Krismasi ya leo ni tulivu haina mbwembwe wala madoido

 
Hii xmas ni tulivu kwa upande wako tu, kuna watu na familia zaozee wanaa kula RAHA
 
Mitaa mingi Niliyopita dar Leo jioni na usiku baa nyingi nyeupe kabisa...
 

Money is the source of all evil(Discuss) - Necta hiyo nimesahau mwaka.
 
Upo sahihi.
Wengi wamefulia. Vikundi vya kusherekea pamoja havijafikia malengo kwani members wengi hawakuchanga.
Ni mfulio tu hakuna sababu nyingine.
 
Mi nimetoka kinyerez mpaka coco beach nateleza tu hamna foleni kabisa. Ilikua saa kumi na moja. Sikuamini yaani. Narudi saa mbili usiku, full kuteleza tena. No foleni. Ilinishangaza.
 
Hata hivo lengo halisi la siku hii halikuwa hilo la kujaza ma g house,ma kumbi ya starehe na kupigana ngumi Bali ni kufuata maelekezo ya muumba.
 
Huku nilipo siku ya tarehe 24 usiku kwenda 25 baa zilijaa sana hadi asubuhi..
Ila jana tarehe 25 nilipita viwanja vieili vitatu kweupeee watu wanejua when to stop spending na sio kutumia had senti ya mwsho
 
Ulikuwa maeneo gani bwashee?

Ununio beach ilikuwa balaa!
 
Ninachoamini kadri miaka inavyo kwenda neno "SIKUKU" Linapungua hadhi ni ama mifumo ya maisha imebadika kwa kiasi kikubwa au fikra zetu zimebadilika pia....

2000's nilikua na maisha aliyonijalia MUNGU lakini likifika swala la sikukuuu aiseee hadi wanyonge huonekana ila now yani no one cares kabisaa.
 
Hali ngumu aisee,hata upande wa biashara zimedoda vibaya,kuna jamaa yangu muuza nyama buchani akaona atumie fursa hii ya krismas vizuri akanunua nyama ya kuuza ya kutosha mara 2 zaidi ya ile anayonunua siku ya kawaida huwezi amini jana nimepita buchani kwake nyama iko vile vile hadi anajilaumu!! Jamani mtaani kwa moto sasa hivi hakushikiki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…