Komandoo ni Cheo au ni mtu wa namna gani?

Komandoo ni Cheo au ni mtu wa namna gani?

Komandoo ni mtu aliyepitia kozi maalumu ya mafunzo ya kijeshi.
Kozi hiyo hufanyika baada ya askari kupitia mafunzo ya kozi ya awali(Recruits training schoo au RTS).

RTS kwa sasa ni RTS Oljoro na RTS Msata(Kihangaiko), ile RTS ya Makutupola Dodoma ilishasitishwa.

Baada ya RTS ndio baadhi ya askari huchaguliwa kwenda kujifunza mafunzo maalumu ya ukomandoo(kwa ufupi hawa ndo high level trained soldiers), kozi yao ni 92KJ Ngerengere hapo Morogoro.

Sitaki swali zaidi ya hapo.
Lengo la maelzo yko ni kujbu hoja ikiwa maelzo yko hayajajitoshelza kwa nn hutaki swali?
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Komando na special force ni kitu kimoja? Mimi sijui lakini sidhani kama ni sahihi..ngoja nisubiri wataalamu
Sio kila special force ni komandoo.

Special force ni watu maalumu waliobobea katika jambo flani, ambapo wao ndio huhitajika kwa ajili ya kukabiliana na tukio lolote linalohusiana na eneo ambalo wao ni wataalamu.

Kwa mfano FFU ni special force kwa polisi kazi yao ni kutuliza ghasia( Field Force Unit).

Magereza wana special force( wanaita special task force au kikosi maalumu cha kutuliza ghasia magerezani-KMKGM).

Jwtz ndio kuna Komandoo ambao ni special task force kwa ajili ya vita nchi mbali mbali (wanaenda missions pia), kwa ufupi komandoo ndio wanajeshi waliopitia mafunzo ya hali ya juu zaidi kuzidi wanajeshi wa kawaida, nao pia wamegawanyika kuna waliojikita katika ukomandoo wa majini(Navy), kuna ambao ni ni wataalamu wa angani na pia kuna wataalamu wa vita ya ardhini lakini wote ni komandoo, kiufupi wao ndio hujifunza karibia kila kitu kuhusu vita na defence.

Kwa sababu ya kuwepo kwa viwango tofauti tofauti vya elimu kuna komandoo ni askari wa kawaida(private mpaka warranty officers) pia kuna maafisa ni komandoo(Luteni usu mpaka Luteni General au hata General kabisa)
Kama hujaelewa uliza mkuu
 
Jeshi na mitandao wapi na iweje?
Jiangalie
Jeshi liko wapi?
Haya ni mambo ambayo hata ukigoogle unayapata sasa wasiwasi wako nini?

Ni kitu gani nilichoandika hapa kinachoshangaza eti? Kuna siri gani niliyoandika hapa?
Haya mambo nayajua kawaida wala sio kupitia jeshini, jisomee ni vitu viko online.
 
Komandoo ni mtu aliyepitia kozi maalumu ya mafunzo ya kijeshi.
Kozi hiyo hufanyika baada ya askari kupitia mafunzo ya kozi ya awali(Recruits training schoo au RTS).

RTS kwa sasa ni RTS Oljoro na RTS Msata(Kihangaiko), ile RTS ya Makutupola Dodoma ilishasitishwa.

Baada ya RTS ndio baadhi ya askari huchaguliwa kwenda kujifunza mafunzo maalumu ya ukomandoo(kwa ufupi hawa ndo high level trained soldiers), kozi yao ni 92KJ Ngerengere hapo Morogoro.

Sitaki swali zaidi ya hapo.
Hutaki swali tena mkuu, umenichekesha.
 
Niongezee kidogo; baada ya RTS baadhi ya askari uchaguliwa kwenda 92kj ngerengere kupata mafunzo ya ukomandoo. Kule ngerengere watapata mafunzo ya awali kwa miezi 18 kwa kupitia vikosi vya jwtz kama Maji; anga; mizinga; nchi kavu na mengine kwa miezi mitatumitatu kwenye kila vikosi ili kua familia na hizo maeneo.

Baadae nitarudi kwa cheo kama full mbawa na half mbawa.
 
Sio kila special force ni komandoo.

Special force ni watu maalumu waliobobea katika jambo flani, ambapo wao ndio huhitajika kwa ajili ya kukabiliana na tukio lolote linalohusiana na eneo ambalo wao ni wataalamu.

Kwa mfano FFU ni special force kwa polisi kazi yao ni kutuliza ghasia( Field Force Unit).

Magereza wana special force( wanaita special task force au kikosi maalumu cha kutuliza ghasia magerezani-KMKGM).

Jwtz ndio kuna Komandoo ambao ni special task force kwa ajili ya vita nchi mbali mbali (wanaenda missions pia), kwa ufupi komandoo ndio wanajeshi waliopitia mafunzo ya hali ya juu zaidi kuzidi wanajeshi wa kawaida, nao pia wamegawanyika kuna waliojikita katika ukomandoo wa majini(Navy), kuna ambao ni ni wataalamu wa angani na pia kuna wataalamu wa vita ya ardhini lakini wote ni komandoo, kiufupi wao ndio hujifunza karibia kila kitu kuhusu vita na defence.

Kwa sababu ya kuwepo kwa viwango tofauti tofauti vya elimu kuna komandoo ni askari wa kawaida(private mpaka warranty officers) pia kuna maafisa ni komandoo(Luteni usu mpaka Luteni General au hata General kabisa)
Kama hujaelewa uliza mkuu
Kwa hyo commando haiangalii level ya elimu yake,ni mafunzo tu bhas??
 
  • Thanks
Reactions: SDG
Kwa hyo commando haiangalii level ya elimu yake,ni mafunzo tu bhas??
ukomandoo ni mafunzo ya medani za kivita, asikari jeshi anaweza kuwa komando ilihali hana cheo chochote yaani private, lakini pia katika mission za kijeshi anayeongoza platoon yoyote ya makomandoo lazima awe amewazidi cheo cha uafisa wale makomandoo anaowaongoza kwenye mission,

Pia ifahamike kuwa asikarijeshi kuwa komando hakumuweki kuwa juu ya maafisa wengine walio juu yake hata kama sio komando, komando ni kikosi ndani ya jeshi hivyo wako chini ya wakuu wa vikosi na kamandi husika.
kazi ya kikosi cha komandoo ni kufanya missions ngumu, kwenye mazingira magumu na hatari ( ambapo asikarijeshi wa kawaida hawezi kutekeleza jukumu hilo) na haraka zaidi ( commando is a time keeper personnel).

kuna madaraja ya ukomandoo, hapa Tanzania vijana kutoka RTS yaani shule za mafunzo za jwtz huchukuliwa na maafisa wa jwtz kutoka kikosi cha komando kwa kuzingatia uimara, mwonekano, nidhamu, saikolojia n.k, vijana hawa hupelekwa kwenye mafunzo ya komando daraja la tatu (commando level 3) pale Ngerengere- sangasanga 92kj- Morogoro kwa miezi 18, baada ya hapo hupelekwa course za kiutendaji vitani. Ila hapa komando anakuwa na nusu mbawa.

by Lt.saguda (a mythical name)
 
Komandoo na special forces ni kitu kimoja.
Wenzetu kule wanaita special force sisi huku tjnaita komando... komando ni jina lilikuwa likitumika zamani.


Mafunzo haya huchukua muda gani, tangu kipyenga cha kwanza kupulizwa kuanza mafunzo mpaka kipyenga cha mwisho kumaliza mafunzo. Je kuna muda wanyongeza na mafunzo yana viwango vya kimataifa au kila nchi ni kivyake vyake.? Ila N.Korea ni wazi wao ni wakipekee.


Na washawasha!
 
Back
Top Bottom