Kosa kubwa alilofanya Hayati Magufuli ni kupambana na adui bandia na kuacha maadui halisi. Wenye ndoto za kuwa Rais mjifunze

Ni kweli mkuu Lowasa, Sumaye na wapinzani wote walikuwa siyo maadui na yeye ili hakujua laiti Ange ungana na lowasa kwenye mambo ya siasa angejua adui zake.

Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
 
Magu kuna mzimu alipandikiza bongo hapa "nawaambia ukweli ndugu zangu mmepigwa Sanaa"
 
Hamna shida mbegu alishaipanda, ndio maana mpaka sasa japokuwa ameshatangulia, bado jamaa wanahangaika.

Hii ina maana kibwa sana kuwa watanzania walimuelewa mwamba japokuwa it's already too late.

R.i.p Magufuli

Magufuli ameacha mbegu ya uchawa na uoga ndio unaotusumbua Sasa.
 
Unadhani magufuli alikuwa hajui maadui zake, ebu refer kwenye ile voice note iloyodukuliwa yakina makamba.

Sent from my TECNO CD7 using JamiiForums mobile app

Magufuli alitumia miaka mitano yote kupambana na CHADEMA. Mwisho wajanja wakamlia timing, halafu CHADEMA ndio wakahabarisha umma kuwa Magufuli kafariki. Yani ccm wote walidai Magufuli ila CHADEMA ambao Magaufuli aliwaona hawastahili kukaa nchini ndio walipambana mpaka msiba wake kutangazwa.
 
Maadui aliwajua Sana tu sema alikosea kuwaamini wale aliokaribu nao!

Nilisoma SEHEMU eti;-

Hata ......nilimiamini hivi!

ACHA wabaki na nchi yao!

Mungu baba Acha nipumzike Sasa!!

Mahufuli angetengeneza reconciliation na CHADEMA hata Mimi ningemlilia , Sasa yeye akatufanya maadui zake .
 

Hata shetani ana wafuasi tena wengi.
 
Kiongozi huwezi kupendwa na wote wala kuchukiwa na wote. Hata huyo aliyekuwepo sio wote wanampenda
 
Acheni uongo
 
Umeandika vizuri Heriel..ni kweli alizungukwa na maadui wengine wakiwa wasaidizi wake kabisa, labda kwa sababu hakuwa amejiandaa kwa kazi hii, lakini inapotokea unakuwa na dhamira njema km alivyokuwa yeye juu ya yale unafanya, ni Mungu tu huwa anaweka ulinzi wake kwako, ni bahati mbaya Magufuli alipotoka akadanganywa na kulewa kusifiwa..ni kama mfalme Sauli ilivyomtokea..PRIDE!!
Maadui zake walihahakisha wanamtenganisha kabisa na kumgombanisha na watu ambao wangekuwa msaada kwake, ikiwemo vyama vya siasa km CHADEMA..uchaguzi wa 2020 ilikuwa kilele cha mambo yasiyofaa si tu kwa binadamu bali kwa Mungu pia, kilichofanyika ilikuwa DHAMBI kubwa ambayo yeye Magufuli aliruhusu ifanyike kwa sabab ya KIBURI cha madaraka na sifa.. hakukuwa na namna zaidi ya ilivyotokea, kwa wanaokumbuka maombi ya Askofu Mwakibolwa wakati yeye Magufuli alikuwa anahitimisha ziara ya mkoa wa Dsm, ilikuwa kama Baba Askofu anamuombea msamaha kwa Mungu kwa yale yaliyotokea ili amsamehe..Askofu alitoa sala nzito tena kwa machozi hata Magufuli alitoa machozi pia..lakini Mungu alikuwa ameshaamua! Watumishi wa Mungu waaminifu huwa wanaonyeshwa katika ulimwengu wa Roho yale yatakayotokea kwa watu ambao Mungu anapenda wajue na wajifunze..sisi watu wengine si rahisi kufikia level hiyo..funzo hapa ni ni kuwa Ukiwa kiongozi kitu unachopaswa kukiogopa kama kifo ni KUSIFIWA naona bado somo halijaeleweka watu wanarudia yale yale..ngoja tuone!
 
Kwa mistari michache, kama hamtojali nani anaandika..ni kuwa baada ya uchaguzi wa 2020 na huu wa ndani ya CCM kitu kimoja kiko wazi sasa, kuna watu wachache wameamua kwa niaba yetu nchi hii ifuate mfumo wa kiutawala na kiuongozi wa China, yaani kiwepo chama kimoja tu kama vile China(CCP)..ila kwa vile sisi hatuna nguvu za kusimama wenyewe kama China, viwepo vyama vya siasa kama geresha kuwaghilibu watu wa magharibi ili wasitutenge..ndiyo maana wakati wa uchaguzi kunakuwa na ushawishi mkubwa sana kutoka CCM kushawishi watu wa aina zote, matajiri, wapishi, maskini, wasomi, wasanii, wanahabari, kila aina washiriki uchaguzi hata kwa kuchukua fomu tu ili kuonyesha umma na dunia kuwa vyama vya siasa havihitajiki hapa! Kwa vile makundi yote kwenye jamii ni wanaCCM hata kama CCM yenyewe inavurunda; rushwa, upendeleo, wizi, kukosa uwezo wa kuongoza nk. Hii ni LAANA! watanzania tukikubali hii laana tukadhani ni kitu cha kawaida basi tumekwisha! Tuikatae hii laana kwa nguvu zetu zote tena sasa hivi! tusiimbe tu katiba au tume huru kama ushabiki wa simba na yanga..tutafakari yanayotokea, tumuombe Mungu sana bila kuchoka na tuchukue hatua kwa yale yaliyo ndani ya uwezo wetu!
 
Hamna shida mbegu alishaipanda, ndio maana mpaka sasa japokuwa ameshatangulia, bado jamaa wanahangaika.

Hii ina maana kibwa sana kuwa watanzania walimuelewa mwamba japokuwa it's already too late.

R.i.p Magufuli
aRIP na kuoza, mnatuchosha
 
Ni kweli mkuu,hata shetani Ni hivyo hivyo.
 
Angejua angetumia njia ya mmarekani ya kupambana magaidi wa kiislam wa september 11

USA baada ya kulipuliwa september 11.. aligundua osama bin laden wa al qaeda ndie muhusika na adui yake mkuu.. na akagundua ana sapoti ya waislam dunia nzima ambao wako wengi zaidi ya bilioni.

USA akawaza kwamba ili niweze kummudu osama vizuri inapaswa niwatishe magaidi waislamu wa dunia nzima ili waogope kumficha osama.. wajue sitaki utani..

Naua viongozi wote wenye nguvu ambao magaidi wa kiislamu wanawategemea ili wajue sina utani. Hapo ndipo saddam hussein akauwawa, ghadaffi akauwawa, mullah omar akauwawa, zawahir akauwawa.. then ndipo osama akauwawa.

Hii ikawatisha magaidi wa kiislam kumficha osama dunia nzima.. maana wababe wao waliowategemea wameuwawa sasa sisi wanyonge tutaweza kweli. Wote wakamuogopa mmarekani kabisa

Magu alipaswa aondoe mibuyu kwanza
 
Aliwastahi,

Katika kitabu cha 48 Laws of power, Sheria namba 15 inaitwa CRUSH YOUR ENEMY COMPLETELY, ukishamjua adui yako usimpe nafasi wala room ya majadiliano, wala usimuonee aibu!!
Unaweza kunitumia soft copy ya hicho kitabu?
 
Tena wakaua watoto wao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…