Korea Kaskazini imesema itatuma wanajeshi wake nchini Ukraine kuisaidia Urusi

Korea Kaskazini imesema itatuma wanajeshi wake nchini Ukraine kuisaidia Urusi

Wanaukumbi.

🇰🇵 🇷🇺 Korea Kaskazini kutuma wanajeshi Ukraine kupigana pamoja na Urusi.

Mkataba wa ulinzi uliotiwa saini kati ya Urusi na Korea Kaskazini mnamo Juni 19, 2024, unajumuisha kifungu cha usaidizi wa kijeshi wa pande zote katika tukio la vita. Muda mfupi baada ya mkataba huo kutiwa saini, Korea Kaskazini ilitangaza mipango ya kutuma kitengo cha kijeshi cha uhandisi kusaidia vikosi vya Urusi katika mkoa wa Donetsk nchini Ukraine, huku kukitarajiwa kutumwa ndani ya mwezi ujao.

Haya yanajiri kufuatia mkutano wa hivi majuzi kati ya Rais wa Urusi Vladimir Putin na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un huko Pyongyang, kuashiria ziara ya kwanza ya Putin nchini Korea Kaskazini katika takriban miaka 25. Makubaliano hayo ya kijeshi yanaeleza kuwa iwapo nchi yoyote itavamiwa, nchi nyingine lazima itoe msaada wa kijeshi na msaada mwingine.

Korea Kaskazini tayari imekuwa msambazaji mkubwa wa misaada ya kijeshi kwa Urusi, ikiwa ni pamoja na risasi za kivita, roketi, na makombora yanayodaiwa kuwa ya balistiki, tangu mkutano wa viongozi hao nchini Urusi Septemba mwaka jana.

Pentagon imeelezea mashaka juu ya kutumwa kwa wanajeshi wa Korea Kaskazini, na kupendekeza kuwa wanaweza kuwa "kulisha kwa mizinga" katika mzozo huo. Marekani inafuatilia kwa karibu uhusiano wa kijeshi unaozidi kuimarika kati ya Urusi na Korea Kaskazini.

Wachambuzi wengine wanaamini kuwa Korea Kaskazini inatumika kama daraja la kimkakati kati ya Urusi na Uchina, kuwezesha uhamishaji wa zana za kijeshi kutoka China hadi Urusi bila kukiuka vikwazo vya Magharibi. Jukumu la Korea Kaskazini katika ushirikiano huu linaonekana kuwa la manufaa ya kifedha na kijeshi.

Baraza la Usalama la Taifa la Marekani limeukosoa muungano unaoundwa na Urusi, Korea Kaskazini, Iran na Syria, na kuutofautisha na uungaji mkono mpana wa kimataifa kwa Ukraine na kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa.


View: https://x.com/bricsinfo/status/1805969506990219268?s=46&t=mTROWpaJUT8H393JMgWOvw

Wanaenda kuliwa vichwa tu hao putini ashaulisha watu wengi sana kwa mtindo kama huu, Wagner leo wako wapi? vijana aliowaaajiri, wafungwa na sasa north korea na hata wanajeshi wa russia superpower anatapa tapa
 
Yaan mnyama hajaingia kwenye uwanja wa vita miaka yote 3 putini anaajiri vikosi kutoka North Korea..! nakubali sana Ukraine mziki mnene
 
Yaani Urusi isaidiwe? Hapana. Urusi ipo vizuri sana kijeshi. Haihitaji msaada.
Kila mtu na washirika wake,
USA alikua na Yuko na NATO.
USSR alikua na Warsaw Pact.
Sasa hivi Russia nae ana washirika wake.
Maisha ndivyo yalivyo.
Sio kwamba amezidiwa la ha Sha Bali ni washirika,kwa sababu Ukraine nae anasaidiwa na NATO
 
Kwanini Putin asi withdrawal na kurudi Moscow. Akubali tu kuishi vizuri na jirani yake mwenye uhuru kamili.
Kwa Nini Ukraine asikubali kuachana na mpango wake wa kutaka kujiunga na NATO?
Ambayo ni adui mkubwa wa Urusi ili aishi vizuri na jirani yake Urusi kwa amani na uhuru?
 
Urusi ndo wa kuomba jeshi kusaidiwa kupigana na ka nchi ka Ukraine?
Kwani kwa mujibu wa ranki zenu kati ya Urusi na Marekani ni nchi Gani Ina jeshi kubwa ,bajeti ya ulinzi silaha Bora na sifa nyingine nyingi?
Lakini mbona USA ana ombaga msaada wa nchi nyingine kwenda hata kupigana na watalaban TU?
Sasa kama USA ana omba msaada kwa NATO na washirika wengine kwa Nini Urusi nae asiombe msaada kwa marafiki zake kupigana na NATO ?
 
Hawa mashabiki wa USA na NATO bana,ni watu wa ajabu sana.
Wako kama USA yenyewe yaani ni unafiki TU kwa kwenda mbele.

Hebu fikiria.

Marekani kwenda kupigana na Iraq,Watalaban, Yugoslavia na Sasa kuisaidia Ukraine alikokota na amekokota nchi Dunia nzima pamoja na NATO yake ili zimsaidie.
Je huyu si hua tunaambiwa kua ndio jeshi namba moja duniani na Wana bajeti kubwa hata ziungane nchi zote duniani haziwezi kuifikia bajeti ya USA ?
Je kwa Nini asiende vitani peke yake?

Urusi tunaambiwa na haohao pro NATO kua ni nchi masikini na Ina jeshi dhaifu,je kama ni nchi masikini mbona akisaidiwa na marafiki zake TU mnaanza kupiga kelele?

Au mmesahau kua wakati wa USSR kulikua Kuna NATO na Warsaw Pact?

Sasa Kuna ubaya Gani Kila mtu kua na washirika wake?
Hofu ya Nini?
Au ndo manapenda vita nyepesi?
Kama NATO wameamua kuisaidia Ukraine basi Urusi nayo Ina haki ya kusaidiwa na marafiki zake.
 
Hawa mashabiki wa USA na NATO bana,ni watu wa ajabu sana.
Wako kama USA yenyewe yaani ni unafiki TU kwa kwenda mbele.

Hebu fikiria.

Marekani kwenda kupigana na Iraq,Watalaban, Yugoslavia na Sasa kuisaidia Ukraine alikokota na amekokota nchi Dunia nzima pamoja na NATO yake ili zimsaidie.
Je huyu si hua tunaambiwa kua ndio jeshi namba moja duniani na Wana bajeti kubwa hata ziungane nchi zote duniani haziwezi kuifikia bajeti ya USA ?
Je kwa Nini asiende vitani peke yake?

Urusi tunaambiwa na haohao pro NATO kua ni nchi masikini na Ina jeshi dhaifu,je kama ni nchi masikini mbona akisaidiwa na marafiki zake TU mnaanza kupiga kelele?

Au mmesahau kua wakati wa USSR kulikua Kuna NATO na Warsaw Pact?

Sasa Kuna ubaya Gani Kila mtu kua na washirika wake?
Hofu ya Nini?
Au ndo manapenda vita nyepesi?
Kama NATO wameamua kuisaidia Ukraine basi Urusi nayo Ina haki ya kusaidiwa na marafiki zake.
Kwani nani kasema kuna ubaya kila mtu kuwa na washirika wake?

Au ni wewe ndio umefikiria halafu ukaota kwamba Pro NATO ndio wamesema?
 
Back
Top Bottom