Kosa la Adolph Hitler la Septemba mosi 1939 linataka kurudiwa na Vladimir Putin

Kosa la Adolph Hitler la Septemba mosi 1939 linataka kurudiwa na Vladimir Putin

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Wanasiasa hufanya makosa mengi sana wakiwa madarakani. Wanapoyafanya huwa hawana uwezo wa kupima ukubwa na madhara ya wanachokusudia kukifanya. Ni pale wanapokuwa wanapokea lawama nyingi ndio hujisumbua kuangalia kwa kina namna ambavyo wangeweza kuzuia kile walichokifanya, wangefanya hivi na wakafanya vile ndio huwa ni wazo lililochelewa wakati wake. Wanapokuwa wakiamua kufanya maamuzi yanayoongozwa na upofu au ulevi wa madaraka huwa wamezungukwa na wapambe wanaosema kitu wanachotaka kukisikia. Wao kuwa na maamuzi ya mwisho wakati mwingine huwanyima ile busara ya kuwa mawazo yao sio kila wakati huwa ndio ya kutekelezwa na yakaja na jibu lililokusudiwa na lenye faida.

Rais wa Russia Vladmir Putin anataka kufanya kosa litakalompa umaarufu mbovu kama ule aliokuwa nao Adolph Hitler mwaka 1939. Putin anataka kufanya kosa kama lile alilolifanya Idd Amin mwaka 1978 kwa kuivamia sehemu ya mkoa wa Kagera, kipigo alichokipata kilimpoteza kabisa miongoni mwa viongozi wa mataifa waliostahili heshima kila walipokatiza. Putin ameiangalia Ukraine katika udogo wake kwa kuilinganisha na Russia hivyo anaamini kwamba anaweza kufanya lolote na dunia ya sasa ikatulia tu na kumtazama. Kitakachompata kitakuwa ni fedheha kama ile iliyomkuta Hitler ambaye aliishia kujinyonga baada ya vita kumalizika akiwa ameshindwa vibaya.

Anatakiwa kukumbushwa kuwa Volodymyr Zelensky licha ya kuwa ni rais wa Ukraine taifa huru lenye maamuzi huru kama ilivyo Russia pia ni myahudi. Kwa asili ya wayahudi huwa ni watu wenye mtandao ulio hai na makini siku zote. Wayahudi wanajuana popote walipo, na mwanasiasa ambaye hata kama upande wa Mama ndio wayahudi huwa wanamchukulia kama ni mtoto wao. Wayahudi wanalinda ushawishi walionao duniani kote. Na ni rahisi kwao kumpachika jina la 'anti semitic' yoyote yule anayekwenda kinyume na falsafa zao au anayewakejeli.

Sembuse maamuzi ya Putin kuivamia nchi huru ya Ukraine inayoongozwa na myahudi mwenzao!!. Putin anakosa washauri wenye kutazama mbali, wenye ushawishi wa kidunia. Atumie busara sana kwani anachofikiria dhidi ya Ukraine kinaweza kumpoteza kabisa na yale yote aliyokwisha kuyafanya tangu 1999 alipoanza kuongoza Russia yakafunikwa na huu 'ujinga' anaouwazia kwa sauti ya juu.

Ulimwengu wa 1939 wakati Hitler akiivamia Austria sio huu wa 2022. Zimetungwa sheria nyingi za kimataifa zinazolinda uhuru wa kila taifa. Wamezaliwa wanasiasa wenye maarifa mazito ya kuongoza. Sayansi haijabaki nyuma zimeundwa silaha za hatari zenye kuweza kuangamiza kila kilichopo juu ya uso wa dunia ndani ya saa chache tu. Anaumizwa sana na ushawishi wa USA kwa jirani yake wa karibu, lakini nguvu nyingi hutumiwa na mwenye maarifa madogo ya uongozi.
 
Ulimwengu wa 1939 wakati Hitler akiivamia Austria sio huu wa 2022. Zimetungwa sheria nyingi za kimataifa zinazolinda uhuru wa kila taifa.
To cut you short, hizo sheria zinazibana nchi kama hizi zetu. US walipovamia Iraq hizo sheria hazikuwepo?!

Wait and see what's gonna happen. Putin si Saddam, ujue hilo. Na hii crisis inakwenda kupelekea Biden kuwa one term president.
 
..Putin angeachana na Ukraine.

..Ukraine hawaungi mkono kuwa chini ya Russia.

..kuna historia mbaya kati yao inayohusisha mauaji ya mamilioni ya Waukraine wakati wa utawala wa Josef Stalin.

..kama kuna majimbo yenye nia ya kujitenga na Ukraine walipaswa kuitisha KURA YA MAONI na sio kutumia nguvu za kijeshi.
 
To cut you short, hizo sheria zinazibana nchi kama hizi zetu. US walipovamia Iraq hizo sheria hazikuwepo?!

Wait and see what's gonna happen. Putin si Saddam, ujue hilo. Na hii crisis inakwenda kupelekea Biden kuwa one term president.
Mkuu Rais wa Ukraine ni myahudi. Kumbuka hawa watu waliuliwa zaidi ya milioni moja kule Poland hivyo tangu wakati huo wana umoja wa ajabu.

Kuvamia nchi nyingine kwa sababu zisizoingia kichwani ni ngumu sana. Ni kweli si Saddam lakini udikteta wa Hitler kwa karne hakuna atakayeuvumilia.
 
Mtoa mada kama hujui hizi zama zimebadilika, hakuna tena mambo ya 90 endeleeni kukaa na maumivu, halaf hamkuumia umoja wa ulaya ulipoenda kuuwa maelfu ya watu Libya bila ya sababu wapuuzi wakubwa nyie mnakuja kuumia Russia kurejesha majimbo yake ya asili ?
 
..Putin angeachana na Ukraine.

..Ukraine hawaungi mkono kuwa chini ya Russia.

..kuna historia mbaya kati yao inayohusisha mauaji ya mamilioni ya Waukraine wakati wa utawala wa Josef Stalin.

..kama kuna majimbo yenye nia ya kujitenga na Ukraine walipaswa kuitisha KURA YA MAONI na sio kutumia nguvu za kijeshi.
Kuna kipindi Putin alijifanya kichaa kwa Marekani enzi zile za Obama, wakauchezea mfumo wa ATM wa Russia ambao waliutengeneza wao wamarekani, warusi walichanganyikiwa.
 
Mtoa mada kama hujui hizi zama zimebadilika, hakuna tena mambo ya 90 endeleeni kukaa na maumivu, halaf hamkuumia umoja wa ulaya ulipoenda kuuwa maelfu ya watu Libya bila ya sababu wapuuzi wakubwa nyie mnakuja kuumia Russia kurejesha majimbo yake ya asili ?
Unaleta sera za usisi zile sera za uafrika. Matatizo yetu na ya wenzetu ni tofauti, kama sisi hatuna umoja maana yake hatuna nguvu ya kuongea chochote tukiwa mezani na wakubwa.
 
Mkuu Rais wa Ukraine ni myahudi. Kumbuka hawa watu waliuliwa zaidi ya milioni moja kule Poland hivyo tangu wakati huo wana umoja wa ajabu.
Russia ni kitu ingine wewe! Kama unafatilia siasa za dunia jaribu kuvuta kumbukumbu ya nini kilifata baada ya ndege ya Russia iliyokuwa kwenye operations Syria kutunguliwa na waturuki.
 
Kuna kipindi Putin alijifanya kichaa kwa Marekani enzi zile za Obama, wakauchezea mfumo wa ATM wa Russia ambao waliutengeneza wao wamarekani, warusi walichanganyikiwa.
Walichanganyikiwa vp tuma link tuone waoivyochanganyikiwa? Kwani unafkiri hayo wanayofanya hawajui wanafanya nn, wanafanya kwa kujiamini
 
Ndio hivyo tena, majimbo tushachukua kwanguvu na hamuwezi kufanya kitu na wambieni hao wapuuzi wenu wasogeze pua waone kitakachowapata
Hayo maneno yamezoeleka kwa wakongwe.Walianza chawa wa Saddam kupiga kelele na kujidai USA hawezi kuwafanya lolote.
Wakafuata vimbwenerehi wa Afghanistan huku wakiwa na magobole yao milimani Torabora na Kandahar.Mwishowe walitoa mlio wa huzuni.
 
Russia ni kitu ingine wewe! Kama unafatilia siasa za dunia jaribu kuvuta kumbukumbu ya nini kilifata baada ya ndege ya Russia iliyokuwa kwenye operations Syria kutunguliwa na waturuki.
Myahudi mmoja anao mtandao mpana sana wa dunia nzima wa kumtetea. Putin analeta mchezo utakaomharibu na yeye pamoja na Russia anayoingoza.
 
Back
Top Bottom