Korogwe: Gari ya marehemu imetelekezwa barabarani

Korogwe: Gari ya marehemu imetelekezwa barabarani

Korogwe Mjini, Tanga Karibu na Magereza, Kuna raia alikuwa na gari private akisafiri kuelekea Moshi kutokea Dsm. Gari ilipata ajali barabarani kabisa kabisa na bar maarufu iitwayo the spirit, karibu na Magereza Korogwe.

Abiria alipelekwa Hospital ya Wilaya Magunga na akafariki the same day. Baadae akawekwa Mochwari kwa siku 7 then akazikwa Korogwe baada ya kukoseakana ndugu kumtambua.


Sasa gari ipo barabarani, ya silver na inatolewa vitu kidogo kidogo roughly.

Shida sana.
Mtu mwenye gari akose kitamburisho?

Dunia ya leo mtu hadi anamiliki gari manaake details zake ziko mbali sana.

Angalieni vitamburisho.

Nendeni polisi watambue mmiliki wahilo gari.
 
Mara nyingi najua inapotokea ajali Polisi hufika eneo la tukio ilikuaje hapo kwahiyo polisi hawana taarifa yoyote kuhusu hiyo ajali?
 
Naona tatizo lile lile wale hawajatoa taarifa ili marehemu aweze kusaidiwa na wewe tena umekuja na pin number kabisa hakuna picha wala taarifa za gari ngoja tuendelee kusubiri..
 
Korogwe Mjini, Tanga Karibu na Magereza, Kuna raia alikuwa na gari private akisafiri kuelekea Moshi kutokea DSM. Gari ilipata ajali barabarani kabisa kabisa na bar maarufu iitwayo the spirit, karibu na Magereza Korogwe.

Abiria alipelekwa Hospital ya Wilaya Magunga na akafariki the same day. Baadae akawekwa Mochwari kwa siku 7 then akazikwa Korogwe baada ya kukoseakana ndugu kumtambua.

Sasa gari ipo barabarani, ya silver na inatolewa vitu kidogo kidogo roughly.

Shida sana.
Hakuna Polisi wanaohusika na ulinzi wa watu na mali zao?
 
Sasa mleta habari unadhani kwa taarifa yako hii umesaidia nini? Taarifa ina mapungufu mengi, ni kama vile umbea flani tu wa mitaani!
Weka picha ya gari, tena inayoonesha plate number ili tutambue usajiri wa hiyo gari.
Umemaliza habari bila kuonesha either unawalaumu traffics kwakushindwa kuchukua hatua stahiki au kuzikwa mapema kwa marehemu kabla ya utambuzi.
Ndiomana mataifa mengine jirani wanatuona watanzania tuna upeo mdogo kwa jinsi tunavyojiexpose kipumbafu kama hivi!
 
Home affairs nao wameshindwa kumtambua marehemu kwa kuangalia ID number yake, maana definitely alikua na driving license yenye ID number na pia why waweke maiti for only 7days?
Inchi hii hawana muda huo,

Labda upige mtu na kitu kizito kisogoni

Au wasikie umekimbia na hela za watu.

Utatafutwa hadi juu ya miti.
 
Pengine tuanze kwa kumshukuru mtoa taarifa.

Huenda kuna kitu alijua hakipo sawa ndo maana hakupiga picha

Garini humu wasingekosa chochote cha kumtambulisha marehemu.

Tatizo la kusafiri pekee yako kwenye gari,

Mali zangu hizo nilizojiwekea, watachezea wengine. RIP
 
Korogwe Mjini, Tanga Karibu na Magereza, Kuna raia alikuwa na gari private akisafiri kuelekea Moshi kutokea DSM. Gari ilipata ajali barabarani kabisa kabisa na bar maarufu iitwayo the spirit, karibu na Magereza Korogwe.

Abiria alipelekwa Hospital ya Wilaya Magunga na akafariki the same day. Baadae akawekwa Mochwari kwa siku 7 then akazikwa Korogwe baada ya kukoseakana ndugu kumtambua.

Sasa gari ipo barabarani, ya silver na inatolewa vitu kidogo kidogo roughly.

Shida sana.
Weka picha tuone namba za gari na gari yenyewe.
 
Inasikitisha sana, traffic case,polisi kitengo cha usalama barabarani walishindwa kuwajibika kwa kulipeleka gari polisi?

Maiti ya dereva,kwanini waiweke siku saba tu,wakati maiti za watu mbalimbali hukaa muda zaidi ya huo?

Rejea mwili wa baba yake Hans Pope,ulikaa Uganda miaka na miaka mingi sana,na ndo ukaja kuzikwa huku, trafiki naona kama wanaweka mgomo flani hivi,kutokana na kauli za wanasiasa.R.I.P.
Tena alikuwa fresh tu, na tuliona sura ya mwisho(Hanspope).
 
Walishindwa hata kumtambua mmiliki wa hiyo gari ni nani??

Vipi kuhusu kuitumia simu yake kuwapata ndgu, jamaa au marafiki!??

Hata mitandao ya kijamii nayo haikuwasadia kumtambua jamaa, so sad.
Hio mitandao ya kijamii unafikaje bila password Kuna smart haina password? Kingne ungeweza weka laini kwa simu yako ikae on usubiri mtu yoyote akimtafuta umpe taarifa lkn pia mitandao siku hizi laini kuwaka ni lazima uweke PiN huu nao ni upumbavu viongozi wetu hawawezi fikiria Kama Kuna majanga Kama hayo hao wanachowaza ni kuibiwa tu
 
Back
Top Bottom