Kongamano la Wahariri limeacha maswali mengi. Nani yuko nyuma?

Kongamano la Wahariri limeacha maswali mengi. Nani yuko nyuma?

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Kongamano la Wahariri naweza kusema limeacha maswali mengi sana kuliko mafanikio tuliyotarajia tuyaone kutokea hapo.

1. Nani aliyewalipa posho na malazi kwa siku zote walizokaa Iringa(Yeye mlipaji ananufaikaje kwa fedha zake alizotoa)

2. Wametajwa wabunge, majaji, mawaziri kuwa ndio wanalimiki Ranchi ya Usangu je ni Kweli Ranchi ya Usangu inamilikiwa na watu binafsi au Serikali? ukweli ukoje kwenye hili. (Kwanini hadi leo wameshindwa kutaja majina yao)

3. Wametajwa watu wanaotumia maji ya mto Ruaha kwa shughuli za Kilimo, je Sheria inasemaje kuhusu wanaotumia maji? ziko Water Use Permit zinazotolewa na Mamlaka za Kiserikali za Mabonde ya Mito chini ya Wizara ya Maji na zinalipiwa ada nadhani kila mwaka kama sikosei.

Kosa la hao wenye vibali vya kutumia maji liko wapi? kwanini watangazwe kwamba ni wahalifu ilihali wanatumia maji kisheria na kama mtu anatumia maji bila kibali sheria inasemaje?

4. Kuna Fununu kwamba Kongamano hilo limeandaliwa mahususi kuwahadaa watanzania kwamba Mradi wa Bwawa la JNHPP hautafanya kazi hata kama utakamalika kwa sababu maji ya mto Ruaha yamekaushwa na wakulima na wafugaji.

5. Point Namba 4 ndio inatajwa sana kufadhili kongamano na kundi hilo hilo hilo la wahariri ndio kila leo linakwenda kwenye Mradi wa JNHPP na kusifia kwamba hakuna kilichosimama.

Huku wakitambua mradi huo umecheleweshwa na mkandarasi kwa miaka 2na una mambo mengi yanahitaji majibu kuhusu shilingi Trilioni 1.5 ambazo mkandarasi alipaswa kuilipa Serikali kwa kuchelewesha mradi kwa mujibu wa mkataba.

Maswali ambayo Kina Balile na Kina Pascal Mayala licha ya kuwa Wanasheria wabobevu wameshindwa kuyauliza kwenye mamlaka husika hadi leo na hatujui kwanini wanafanya hivyo?

Kwa ufupi Wahariri wote wameandaa kongamano hilo ili kutengeneza hadaa na kuwaandaa kisaikolojia watanzania li kufanikisha lengo lao la kuonyesha tatizo la umeme halitakwisha leo wala kesho ili zile biashara zingine za Majenereta na Mikataba mingine iendelee ya kuiuzia umeme Tanesco. kwa kigezo cha kukosekana maji

Uthibitisho ya hayo siku chache Kabla ya Kongamano hilo, Mwenyekiti wa MERICA, Habib Mchange alifanya PRESS alitamka kwamba tutamlaumu Januari Makamba umeme wa mgao atafanya nini kama maji Ruaha hayapo?

MERICA imeshindwa kuuliza kwa nini umeme haukukatika katika kipindi chote cha miaka 6 iliyopita je hali ya ukame imekuja tu baada ya Januari kuwa Waziri? na je kuhusu madai ya baadhi ya watumishi wasio waadilifu wa TANESCO kufungulia maji ya Mabwawa ili yasijae kuzalisha umeme nalo kwa nini halizungumziwi.

Kwanini wazungumziwe kundi moja tu la wakulima na wafugaji ndio waliomaliza maji? na je miaka yote 6 ambayo umeme ulikuwa haukatiki wafugaji na wakulima waliacha shughuli za kilimo na ufugaji? kwanini maswali hayo hayapati nafasi? na kwanini kongamano hilo halikuwashirikisha wakulima na wafugaji kupitia vyama vyao kama MVIWATA na Chama cha Wafugaji Tanzania.

Tuendelee kutafakari kwa pamoja kuhusu kongamano hili na mambo yaliyojificha nyuma ya pazia ila uzuri duniani hakuna siri hasa jambo likishashirikisha watu zaidi ya mmoja na Makamu wa Rais ukweli aliofichwa ataufahamu.

Rejea nyingine muhimu juzi Waziri wa Nishati, Januari Makamba alinukuliwa akisema itahitajika misimu 2 ya mvua kujaza bwawa la nyerere.

Saidoo25.

 
mimi pia nilijiuliza maswali mengi sana, ila ukweli utajulikana ngoja waje wajuzi wa mambo wasaidie uchambuzi huu mujarab. ila mtoa post nakupa kongole kwa uchambuzi makini sana. KINA BALILE, MCHANGE, KITENGE waje na maelezo
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Siku nikifa, naomba nizikwe na bendera ya Tanzania. Hata nikiwa na dhambi nyingi kiasi gani, malaika wakiiona bendera , hawatoruhusu nipelekwe jehanamu kwa sababu huku nilikotoka ni jehanamu tosha!

Kwanini niwekwe jehanamu mara mbili?
 
Huu mradi wa umeme wa JNHPP hauwezi kamwe kukamilika na kutoa umeme kwasabb ni tishio kwa donor countries na wasakatonge wa ndani ya nchi.

JPM alisimama kidete kwenda kinyume na matakwa ya hizi "nchi wafadhili". Ikumbuke hata kampuni inayojenga bwawa hili ilitishwa kuwa itapigwa marufuku kufanya kazi nyingine tena sehemu yoyote duniani.

Na ndiyo maana JPM kabla hajafariki ilitangazwa kuwa maji yataanza kujazwa bwawani tarehe 15 Novemba 2021. Alipofariki tu danadana zikaanza na tukaambiwa bwawa liko chini ya 40%.

Sasa tunaambiwa bwawa litajazwa kwa miaka 2. Uliona wapi? Wameandaa drama nyingine katikati ya hiyo miaka 2.

Dunia hii Ina mengi Sana. Tukae tukijua mradi huu haupendwi na wazungu. Na wasilo litaka halitekelezeki ktk nchi hizi za Afrika.
 
Kuna Fununu kwamba Kongamano hilo limeandaliwa mahususi kuwahadaa watanzania kwamba Mradi wa Bwawa la JNHPP hautafanya kazi hata kama utakamalika kwa sababu maji ya mto Ruaha yamekaushwa na wakulima na wafugaji.
 
Huu mradi wa umeme wa JNHPP hauwezi kamwe kukamilika na kutoa umeme kwasabb ni tishio kwa donor countries na wasakatonge wa ndani ya nchi.

JPM alisimama kidete kwenda kinyume na matakwa ya hizi "nchi wafadhili". Ikumbuke hata kampuni inayojenga bwawa hili ilitishwa kuwa itapigwa marufuku kufanya kazi nyingine tena sehemu yoyote duniani.

Na ndiyo maana JPM kabla hajafariki ilitangazwa kuwa maji yataanza kujazwa bwawani tarehe 15 Novemba 2021. Alipofariki tu danadana zikaanza na tukaambiwa bwawa liko chini ya 40%.

Sasa tunaambiwa bwawa litajazwa kwa miaka 2. Uliona wapi? Wameandaa drama nyingine katikati ya hiyo miaka 2.

Dunia hii Ina mengi Sana. Tukae tukijua mradi huu haupendwi na wazungu. Na wasilo litaka halitekelezeki ktk nchi hizi za Afrika.
1. Mkuu labda tusaidiane kwanini wazungu hawapendi mradi huo ilihali ndio hao hao sio tu wametukopesha tujenge ila wanatuuzia vifaa na teknolojia??

2. Ndani ya nchi kina nani hawataki Bwawa liishe? Mbona umeme wa Tanzania kwa 60% unategemea gesi kwanini wasihujumu gesi ambayo ni gharama zaidi ila wahujumu umeme wa Maji ambao ni cheap? Yaani why uhujumu 40 percent uache 60 percent?

Nadhani ifike mahala tuchukue responsibility wenyewe maana hii tabia ya kusakizia Kila kitu mabeberu kwa failure zetu wenyewe hazitusaidii lolote.
 
Kwa ufupi Wahariri wote wameandaa kongamano hilo ili kutengeneza hadaa na kuwaandaa kisaikolojia watanzania li kufanikisha lengo lao la kuonyesha tatizo la umeme halitakwisha leo wala kesho ili zile biashara zingine za Majenereta na Mikataba mingine iendelee ya kuiuzia umeme Tanesco. kwa kigezo cha kukosekana maji.
Mkuu naomba niulize jambo maana hii issue ya kwamba mgao inatengenezwa Ili majenereta ama mikataba ya IPTL/DOWANS irudi inarudiwa rudiwa Sana.

Tanzania kwenye mpango wa taifa imeeleza kufocus kwenye energy mix yaani umeme sio tu kupitia Maji ila gesi, joto ardhi, upepo, solar n.k Sasa wote tunafahamu focus ipo kwenye gesi in fact Kinyerezi 3 Iko mbioni kujengwa Ili gesi izidi kuongeza mchango wake kwenye umeme.

Sasa wote tunafahamu zaidi ya 60% za umeme wa Tz unategemea gesi sio Maji na pia umeme wa gesi ni gharama sana kufua kuliko wa Maji.

1. Je kwanini wapiga Dili wasihujumu gesi maana ndio tegemeo kwenye umeme Tz?

2. Maintenance ya Bomba/mitambo ya gesi ni gharama kuliko umeme wa Maji kwanini wasihujumu gesi wavune mabilion?

3. Pia majenereta Yana faida kiasi gani Hadi yarudishe cost za mgao? Sababu hata hao mafisadi Wana viwanda/mashamba/mahoteli n.k?

Ntashukuru kwa majibu yenu
 
Mkuu naomba niulize jambo maana hii issue ya kwamba mgao inatengenezwa Ili majenereta ama mikataba ya IPTL/DOWANS irudi inarudiwa rudiwa Sana.

Tanzania kwenye mpango wa taifa imeeleza kufocus kwenye energy mix yaani umeme sio tu kupitia Maji ila gesi, joto ardhi, upepo, solar n.k Sasa wote tunafahamu focus ipo kwenye gesi in fact Kinyerezi 3 Iko mbioni kujengwa Ili gesi izidi kuongeza mchango wake kwenye umeme.

Sasa wote tunafahamu zaidi ya 60% za umeme wa Tz unategemea gesi sio Maji na pia umeme wa gesi ni gharama sana kufua kuliko wa Maji.

1. Je kwanini wapiga Dili wasihujumu gesi maana ndio tegemeo kwenye umeme Tz?

2. Maintenance ya Bomba/mitambo ya gesi ni gharama kuliko umeme wa Maji kwanini wasihujumu gesi wavune mabilion?

3. Pia majenereta Yana faida kiasi gani Hadi yarudishe cost za mgao? Sababu hata hao mafisadi Wana viwanda/mashamba/mahoteli n.k?

Ntashukuru kwa majibu yenu
Kwani wanao uza Majenereta si ndiyo kikosi ichoicho kinachofanya Biashara ya gesi!!
 
2023 ni mwaka wa kufungua CODES,

Mambo ya Siri I yakakuwa peupeee!

Hata code ya HIV yaweza kuwa wazi.

Tusubiri.
 
Kwani wanao uza Majenereta si ndiyo kikosi ichoicho kinachofanya Biashara ya gesi!!
Ndio nauliza kwanini wasihujumu gesi maana maintenance ya Bomba tu itacost mabilion na itazima 60% ya umeme why wahangaike na 40% ya umeme wa Maji ambao maintenance Yao ni ndogo?

Tusaidiane hapo
 
2. Ndani ya nchi kina nani hawataki Bwawa liishe? Mbona umeme wa Tanzania kwa 60% unategemea gesi kwanini wasihujumu gesi ambayo ni gharama zaidi ila wahujumu umeme wa Maji ambao ni cheap? Yaani why uhujumu 40 percent uache 60 percent?
Mkuu bila serikali kusimama kidete na kuacha kufauta matakwa ya hawa wazungu hilo bwawa litapigwa danadana Sana.

Kujibu swali lako kwann hawataki likamilike? Kukamilika kwa bwawa hilo kutamaanisha uhakika wa umeme tena wenye gharama nafuu na hivyo kichochea shughuli za kiviwanda na kukua kwa uchumi. Kitu ambacho kitapunguza utegemezi wa Tanzania kwa hawa donor countries. Ndiyo maana wanaleta za kuleta.

Kwann hahujumu umeme wa gesi? Umeme wa gesi uzalishaji wake unahitaji teknolojia ya hali ya juu sana na mitambo ya kisasa na gharama yake ni kubwa pia umeme wake ni ghali.

Tunayo hiyo teknolojia na hiyo mitambo? Jibu ni hapana. Kwahiyo hakuna ukombozi wowote wa kiuchumi kupitia umeme wa gesi. Tutaendelea kuwategemea
 
Kongamano la Wahariri naweza kusema limeacha maswali mengi sana kuliko mafanikio tuliyotarajia tuyaone kutokea hapo.

1. Nani aliyewalipa posho na malazi kwa siku zote walizokaa Iringa(Yeye mlipaji ananufaikaje kwa fedha zake alizotoa)

2. Wametajwa wabunge, majaji, mawaziri kuwa ndio wanalimiki Ranchi ya Usangu je ni Kweli Ranchi ya Usangu inamilikiwa na watu binafsi au Serikali? ukweli ukoje kwenye hili. (Kwanini hadi leo wameshindwa kutaja majina yao)

3. Wametajwa watu wanaotumia maji ya mto Ruaha kwa shughuli za Kilimo, je Sheria inasemaje kuhusu wanaotumia maji? ziko Water Use Permit zinazotolewa na Mamlaka za Kiserikali za Mabonde ya Mito chini ya Wizara ya Maji na zinalipiwa ada nadhani kila mwaka kama sikosei.

Kosa la hao wenye vibali vya kutumia maji liko wapi? kwanini watangazwe kwamba ni wahalifu ilihali wanatumia maji kisheria na kama mtu anatumia maji bila kibali sheria inasemaje?

4. Kuna Fununu kwamba Kongamano hilo limeandaliwa mahususi kuwahadaa watanzania kwamba Mradi wa Bwawa la JNHPP hautafanya kazi hata kama utakamalika kwa sababu maji ya mto Ruaha yamekaushwa na wakulima na wafugaji.

5. Point Namba 4 ndio inatajwa sana kufadhili kongamano na kundi hilo hilo hilo la wahariri ndio kila leo linakwenda kwenye Mradi wa JNHPP na kusifia kwamba hakuna kilichosimama.

Huku wakitambua mradi huo umecheleweshwa na mkandarasi kwa miaka 2na una mambo mengi yanahitaji majibu kuhusu shilingi Trilioni 1.5 ambazo mkandarasi alipaswa kuilipa Serikali kwa kuchelewesha mradi kwa mujibu wa mkataba.

Maswali ambayo Kina Balile na Kina Pascal Mayala licha ya kuwa Wanasheria wabobevu wameshindwa kuyauliza kwenye mamlaka husika hadi leo na hatujui kwanini wanafanya hivyo?

Kwa ufupi Wahariri wote wameandaa kongamano hilo ili kutengeneza hadaa na kuwaandaa kisaikolojia watanzania li kufanikisha lengo lao la kuonyesha tatizo la umeme halitakwisha leo wala kesho ili zile biashara zingine za Majenereta na Mikataba mingine iendelee ya kuiuzia umeme Tanesco. kwa kigezo cha kukosekana maji

Uthibitisho ya hayo siku chache Kabla ya Kongamano hilo, Mwenyekiti wa MERICA, Habib Mchange alifanya PRESS alitamka kwamba tutamlaumu Januari Makamba umeme wa mgao atafanya nini kama maji Ruaha hayapo?

MERICA imeshindwa kuuliza kwa nini umeme haukukatika katika kipindi chote cha miaka 6 iliyopita je hali ya ukame imekuja tu baada ya Januari kuwa Waziri? na je kuhusu madai ya baadhi ya watumishi wasio waadilifu wa TANESCO kufungulia maji ya Mabwawa ili yasijae kuzalisha umeme nalo kwa nini halizungumziwi.

Kwanini wazungumziwe kundi moja tu la wakulima na wafugaji ndio waliomaliza maji? na je miaka yote 6 ambayo umeme ulikuwa haukatiki wafugaji na wakulima waliacha shughuli za kilimo na ufugaji? kwanini maswali hayo hayapati nafasi? na kwanini kongamano hilo halikuwashirikisha wakulima na wafugaji kupitia vyama vyao kama MVIWATA na Chama cha Wafugaji Tanzania.

Tuendelee kutafakari kwa pamoja kuhusu kongamano hili na mambo yaliyojificha nyuma ya pazia ila uzuri duniani hakuna siri hasa jambo likishashirikisha watu zaidi ya mmoja na Makamu wa Rais ukweli aliofichwa ataufahamu.

Rejea nyingine muhimu juzi Waziri wa Nishati, Januari Makamba alinukuliwa akisema itahitajika misimu 2 ya mvua kujaza bwawa la nyerere.

Saidoo25.


Jamani mafisadi yamerudi kwa kasi ya kutisha sasa yanateketeza hakuna kitakachobaki. Kwa sasa yanajipanga kuiba kura 2025 ili yaendelee kubaki madarakani
 
Back
Top Bottom