Kodi nyingi zitatuzindua usingizini Watanzania na kudai haki zetu, Nchemba umechemka kuhusu 18 years kulipa kodi ya kichwa

Watalipa Kwa lazima ndio maana watatambuliwa kwa njia ya TIN na anuani za makazi..
Kaka kulipa kodi kwa lazima au enforcement kuna consequences zifuatazo:-
1. Administrative expenses maana magari yawekwe mafuta kufuatilia walipa kodi, posho za tax collectors etc.

2. Tax evasion sababu mmeingia kwenye ubabe basi watu wataanza ku evade tax.
3. Cooperation kati ya administrators na taxpayers haitakuwa nzuri hivyo kusababisha malengo kutokufikiwa, na nyingine nyingi na ndio maana wanahimiza self assessment yaani kufanya watu wajikadilie ili kuepusha hayo matatizo.
 
Uko sahihi kabisa ukondoo huu unasababishwa na kutokujua wajibu wetu kwa nchi yetu tulipe kodi na tuisimamie serikali kwa matumizi yake
 
Wewe ungefuatikia Jana mjadala wa Bajeti TBC ungeelewa..

Huwezi cut majadiliano Kati ya muuzaji na mnunuzi bila enforcement..

Polisi wanafanya Kazi gani barabarani? Si unawaongezea tuu jukumu badala ya doria ya kawaida na siku zote unawapa na hili la kusimamisha msafiri yeyeote Ili kukagua risiti..

Hilo sio swala la kumuachia TRA pekee..Hakuna mtu anayependa kulipa Kodi sio Tanzania tuu bali Duniani kote ndio maana kuna sheria kali sana huko Duniani na hawana kuchekeana..

Hapa Tanzania serikali inafanya mzaha,harafu wanaodai huduma Bora hata Kodi hawalipi..
 
Ndo maana elimu kwa mlipa kodi inahitajika ili kila mtu ajue ana wajibu anapo nunua kudai receipt, au mlipa kodi ajione anajukumu la kulipa kodi
 
Ndo maana elimu kwa mlipa kodi inahitajika ili kila mtu ajue ana wajibu anapo nunua kudai receipt, au mlipa kodi ajione anajukumu la kulipa kodi
Hakuna asiyejua kwamba anatakiwa kulipa Kodi ndio maana wanafanya hayo majadiliano kwa sababu anayi hiyo elimu bali anakwepa Kodi Ili auziwe bei ya chini..

Hilo halihitaji elimu tena bali enforcement
 
Hakuna asiyejua kwamba anatakiwa kulipa Kodi ndio maana wanafanya hayo majadiliano kwa sababu anayi hiyo elimu bali anakwepa Kodi Ili auziwe bei ya chini..

Hilo halihitaji elimu tena bali enforcement
Doooh! Hili jambo ni la kitaalamu Mkuu na watu wamefanya tafiti na kuandika voluntary compliance huongeza revenue collection kwasababu hata yule anayeogopa kufanya biashara kwa kuhofia kuwekewa tax burden kubwa anapojifanyia self assessment ni rahisi kushawishika kufanya biashara na kuongeza wigo wa makusanyo.

Enforcement ina mahala pake lakini sio kila mahali. Unafikiria TRA walikurupuka kuleta self assessment?
 
We bwana una shida,ndio maana Lisu aliwahi ita professorial rubbish..

Unakomaa tuu na kitaalamu wakati huo utaalami haufanyi Kazi..

Hawa unaowaona humu jf wanakwepa Kodi hawana elimu? Hizi comments unaona wako tayari kulipa Kodi kwa hiari?

Nini maana ya kuwa na sheria basi? Zifutwe basi ilinuendelee kuwaelimisha tuone kama watalipa Kwa hiari..

Hata mimi hapa huwa nakwepa inapobidi ila kwa kuwa kuna kukamatwa nalipa,kwani sina elimu?

Narudia tena hakuna mtu yuko tayari kulipa Kodi kwa hiari yaani upunguze mapato yako kirahisi tuu? Trump ana kesi ya kukwepa Kodi na nintajiri,huyo hana elimu?

Kuwa serious mzee.
 
Mzee zile sheria za kodi tayari ni amri zinatoa due dates, zinatoa offences,interests and penalties na hata imprisonment lakini ili kuadminister sheria kunakuwa na vingine kama practice notes, regulations and etc. Pia ni haki kwa taxpayer kupewa presumption of honest na kuwa treated vizuri.

Eti kwasababu jambazi amejichanganya na watu basi hekima ya polisi iwe ni kufyatua risasi kwenye umati wa watu?
 
Hivi hiyo kodi ya mutwe ni sh ngapi au itaanzia kiwango kile kile alichokomea mkapa

Waziri ameshatoa maelezo akizingatia Section 4 ya Income tax Act CAP 332 RE 2019 ambayo inaelezea imposition of Income tax ambapo moja ya kipengele kinasema kodi itatozwa kwa mtu mwenye "total income during the year of income...."

Total income maana yake ni jumla ya vipato toka kwenye ajira,biashara na uwekezaji sasa kama mtu hana income maana yake si NIL na First schedule ya sheria hiyo hiyo inaonesha namna ya utozaji wa kodi ulivyo. Waziri amekanusha hayo akiwa anahojiwa na Azam Tv kuwa si kweli kwamba watu wenye umri wa miaka 18+ watalazimishwa kulipa kodi kama inavyoaminishwa.
 
Nimekubali 100%. Hii nchi tunatakiwa tuteseke sana ili kuzinduka usingizini asante lameck madelu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…