukio baada ya mechi.

Kuna mwana ya ga mmoja alitoa ushauri ambao binafsi nakubaliana naye kwa % kubwa.

Alisema tanzania tunaweza tukajijenga vizuri kisoka na tukafanya mambo makubwa ya kuwashangaza mataifa mengine endapo tutakubali kuwa wachoyo

Kwamba leo tukicheza na timu kubwa pinzani, wachezaji wetu wataoonesha ublra zaidi na kuwafanya timu hizo pinzani zisifunge basi management ya timu hizo zitataka kuwanunua hao.

Tatizo linapokuja ni baada ya sisi kuwauza hao wachezaji wazuri na kubakisha hawa wenye average ya kati.

Sasa badala ya hizo Pesa tulizopata baada ya kuuza wachezaji wetu kwa Pesa kubwa tuzitumie kununua wachezaji wengine wakubwa wa aina hoyo au zaidi ya hapo ikiwezekana hata katika hiyo Pesa tuongeze na nyingine ili kupata mchezaji mwenye uwezo wa juu kufikia malengo, tunaanza kuhangaika na sajili za laki mbili eti tuwakuze

Na ndio maana tunaishia kufukuza makocha, lakini sio kweli kuwa kila matokeo mabaya yanayopatikana basi Sababu ni kocha.

Simba inabidi ifahamu kuwa saizi ni muda wa kufanya makubwa zaidi ya kuishia robo, Wafanye sajili kubwa tano za maana.

Mugalu asepe, bocco tunamheshimu lakini hatuna namna, kagere plus na umri hata yeye mwenyewe analijua, wawa hatufai ana vi cross vya hovyo sana, sakho akishindwa kujirekebisha na tabia yake ya kucheza na jukwaa afungashiwa vilago...
Kwa sakho nakubali, akizidisha masifa ya nje ya uwanja asepeshwe.
Na bwalya aondoke tyuuh.
 
Nakubaliana na wewe kwa 80% Ila na yeye anashida kwenye selection ya wachezaji unakuta anakuja na formation nzuri Ila anajaribu selection.
Mfano mechi ya Orlando nafasi aliyokuwa akicheza Israel mwenda kwanini hakuwa Gadiel? Maana tunajua Shabalala anaudhaifu kidogo kwenye kukaba?
Na hata kwenda SA bila Bocco ilikuwa ni risk pia.

Pia Leo akaja na formation nzuri Ila akamkosa Peter Banda ama Jimmyson mwanuke hata Benchi
banda anamaajabu gani?
 
Anaifanya kazi ionekane rahisi sana hata kwetu tusioijua.

Wanafanya sub za kipimbi sana.Anajiangalia yeye na timu yake badala ya kuangalia mpinzani wake pia.

Leo yanga walishindwa kutawala kwa sababu akili zao zilimakinika kwa Morrison,Chama na Sakho.
Mara walipotolewa kidogo wakaanza kuwa aggressive.
Tushukuru Mungu tu huwa wanakata upepo kipindi cha pili ndio maana hata mkaona Simba inafanya angalau shot on target mbili.
Nina uhakika Morrison angekuwepo kulikuwa na goli achana na hizo shot on target.
Mimi simuelewi huyu jamaa
Kocha wa Simba SC, Pablo Franco Martin ni mwalimu mzuri sana, ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake ili ufanisi wa kazi yake uonekane zaidi Tanzania na Nje.

Kwenye mchezo dhidi ya Orlando Pirates, Simba SC walicheza Football Pass, mbinu ambayo inawafanya wasikae na mpira muda mrefu, huku wakiwa na nidhamu ya kujilinda zaidi.

Kocha Pablo aliingia kwa kuzuia huku akiwa ametengeneza mistari mitatu [5-3-2] wakati ambao Simba hawana mpira Sakho na Mugalu walibaki kwenye mstari kusaidia timu kujilinda, kwa mbinu hii Kocha Pablo alifanikiwa mno ila tatizo likawa kwa mabeki kutokuwa bora kwenye kuanzisha mashambulizi vizuri kutoka chini.

Kwenye mchezo wa Derby ya Kariakoo Kocha Pablo Franco alikuja na mfumo wa [4-2-3-1] kuonyesha kuwa alitaka matokeo ya ushindi lakini Simba hawakuwa bora kwenye idara yake ya ushambuliaji, mipango yote iliishia kushindwa kupiga pasi mpenyezo nyuma ya mabeki wa Yanga.

Kocha Pablo amejipambanua kuwa ni mwalimu mzuri sana ila anahitaji wachezaji ili kuweza kuongeza nguvu kwenye kikosi chake kizidi kuwa tishio na imara ili kuweza kutoa upinzani haswa na kuweka sawia mipango yake uwanjani na kufikia lengo la timu.

Kulitaka Mwana Kulipewa Mwana
 
Kuna siku nilikuwa nafatilia interviews za matukio baada ya mechi.

Kuna mwana yanga mmoja alitoa ushauri ambao binafsi nakubaliana naye kwa % kubwa.

Alisema tanzania tunaweza tukajijenga vizuri kisoka na tukafanya mambo makubwa ya kuwashangaza mataifa mengine endapo tutakubali kuwa wachoyo

Kwamba leo tukicheza na timu kubwa pinzani, wachezaji wetu wataoonesha ubora zaidi na kuwafanya timu hizo pinzani zisifunge basi management ya timu hizo zitataka kuwanunua hao.

Tatizo linapokuja ni baada ya sisi kuwauza hao wachezaji wazuri na kubakisha hawa wenye average ya kati.

Sasa badala ya hizo Pesa tulizopata baada ya kuuza wachezaji wetu kwa Pesa kubwa tuzitumie kununua wachezaji wengine wakubwa wa aina hiyo au zaidi ya hapo ikiwezekana hata katika hiyo Pesa tuongeze na nyingine ili kupata mchezaji mwenye uwezo wa juu kufikia malengo, tunaanza kuhangaika na sajili za laki mbili mbili eti tuwakuze.

Hapa katikati tutatumia muda mwingi mpaka kunijenga wakati wenzetu wahafika mbaliz na kukishajijenga watakuja tena na madau yao kununua wachezaji ambao wao wanawaona ni tishio kwao.

Kwanini tusiwe wachoyo tusikubali kuwauza, au tuwauze kwa bei kubwa afu tununue wa aina hiyo au zaidi ya hao?

Na ndio maana tunaishia kufukuza makocha, lakini sio kweli kuwa kila matokeo mabaya yanayopatikana basi Sababu ni kocha.

Simba inabidi ifahamu kuwa saizi ni muda wa kufanya makubwa zaidi ya kuishia robo, Wafanye sajili kubwa tano za maana.

Mugalu asepe, bocco tunamheshimu lakini hatuna namna, kagere plus na umri hata yeye mwenyewe analijua, wawa hatufai ana vi cross vya hovyo sana, sakho akishindwa kujirekebisha na tabia yake ya kucheza na jukwaa afungashiwa vilago...
Huyu wanayanga nimemuelewa..!

Hata hivyo wapo hata Wanasimba nao walitoa maoni yao kama hayo.

Mmoja alisema kuwa iwapo kama unamuuza Luis Miquissone inatakiwa kumleta replacement wa maana ili kulinda ubora uliopo au uzidi ubora na si kupungua.
 
Huyu wanayanga nimemuelewa..!

Hata hivyo wapo hata Wanasimba nao walitoa maoni yao kama hayo.

Mmoja alisema kuwa iwapo kama unamuuza Luis Miquissone inatakiwa kumleta replacement wa maana ili kulinda ubora ulipo au uzidi ubora na si kupungua.
Ndio inavyotakiwa usifanya club ya soka kuwa day care

Uwe unaleta wachezaji kwa lengo la kuwakuza afu wakikua uwauze what a shit?
 
Yawezekana mjadala ukawa haunihusu sababu mimi ni Yanga, lakini kiushabiki wa mpira tupo wote.

Honestly, Bwallya anawachelewesha tu. Hamna kitu anaweza ku-offer tena. The same kwa Mugalu na Bocco, tayari shughuli zishaisha pale.

Sakho naye muda mwingine anakuwa machachari sana kuliko kuwa hatari sana. Ila muda na nafasi ya kubadilika bado anayo.

Morrison ni mchezaji mzuri lakini uwezo wake wa kuhimili dakika 90 ni mdogo mno especially kwenye tough games. Anakuwa hatari ndani ya dakika chache then anageuka kuwa mzigo maana hakabi ... huwa namwelewa sana kocha anapomweka dakika za 70 au 60 huko.

Zaidi, Pablo ana mengi pia ya kujisahihisha. Kuna muda anapanga kikosi kama mtu asiyehitaji ushindi, tumeona mara kadhaa katika baadhi ya mechi zilizoishia draw au kufungwa.
 
Yawezekana mjadala ukawa haunihusu sababu mimi ni Yanga, lakini kiushabiki wa mpira tupo wote.

Honestly, Bwallya anawachelewesha tu. Hamna kitu anaweza ku-offer tena. The same kwa Mugalu na Bocco, tayari shughuli zishaisha pale.

Sakho naye muda mwingine anakuwa machachari sana kuliko kuwa hatari sana. Ila muda na nafasi ya kubadilika bado anayo.

Morrison ni mchezaji mzuri lakini uwezo wake wa kuhimili dakika 90 ni mdogo mno especially kwenye tough games. Anakuwa hatari ndani ya dakika chache then anageuka kuwa mzigo maana hakabi ... huwa namwelewa sana kocha anapomweka dakika za 70 au 60 huko.

Zaidi, Pablo ana mengi pia ya kujisahihisha. Kuna muda anapanga kikosi kama mtu asiyehitaji ushindi, tumeona mara kadhaa katika baadhi ya mechi zilizoishia draw au kufungwa.
Mkuu yaelekea Utopolo wako ni WA kulazimishwa...au lilikuwa sharti la kupewa Mke uowe!
 
Kocha hana first 11 mpaka leo na anachelewa sana kufanya sub. Mugalu ni kama vile kamroga. Hana tija yoyote uwanjani na bado anacheza dkk karibia zote.
Kwa mtazamo wako mpira wa Derby ya Kariakoo angecheza nani badala ya Mugalu..?

Kagere hakuwepo hata benchi..Na Bocco hakuwa na match fitness kwa kuanza, kwakuwa alikuwa majeruhi muda..!
 
Simba inahitaji marekebisho makubwa snaa kwenye kikosi chake .striker mmoja wa kimataifa na mmoja wa ndani dizain ya mpole.

Beki wawil wa kimataifa.
Winga mbili za kimataifa .
Hapo kazi Kwisha.

Ila km kawaida viongozi wakileta habari za kuoneana aibu hakika tutakua tunaishia robo tu kila msimu.

Mugalu na kagere hao waachwe Mara moja.

Bocco aachwe Mara moja nafas yake achukue mpole .

Wawa ,lwanga waachwe kupata beki mbili za uhakika.

Bwalya aachwe kupata winga matata msumbufu Zaid ya Morrison.

Sakho aambiwe ukwel kuwa sifa zimemzid so ajiangalie maana kadri siku zinavyokwenda anazid kuharibu ila Ana nafas ya kubadirika km hatabadirika benchi imhusu Sana ili ajue ni wa kawaida Sana.

Banda aendelee kuwepo maana namwona mbelen atakua msaada kwa Simba.

Morrison aendelee kubaki.

Kwa upande wa wazawa toa Gadiel,mhilu,Nyoni,mzamiru leteni wapya.

Km watafanya hivyo Nina iman kocha atafanya vzr maana Ana mbinu Sana na ameanza kulielewa soka la Africa.
 
Kagere sijui kwamba ni formation ndio inayomfanya ashindwe kuwa na madhara sana au namna gani
Kagere bado namwona ni finisha mzuri. Tatizo naliona kwa viungo wachezeshaji na wapembeni ambao hawatengenezi nafasi kwa MK14.

Waangalie watani zetu yanga, katika mechi ya Jana, viungo wao walikuwa Bora katika kutengeneza mashambulizi. Moloko., Djuma kwa pembeni, Feisali Kama kiungo mshambuliaji wakishirkiana na Ntibazonkiza na wote hao ukiangalia move zao zinaekekea kwa Mayele ili aweze kufunga. Kama si ubora wa mabeki (INONGA NA BABU ONYANGO)wetu Jana, Mayele angeshafanya yake.

Kwa upande wetu Simba hatuna watu wa kutengeneza nafasi kwa Kagere. Watu mfano wa Mikson hawapo.

Tunahitaji maboresho Sana katika viungo na forward.
Kagere wamfikirie kubaki Ila Bocco, Mugalu waondoke, Wawa aondoke, Mzamiru aondoke, Gadiel aondoke, Mhilu aondoke, Sakho ajiangalie, Rally aondoke.

Sent from my TECNO KE5 using JamiiForums mobile app
 
Anaifanya kazi ionekane rahisi sana hata kwetu tusioijua.

Wanafanya sub za kipimbi sana.Anajiangalia yeye na timu yake badala ya kuangalia mpinzani wake pia.

Leo yanga walishindwa kutawala kwa sababu akili zao zilimakinika kwa Morrison,Chama na Sakho.
Mara walipotolewa kidogo wakaanza kuwa aggressive.
Tushukuru Mungu tu huwa wanakata upepo kipindi cha pili ndio maana hata mkaona Simba inafanya angalau shot on target mbili.
Nina uhakika Morrison angekuwepo kulikuwa na goli achana na hizo shot on target.
Mimi simuelewi huyu jamaa
Morrison asingemaliza hii game salama.

Kumbuka alishakuwa na Yellow na alikuwa anaendelea kukamiwa na wapinzani huku wakimtoa mchezoni

Kocha akaona yasije yakajitokeza kama ya Mugalu dhidi ya Orlando Pirates.
 
Simba inahitaji marekebisho makubwa snaa kwenye kikosi chake .striker mmoja wa kimataifa na mmoja wa ndani dizain ya mpole.

Beki wawil wa kimataifa.
Winga mbili za kimataifa .
Hapo kazi Kwisha.

Ila km kawaida viongozi wakileta habari za kuoneana aibu hakika tutakua tunaishia robo tu kila msimu.

Mugalu na kagere hao waachwe Mara moja.

Bocco aachwe Mara moja nafas yake achukue mpole .

Wawa ,lwanga waachwe kupata beki mbili za uhakika.

Bwalya aachwe kupata winga matata msumbufu Zaid ya Morrison.

Sakho aambiwe ukwel kuwa sifa zimemzid so ajiangalie maana kadri siku zinavyokwenda anazid kuharibu ila Ana nafas ya kubadirika km hatabadirika benchi imhusu Sana ili ajue ni wa kawaida Sana.

Banda aendelee kuwepo maana namwona mbelen atakua msaada kwa Simba.

Morrison aendelee kubaki.

Kwa upande wa wazawa toa Gadiel,mhilu,Nyoni,mzamiru leteni wapya.

Km watafanya hivyo Nina iman kocha atafanya vzr maana Ana mbinu Sana na ameanza kulielewa soka la Africa.
Yes, huu ndo uchambuzi tunataka kutoka kwenu..!

Kwenye maboresho ya timu unaweza kufanya kwa pande zote yaani Kocha na Wachezaji, lakini kwa sasa ni wachezaji tu

Asante mkuu..!
 
Back
Top Bottom