Kosa la mwaka 1960-1975 linajirudia mwaka 2015

Kosa la mwaka 1960-1975 linajirudia mwaka 2015

Kwa hiyo hata Katiba ikichukuwa miaka 10 au zaidi chini ya CCM hakuna tatizo.

Acha kupotosha nilichosema Ritz,

Mbona unakuwa mzabizabina ndugu yangu?

Nimesema kuwa mchakato hata uchukue miaka kumi mbele, lakini kwa sasa mda uliosalia kwa uchaguzi 2015, tufanye marekebisho ya katiba iliyopo ili ituongoze kwenye uchaguzi mkuu 2015,

Chama chochote kitakachokuwa madarakani kitakuwa na wajibu wa kuendeleza mchakato uliopo,

Sasa spinning unazofanya ni za kitoto ndugu,
 
Acha kupotosha nilichosema Ritz,

Mbona unakuwa mzabizabina ndugu yangu?

Nimesema kuwa mchakato hata uchukue miaka kumi mbele, lakini kwa sasa mda uliosalia kwa uchaguzi 2015, tufanye marekebisho ya katiba iliyopo ili ituongoze kwenye uchaguzi mkuu 2015,

Chama chochote kitakachokuwa madarakani kitakuwa na wajibu wa kuendeleza mchakato uliopo,

Sasa spinning unazofanya ni za kitoto ndugu,
Basi kama ndiyo hivyo basi maoni yako yatafanyiwa kazi na serikali ya CCM.

Nakumbuka Mwalimu Nyerere alishawahi kusema hii katiba inamfanya rais kuwa dikteta kama akiamua kuitumia kama ilivyo sasa wewe unataka endelee kutumika hata miaka 10 mbele na zaidi.

Yericko Nyerere, mbona unakuwa mzabinazabina, unaweza kutupa ushahidi kama hii Katiba imeandikwa kwa mikono ya Nyerere kama unavyodai.

Kwanza Mwalimu Nyerere hakuwa mwanasheria sijui hiyo Katiba aliiandika vipi.
 
Last edited by a moderator:
Kukusanya maoni ya wananchi kunahitaji miaka mingapi? Siku hizi dunia ni ndogo. CDM wamezunguka sehemu kubwa ya Tanzania kwa machopa, kwa kipindi kifupi.

Naamini mleta mada ana nia nzuri, lakini hajatoa sababu ya kuridhisha ya kuonyesha kwamba katiba mpya haiwezi kupatikana kabla ya 2015. Kuwa na deadline kwenye project yoyote ni muhimu.

Kenya wamepata katiba mpya kwa mchakato wa kipindi kifupi kama sisi, na tunadhani wamepata katiba nzuri. Kwa nini kwetu isiwezekane?

Kuingia kwenye uchaguzi mkuu mwingine bila kuwa na katiba yenye chombo huru cha kusimamia huo uchaguzi haikubaliki. CCM ni wezi wa kura, lazima kuwe na vyombo huru (ikiwa ni pamoja na Polisi huru na Usalama wa Taifa huru) kwanza.

The bottom line is: Lazima ipatikane katiba mpya kabla ya 2015, na uchaguzi mkuu ufanyike 2015. Hakuna kuchelewesha katiba au kumpa JK muda zaidi.
Kuna mambo ya msingi yanayohusu uchaguzi kama daftari la wapiga kura, mgombea binafsi, tume huru ya uchaguzi yanaweza kufanyiwa mabadiliko ya msingi kabla ya 2015 election, lakini mambo mengine yaendelee kujadiliwa kabla katiba mpya haijaandikwa. Kwamba kenya walichukua muda mfupi, nasikitika kusema umekosea sana kihistoria. Unafahamu kitu kinaitwa bomas au Prof. Yash Ghai Draft ya 2000-2004 katika historia ya mchakato wa katiba ya Kenya? Katiba ya Kenya imechukua zaidi ya muongo mmoja kupatikana tena kwa gharama kubwa ikiwamo maisha ya watu. Kwa nini mchakato uchukue muda mrefu? Hii itawasaidia walevi wa madaraka kama akina Chikawe, Wasira, Lukuvi, Werema, Ndugai, Sophia Simba na wengine ambao ni wazito kuelewa kwa muda mfupi nini mana ya katiba ya wananchi waweze kuelewa japo kiasi. Kwani wao hawaelewi kitu kingine zaidi ya CCM duniani hapa.
 
Basi kama ndiyo hivyo basi maoni yako yatafanyiwa kazi na serikali ya CCM.

Nakumbuka Mwalimu Nyerere alishawahi kusema hii katiba inamfanya rais kuwa dikteta kama akiamua kuitumia kama ilivyo sasa wewe unataka endelee kutumika hata miaka 10 mbele na zaidi.

Yericko, mbona unakuwa mzabinazabina, unaweza kutupa ushahidi kama hii Katiba imeandikwa kwa mikono ya Nyerere kama unavyodai.

Nitaendelea kukukosoa mda wote,

Hakuna niliposema katika hii tuliyonayo iendelee kutuongoza kama ilivyo,

Nilichosema nikuwa ifanyiwe marekebisho kwenye maeneo muhimu ili ituongoze kwenye uchaguzi 2015,

Kuhusu katiba ya TANU kuandikwa na Julius Nyerere hilo sihitaji hata kukufundisha upya, kwani nilishakufundisha sana huko nyuma,

Na kwamba katiba ya Tanganyika ilihuishwa ile ya TANU hilo nalo elewa hivyo mkuu,
 
Mwenzetu huyo huenda anakipaji maalumu,

Akiona sentensi moja tu basi huelewa mada nzima,

Sio kosa lake ndio kizazi cha bongo movies

exactly! Ndio maana huwa najiapiza kwamba, ni bora niitwe baba dicteta au mkoloni lakini kamwe sitaacha my daughter awe addicted na Bongo Movies! For the benefit of her thinking capacity!
 
Kuna mambo ya msingi yanayohusu uchaguzi kama daftari la wapiga kura, mgombea binafsi, tume huru ya uchaguzi yanaweza kufanyiwa mabadiliko ya msingi kabla ya 2015 election, lakini mambo mengine yaendelee kujadiliwa kabla katiba mpya haijaandikwa. Kwamba kenya walichukua muda mfupi, nasikitika kusema umekosea sana kihistoria. Unafahamu kitu kinaitwa bomas au Prof. Yash Ghai Draft ya 2000-2004 katika historia ya mchakato wa katiba ya Kenya? Katiba ya Kenya imechukua zaidi ya muongo mmoja kupatikana tena kwa gharama kubwa ikiwamo maisha ya watu. Kwa nini mchakato uchukue muda mrefu? Hii itawasaidia walevi wa madaraka kama akina Chikawe, Wasira, Lukuvi, Werema, Ndugai, Sophia Simba na wengine ambao ni wazito kuelewa kwa muda mfupi nini mana ya katiba ya wananchi waweze kuelewa japo kiasi. Kwani wao hawaelewi kitu kingine zaidi ya CCM duniani hapa.

Naaaam naaaam naaam

Mkuu umetoa elimu pana sana hasa kwa wahafidhina wa vyama badala ya taifa
 
Unafamhamu Dr. Mutahangarwa? Unafahamu Dr. Lugaiza? Wapo wengi tuanze na hawa unajua elimu zao?

duh nimeshtukaje!!,mkuu nilivyona maneno Dr. nikadhani yataishia na ali,muhamed...aise kumbe watu wa tz bara including nyerere ndo walikuwa wasomi wa mwanzo tz.?!
 
Kukusanya maoni ya wananchi kunahitaji miaka mingapi? Siku hizi dunia ni ndogo. CDM wamezunguka sehemu kubwa ya Tanzania kwa machopa, kwa kipindi kifupi.

Naamini mleta mada ana nia nzuri, lakini hajatoa sababu ya kuridhisha ya kuonyesha kwamba katiba mpya haiwezi kupatikana kabla ya 2015. Kuwa na deadline kwenye project yoyote ni muhimu.

Kenya wamepata katiba mpya kwa mchakato wa kipindi kifupi kama sisi, na tunadhani wamepata katiba nzuri. Kwa nini kwetu isiwezekane?

Kuingia kwenye uchaguzi mkuu mwingine bila kuwa na katiba yenye chombo huru cha kusimamia huo uchaguzi haikubaliki. CCM ni wezi wa kura, lazima kuwe na vyombo huru (ikiwa ni pamoja na Polisi huru na Usalama wa Taifa huru) kwanza.

The bottom line is: Lazima ipatikane katiba mpya kabla ya 2015, na uchaguzi mkuu ufanyike 2015. Hakuna kuchelewesha katiba au kumpa JK muda zaidi.

Mimi naamini tunaweza kufanya marekebisho madogo kwenye hii katiba tuliyonayo natukafanya uchaguzi ulio haki na huru,ili tupate katiba bora ya wananchi tunahitaji muda.
 
Nitaendelea kukukosoa mda wote,

Hakuna niliposema katika hii tuliyonayo iendelee kutuongoza kama ilivyo,

Nilichosema nikuwa ifanyiwe marekebisho kwenye maeneo muhimu ili ituongoze kwenye uchaguzi 2015,

Kuhusu katiba ya TANU kuandikwa na Julius Nyerere hilo sihitaji hata kukufundisha upya, kwani nilishakufundisha sana huko nyuma,

Na kwamba katiba ya Tanganyika ilihuishwa ile ya TANU hilo nalo elewa hivyo mkuu,
Yericko Nyerere,

Ukileta babandiko yako lazima huwe tayari kuyatetea kwa hoja siyo kwa viroja.
Hakuna niliposema katika hii tuliyonayo iendelee kutuongoza kama ilivyo,

Nilichosema nikuwa ifanyiwe marekebisho kwenye maeneo muhimu ili ituongoze kwenye uchaguzi 2015,
Hebu jisome mwenywe hapa chini kutoka kwenye bandiko lako.
Tangu Tanganyika ipate uhuru 09/12/1961 hadi kifo chake chenye utata 1964, ilitumia KATIBA ya chama cha Ukombozi cha TANU iliyoandikwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mahuisho mengi yaliyopita kama yale ya 1962, 1965, 1977, 1992 bado asili ya katiba hii tuliyonayo leo ni ya MKONO wa Julius Nyerere,

Marekebisho makubwa ya Katiba yalikuwa ni mwaka 1977, lakini asili ya KATIBA ile ya Mkono wa Nyerere imeendelea kuishi na kulitendea haki Taifa na wajihi wake!
Sijui ulikuwa na maana gani hapo.
Tangu Tanganyika ipate uhuru 09/12/1961 hadi kifo chake chenye utata 1964, ilitumia KATIBA ya chama cha Ukombozi cha TANU iliyoandikwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mahuisho mengi yaliyopita kama yale ya 1962, 1965, 1977, 1992 bado asili ya katiba hii tuliyonayo leo ni ya MKONO wa Julius Nyerere,

Marekebisho makubwa ya Katiba yalikuwa ni mwaka 1977, lakini asili ya KATIBA ile ya Mkono wa Nyerere imeendelea kuishi na kulitendea haki Taifa na wajihi wake!
Kwa faida ya Wanaukumbi ungetupa ushahidi siyo kuja na maneno matupu hapo kwenye bold siyo kweli.
 
Last edited by a moderator:
duh nimeshtukaje!!,mkuu nilivyona maneno Dr. nikadhani yataishia na ali,muhamed...aise kumbe watu wa tz bara including nyerere ndo walikuwa wasomi wa mwanzo tz.?!
du!!!! hebu jipongeze na huu mpini kiduchu kisha tuendelee na mjadala.
The Life and Times of Hamza Mwapachu

On September 18, 2012, in English, Print, by Joji




By Amb. Juma Mwapachu
BabuHamza.jpg
50 years ago, on 17[SUP]th[/SUP] September, 1962, Hamza Kibwana Bakari Mwapachu, father to Harith Bakari Mwapachu, Rahma Mark Bomani, Juma Volter Mwapachu, Wendo Mtega Mwapachu, Tunu Mwapachu and Jabe Jabir Mwapachu died in Dar-es-Salaam at the early age of 49. He was at the time a Principal Assistant Secretary in the Ministry of Home Affairs.
Born in Tanga, the late Hamza attended primary and secondary schools in Tanga. On completing standard 10, at that time the highest secondary school education standard in Tanganyika, he pursued medical studies at the Sewa Haji Hospital Medical School in Dar-es-Salaam qualifying in 1935 as a Medical Assistant. In 1937, he was posted as a Tutor to the Mwanza Medical School which trained medical support staff. In Mwanza, Hamza met Juliana Volter whom he married in 1938.
An ambitious Hamza succeeded to be admitted at Makerere College, Uganda in 1943 to pursue a Diploma in Medicine. Makerere had not started offering degrees of any kind at that time. As history would have it, Hamza and Julius Kambarage Nyerere joined Makerere at the same time beginning a journey of a very close friendship and political relationship despite a nine years age difference between them. At Makerere, the two befriended Andrew Tibandebage, a fellow education student to Nyerere who was a year senior at the College and the trio established a politically charged Tanganyika Welfare Students Organisation in late 1943. They applied for recognition as an affiliate of the Tanganyika African Association (TAA), but received no response from its head office in Dar-es-Salaam.
On completion of their studies in 1945, both Hamza Mwapachu and Julius Nyerere found themselves in Tabora; Hamza at the Government Hospital and Nyerere at St. Mary's Secondary School where Tibandebage was already a teacher. The trio joined the TAA Branch in Tabora and in 1946 took over its reins with Hamza as President, Nyerere as Secretary and Tibandebage as Treasurer.
At that stage, Hamza had increasingly found his medical profession lacking in the intellectual depth needed to understand the complex dynamics of politics and constitutionalism for an informed attack against colonialism. Thus in 1947 he quit medical practice and joined the University College of South Wales at Cardiff to read a Diploma in Social Work. Whilst in the UK, Hamza was attracted to the Post Second World War Labour Party politics and socialism. He joined the Fabian Society then known as Fabian Colonial Bureau and established a network of close friends who, until he died, were frequent suppliers of books and reading materials to Hamza.
Nimetulia tuli nakula zangu Faluda, teh teh teh...

Cc: kahtaan, THE BIG SHOW, Tayeb, gombesugu,
 
Last edited by a moderator:
exactly! Ndio maana huwa najiapiza kwamba, ni bora niitwe baba dicteta au mkoloni lakini kamwe sitaacha my daughter awe addicted na Bongo Movies! For the benefit of her thinking capacity!

Daaah nimecheka sana mkuu!

Hahaha aisee
 
du!!!! hebu jipongeze na huu mpini kiduchu kisha tuendelee na mjadala.

Nimetulia tuli nakula zangu Faluda, teh teh teh...

Cc: kahtaan, THE BIG SHOW, Tayeb, gombesugu,

Kuna uwezekano mkubwa ama hujui kusoma, ama hujui mantiki ya mada iliyopo,

Habari ya Mwapachu na elimu yake inamalizikia hapa chini,

Thus in 1947 he quit medical practice and joined the University College of South Wales at Cardiff to read a Diploma in Social Work.

Sasa nieleze, Mwapachu alikuwa na Masters?

Alikuwa na PhD?

Nilichoona na ninachofahamu amefariki akiwa na Diploma in Social Work.

Kama kuna habari zingine mpya juu yake hebu zilete hapa wanajamvi wakusome
 
Last edited by a moderator:
Yericko Nyerere,

Endelea kuwadanganya jamaa zako najua hauwezi kutoa majibu ninachofanya ni kuwasaidia wana JF wasimeze pumba kama hizi hapa.
Mfano Tanganyika ilipata Uhuru ikiwa na wasomi wachache wenye ngazi ya shahada ya Uzamili (Masters) ambae ni Julius Nyerere, na Shahada ya Uzamivu (PHd) ni mmoja tu ambaye ni Dr Vedasto Kyaruzi,
Hebu msome huyu hapa chini.
Abdallah Said Fundikira III (2 February 1921 – 6 August 2007) was the Ntemi (chief) of Unyanyembe 1957–1962, when he was deposed by the Tanzanian government. He died as a member of the Chama Cha Mapinuzi party.
Early life
Chief Fundikira attended his primary education at Tanga Primary School. He undertook middle school education at the same school and later joined Tabora School for secondary education where he graduated in 1939. The late Chief Fundikira joined Makerere University in Uganda from 1940 to 1946 and was conferred with a first degree in Agriculture. In 1957, he was ordained as chief of the Wanyamwezi in the Nyanyembe chiefdom.
In 1961 soon after independence, the first Chief Minister Julius Nyerere appointed Fundikira as minister for water, a portfolio he served for one year. He was appointed the first local justice minister when Tanganyika became a republic in 1962. He resigned from Cabinet in 1963 to protest the imminent legislation introducing a one party state.
In 1964, he resigned from the civil service. In 1967, he was appointed as board chairman of the defunct East African Airways until 1972 when his term of office came to an end.
Taratibu takuwa nakupa darsa....
 
Last edited by a moderator:
Yericko Nyerere,

Ukileta babandiko yako lazima huwe tayari kuyatetea kwa hoja siyo kwa viroja.

Hebu jisome mwenywe hapa chini kutoka kwenye bandiko lako.

Sijui ulikuwa na maana gani hapo.

Kwa faida ya Wanaukumbi ungetupa ushahidi siyo kuja na maneno matupu hapo kwenye bold siyo kweli.

Hili tayari nimeshalitolea ufafanuzi ndani ya makala hiyo hiyo, usiwe mvivu mkuu tulia soma,
 
Last edited by a moderator:
Yericko Nyerere,

Endelea kuwadanganya jamaa zako najua hauwezi kutoa majibu ninachofanya ni kuwasaidia wana JF wasimeze pumba kama hizi hapa.

Hebu msome huyu hapa chini.

Taratibu takuwa nakupa darsa....

Mkuu unapoteza mda tu,

Fundikila amefariki akiwa na Degree toka Makerere tu, hakuwa na Masters wala PHD,
 
Last edited by a moderator:
Sikubaliana na wewe kwenye mitazamo inayoshibishwa na propaganda na fikra mgando za ki magharibi. Naendelea kuamini bila ukoloni labda afrika tungekuwa mbali kuliko hap watu wa magharibi na ushahidi upo
1. Mtu wa Kwanza duniani imethibitika anatoka Afrika -Tanganyika
2. Chuo kikuu cha kwanza cha hisabati na Physics kipo Afrika - Egypt
3. Kiwanda cha kwanza cha ngupo (barking cloth) kilikuwa afrika - Nigeria
4. Kiwanda cha kwanza cha chumvi kilikuwa Afrika -Tanganyika

Baada ya explorers, traders na missionaries kuja walitulazimisha kufuata mitazamo na fikra zao, wakatufanya tuone fahari zetu kuwa ujinga na tumechelewa, wakaita AFRIKA the DARK CONTINENT ili hali linavitu vingi vikidhibitsha uongo na ujinga wao.

Kuhusu elimu, naamini Afrika ilikuwa na elimu yake nzuri na bora kwa mazingira yake ila elimu ya magharibi imetufanya tuone elimu yetu ni ya kijinga, fikiria zamani wazee walifundishwa kuishi kutokana na mazingira yao wenyewe leo GEOGRAPHY inafundishwa ya ULAYA ili hali ya Mkuranga kwetu wenyewe hawafundishwi, leo HISTORIA na MASHUJAA WOTE ni wazungu ili hali babu zetu wengi tu wana dhihakiwa.

Nakubaliana mwishoni namna mchakato wa katiba mpya ulivyobakwa, namna wanasiasa wanavyotaka kufanikisha kwa maslahi yao wenyewe


Mnamo tarehe 9 Desemba 1961, Tanganyika ilipata Uhuru chini ya Waingereza waliokuwa waangalizi wetu tu,

Ni nyakati hizo ambapo mataifa ya Afrika yalikuwa kwenye vuguvugu la kupata uhuru wao kamili yakiongozwa na Nchi ya Gold Coast iliyojinyakulia uhuru kutoka kwa Uingereza mnamo tarehe 6 Machi 1957, na ikawa taifa la kwanza la Afrika Kusini mwa Sahara (Sub-Saharan Africa) kufanya hivyo japokuwa Gold Coast/Ghana haikuweza kutangaza uhuru wake kamili kutoka kwa Uingereza hadi tarehe 1 Julai 1960 ambapo pia nchi ilianza kujulikana kama Jamhuri ya Ghana.

Nchi ya Gold Coast ilianzishwa na Waigereza, "Gold Coast" ni nchi ya Ghana ya leo, Neno Ghana lina maana ya Shujaa Mfalme na lilikuwa ni jina la heshima walilopewa wafalme wa Himaya ya Ghana nyakati za kale za Afrika Magharibi.

Tangu Tanganyika ipate uhuru 09/12/1961 hadi kifo chake chenye utata 1964, ilitumia KATIBA ya chama cha Ukombozi cha TANU iliyoandikwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, pamoja na mahuisho mengi yaliyopita kama yale ya 1962, 1965, 1977, 1992 bado asili ya katiba hii tuliyonayo leo ni ya MKONO wa Julius Nyerere,

Marekebisho makubwa ya Katiba yalikuwa ni mwaka 1977, lakini asili ya KATIBA ile ya Mkono wa Nyerere imeendelea kuishi na kulitendea haki Taifa na wajihi wake!

Nchi ya Gold Coast ilipopata uhuru chini ya Kwame Nkrumah licha ya kubadili jina la nchi na kuitwa Ghana, bado iliendelea kutumia asili ya katiba ya Chama cha The Convention People's Party (CPP)

Labda kwa wale wasiojua niwafahamishe kuwa Katiba ya Tanganyika African National Union (TANU) ilinakiliwa kutoka chama rafiki cha The Convention People's Party (CPP)

Ni mashirikiano mema katika makutano ya fikra za kisiasa kati ya vijana wawili wasomi na imara ambao bara la Afrika halijapata kuwa nao kwa karne hivi sasa, si wengine ni Julius Nyerere na Kwame Nkrumah walipobadilishara fikra na kuzaa matunda ya Afrika na dunia tuyatafunayo sasa,

Nimekuwa na mtazamo hasi kabisa juu ya uhuru wa Afrika kwa mda mrefu sana hasa kwa matukio niyaonayo na niyasikiao toka Afrika,

Miaka ya 1955-1975 ni kipindi ambacho Afrika ilijitoa toka mikononi mwa mkoloni, mimi huwa naamini ni kipindi ambacho Afrika haikuwa na sifa za kuwa tayari kujitawala kwa maana ya kujipatia/kupewa UHURU,

1. Afrika haikuwa na Wasomi wakuongoza nchi

2. Waafrika walikuwa kwenye lindi la kutopea kwenye ujinga, hawakuwa tayari kwa kuupokea uhuru huo,

Mfano Tanganyika ilipata Uhuru ikiwa na wasomi wachache wenye ngazi ya shahada ya Uzamili (Masters) ambae ni Julius Nyerere, na Shahada ya Uzamivu (PHd) ni mmoja tu ambaye ni Dr Vedasto Kyaruzi,

Na hata wale waasisi waliokuwemo kwenye harakati za kupigania Uhuru ndani ya TANU hawakuwa wasomi wa ngazi za juu zaidi ya Julius Nyerere,

Wazee hawa ni Julius Kambarage Nyerere, Ali Sykes, Lameck Makaranga, Gosbert Milinga, Gelmandus Pacha, Joseph Kimalando, Japhet Kirilo, Abubakar Ilanga, Saadan Kandoro, Suleiman Kitwara, Kisunguta Kabara, Tewa Said Tewa, Dosa Aziz, Patrick Kunambi, Joseph Kasela-Bantu, John Rupia, Abdul Wahid Sykes.

Nchi ya Gold Coast/Ghana ilipopata uhuru haikuwa na wasomi wengi wa Shahada, Stashada na Shahada ya Uzamivu na uzamili,

Msomi wa ngazi ya juu alikuwa mmoja tu mwenye shahada ya Uzamili (Master of Science) ndugu Kwame Nkrumah

Japokuwa usomi wa ngazi ya juu kwa watawala sio tiketi ya uwezo wa kutawala katika nchi, Hili huwa naamini ni kosa la Afrika la 1960-1975 kudai Uhuru na kupewa MAPEMA huku Waafrika hawakuwa tayari kujitawala wenyewe,

Hatua hii hunifanya niamini kuwa Afrika haikuwa imepevuka kujitawala kwa ngazi ya karne ile ya 20, huwa naamini kuwa miaka 1975-1985 ndicho kipindi ambacho Afrika ingekuwa kwenye mapito sahihi ya kujitawala, nikipindi ambacho binadamu wa Afrika angekuwa amepevuka,

Sasa ni karne ya 21, kosa lile la Karne ya 20 linajirudia katika muundo uleule kasoro nadharia tu, nalo ni upatikanaji wa Katiba mpya ya Tanzania,

Hali hii ya uhitaji wa katiba mpya kwa Watanzani ni jambo la kupongezwa na kujivunia kwa kila mtanzania, kwakuwa imedhihirika kuwa sasa Taifa limekuwa kifikra, na zaidi idadi ya wasomi katika nchi imeongezeka maradufu,


Lakini jambo la hatari na lisilokubalika nikuwa Taifa limeaminishwa kuwa Katika Mpya itapatikana kabla ya 2015, huu ni ulaghai na wendawazimu wa wazi kabisa,

Katiba ya Watanzania haiwezi kupatikana kwa miaka mitano ama mmoja huu uliosalia, Katika inayohitaji maridhiano, katiba inayopita kwenye misigano ya kitaifa, katiba inayohitaji elimu kwa Watanzania kwanza kamwe haiwezi kupatikana kabla ya 2015, kitakachopatikana kabla ya 2015 kitaitwa katiba ya kisiasa sio katiba ya Watanzania,

Ninachokiamini nikuwa Watanzania tujipe muda, turuhusu fikra na mijadala huru iendelee juu ya upatikanaji wa Katiba mpya, turuhusu majibizano ya hoja ya endelee, turuhusu Watanzania wote wake kwa waume, Wazee kwa vijana wote watoe ya moyoni bila kuogopa mawazo yao,

Katiba bora ya kiraia yenye matakwa halisi ya Wananchi inaweza kuchukua hata miaka 10 mchakato wake mpaka kuipata, hivyo katiba hii ambayo mchakato wake unaendelea SIO lazima isimamie Uchaguzi wa 2015 kama wanasiasa wanavyotusukuma tuamini hivyo,

Nionavyo muhimu katika kipindi hiki nikuwa, Watanzania, wanaharakati na Wanasiasa waendele kusimamia mchakato uendelee lakini upande wa pili wageuzi fikra zao, uanzishwe mchakato wa marekebisho ya Katiba hii iliyopo ili tuingie nayo kwenye uchaguzi 2015.Kinyume na hapo ni kuwalaghai Watanzania kuwa katika itapatika kabla 2015,

Ikumbukwe kuwa Jakaya Kikwete ambae sasa ndiye rais wa Tanzania, katika historia ya siasa zake DUNIANI, hajawahi kuhitaji katiba mpya ya Tanzania wala kuizungumzia tu, hata serikali ya Chama chama Mapinduzi ambacho yeye ndiye Mwenyekiti hakijawahi kuhitaji Katiba Mpya ya Tanzania, na zaidi serikali ya Chama cha Mapinduzi iliyodumu kwa miaka 50 sasa haijawahi kuhitaji katiba Mpya ya Tanzania,

Vyama vya upinzani na Wanaharakati wa Tanzania ndio walioasisi mapambano ya kudai Katiba mpya, tena vikipita katika mapito magumu sana yenye kuhatarisha uhai wao,

Ni baada ya uchaguzi mkuu 2010 ndipo mbinyo wakudai katiba mpya ukiongozwa na chama kikuu cha upinzani nchini huku ccm na wahafidhina wake wakipinga katukatu kuwa Taifa halihitaji Katiba mpya,

Lakini KUFUMBA na KUFUMBUA Jakaya Kikwete alilitangazia Taifa kuwa linaanza mchakato wa Katiba, akitumia neno KUHUISHA katiba.

Tafakari Chukua Hatua, Busara ni mwanzo wa kukaribisha Hekima yenye nguvu za maliza tofauti katika nchi na kupata katiba ya kiraia yenye mkono wa Mtanzania,
 
Nimejifunza mambo mengi sana kwenye uzi huu,

Kumbe mada nzuri, nzito na za kizalendo, wale pro ccm akina Hamy-D, MwanaDiwani, Chris Lukosi, Mwigulu Nchemba, Nape Nauye na wengine huwa hawagusi kabisa,

Wao mahala pau ni uzi za vurugu na uchochezi tu,

Heko sana kamanda Yeriko,
 
Back
Top Bottom