Kongole kwako Profesa Jay kuwa mtangazaji wa redio Clouds

Sitak kuamin, kama yale marupu rupu ya bungeni, pesheni, n.k alishindwa kuanzisha hata shamba kuubwa la mbuzi asimamie na kuuza nyama comoro aje kuwa mtangazaji wa kulipwa milion ma ushee ili apate nn haswa anachohisi hela alizopata hazikutosha kukifanya.

Naamin basi hili jambo labda sio kweli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Waliojaza mavyeti makabatini wengi hawana charisma, Clouds media ni franchise na wanaangalia nani atawafaa kibiashara kulingana na ushindani ulivyo.
True..japokuwa tunahitaji professionalism kwenye media ila kwenye hizi Entertainment media utapewa kazi kwa kuwa kwanza na kipaji na popularity.

Degree yako ya journalism haitoshi wewe kuwa radio presenter au pre-actor..inabidi uwe na kipaji na sauti na lafudhi inayoweza kusikilizika redioni..
 
Umetumia nguvu nyingi sana kujibu majungu...
 
[emoji817][emoji3581]
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Weee heshimu kazi za watu then usiropoke usichokijua kuus prof J, ulizia kwanza uwekezaji wake na michongo aliyonayo. Usikurupuke
 
Clouds ndiyo walianzisha mfumo huu na sasa ndiyo unaotumika sana Tz, nakumbuka Ruge(late) ndiyo alianza kusema hawezi kuwa anatafuta presenters kwa kuangalia vyeti wakati wanachohitaji ni presenter atakayevutia wasikilizaji na makampuni yanayohitaji matangazo yao yawe yanarushwa kupitia Clouds media.
Ndipo zilipoanza informal dress codes and kinky hair styles ambavyo kwa ma conservatives lilikuwa jambo controversial sana back then, siku hizi mpaka vipensi vinavaliwa.
Mashirika kama TBC na ITV ndiyo yamebaki na mfumo wa enzi na enzi.
 
Viongozi wanasema. Vijana mjiajiri ila wao wanajiajiri.
Leo ukimwambia Jafo acha kazi ujiajiri anaweza kukufunga.
Tunacheza michezo ya kuigiza sana. Ukiona sehemu yoyote wewe jiweke haijalishi ya kuajiriwa au ya kujiajiri ili mradi mkono uende kinywani
 
Jamaa ananjaa sana baada ya kukosa ubunge ni kama kachanganyikiwa sijui hakujiandaa alikuwa anachezea pesa
[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2][emoji2] anahofia Lisa asije akahama kutoka feza kwenda shule za kata [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]
 
ALE NA NJAA YEYE, KWA SABABU YA MITAZAMO YAKO?
 
Kiinua mgongo alichopata kwenye Ubunge ni mtaji tosha wa kuanzisha kilimo cha kisasa kuliko kuwa mpiga kelele redioni.
Ile mentality ya kukaa na kusubiri salary mwisho wa mwezi ni ugonjwa mbaya sana.

Sijui hata kama net pay yake hapo inazidi 4M harafu ukute ile kiinua mgongo yake ya Ubunge (TZS. 250M+) kaifungia bank bila kujua aifanyie nini
 
Unajuaje Kama hajawekeza?
 
Bwashee usiamini kila unavhokisoma hapa Jf!
Huo ubunge alioshindwa unafikiri kampeni alifanyia nini kama sio hicho kiinua mgongo?
 
Acha uongo mtoa mada,amekaribishwa tu kwa ajili ya promo ya show yake na Jide
Hata mimi nilitaka kushangaa! Maana kwa muda wake wa miaka mitano ya kuhudumu Bungeni, alikua na uwezo wa kuanzisha kituo chake cha Redio na yeye kuwa CEO!

Anyway, hakuna kinacho shindikana chini ya jua. Kupanga ni kuchagua, na hatma ya maisha yake pia iko mikononi mwake.
 
Kwani sheria mpya mpya habar inasemaje.

Alisomea wapi iyo diploma ya utangazaji?

Au ndo Yale Yale ya wasafi na baba levo?
 
Mbona mimi hata sionekani inamaana hata @E-FM ya majizzo hawanioni.
 
Nasikia amechukua nafasi ya Babra ambaye ameondolewa baada Ya kugombana hewani na masoud kipanya.... Inavyosemekana
Lini hiyo mkuu na huo ugomvi ulikua unahusu nini??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…