Kocha wa Simba SC, Pablo Franco ni Kocha mzuri ila anahitaji wachezaji

Kocha wa Simba SC, Pablo Franco ni Kocha mzuri ila anahitaji wachezaji

Pablo ni kocha mzuri. Tatizo la Tanzania mara nyingi hatuangalii tulipojikwaa ila tunakimbilia kuangalia tulipoangukia. Pablo kaja Simba kakuta Chama na Luis wameuzwa halafu Mugalu, Boko na Kagere viwango vimeporomoka na huku wana majeraha ya mara kwa mara. Kwa maana hiyo Pablo kaja kakutana na changamoto ya nguvu kwenye safu yake ya ushambuliaji. Na hili la kuporomoka viwango kwa washambuliaji wa Simba lilikuwa dhahiri kabla msimu uliopita kwisha lakini viongozi hawakuliona kwa sababu mafowadi walikuwa wanafunga lakini hakuna mtu alikuwa anajiuliza japo wanafunga magoli lakini katika kila mchezo walikuwa wanapoteza nafasi hata zaidi ya kumi. Pia Chama na Luis walikuwa wanawafichia mafowadi wa Simba madhaifu yao kwa muda mrefu kwani walikuwa wanafunga mara kwa mara pale washambuliaji wa Simba wanaposhindwa kufunga.

Viongozi wa Simba wakatae wakubali kuwa walijikwaa pale walipowauza Chama na Luis halafu wakawaleta Sakho, Duncan Nyoni na Peter Banda kuziba nafasi zao halafu wakategemea wapate ubora ule ule. Pesa waliyopata kwa Luis ndio iliwapa tamaa ya kusajili wachezaji vijana ili wapige pesa ndefu huko mbele ya safari wakasahau kuwa kuna swala la matokeo uwanjani na hilo linaamuliwa na wachezaji wenye uzoefu tu na si vinginevyo. Sakho na Banda kuipa Simba makombe kama wachezaji tegemezi sio chini ya misimu miwili ijayo

Nini kifanyike Simba? Ni maamuzi magumu tu yanahitajika bila kuangalia wachezaji usoni. Kwanza kabisa wapige chini safu yote ya ushambuliaji baada tu ya ligi kwisha.

Na kama kweli wana nia ya kufika nusu fainali au fainali kabisa Afria basi wavunje benki waachane na baadhi ya wachezaji na wasajili wengine wapya. Kwangu mimi nafikiri ni wakati wa Simba kusajili wachezaji ambao pamoja na vipaji vyao lakini wawe wapambanaji kweli kweli uwanjani kwa dakika zote tisini na si vinginevyo. Kuna wakati unaangalia Simba inavyocheza mpaka unawaonea huruma kwa kweli kwani kuna watu wanatoka machozi, jasho na damu kwa dakika zote tisini wakina Kapombe, Zimbwe, Onyango na Inonga halafu kuna wengine wanazurura tu uwanjani wanasubiri mechi iishe wakachukue posho zao kama wakina Bwallya japo huyu ana kipaji kikubwa sana lakini si mpambanaji kabisa. Unakuta mchezaji anapoteza mpira kwa adui halafu anatembea matokeo yake anawafanya wenzake wafanye kazi kubwa uwanjani.

Simba kama kweli wana nia ya kufika nusu fainali/ fainali Afrika basi inahitajika isajili kama ifuatavyo:-
1. Iwaache Mugalu na Kagere badala yao isajili mafowadi wawili wa kimataifa. Angalizo lazima wawe na uwezo kuwazidi hao wanaoachwa.
2. Imuhamishie Boko kwenye benchi la ufundi au kumpeleka kufundisha timu ya vijana nafasi yake achukue Lusajo wa Namungo.
3. Itafute viungo wawili wa kimataifa ambao wote wawe na uwezo wa kucheza kiungo cha chini na cha juu bila wasiwasi. Hapa bila kupepesa
iachane na Bwallya. Nasisitiza iachane na Bwally japo ana kipaji kikubwa sana lakini anakosa kabisa "spirit" ya upambanaji uwanjani.
Ukitaka kujua namaanisha nini basi rudi kaangalie "clip" za Lwanga na Fraga ndio utajua maana ya kujitoa kwa ajili ya timu.
4. Iachane na Muzamiru na Nyoni badala yake wamsajili Cleophas Mukandara kuchukua nafasi yake na pia imrudishe Abdulswamad
aliyetolewa kwa mkopo.
5. Iaachane na Wawa na itafute beki mmmoja wa kimataifa ambaye yupo sawa na Inonga au anayemzidi uwezo Inonga.
6. Itafute beki mmoja mmoja awe wa ndani au wa kimataifa ambaye ana uwezo wa kucheza mbavu zote mbili bila wasi wasi ili kuwasaidia
Kapombe na Zimbwe. Mwenda na Gadiel wameshindwa hili jukumu. Gadiel anakaba vizuri sana ila ana uwezo mdogo wa kupandisha
mashambulizi. Mwenda anaweza kupanda ila krosi zake hazina macho na si mkabaji mzuri. Bahati ni kuwa Kapombe na Zimbwe
hawakupata majeraha ya muda mrefu msimu huu maana ingekuwa aibu kwa Simba.
7. Sakho, Mhilu, Mwanuke na Banda waachwe waendelee kuwepo Simba wazidi kukomaa kwani watakuwa na faida Simba ndani ya misimu
miwili ijayo iwapo watakuwa na mwendelezo walio nao sasa hivi.
8. Morison aendelee kubaki Simba. Atumike tu kuamua matokeo kwenye baadhi ya mechi muhimu kwani amethibitsha hilo analiweza.
Adhibitiwe tu kwenye nidhamu basi. Huyu mtu siku akiamua kucheza mpirra anacheza kwa sababu anauweza sana. Ila siku akiamua
kuaharibu anaharibu kweli sijui huwa ana nini kichwani.

Ni mtizamo tu.
Umetoa mtazamo murua kabisa..!
 
Wengi wenu naona mnapoint wachezaji wa kuondoka bila kusema timu ijengwe vipi.

Ukiangalia kikosi chetu kwa sasa kuna wachezaji karibia 7 waliotupa mafanikio misimu minne iliyopita wanaweza kuondoka mwisho wa msimu kutokana na kukosa makali au umri wao kuwatupa mkono.
1. Paschal Wawa
2. Erasto Nyoni
3. Meddie Kagere
4. John Bocco
5. Tadeo Lwanga
6. Rally Bwalya
7. Bernad Morisson
8. Hassan Dilunga.
9. Gadiel Michael

Hii ni idadi kubwa sana ya senior players ambao yawezekana zaidi ya nusu yao hatutakuwa nao msimu ujao.

Wapi tuboreshe kwa usajili upi na yupi abaki kwenye hiyo list.?

Kwa upande wangu mimi naona Simba wanahitaji kusajili DM mwingine local mchanga na kwa haraka haraka namuona Aziz Andabwile wa Mbeya City kuwa best pick au Kelvin Nahashon Naftali wa Geita Gold FC.

Kwa upande wa left back Simba wanahitaji back up nzuri zaidi ya Gadiel kwangu mimi namuona Kouassi Attohoula Yao wa Asec Mimosas 25 years of age.

Upande wa kulia iwapo Simba watafanikisha kumsajili Victorien Adebayor waachane na Morisson tayari tuna best wing upande huo ambaye ni Peter Banda, Kibu Denis, Hassan Dilunga. Iwapo Simba wataachana na Dilunga msimu huu warudi pale Azam wakamchukue Tepsie Evans ni fringe player mzuri kwa timu kama Simba.

Upande wa central midfield uwezo wa Bwalya hauongezeki tena tunahitaji a more imposed na creative midfielder zaidi yake Simba wamuone Gilbert Beruti kuwa best like to like replacement ya Bwalya ambaye anaweza kucheza position ya Chama pia anapoflop.

Kuondoka kwa Wawa na Nyoni kutatuachia pengo kubwa sana kikosini kwetu tunatakiwa kupata either local versatile player lakini kuziba pengo hilo ni kuwanyang'anya utopolo yule Yannick Bangala by the way ana mkataba wa mwaka mmoja tu.

Kwenye defensive Midfield akiondoka Tadeo Lwanga na kutokana na injury records zake ni heri tuvunje benki tuende TP Mazembe kumchukua Zemanga Soze au tubaki na tulionao.


Kwenye striking force tunahitaji local striker ambaye atakuwa like to like replacement ya Bocco kwangu mimi namuona Lusajo Reliant amekuwa consistent kwa misimu mingi kwa timu kubwa kama Simba tunaweza kunufaika nae wakati huo tukitafuta mbadala wa Kagere na Mugalu though naona bora kubaki na Mugallu ili tusipoteze wote.
We jamaa unajua sana wachezaji na mpira,
 
Huyu zemanga soze ndio yule wa tp mazembe!? Hao wengine woote siwajui, na huenda wakawa wanavipiga katika club zinazoshiriki michuano ya caf.

Je stephano ki aziz anacheza mido ya kati!!?
Aziz Ki ni central midfielder.
Zemanga Soze ni TP Mazembe
Ngoma yupo Raja Casablanca
Collins Sikombe yupo Napsa Stars
Gilbert Baruti yupo Jwaneng Galaxy yule kipara namba 22 aliyekuwa akiitawanya midfield yetu pale kwa Mkapa kama watoto wadogo.
 
Kuna sehemu nimezungumzia mambo ya jukwaan!? Mie kwangu kanoute sio midfield ya kusema anauwezo wa kusambaratisha kiungo pinzani, aidha kwa pass zake, movements zake na kadhalika, nahisi hata mimi nikicjeza na kanoute naweza kuenjoy tu dimba la kati, yuko na pass accuracy mbovu kupitiliza.

Kila mtu na jicho lake.
Bas poaaaah.
 
Back
Top Bottom