Kombe la Shirikisho Barani Afrika 'CAF' Azam FC dhidi ya Triangle United, Wazimbabwe Lazima Wakae!

Kombe la Shirikisho Barani Afrika 'CAF' Azam FC dhidi ya Triangle United, Wazimbabwe Lazima Wakae!

Patashika ya Kombe la Shirikisho Soka Barani Afrika, Kuendelea kutimua vumbi leo Jumapili ya September 15, 2019 ambapo wawakilishi wa Tanzania Azam FC wakiwakaribisha Triangle United ya kutoka nchini Zimbabwe kwenye Uwanja wa nyumbani wa Azam Complex.

Azam FC walisonga mbele kufikia hatua hii baada ya kuitoa Fasil Kenema ya Ethiopia kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya mechi ya awali iliyopigwa nchini Ethiopia ambapo Fasil Kenema waliibuka na ushindi mwembamba wa bao 1-0 na kufuatia mechi iliyopigwa jijini Dar es salaam ambapo Azam FC walitakata kwa ushindi wa mabao 3-1.

Mchezo huu ni burudani ya pekee wiki hii kwenye Kombe la Shirikisho, burudani ambayo si ya kukosa ewe Mzalendo, Mshabiki, Mwanachama na Mdau wa Kandanda, kwani Azam FC ndo wawakilishi wetu Kimataifa hapa nchini Tanzania, hivyo basi twendene kwa wingi tukaujaze Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Mbagala na kuwashangili vilivyo wawakilishi wetu wa ukweli Azam FC.

Wazimbabwe Lazima Wakae.....!KwaHisaniYaNguvuMoja..!Usikose Ukaambiwa, kumbuka mchezo ni kuanzia saa 10:00 jioni.View attachment 1208104View attachment 1208106
Shida nikwamba wanaungwa mkono nawenye mikosi yao
 
Azam FC 0-1 Triangle United...!

Dakika zinayoyoma huku matumaini yakiwa hafifi kupata bao, lakini mpira dakika 90'
 
Mchezo tunaoweza ni kuwa mawakala wa MABEBERU tu, mingine hatuwezi.
 
80' Chirwa anakwendaaaaa, Off Side..Mwamuzi msaidizi kibedera kiko juu
Mungu ibariki Azam FC
 
85' Namna gani hapa Salum Abubakar anapoteza mpira kirahisi, pressure ni kuwa kwa wenyeji, huku faida kwa Triangle
 
Kwa Tanzania hii ndo hatua ya mwisho kwa timu za Tanzania
 
90+5'

Kuelekea kumalizika kwa mchezo huu wa kombe la Shirikisho Afrika CAF.

Azam FC 0-1 Triangle United
 
90'+5'

Naaaaaaaaaaaaaaam...Mpira umekwisha uwanja wa Azam Complex, ambapo Azam FC wakipoteza kwa kufungwa bao moja bila majibu lililofungwa na Nahodha Ralph Kawondera

Mategemeo pekee yapo kwenye mechi ya marudiano huko Zimbabwe..!huenda Azam FC wakapindua matokeo

Azam FC 0-1 Triangle United

Asanteee sanaaaaa wako Ghazwat
 
Back
Top Bottom