Kofi la mkunga kwa mama mjamzito limebeba ujumbe mzito; Wakunga wana mema mengi ya kusimulia

Kofi la mkunga kwa mama mjamzito limebeba ujumbe mzito; Wakunga wana mema mengi ya kusimulia

Kwa maelezo ya mashuhuda wanasema mkunga alimkata kofi mgonjwa kwakuwa mgonjwa alitaka kumuharibia kazi kwa kitendo cha kujifungulia chini
Kwanini asijifungulie kitandani ,,alikuwa mkorofi
 
Hata Mimi hapo zamani nilikuwa nawasema vibaya sana wakunga!

Ikanibidi nifanye utafiti; je lawama zile kwa wakunga Zinawastahili!?...
Hiyo ndio ukisikia siasa. Waache wafanye siasa kwenye secta ya afya wakisha wavuruga madaktar kilio kitasikika kwa wanannchi. Ccm mbele kwa mbele.
 
Halitabeba ujumbe kwa wale wajawazito walozoea pigwa kofi/vikofi na wapenzi wao wawapo 7 x 6

hasa wakati wa morning gloryyy 🤣🤣🤣 treni lishashika kasiii mara unasikia papap apapapap paaa
 
Mimi Kama mzazi mleta mada nimekuelewa mno.

Makosa kwa baadhi ya wakunga hayakosaniki, lakini kwa vile matokeo ya makosa yao athari zake zimekua ni ndogo Basi hukumu dhidi yao isiwe kubwa.

Hakuna kada isio kosea hata wachungaji wanakosea katika kazi zao za kichungaji mfao juzi tu mchungaji mmoja ameomba radhi kwa Uma kwa kukosea.

Lakini kukosea kwa kwake hakuiondolei thamani huduma au umuhimu wake, kadhalika na wakunga nao.

Wanachopaswa ni kupongezwa kutiwa mojo kupewa motisha na kusahihishwa.
 
Umesikiliza vizuri hii habari au umekurupuka? Kwa vile mkeo kakuletea mtoto tulia ulee mwanao usituletee ngojera hapa.
Hata sisi tumesikiliza usidhani umesikia peke yako, na wengine kwa kazi zetu tumefika Mazwi Sumbawanga pembeni mwa hospitali ya Mkoa kilipo Kituo cha Afya Mazwi na kupata maelezo toka pande zote mbili na kilichotokea kinaakisi maneno ya mleta mada.

1.Uchache wa wauguzi uliopelekea muuguzi kuwa na wajawazito 20+ kwa usiku mmoja na 9 kati yao wakazalishwa na mkunga huyo.

2.Kutojua nini cha kufanya kwa mjamzito husika huku mkunga akitarajia mjamzito kujiongoza katika baadhi ya mambo ili aweze kuhudumia wengine pia. Yaani kutokana na kuwa peke yake alitarajia kufanya kazi kwa kutoa maelekezo zaidi badala ya kuwa delivery assistant.

3.Majibu ya karaha toka kwa mjamzito yaliyomkarahisha Mkunga hadi kufikia kumpiga kofi.

4.Kukosa uvumilivu kwa Mkunga kulikotokana aidha uchovu, hasira za kibinadamu.

5.Mbali ya Kofi alilomtandika mzazi yule lakini bado alifanya kazi yake vizuri kwa kumzalisha na kumpa huduma bora mtoto aliyezaliwa na mapungufu baada ya kunywa maji machafu na kwa sasa anaendelea vizuri.

NB: Binafsi nampa pole Mkunga yule na Wakunga wengine kwa madhira wanayokutana nayo toka kwa kina mama wajawazito lakini bado wanavumilia na kuwazalisha pasipo kuwaacha waumize viumbe walioko tumboni.

Nampa pole mama yule mzazi Kwa "Kofi" alilotandikwa ambalo halikuwa na madhara kwake kama uchungu aliokuwa anapata kabla ya kujifungua. Namsihi azingatie tuliyomwambia wakati tunaongea naye; "AMSAMEHE MKUNGA YULE" na ajenge urafiki na Wauguzi kwani bado ana safari ndefu ya maisha atakayojaliwa na Mwenyezi Mungu na katika maisha yake bado ataendelea kuwahtaji Wakunga, Wauguzi na Madaktari ambao ni kitu kimoja katika utendaji wa kada muhimu ya Afya.
 
Mimi Kama mzazi mleta mada nimekuelewa mno...
Ingekuwa kosa la mmoja wamehukumiwa wote ningekuelewa ila kama anahukumiwa aliyekosea hakuna shida, siijui jinsia yako ila kama we ni mwanamke nadhani unajua machungu mnayopitia wakati wa kujifungu, wengi wenu hadi mnapoteza maisha kisa kujifungua sasa fikiri mtu anakusindikiza na kofi
 
Hata sisi tumesikiliza usidhani umesikia peke yako, na wengine kwa kazi zetu tumefika Mazwi Sumbawanga pembeni mwa hospitali ya Mkoa kilipo Kituo cha Afya Mazwi na kupata maelezo toka pande zote mbili na kilichotokea kinaakisi maneno ya mleta mada...
Well said
 
Nakubaliana na ww wanawake wengi hupigwa makofi mapajani na wakunga pale wanapobana mapaja hali inayoweza kusababisha mtoto kubanwa na mapaja na kupoteza maisha.

Pia kuna wanawake hawataki ku push wakati mtoto ameshatoa kichwa hali inayopelekea mtoto kubanwa kichwa hapo mkunga analazimika kumchapa kofi ili kumshtua apush mtoto atoke. Chunguza watoto wengi wana mstari Katikati ya vichwa vyao sababu ya kubanwa na mama zao.


Ukiacha adha ya kushughulika na maji machafu pamoja na vinyesi kutoka kwa mama mjamzito, wakunga wanapambana sana na makofi yale huwa ni kwa faida ya mama na mtoto. HAKIKA WANASTAHILI PONGEZI
 
Kwa hiyo kama anafanya kazi katika mazingira magumu hasira zake ndio ahamishie kwa wamama wenye uchungu?

Wakati anasomea hiyo hakujua anaenda kukutana na mazingira gani?

So Pathetic.
 
Kwa hiyo kama anafanya kazi katika mazingira magumu hasira zake ndio ahamishie kwa wamama wenye uchungu?

Wakati anasomea hiyo hakujua anaenda kukutana na mazingira gani?

So Pathetic.
Ndiyo
 
Hata mimi hapo zamani nilikuwa nawasema vibaya sana wakunga!

Ikanibidi nifanye utafiti; je lawama zile kwa wakunga zinawastahili!?

Katika chunguza chunguza niliweza kufika kwenye hospitali moja kama mme wa mzazi mmoja aliyekuwa leba kusubili kujifungua!

Nilifanikiwa kuwa karibu sana na mkunga kiasi kwamba nilishuhudia mambo magumu sana wakunga wanayokutana nayo!

Hebu fikiria mkunga mmoja anategemewa kuzalisha wanawake karibu 20 au zaidi!

Ndani kundi hilo la wajawazito!

Kila mjamzito aliyeleba anastyle mbalimbali ya kuugulia uchungu wake!
  • Kuna wale wajawazito mimba zao za kwanza wasioelewa hata kupush
  • Kuna wapo wajawazito wanaopush na kujamba pamoja
  • Kuna wale wajawazito wanaopayuka na kutukana hovyohovyo wodini
  • Kuna wale wanaowatukana waume zao kwa kuwataja majina wakiwa leba,...mfano utasikia; wee Mudy ulini.......mba ukanipa mimba, sahivi uko huko unakula raha na mahawala wengine, wee muddy Malaya mkubwa!...oooh Muddy wee mwanaume hufai kabisa, ona ninavyotaabika....etc
  • Wapo wanaoingia uvunguni mwa kitanda wanapomuona mkunga kaingia!
  • Wapo wanaobana mapaja kiasi cha kuhatarisha maisha ya mtoto na ni wabishi wanapoelekezwa
  • Wapo wanasikilizia maumivu ya maji ya uchungu kiasi cha kusahau maelekezo ya mkunga!
  • Wapo wajawazito wanadiliki kutukana hadi wakunga n.k
Hebu fikiria kufanya kazi katika mazingira magumu kama hayo!

Jamii imekuwa ya lawama sana kiasi cha kukumbatia matukio yanayoonekana mtandaoni!

Mtakumbuka Askari zimamoto kule Kigoma alivyopongezwa na kupewa promotion kwa kuokoa mtoto kutoka kwenye shimo la choo!.

Askari ambaye kila siku anafanya mazoezi ya kushuka au kupanda na kamba, hivyo kuokoa ni wajibu wa kazi yake kama kazi zingine!

Hatukatai kuwapongeza, lakini nachotaka kusema hapa, ni vile jamii inamuona shujaa ni huyo askari anaeshuka na kamba kuopoa mtoto shimoni, lakini jamii ileile inamsimanga mkunga aliyeopoa kichanga kutoka tumboni!

ikumbukwe kosa moja tu la mkunga linasababisha kumkosa mama na mtoto au kupata mtoto kilema!

Sasa katika mazingira magumu ya kazi mkunga akipitiwa kidogo tu kumuweka sawa mama mjamzito inakuwa story!

Kwanini hatuwapi promotion WATU kama hawa? Kwanini hatuweki hata dodoso la siri kwa kila mjamzito anaejifungua ajaze max na jina la mkunga anaeona huduma yake ni nzuri hata tukawapongeza watu hawa?
Ebu fikiria mtu kutwa anagusa sehemu za siri tupu za kila aina!

Ebu vaeni uhusika wa ukunga japo siku moja, halafu mlipwe kwa LAWAMA muone mtajisikiaje!

Kama hatuwezi kuwapunguzia Msongamano Wakunga mahospitalini basi tuwape japo faraja na maneno ya shukrani!

ingekuwa Amri yangu! Wakunga wote ningewapa Special Allowance kila mwezi!
Basi sawa wakunga wote peponi au nasema uongo ndugu zangu ?
 
Hata sisi tumesikiliza usidhani umesikia peke yako, na wengine kwa kazi zetu tumefika Mazwi Sumbawanga pembeni mwa hospitali ya Mkoa kilipo Kituo cha Afya Mazwi na kupata maelezo toka pande zote mbili na kilichotokea kinaakisi maneno ya mleta mada.

1.Uchache wa wauguzi uliopelekea muuguzi kuwa na wajawazito 20+ kwa usiku mmoja na 9 kati yao wakazalishwa na mkunga huyo.

2.Kutojua nini cha kufanya kwa mjamzito husika huku mkunga akitarajia mjamzito kujiongoza katika baadhi ya mambo ili aweze kuhudumia wengine pia. Yaani kutokana na kuwa peke yake alitarajia kufanya kazi kwa kutoa maelekezo zaidi badala ya kuwa delivery assistant.

3.Majibu ya karaha toka kwa mjamzito yaliyomkarahisha Mkunga hadi kufikia kumpiga kofi.

4.Kukosa uvumilivu kwa Mkunga kulikotokana aidha uchovu, hasira za kibinadamu.

5.Mbali ya Kofi alilomtandika mzazi yule lakini bado alifanya kazi yake vizuri kwa kumzalisha na kumpa huduma bora mtoto aliyezaliwa na mapungufu baada ya kunywa maji machafu na kwa sasa anaendelea vizuri.

NB: Binafsi nampa pole Mkunga yule na Wakunga wengine kwa madhira wanayokutana nayo toka kwa kina mama wajawazito lakini bado wanavumilia na kuwazalisha pasipo kuwaacha waumize viumbe walioko tumboni.

Nampa pole mama yule mzazi Kwa "Kofi" alilotandikwa ambalo halikuwa na madhara kwake kama uchungu aliokuwa anapata kabla ya kujifungua. Namsihi azingatie tuliyomwambia wakati tunaongea naye; "AMSAMEHE MKUNGA YULE" na ajenge urafiki na Wauguzi kwani bado ana safari ndefu ya maisha atakayojaliwa na Mwenyezi Mungu na katika maisha yake bado ataendelea kuwahtaji Wakunga, Wauguzi na Madaktari ambao ni kitu kimoja katika utendaji wa kada muhimu ya Afya.
Shukrani kwa ufafanuzi wa kina mkuu
 
Heshima kwa wakunga woote...usitukane wakunga na uzazi ungalipo...unakuta mtu anajifanya anorld shwaziniga na kutukana wakunga wakati hata mtoto wa kusingiziwa Hana.
 
Kwa maelezo ya mashuhuda wanasema mkunga alimkata kofi mgonjwa kwakuwa mgonjwa alitaka kumuharibia kazi kwa kitendo cha kujifungulia chini
Na hayo matamshi wanayo wengi, pale Makole maabara kuna namba ya simu mlangoni wengi hawajui Ile namba ni ya Nani, ukifika maabara unaweza usimkute mtu pale ndani nasemea wakati wa usiku kumbe labda yupo anawajibika huko ndani au ametoka unakaa kumsubiri haji Kwa vile kuna namba mlango unaamua kupiga [emoji15] kosa umempigia boss naye anamtafuta. Hapo sasa umelianzisha cha kwanza atakuuliza Kwa nini usimuulize mlinzi hapo getini, unataka kuniharibia kazi, sasa kuna huyu mama ananongwa kila akikuona lazima akumbushie namwambia hivi ipo siku nitamrekodi halafu namuonyesho huyo boss wake na hanioni tena Makole, Bora angekuwa ndani lakini katokea maeneo ya getini, hospital zipo nyingi.
 
Back
Top Bottom