Kocha wa Yanga asema ligi ya Tanzania ni dhaifu ndio maana Yanga wametolewa

Ndio ukweli wenyewe.
KAZI ni kipimo cha UTU
Hapana huu ni ukweli nusu.

Inawezekana ligi A ikawa dhaifu kuliko ligi B lakini ligi A ikawa na baadhi ya timu imara kuliko ligi B.

Kwani Yanga mwaka jana wakati anamfunga CR Belouzidad 4-0 na kutinga robo fainali CR Belouzdad ni timu kutoka wapi? Sio Algeria?

Awe mkweli aache ubabaishaji zipo sababu za kiufundi kwanini jana yanga ilishindwa kupata goli.

Visababu vya kuokoteza havitamsaidia.
 
Reactions: Tui
JF inasomwa na wengi na hivyo habari hata kama ni uzushi ukitiwa mkazo jukwaani,mgeni akipitia huo uzushi ni rahisi kuaminika.Binafsi yanikera kwani inazorotesha ubora wa JF.Kama kuna ukweli leta jukwaani tudadavue nao Yanga Officials watakuja kutoa utetezi wao nasi tvawahukumu.
 
Kauli za kifedhuli.

Sasa yeye anafanya nini kwenye ligi dhaifu?
 
Hii ishu niliona siku moja wanaiongelea watu wa Africa Kusini. Hasa baada ya Nabi kufanya vizuri akiwa Yanga wakati sehemu zingine akiwa amefeli na kuonekana kufeli Kaizer Chiefs, wakatoka kwa Nabi wakaja kwa kocha Fadlu ambaye anaonekana kwenye ligi anaongoza ligi wakati hakuwahi kufanya vizuri popote pale na wakamalizia na kocha Saed
 
Wabongo mkiambiwa ukweli na wataalamu mnatukana.

Ligi yeni ni dhaifu haimpi changamoto kabisa
 
Vipi calculator za rankings za klabu za CAF zimeishaje?Mbona hamna follow up ya kile kichaka?Si kuna kichaka kilikuwa kifekwe?
 
Vipi calculator za rankings za klabu za CAF zimeishaje?Mbona hamna follow up ya kile kichaka?Si kuna kichaka kilikuwa kifekwe?
Kwani Yanga kashinda? Uzi si uliandikwa endapo Yanga atashinda
 
Ligi ya Tanzania anaiona laini kwa sababu ananunuliwa mechi kwa kuhonga marefa na pia kuhonga timu pinzani kupitia udhamini feki.Sasa huko CAF hakuna huo ujinga.
Fact
 
Reactions: Tui
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…