Kodi mpya ya Majengo kupitia LUKU inatakiwa kulipwa na Mmiliki wa Jengo na sio Wapangaji wa Jengo

Kodi mpya ya Majengo kupitia LUKU inatakiwa kulipwa na Mmiliki wa Jengo na sio Wapangaji wa Jengo

Withholding tax inakipwa na wapangaji na sio wenye nyumba, hapa hata hii property tax bado italipwa na wangaji na sio wenye nyumba.

Ukibisha utaambiwa hama Kama unashindwa kulipa na hao wabunge na maofisa wengi serikalini Ni miongoni mwa wamiliki wa majengo ambao watatumia mwanya huu kuikwepa kulipa Kodi. Mna umiza Sana watu bila sababu za msing...
Duniani kote kodi za majengo ni chanzo muhimu sana cha mapato kwa Local Authorities na mapato hayo yanakwenda moja kwa moja kuwaletea maisha bora wakazi wa mji husika . Fedha haziendi serikali kuu na wala property tax ya Dar haiwezi kwenda kujenga miradi Bukoba. Property tax hutozwa kwa kuzingatia thamani ya jengo na siyo flat rate. Kodi hiyo hutozwa mijini.

Nyumba vijijini hazilipishwi kodi hiyo. Thamani ya jengo inapatikana kwa halmashauri ya mji/jiji husika kuajiri wathamini wa kutosha kufanya kazi hiyo au kutumia kampuni binafsi za Uthamini zilizosajiliwa. Valuation rolls huandaliwa zikionesha majina ya wamiliki wa majengo, mahali jengo lilipo, thamani ya jengo, kiwango cha kodi kwa jengo husika na mmiliki anaweza kwenda kulalamika kama anaona amebambikiwa kodi kubwa na marekebisho hufanyika.

Hili la kutoza kodi hii kupitia bili ya umeme ni hapa Tanzania tu. Hakuna nchi ingine inayofanya hivyo. Ushauri kwa wenye mamlaka turudi kwenye misingi mikuu ya kodi hii. Halmashauri zihusike kikamilifu, ziajiri wathamini wamejaa tele mitaani wamesoma Ardhi University degrees na vyuo vya cheti na diploma vinawazalisha kila mwaka.

Wakafanye hiyo kazi kwenye ngazi ya Kata na Mitaa mijini, wapimwe kwa mafanikio watakayopata, Makusanyo yatakayopatikana yatatosha kuwalipa pia mishahara na huo ndiyo uwekezaji wenye tija. AJIRA.

Acheni kabisa kuwasumbua wazee wastaafu vijijini kwa kodi za aina hii kupitia Umeme. Hii kodi inayotozwa kupitia umeme ipewe tu jina jingine ili watanzania waielewe na kuilipa kwa hiari. Isiitwe kodi ya majengo maana inaacha maswali mengi sana yasiyo na majibu
 
Kwa waanoishi nyumba za National housing inakuwaje...?
Soma hapo
JamiiForums496568829.jpg
 
Mbona hiyo ki2 rahisi sana,mpangaji alipe kodi kwa pungufu ya 1k kwa kila mwezi,kma analipa kodi ya mwaka analipa kodi ya mwaka toa 12k.
 
Duniani kote kodi za majengo ni chanzo muhimu sana cha mapato kwa Local Authorities na mapato hayo yanakwenda moja kwa moja kuwaletea maisha bora wakazi wa mji husika . Fedha haziendi serikali kuu na wala property tax ya Dar haiwezi kwenda kujenga miradi Bukoba. Property tax hutozwa kwa kuzingatia thamani ya jengo na siyo flat rate...
Mimi Ni mthamini mzoefu, nilishiriki kuanda valuation roll ya kinondoni, Bukoba, Temeke, ilemela na Ilala, kimsingi Kodi aliyoleta bwana Mwigulu sio Kodi ya jengoa labda ipewe jina jingine. Kodi ya jengoa huwa ni kwenye mamlaka za Mimi pekee kwa kuzingatia Sheria ya ugatuzi wa madaraka yaani Local Authority Act No 2 ya mwaka 1982 na Urban Rating Act No 3 ya mwaka 1983.

Pia Kuna Kodi ya jengoa ambayo hutolewa ili kufidia gharama iliyotumika kujenga miundombinu iliyochangia kukua kwa thamani ya majengo (Land Value Capture). Sasa hii ya mwingulu ni looting Act, kwa Nini tuzirudi kwenye utamadudi wa Sheria ili kimbaini mmiliki halisi wa jengo na sio kuweka mzigo kwa wapangaji.

Wekezeni pesa, watumieni wathamini wawa saidie na sio hizo porojo za kisiasa. Mnawapora kwenye withholding tax na bado mmewafuata kwenye property tax, hii sio haki kabisa.
 
Kwani hajui uswazi namna tunavyonunua umeme ni wapangaji wenyewe tunachangishana na mkijiloga hata kumkabidhi mwenye nyumba anazilamba mnalala giza?
[emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38][emoji38]
 
Kuna uhuni tu utaendelea kupitia hii tozo
Muda huu baada ya kuona huu uzi , nimetest kununua units za miatano (chini ya kiwango chao wanachotaka 1000tsh), ngoma inagoma kabisa wanadai eti "Tender more money😝"

Nimemwambia mke wangu ajaribu na yeye wanamuandikia hivyo.

Nilichogundua ni kwamba hii tozo ya LUKU atakatwa mtu yoyote bila kujali anamiliki NYUMBA au laah.

Huu ni upuuzi mkubwa sana,yani hawaridhiki na hela za miamala na mafuta Sasa wamehamia kwenye LUKU, na kibaya zaidi hela zetu zinatumiwa na mpumbavu mmoja kufanya ziara za kijinga tu, kutw anazinguka na misafara kwenye nchi za watu.

Muda sio mrefu wanaume tutaanza kutozwa tozo ya pumbu kmmk🤒
 
Kwani hajui uswazi namna tunavyonunua umeme ni wapangaji wenyewe tunachangishana na mkijiloga hata kumkabidhi mwenye nyumba anazilamba mnalala giza?
Umenikumbusha story moja juzi kati,nimekatiza sehemu Tanesco wamegundua nyumba wanaiba umeme,kuuliza wapangaji wanasema wako 8 na kila mwezi mwenye nyumba anachukua elf 10 kila mpangaji,kumbe jamaa hanunui umeme,kacheza na vishoka wame set umeme unaingia direct...
 
Kuna wale makapuku, umeme wa 2000 tu unatosha. Sasa sijui watafanyaje. Watakata buku yao na buku nyingine iwe kwenye luku?
Buku 2 hupati unit hata moja 🤣 🤣 🤣 ,ndo vimeumana hvyo mkuu-Mama anakata buku 2 makato kwenye LUKU bila huruma
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo...
Jamani vp kuhusu wenyenyumba za matembe?na za nyasi zenye umeme nao watakatwa?maana mimi naishi humo kama watakata bora niendee zangu mjini maana nitakuwa nimepanda hadhi [emoji123][emoji123][emoji123]
 
Muda huu baada ya kuona huu uzi , nimetest kununua units za miatano (chini ya kiwango chao wanachotaka 1000tsh), ngoma inagoma kabisa wanadai eti "Tender more money...
Sooner bradha yani kabla hujasema su kutakuwa na “Balls hanging Tax”
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo...
Wananchi masikini wanakamuliwa, hizi kodi zingetozwa kwa wenye nyumba ambao wana ajira serikalini, wabunge au wafanyabiashara wakubwa wenye majengo maeneo ya biashara sio mtu maskini kijijini kibanda chake kaweka luku tena inakuwa shida na makodi ya jengo analipa hizo kodi ni kuwadhalilisha wananchi hela ya jengo ataitoa wapi?
 
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imesema kuwa kodi ya majengo kwa njia ya ununuzi wa umeme ambayo itaanza kutumika Agosti 20, 2021 inatakiwa kulipwa na wamiliki wa majengo na sio wapangaji kwenye majengo hayo.

Hayo yameelezwa na Lazaro Lucas katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) ambapo ameongeza kuwa kwa sasa kuna changamoto wa kutofautisha mnunuzi wa umeme kama ni mwenye nyumba au mpangaji, hivyo kwa mwanzoni mpangaji anaweza kukatwa kodi hiyo kimakosa.

“Hiyo kodi inapaswa kulipwa na mwenye jengo lakini kwa mwanzo kumekuwepo na changamoto ya kujua ni yupi mwenye jengo ni yupi mpangaji kwa hiyo mwanzoni [mpangaji] unaweza ukapata ‘bill’… mwenye jengo afike ofisini aseme nyumba zangu ni moja, mbili, tatu, ili wenye zile mita ziondolewe,” amesema Lucas.

Lucas ameongeza kuwa mwenye jengo anaweza kulipia kodi ya nyumba za wapangaji taslimu shilingi 12,000 kwa kila nyumba ya kawaida kwa mwaka na namba za mita za wapangaji zitaondolewa kwenye mfumo, au kodi hiyo itahamishiwa kwenye mita yake.

Aidha, TRA imesema kuwa endapo mwenye jengo hatowasilisha taarifa za wapangaji TRA, wapangaji wanaweza kupeleka malalamiko yao kwamba wanatozwa kodi ya jengo kimakosa.

Viwango hivyo kwa sasa ni shilingi 12,000 kwa kila jengo la kawaida ndani ya kiwanja kutoka shilingi 10,000 iliyokuwa ikitozwa awali, na shilingi 60,000 kwa kila sakafu ya ghorofa kutoka 50,000. Hata hivyo kwa upande wa halmashauri za wilaya na miji midogo nyumba za ghorofa bila kujali idadi ya sakafu zitatozwa shilingi 60,000.

Kwa utaratibu huo kila mnunuzi wa umeme atakatwa shilingi 1,000 kwa mwezi kwa nyumba ya kawaida na shilingi 5,000 kwa mwezi kwa kila sakafu ya ghorofa. Kwa wanaotumia mita za ankara watalipa kodi hiyo kwa pamoja katika Ankara zao za mwezi.
Kwahiyo Kama Una nyumba haina. Umeme wewe ndo basi tena kulipita bili ya majengo. Hapo TRA nimewapata
 
Kodi ya Majengo Kwenye Luku ni ya Mwenye Nyumba Sio Mpangaji

SERIKALI imetoa ufafanuzi kuhusu kodi ya majengo ambayo imeanza kulipwa jana Agosti 20, 2021 kupitia makato wakati wa ununuzi wa LUKU za umeme baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha sheria hiyo hivi karibuni.

Katika mkutano uliofanyika leo Jumamosi, Agosti 21, 2021 katika mtandao wa ZOOM ukiongozwa na Taasisi ya Watch Tanzania, mkutano huo umewashirikisha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ambao ndio wakusanyaji wa mapato, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Pamoja na Bunge ambalo ndilo lilitunga sheria hiyo.

MWAKILISHI WA MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA (TRA)

Mkurugenzi wa Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo

Kodi ya majengo sio kitu kipya, imekuwa ikitozwa kwa namna tiofauti, mwanzoni ilikuwa kwa asilimia ya thamani ya jengo baadae tukaja na flat rate. Changamoto ilikuwa kila mwaka mtu afuate control number kisha alipe kwa wakala au simu yake.

Serikali inatakiwa ipate pesa yake, mwananchi wengine walikuwa akipata penati kutokana na madeni haya.

Kodi hii inatozwa kwa majengo ambayo yamefanyiwa uendelezaji wa ardhi, iwe imepimwa au haijapimwa. Na hii itafanyika katika majiji na manispaa Tsh 12,000 (kwa mwaka) yaani Tsh 1,000 kila mwezi kwa nyumba za kawaida, tutakusanya kupitia manunuzi ya umeme.

Jengo la ghorofa moja litachajiwa chini atalipa Tsh 60,000 na juu Tsh 60,000 jumla Tsh 120,000. Itakuwa tsh 5000 kwa kila sakafu hivyo 10,000 kwa mwezi. Majengo yaliyo makao makuu ya wilaya, ghorofa itatozwa jumla ya Tsh 60,000 tu bila kujali ni ghorofa moja au Zaidi.

Jengo la kawaida haijalishi lipo wapi kwenye jiji au manispaa, itakuwa 12,000 maeneo yote. Kwa nyumba ambazo hazitumii luku lakini zinatumia umeme wataendelea kulipa kupitia Ankara zao za kawaida (bill) lakini ambao hawana umeme au wanatumia sola wataendelea kulipa kwa sababu ni wajibu wao kisheria kulipa.

Nyumba za vijijini hazihusiki, hazitozwi. Nyumba ambazo zimejengwa kwa vifaa ambazo hazidumu hazitozwi, za udongo na nyasi pia hazitozwi.

Wanaohusika wakitozwa wafike TRA kutoa taarifa, maofisa wetu wameshapewa maelekezo wasiohusika (waliosamehewa) na nyumba ambazo hazina vigezo vya kutozwa wasitozwe, wakiwemo wazee ambao wana msamaha.

Kwa mwenye nyumba kama ana luku mbili kwenye nyumba moja, kwa sasa luku zote zinatozwa, lakini anaweza kuja Tanesco na kueleza nil uku ipi itatumika kulipa kodi.

Kodi hii inatakiwa kulipwa na mwenye nyumba na si mpangaji, hivyo anaweza kufanya mawili… mwenye nyumba anaweza kupunguza kwenye kodi yako ya nyumba Tsh 12,000 au kumnunulia mpangaji wake umeme wa Tsh 12,000 kwa mwaka, lakini kama watashindwa kuelewana mwenye nyumba na mpangaji wake hiyo ni juu yao.

Kwa ambao walikuwa wameshalipa kwenye mfumo wa zamani basi wafike ofisi ya TRA iliyo karibu nae tuone namna ya kufanya. Kama alikuwa anadaiwa hilo deni lipo kwa mujibu wa sheria atalazimika kulipa, kubadilisha mfumo haimanishi deni limeisha.

Tozo hiyo atakatwa kila mwezi, mara moja tu kwa mwezi, hatutozi ya mwaka mzima kwa pamoja, ila kama umelimbikiza madeni utalazimika kuyalipa kwanza pale tu utakaponunua umeme.

Kama una nyumba na kibabda cha kuchajisha simu utalipa kama kawaida. Nyumba za serikali zinazotoa huduma kama shule za umma, hospitali za umma, majengo ya halmashauri, huduma za TRA hayo hayalipiwi, lakini kama unaishi nyumba ya serikali utalipa.

Nyumba zinazotoa huduma kama shule binafsi nna hospitali binafsi zitalipishwa sababu zinafanya biashara. Utaratibu watu hawajauzoea, ilitakiwa ianze Julai mosi, ndio maana walionunua jana, wamekatwa tozo ya Julai na mwezi Agosti.

Kwa wazee, waje na uthibitisho wa nyumba moja anayoishi ikionyesha umri wake, isiwe nyuba ya biashara iwe ya kuishi, kama imepangishwa itakosa sifa na badala yake atalipa sababu inaingiza kipato. Kama anazo nyumba mbili au tatu na ana wake wawili watatu kila mmoja kwenye nyumba yake, nyumba moja haitalipiwa nyingine zote zitatozwa.

Makanisa na nyumba ya ibada yatasamehewa, ila nyumba nyingine kama zipo eneo la kanisa ambazo hazitoi huduma ya ibada, labda ni ofisi ama nyumba za kuishi watumishi wa Mungu, zitatozwa.

Kodi hii itasaidia mengi, kwanza kwa TRA hakuna paper work, itarahisisha makato na kuondoa ulimbikazi wa madeni, Serikali itapata kodi yake kwa wakati.

MWAKILISHI WA BUNGE

Mbunge wa Busega Simiyu, Mhe. Simon Songwe

Mapendekezo ya sheria hii yamepitishwaa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu June 22, mwaka huu ililetwa na Waziri ikaenda kamati ya bunge. Concern za Waziri zilikuwa nyingi na kuhitaji serikali kubadili mfumo.

Kumsaidia mwananchi kusahau na kuondokana na penati, Serikali ilikuwa haikusanyi mapato ya kutosha kupitia kodi hii ya majengo.

Hii itasaidia sasa kupunguza gharama kwa mwananchi badala ya kusaifiri kwenda TRA kutafuta control number na kulipa, itapunguza gharama za ufuatiliaji kwa serikali, itasaidia kukusanya fedha hizi kwa wakati

Ni sehemu ya jukumu letu kama wabunge kuendelea kuwaelimisha wananchi, sisi tutaendelea kuwaelimisha wananchi lakini pia TRA waendelee kutoa elimu. Sisi sote ni Watanzania na nchi yetu itajengwa na Watanzania wote. Kodi ni jukumu la mwenye nyumba, wasiwanyanyase wapangaji.

MWAKILISHI WA TANESCO

Meneja Mkuu Huduma kwa Umma, Martine Mwambene

Kodi hii hakuna fungu linalokuja TANESCO bali tunashirikiana na Serikali kukusanya pesa hizo, lakini kuna asilimia flani inakwenda TAMISEMI.

Nyumba moja yenye luku 2, kwa kuanzia kwa sasa mita zote ziwekewe, kisha baadae wenye nyumba watasema luku ipi itumike kulipia kodi hii.
 
Kodi ya Majengo Kwenye Luku ni ya Mwenye Nyumba Sio Mpangaji

SERIKALI imetoa ufafanuzi kuhusu kodi ya majengo ambayo imeanza kulipwa jana Agosti 20, 2021 kupitia makato wakati wa ununuzi wa LUKU za umeme baada ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitisha sheria hiyo hivi karibuni...
hii kitu haiko sawa ilibidi watengeneze utaratibu mzuri kabla ya kuanza kutumia mfumo. Leo kuna watu wamekatwa zaidi ya mara moja na wanasema mkatoe taarifa tanesco na watumishi wa nchi hii walivo miungu watu itakuwa shida kweli.
 
Mzee mwenye nyumba na yupo msamahaa na analuku basi analipa kama kawaida. Msahamawa wake ni nini?
 
Back
Top Bottom