Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu

Sekta isiyi rasmi ni kubwa haitozwi kodi,acheni siasa kwenye kodi je mama ntilia,gereji bubu, mafundi washi locals nk wanatozwa kodi. Panua wigo wa walipa kodi na kisha msururu wa kodi upungue, muwe wabunifu na matumizi mabovu yadhibitiwe. Pesa kubwa iende kwenye maendeleo na siyo matumizi na kulipa madeni. No
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6


====
Pia soma:
Tatizo wananchi hatuoni faida ya kulipa kodi. Endapo kukiwa na matumizi sahihi ya kodi zinazokusanywa wananchi watahamasika wenyewe kulipa kodi. Watu wanakwepa ulipaji kodi kwasababu ya dhana kuwa fedha zinazokusanywa zinatumika vibaya

Kwa mfano hapo, mnajisifu kuongeza makusanyo bila kutuonyesha zimetumikaje. Miradi mingi ya maendeleo inaendeshwa na mikopo ambayo masharti yake Mh. Rais kashasema yanakera. Kodi zetu zinafanya kazi gani?
 
Kodi zetu ndio Maendeleo ya Taifa letu.

Mwaka 2021/22- Trillions 22.2.
Mwaka 2022/23- Trillions 24.1.
Mwaka 2023/24- Trillions 27.6


====
Pia soma:
Tatizo ni USIMAMIZI MBOVU wa miradi, mapato, ufisadi na uzembe. Uliona kile ki temporary camp cha bwawa la handeni? Uliona kile kibanda cha ofisa wa police pale tabora? Haya nambie kama pesa zinaliwa hovyo namna ile je hizo kod tunazolipa zinatusaidia vipi?
 
We nae ni Waziri wa Ajabu sana. Kodi haziwezi kuleta maendeleo kama mtaendelea kufanya overspendings zisizo na kichwa wala miguu, mfano mdogo tu Mnatumia takriban nusu trilioni(Kwa mujibu wa gazeti la mwananchi) kununua magari mapya kwa mwaka, hivi kwa nchi masikini kama Tanzania hizi ni akili au matope?
Mmetengeneza departements nyingi nyingi ambazo hazina umuhimu na zina uwezo wa kuwa merged kuwa departments moja.

Safari za nje kibao, Mnashindwa nini kutumia serikali mtandao mkafanya hivyovikao online ili kusave pesa za umma?

Serikali kwa kauli ya Mh Rais anakili kuna wizi(Japo wewe unakanusha) sasa unategemea hizo kodi zitafanya nini cha maana kama kuna upigaji?

Wewe kama kweli ni waziri msomi (Which I highly doubt) fanya yafuatayo.

1) Implement Zero Based Budgeting.
Kila idara ya serikali itengeneze bajeti yake from scratch acheni ku edit templates za previous years. Hii itasaidia kuondoa unnecesary expenditures

2) Cut Non-Essential Travel and Allowances.
Mambo mengine ni ya kujiongeza tu, badala ya kupeleka wasanii wanaoigiza ujinga ujinga nje, kwa nini hizo pesa msitumie kusomesha radiologist na kada nyingine za afya ambazo zina uhitaji wa hali ya juu (Value for Money)

3) Acheni upigaji na wapigaji wachukuliwe hatua, Miaka karibu miwili mfululizo CAG anaripoti madudu kibao lakini hakuna kinachoshughulikiwa(Kwanza ningekuwa CAG ningeshajiuzulu maana hizo ni dharau). Hivi hamuoni aibu unaiba pesa za umma ukanunue magari sijui ukajenge majumba ya kifahari I swear yatawatokea puani MUNGU HADHIHAKIWI.

4) Mnakusanya kodi kwa maguvu badala ya akili.
Unasema walipa kodi Tanzania ni chini ya asilimia 20 tu, umeshafanya tafiti ukajua kwanini asilimia 80 hawalipi kodi???? Mbona majibu yapo wazi?

5) Kama kweli mna uzalendo mawaziri wote (Ambao kimsingi ni wabunge) Mishahara yenu ya mawaziri ikatwe nusu na pia msilipwe kama wabunge.
Ile sheria ya kuwalipa wake wa vigogo wastaafu ni sheria ya kipuuzi ifutwe haraka sana (President Ruto amefuta huu ujinga). Sheria ziko wazi serikali haiwezi kufanya malipo mara mbili mbili kwa mtu mmoja huyo huyo mke wa mstaafu lakini yeye mwenyewe bado yupo bungeni au serikalini.

6) Magari ya kifahari sijui VXR sijui V8 mwisho kwa mawaziri na majaji basi.
Watumishi wengine sijui wakuu wa mikoa, sijui ma dc sijui RAS , DAS wote hao wapewe Totoya Vanguard au kama mnataka durability basi Land cruiser hardtop zinawafaa. Hii itasaidi kupunguza spendings zisizo na kichwa wala miguu. Imagine nchi masikini kama Tz RAS anatembelea gari ya 300M+ (Ila nyie mna dhambi nyie Mungu awasaidie sana mbadilike)

Yes tunajua nchi yetu haiwezi kujiendesha yenyewe kwa kutegemea bajeti ya ndani. Hii ni kweli kabisa sasa punguzeni matumizi yasio ya lazima, kamateni wabadhirifu, wekeni kodi rafiki kulingana na kipato cha mtu bila kumkandamiza, Haiwezekani niagize kifaa cha 30,000 Alibaba halafu kikifika mnataka nilipe kodi ya 30,000 yaani thamani ya kifaa ni sawa na kodi 🤣🤣🤣.

Kwa kifupi wewe baba uchumi wa nchi upo hovyo gharama ya maisha inapanda kila siku sijui mnataka yaje ya zimbabwe?
Spendings.png
 

Attachments

  • CAG.png
    CAG.png
    161.9 KB · Views: 2
  • Wizi Mtupu.jpg
    Wizi Mtupu.jpg
    121.6 KB · Views: 3
  • Wizi.jpg
    Wizi.jpg
    92.6 KB · Views: 2
  • Cars speninds.png
    Cars speninds.png
    42 KB · Views: 2
Mkiacha uvivu na tamaa binafsi mkaanza kuwafuatilia walipakodi wakubwa mapato yataongezeka zaidi ya hapo.

Punguzeni matumizi ya anasa kwenye kodizetu.
Tunachukizwa sana na ripoti za CAG zinazoonyesha matumizi mabaya ya kodizetu.
 
Back
Top Bottom