KING ASSENGA
JF-Expert Member
- Oct 8, 2016
- 928
- 1,478
Kosa langu nini ni Vannesa?
Mchana usiku bado nakuwaza Vannesa. Siku wiki miaka inapita bado nakuwaza Vannesa . Kosa langu nini Vannesa?
Kwa jina naitwa Assenga Mashauri . Ni kijana wa miaka 28 kwa sasa. Bila shaka wengi mshajua mimi ni mzaliwa wa wapi kutokana na jina nililo watajia ila kwa ambao hamjapata kujua nilizaliwa Wilaya ya Rombo mkoani kilimanjaro. Ni kijana wa pili kuzaliwa kutoka kwenye familia ya Mzee Assenga na mamasawe . Familia yetu niya maadili sana na imekolea itikadi kali ya kidini. Tokea nikiwa mdogo nimelelewa kumjua Mungu kusoma maandiko na kuhudhuria kwenye nyumba ya ibada mara nyingi sana. Mimi mwenyewe nilipenda maisha hayo . Nilipata kuijua sana Dini na kujua kufundisha vizuri sana.
Mwaka 2003 nilianza darasa la kwanza mpaka nafika darasa la tano nilikuwa nikishika nafasi ya 30 mpaka 40 na kwa darasa letu lililokuwa na wanafunzi 60 na . Ila kufikia Darasa la tano kuna mwalimu alihamia shuleni kwetu anaitwa Madam Ngowi . Huyu mwalimu sijui kwanini alitokea kunipenda sana na akawa karibu sana na mimi na kunisisitiza kusoma . Alinibadilisha nikaanza kupenda kusoma . Nilibadilika haraka sana mpaka walimu wa masomo mengine walinishangaa pale nilipotoka nafasi za 30 na mpaka kuwa mtu wa tano kwenye mitihani ya mwisho wa mwaka . Huyu mwalimu alinibadilisha sana mpaka namaliza darasa la saba haikuwa ajabu tena kuwa mtu wa pili au watatu . Namshukuru sana huyu mwalimu kwani mpaka nafika chuo naamini mwamko alionipa ndio ulionifikisha.
Mpaka nafika kidato cha sita niliendelea kuwa kijana mcha Mungu sana kwa imani na vitendo . Baadhi ya mapadre walijaribu kunishawishi nikawe padre lakini naamini huo wito sikuwa nao . Mpaka namalizia kidato cha sita sikuwa nimekutana kimwili na msichana au kutumia kiungo changu cha uzazi kwa matumizi mengine zaidi ya kutolea haja ndogo. Niliendelea kuishi kimaadili sana hata nilipopata smartphone nilijiingiza tu kwenye magroup ya kidini Facebook na watsap. Wakati huo niliandika makala mbalimbali zinazotoa ufafanuzi wa maeneo mengi linapolalamikiwa kanisa katoliki na makala hizo zilienda mbali sana . Nilikuwa nimeiva sana kwenye biblia na imani yangu.
Huo ulikuwa utangulizi tu wa stori nzima ya kweli kunihusu. kosa langu nini ni Vannesa. ?
Nilikukosea nini Vannesa [emoji178]?
Sehemu ya pili ............
Mchana usiku bado nakuwaza Vannesa. Siku wiki miaka inapita bado nakuwaza Vannesa . Kosa langu nini Vannesa?
Kwa jina naitwa Assenga Mashauri . Ni kijana wa miaka 28 kwa sasa. Bila shaka wengi mshajua mimi ni mzaliwa wa wapi kutokana na jina nililo watajia ila kwa ambao hamjapata kujua nilizaliwa Wilaya ya Rombo mkoani kilimanjaro. Ni kijana wa pili kuzaliwa kutoka kwenye familia ya Mzee Assenga na mamasawe . Familia yetu niya maadili sana na imekolea itikadi kali ya kidini. Tokea nikiwa mdogo nimelelewa kumjua Mungu kusoma maandiko na kuhudhuria kwenye nyumba ya ibada mara nyingi sana. Mimi mwenyewe nilipenda maisha hayo . Nilipata kuijua sana Dini na kujua kufundisha vizuri sana.
Mwaka 2003 nilianza darasa la kwanza mpaka nafika darasa la tano nilikuwa nikishika nafasi ya 30 mpaka 40 na kwa darasa letu lililokuwa na wanafunzi 60 na . Ila kufikia Darasa la tano kuna mwalimu alihamia shuleni kwetu anaitwa Madam Ngowi . Huyu mwalimu sijui kwanini alitokea kunipenda sana na akawa karibu sana na mimi na kunisisitiza kusoma . Alinibadilisha nikaanza kupenda kusoma . Nilibadilika haraka sana mpaka walimu wa masomo mengine walinishangaa pale nilipotoka nafasi za 30 na mpaka kuwa mtu wa tano kwenye mitihani ya mwisho wa mwaka . Huyu mwalimu alinibadilisha sana mpaka namaliza darasa la saba haikuwa ajabu tena kuwa mtu wa pili au watatu . Namshukuru sana huyu mwalimu kwani mpaka nafika chuo naamini mwamko alionipa ndio ulionifikisha.
Mpaka nafika kidato cha sita niliendelea kuwa kijana mcha Mungu sana kwa imani na vitendo . Baadhi ya mapadre walijaribu kunishawishi nikawe padre lakini naamini huo wito sikuwa nao . Mpaka namalizia kidato cha sita sikuwa nimekutana kimwili na msichana au kutumia kiungo changu cha uzazi kwa matumizi mengine zaidi ya kutolea haja ndogo. Niliendelea kuishi kimaadili sana hata nilipopata smartphone nilijiingiza tu kwenye magroup ya kidini Facebook na watsap. Wakati huo niliandika makala mbalimbali zinazotoa ufafanuzi wa maeneo mengi linapolalamikiwa kanisa katoliki na makala hizo zilienda mbali sana . Nilikuwa nimeiva sana kwenye biblia na imani yangu.
Huo ulikuwa utangulizi tu wa stori nzima ya kweli kunihusu. kosa langu nini ni Vannesa. ?
Nilikukosea nini Vannesa [emoji178]?
Sehemu ya pili ............