Kodi mpya ya Majengo kupitia LUKU inatakiwa kulipwa na Mmiliki wa Jengo na sio Wapangaji wa Jengo

Kodi mpya ya Majengo kupitia LUKU inatakiwa kulipwa na Mmiliki wa Jengo na sio Wapangaji wa Jengo

Na wanao kaa nyumba za serikali, malalamiko wana peleka wapi? Mwenye nyumba tuna mshitaki vipi?
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo.

Hayo yameelezwa na Lazaro Lucas katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambapo ameongeza kuwa kwa sasa kuna changamoto wa kutofautisha mnunuzi wa umeme kama ni mwenye nyumba au mpangaji, hivyo kwa mwanzoni mpangaji anaweza kukatwa kodi hiyo kimakosa.

“Hiyo kodi inapaswa kulipwa na mwenye jengo lakini kwa mwanzo kumekuwepo na changamoto ya kujua ni yupi mwenye jengo ni yupi mpangaji kwa hiyo mwanzoni [mpangaji] unaweza ukapata ‘bill’… mwenye jengo afike ofisini aseme nyumba zangu ni moja, mbili, tatu, ili wenye zile mita ziondolewe,” amesema Lucas.

Lucas ameongeza kuwa mwenye jengo anaweza kulipia kodi ya nyumba za wapangaji taslimu shilingi 12,000 kwa kila nyumba ya kawaida kwa mwaka na namba za mita za wapangaji zitaondolewa kwenye mfumo, au kodi hiyo itahamishiwa kwenye mita yake.

Aidha, TRA imesema kuwa endapo mwenye jengo hatowasilisha taarifa za wapangaji TRA, wapangaji wanaweza kupeleka malalamiko yao kwamba wanatozwa kodi ya jengo kimakosa.

Viwango hivyo kwa sasa ni shilingi 12,000 kwa kila jengo la kawaida ndani ya kiwanja kutoka shilingi 10,000 iliyokuwa ikitozwa awali, na shilingi 60,000 kwa kila sakafu ya ghorofa kutoka 50,000. Hata hivyo kwa upande wa halmashauri za wilaya na miji midogo nyumba za ghorofa bila kujali idadi ya sakafu zitatozwa shilingi 60,000.

Kwa utaratibu huo kila mnunuzi wa umeme atakatwa shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba ya kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa kila sakafu ya ghorofa. Kwa wanaotumia mita za ankara watalipa kodi hiyo kwa pamoja katika Ankara zao za mwezi.
Sijaelewa hata punje
 
Kodi ya jengo
Kodi bandarini ukiagza mzgo
Kodi airpot
Kodi kwny mafta ya gari
Kodi ukinunua vocha
Kodi ukinunua umeme
Tozo

Kila siku kodi kodi kodi
 
Mamlaka ya Mapato ni wanafiki, mbona Withholding Tax inalipwa na wapangaji badala ya mwenye jengo! Mwenyenyumba neno lake ni lipa au hama kapange huko TRA.

Wakati unamlipa kodi mwenye nyumba unatakiwa wewe umkate hicho kiwango cha withholding tax then uka remit TRA or else umlipe full yeye ndio akalipe TRA ambapo mara nyingi huwa hawapeleki
 
Maboko yameanza mapema sana sasa sijui hii ni sabotage au nini kinaendelea ila boko zinapigwa nyingi sana na huko mbeleni ndio naona giza zaidi siwaoni wakipata hekima mbeleni
Kuna umuhimu wa kuendelea na ile novena yetu maana the hard headed never learns
 
kuna kamgogoro kananukia between wapangaji na wenye nyumba.....na kuna kulipia double double.....maana ni kila anayenunua LUKU....kweli TANZANIA raha....hili pia wemekurupuka.....wangetoa muda wenye nyumba wajiorodheshe kwanza.......la sivyo kuna pesa nyingi za DHULUMA zitakusanya na serikali yetu DHALIMU.....
 
Mie simpangishii mteja umeme bali nampamgishia nyumba kama hataweza kujilipia umeme asinunue. Siwezi kumlipia mpangaji umeme.
 
Wana akili hizo basi? Na ndio maana ikifika kwenye uchaguzi kazi yao ni kuchapisha makaratasi ya ziada na kujipigia kura majumbani mwao. Ukiwaambia habari ya katiba mpya, busha linawashuka ghafla. Wanajua wananchi hawayapendi haya madudu.
kuna kamgogoro kananukia between wapangaji na wenye nyumba.....na kuna kulipia double double.....maana ni kila anayenunua LUKU....kweli TANZANIA raha....hili pia wemekurupuka.....wangetoa muda wenye nyumba wajiorodheshe kwanza.......la sivyo kuna pesa nyingi za DHULUMA zitakusanya na serikali yetu DHALIMU.....
 
Kuna wale makapuku, umeme wa 2000 tu unatosha. Sasa sijui watafanyaje. Watakata buku yao na buku nyingine iwe kwenye luku?
Lakini pia kuna nyumba zenye mita zaidi ya moja, je huoni huu ni wizi pia? Maana nyumba moja wataka kodi kwa kila luku.
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo.

Hayo yameelezwa na Lazaro Lucas katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambapo ameongeza kuwa kwa sasa kuna changamoto wa kutofautisha mnunuzi wa umeme kama ni mwenye nyumba au mpangaji, hivyo kwa mwanzoni mpangaji anaweza kukatwa kodi hiyo kimakosa.

“Hiyo kodi inapaswa kulipwa na mwenye jengo lakini kwa mwanzo kumekuwepo na changamoto ya kujua ni yupi mwenye jengo ni yupi mpangaji kwa hiyo mwanzoni [mpangaji] unaweza ukapata ‘bill’… mwenye jengo afike ofisini aseme nyumba zangu ni moja, mbili, tatu, ili wenye zile mita ziondolewe,” amesema Lucas.

Lucas ameongeza kuwa mwenye jengo anaweza kulipia kodi ya nyumba za wapangaji taslimu shilingi 12,000 kwa kila nyumba ya kawaida kwa mwaka na namba za mita za wapangaji zitaondolewa kwenye mfumo, au kodi hiyo itahamishiwa kwenye mita yake.

Aidha, TRA imesema kuwa endapo mwenye jengo hatowasilisha taarifa za wapangaji TRA, wapangaji wanaweza kupeleka malalamiko yao kwamba wanatozwa kodi ya jengo kimakosa.

Viwango hivyo kwa sasa ni shilingi 12,000 kwa kila jengo la kawaida ndani ya kiwanja kutoka shilingi 10,000 iliyokuwa ikitozwa awali, na shilingi 60,000 kwa kila sakafu ya ghorofa kutoka 50,000. Hata hivyo kwa upande wa halmashauri za wilaya na miji midogo nyumba za ghorofa bila kujali idadi ya sakafu zitatozwa shilingi 60,000.

Kwa utaratibu huo kila mnunuzi wa umeme atakatwa shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba ya kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa kila sakafu ya ghorofa. Kwa wanaotumia mita za ankara watalipa kodi hiyo kwa pamoja katika Ankara zao za mwezi.
Wacha mpangaji alipe kisha kodi yake ya mwisho wa mwaka ataipunguza kwenye malipo yake ya pango kwani kunatatizo gani?
 
Tatizo la kodi hii ni implementation yake...

Mimi nashauri yafuatayo ili kufanya kodi hii ilipwe fairly na mmiliki Wa jengo;

1. Kwamba serikali inataka fedha (mapato) lakini haitaki kuwekekeza ktk mifumo ya mapato. Kwa hiyo, ianze kuzitambua nyumba zote hapa nchini zinazostahili kulipiwa kodi na wamiliki wake na hao ndiyo wawekwe kwenye data base na wakati wowote walipie kodi majengo yao kwa njia yoyote....

2. Mifumo yote ya TANESCO - LUKU, Wizara ya ardhi, mitandao yote ya simu na benki na NIDA ni sharti ioane au itambuane...

Kwa maana hiyo basi, hata kama mimi nitanunua umeme wa LUKU isiyo yangu sitakatwa kodi hiyo maana mfumo hautanitambua kama ni mwenye jengo kwa sababu ya jina langu kutofautiana na mmiliki wa nyumba/jengo...

Nasema hivi kwa sababu hapa ndipo ilipo shida ya kodi hii, kuwa, kama kila simu itakayonunua umeme ktk LUKU meter fulani itakuwa inakatwa kodi ya jengo, basi hii kodi itakuwa ya holela sana na itakuwa ni kuwaibia watu na hii ndiyo concern ya watu...!

3. Serikali ihamasishe watu wote waliouziana nyumba kwenda ofisi za ardhi kuhamisha umiliki wa majengo hayo kutoka kwa mmiliki wa awali kwenda kwa mmiliki mpya ili kuepusha mmiliki kulipa kodi hii maana ktk mfumo ataendelea kusomeka hivyo kumbe ameshauza nyumba yake kitambo....

Kurahisisha hili, serikali iondoe urasimu usio wa lazima pamoja na kuondoa au kupunguza gharama za occupation transfer of property...

4. Wale wote wasio na hati miliki, serikali ifanye utaratibu kwa nchi nzima kuwafanyia registration hata ya muda wote wanaomiliki nyumba na iwatambue kisheria lengo likiwa ni kuwaingiza ktk data base ya ardhi na TRA...
 
Ningeishauri serikali waoneshe breakdown ya hiyo risiti ya LUKU itakaaje. Ili nitoe wazo. Maana kwa mwaka ni 12k nyumba ya kawaida kwa mfano basi wakati wa kuingia mkataba mwenye nyumba alipie kwa mkupuo (hii option iwepo) kabla ya kumuiingiza mpangaji au wakati wa kurenew mkataba.
Sahihi kabisa. Imekaa vizuri hii.
 
Mie simpangishii mteja umeme bali nampamgishia nyumba kama hataweza kujilipia umeme asinunue. Siwezi kumlipia mpangaji umeme.
Mkuu naona wenye nyumba mshaanza kutupa za uso. Lol
 
Hivi kwa mwezi ukinunua umeme mara 3 inakatwa buku 3 maana si elfu 12 kwa mwaka ikikamilika ndio utakuwa free mpaka mwaka mpya
Hii imekaaje
Hapana. Hata ukinunua mara 10 ndani ya mwezi huo mmoja, inakatwa mara moja tu. Ni yale manunuzi ya kwanza katika huo mwezi ndiyo yatakumbana na hiyo tozo.
 
Back
Top Bottom