Kodi ya majengo kupitia luku baadhi ya watu wanaumia Kwa kuibiwa

Kodi ya majengo kupitia luku baadhi ya watu wanaumia Kwa kuibiwa

Naona mambo ya sensa
Kazi yake ishaanza kuonekana

Ova
Maana kwenye taarifa yao wamesema walifanya tafiti baada ya sensa hivyo wakaamua vinginevyo.
Mdogo mdogo tutaanza lipa kulingana na thamani ya kiwanja na nyumba.

Mdogo mdogo mashamba watayaachia
 
Hii ni kama ku discourage kujenga maghorofa.
Mimi naona wenye maghorofa ndio wangepewa unafuu zaidi ili ku encourage ujenzi wa maghorofa zaidi maana wanasevu maeneo kwa kuitumia vilivyo ardhi tuloyonayo.
Hata kama kusingekuwa na upendeleo huo, haiingii akilini eti mwenye sakafu mbili analipa 10,000 kwa mwezi wakati mwenye sakafu moja (nyumba ya kawaida)anakipa 1,000 tu kwa mwezi.
Nadhani kuna haja ya kuviangalia upya hivi viwango ili kuweka usawa miongoni mwa wananchi.
Viwango hivi vilivyowekwa vinatengeneza matabaka miongoni mwa wananchi, kitu ambacho ni hatari kwa mstakabali wa umoja wetu.
Au nasema uwongo ndugu zangu?
Baada ya 2025 wataanza thaminisha jengo kabisa unakatwa kupitia umeme au simu au maji hadi deni litimie
 
habari wakuu, leo nimekuja na mrejesho. niliwahi post humu mwezi uliopita kuwa nimekatwa 6,000 kama deni kodi ya majengo ilihali mimi mita yangu ina miezi miwili tu.

sasa mwezi huu (leo)nimenunua tena umeme nimekatwa 6,000 ikabidi nipige simu TANESCO majibu niliyopewa hakika yanavunja moyo.

jengo nimejenga mwaka huu, tangu likamilike halina hata miezi mitatu. lakini tanesco wameniambia hiyo 12,000 niliyokatwa kwa miezi miili nimelipia kodi ya jengo katika kipindi cha mwaka wa fedha kuanzia mwaka jana mwezi wa 7 au 8 hadi mwaka huu mwezi wa 7 au 8 mwaka wa fedha utakapoisha.

na wakati huo huo naambiwa kuanzia mwezi unaofuata nitakuwa nakatwa 1,000. sasa kama ni mwaka wa fedha na washachukua 12,000 tayari na mwaka wa fedha haujaisha mbona kama ntaliwa tena pesa au mimi ndio sijui mwaka wa fedha ni mwezi wa ngapi unaanza.

na kwanini nikatwe miezi ya nyuma ilihali sikuwa na jengo lolote.?
 
Tanesco ipo kwenye mikono salama mkuu...kipara Jana kapigiwa makofi mengi sana.
 
habari wakuu, leo nimekuja na mrejesho. niliwahi post humu mwezi uliopita kuwa nimekatwa 6,000 kama deni kodi ya majengo ilihali mimi mita yangu ina miezi miwili tu.

sasa mwezi huu (leo)nimenunua tena umeme nimekatwa 6,000 ikabidi nipige simu TANESCO majibu niliyopewa hakika yanavunja moyo.

jengo nimejenga mwaka huu, tangu likamilike halina hata miezi mitatu. lakini tanesco wameniambia hiyo 12,000 niliyokatwa kwa miezi miili nimelipia kodi ya jengo katika kipindi cha mwaka wa fedha kuanzia mwaka jana mwezi wa 7 au 8 hadi mwaka huu mwezi wa 7 au 8 mwaka wa fedha utakapoisha.

na wakati huo huo naambiwa kuanzia mwezi unaofuata nitakuwa nakatwa 1,000. sasa kama ni mwaka wa fedha na washachukua 12,000 tayari na mwaka wa fedha haujaisha mbona kama ntaliwa tena pesa au mimi ndio sijui mwaka wa fedha ni mwezi wa ngapi unaanza.

na kwanini nikatwe miezi ya nyuma ilihali sikuwa na jengo lolote.?
Mkuu hapo mbona ipo wazi kabisa kua unaibiwa wewe, hebu nenda ofisini ya tanesco uwaelezee vizuri achana na kupiga simu, yaani hii nchi Kuna mambo yanakera Sana aisee, halafu Kuna kitu nimenotice kwenye hiyo taarifa yao wanasema walikua hawana taarifa za watu wenye maghorofa mimi nadhani wanafanya trial and error wanamtoza mtu Bei ya ghorofa(6000) badala ya 1000 kwa mwezi usipolalamika wanaendelea kukutoza Kama mtu wa ghorofa ukilalamika wanakurudisha kawaida😃😃😃 maana kwa ninavyojua hii nchi hizo taarifa za ghorofa hawana na Kama wanategemea zile za sensa Basi huu usumbufu utaendelea Sana.
Mkuu Mimi nadhani kwenye system umewekwa Kama mtu wa ghorofa hebu fuatilia utashangaa ukiweka Tena unakatwa 6000.
 
Mkuu hapo mbona ipo wazi kabisa kua unaibiwa wewe, hebu nenda ofisini ya tanesco uwaelezee vizuri achana na kupiga simu, yaani hii nchi Kuna mambo yanakera Sana aisee, halafu Kuna kitu nimenotice kwenye hiyo taarifa yao wanasema walikua hawana taarifa za watu wenye maghorofa mimi nadhani wanafanya trial and error wanamtoza mtu Bei ya ghorofa(6000) badala ya 1000 kwa mwezi usipolalamika wanaendelea kukutoza Kama mtu wa ghorofa ukilalamika wanakurudisha kawaida😃😃😃 maana kwa ninavyojua hii nchi hizo taarifa za ghorofa hawana na Kama wanategemea zile za sensa Basi huu usumbufu utaendelea Sana.
Mkuu Mimi nadhani kwenye system umewekwa Kama mtu wa ghorofa hebu fuatilia utashangaa ukiweka Tena unakatwa 6000.
shukrani kiongozi itabidi nilitilie mkazo hili swala.
 
Back
Top Bottom