Kosa langu ni kuamua kuishi maisha yangu

Kosa langu ni kuamua kuishi maisha yangu

Ndo binadamu walivyo,usigeuke nyuma...wengine tulitoswa na ndugu tukiwa wadogo kabisa!
Leo mtu umepambana una maisha yako wanaanza kujifanya wanajali, kwangu hata kwa maigizo tu siwezi kuwa karibu na watu wa aina hiyo!
Niliamua nitegeneze ndugu zangu ambao ni wanangu tu, ndugu wa kiafrica ni mtihani ukiwazidi mari ni kosa, ukisoma kuwazidi kosa ukioa mke mwenye maendeleo na mzuri kosa, ukisomesha wanao shule nzuri kosa ukiwa fukara kosa, dawa ni kuwa ignore na ku move on with your private life, tena kama unauwezo hama kabisa kijiji au mji ukae mbali nao.
 
Kuna watu unaweza kuwa karibu nao lakini wasitambue umuhimu wako. Wanaweza kuwa ndugu, jamaa au marafiki. Na unapoamua kuachana nao na kuishi maisha yako,wanakuona kama umewatenga.

Binafsi nimewahi kupitia changamoto za kukataliwa na watu wangu wa karibu. Kila nilipojaribu kuwa mwema kwao, waliniona mbaya. Sasa nimeamua kuishi maisha yangu bila kutegemea sana hisia zao juu yangu.
Cha ajabu leo hii naonekana kama vile nimewatenga ilihali wao ndio walianza kuniumiza kwa maneno na matendo yako.

Najua wapo wengi kama mimi na wengine waliamua kuhama hadi nchi yao na pengine kubadili uraia wao. Ama kweli dunia ina mengi!
Ndugu yangu mimi muhanga wa hilo nimeamua niishi stahili yako .nimeona faida yake kuna wanadamu ata ufanye wema sawa na bure cha msingi ni kuishi maisha yako na mungu wako
 
Kuna watu unaweza kuwa karibu nao lakini wasitambue umuhimu wako. Wanaweza kuwa ndugu, jamaa au marafiki. Na unapoamua kuachana nao na kuishi maisha yako,wanakuona kama umewatenga.

Binafsi nimewahi kupitia changamoto za kukataliwa na watu wangu wa karibu. Kila nilipojaribu kuwa mwema kwao, waliniona mbaya. Sasa nimeamua kuishi maisha yangu bila kutegemea sana hisia zao juu yangu.
Cha ajabu leo hii naonekana kama vile nimewatenga ilihali wao ndio walianza kuniumiza kwa maneno na matendo yako.

Najua wapo wengi kama mimi na wengine waliamua kuhama hadi nchi yao na pengine kubadili uraia wao. Ama kweli dunia ina mengi!
Ukiwajua binadam hawaumizi vichwaa
 
Nilidhania nipo pekee yangu,kumbe tupo wengi tu....mimi rafiki yangu ni jf na tv, tofauti na hapo napanda baiskeli kwenda kijiji cha tatu huko wasiponifahamu naenda kucheza michezo ya kila aina(Usisahau kutongoza 😋😋) ili mradi nifurahi.

Nikirudi maskani ni ndani na kazini tu
Mi marafili zangu wengi ni mtaani na napenda kuwa online kweny social media zote group za marafiki zangu ni o level tu basi maana wengi tulikaa mtaa mmoja ila kuanzia advance ,chuo mpaka kazini sina mzuka nao watu wake...

sikufichi nilijaribu kumingle na vijana na wengine watu wazima kwangu wanakaribia miaka 50 ila eti story zao ni ngono tu na kingine kwa maeneo ya kazini sitaki kujua lifestyle ya mtu sijui anaishi wapi...Kawaida na yote ila sijawahi kuingia kweny kesi wala kugombana na mtu .

Watu wale tunaoenda msikitini basi ndo inatokea tunaongoza mda wa kazi maana hata watu wakubwa wapo..

Shughuli za kijamii kama msiba naweza hata kuosha vyombo japo ni mwanaume ili mradi nishiriki na kusindiza jeneza ila harusi hata iwe ya ndugu au rafiki yangu ntatoa mchango ila kuhudhuria naona balaa.


Binafsi naona kuna faida kubwa sana na furaha yangu nimewekeza kweny familia yangu na jamaa wa kitaa tena hata wao wapo bussy ....Mimi ratiba zangu kuchek mpira hata movie sio sana
 
Nilidhania nipo pekee yangu,kumbe tupo wengi tu....mimi rafiki yangu ni jf na tv, tofauti na hapo napanda baiskeli kwenda kijiji cha tatu huko wasiponifahamu naenda kucheza michezo ya kila aina(Usisahau kutongoza [emoji39][emoji39]) ili mradi nifurahi.

Nikirudi maskani ni ndani na kazini tu
Subiri uugue uone hao kijiji cha tatu kama watachukua bicycle kuja kukuuguza au kukusaidia!
Kiufupi ishi na ndugu zako kiupendo pamoja na makandokando yao usiwatenge hata wakikutenga. Wajenge, waunge na wasaidie pia kuna siku watajirekebisha labda kama ni wachawi.
 
When u begin to mind your damn business huwa wanaanza kuchonga.

Mfano Mimi pia naonekanaga nimejitenga sana kwa baadhi ya ndugu.

Sifanyi hivyo kwa kupenda ila Kuna watu pengine wamenifosi niishi hivyo.

Mfano Kuna mmoja nilikuwa natembelea kwake wakati nikipata likizo kazini kumsababahi akawa analipa Hela Kila nikienda kama vile ananipa msaada Wala mimi sikumuomba nikawa najisikia vibaya najiona kama naenda kuomba msaada na huu utu uzima .

Nikaamua nikate mguu mazima Leo naonekana nimewasusa wako wengi sana.

Siku hizi naokana kwenye events tu msiba,ugonjwa (nikishirikishwa), sherehe(nikishirikishwa) otherwise huwa sitokei kokote kule.

Niko bize na maisha yangu na mbaya zaidi sinaga mambo ya kujikomba
Sawa elon musk 😁😁
 
Ndo binadamu walivyo,usigeuke nyuma...wengine tulitoswa na ndugu tukiwa wadogo kabisa!
Leo mtu umepambana una maisha yako wanaanza kujifanya wanajali, kwangu hata kwa maigizo tu siwezi kuwa karibu na watu wa aina hiyo!
I see!
Na wengi hawajui kama wakati wa utoto ndio wakati sahihi wa kupanda kile ulichokusudia. Kama ni upendo au chuki, haiwezi sahaulika hadi ukubwani
 
Subiri uugue uone hao kijiji cha tatu kama watachukua bicycle kuja kukuuguza au kukusaidia!
Kiufupi ishi na ndugu zako kiupendo pamoja na makandokando yao usiwatenge hata wakikutenga. Wajenge, waunge na wasaidie pia kuna siku watajirekebisha labda kama ni wachawi.
sijatenga ndugu,ukiugua nakuja kujulia hali,ukifiwa nahani msiba kwa kifupi kwenye masuala ya msingi nipo sana ila siyo tujuane sana tutaaribiana cv
 
Aise kama ni ndugu ww endelea kuishi maisha yako hata wakikusema vibaya puuzia chief
Tafta circle ya marafiki wa kweli wakusaidiana kwenye hali zote ...usitegemee sana misada kutoka kwa ndugu
Ishi vzuri ukimpendeza Jehova nasio kuishi dunia inavyotaka...
Punguza mazoea sana na hao ndugu kwenye matatizo ww fika wape poleee ondokaaa usikae sana karibu nao,na fanya namna yoyote ile wasikuelewe mishe zako yani kua mtu wa kutoeleweka na usiwe muongeaji sanaa unapokua nao
Na usiwe muongeaji sana unapokuwa nao, nimeipenda hii.
 
Back
Top Bottom