Krismasi za kukumbuka (sad memories)

Krismasi za kukumbuka (sad memories)

Nakumbuka 2022 baada ya kumaliza chuo nipo Jobless pale Dar baada ya michongo yangu kufeli mazima nilikuwa Ghetto na mshkaji wangu mmoja tulipiga Ugali dagaa safii kabisa sikuwa na hata mia maana nakumbuka Dagaa zenyewe tulikopa kwa Mangi. Jioni kulikuwa na Mechi ya Yanga vs Azam kuna msamaria akanitumia Liten at least ndio nikaweza kutoka ndani.
 
Duh
Simulizi ya pili
Hii ni 1994. Nimefanya Kazi kwa mtu kule SABASABA mpaka tar.20.. Nikaambiwa mshahara tar 23.. Kumbe tajiri kajipanga kuondoka tar 22.. Nafika kwake tar 23 naambiwa kaondoka jana kwenda mkoani😭 sikuwa na pesa kabisa
Aliyenikoa ni bibi mmoja aliyekuwa anauza maji pale SABASABA (sikuwahi kumlipa wema wake ule) alinipa shiLingi 5000 ilikuwa kubwa sana kipindi Hicho
Sasa ni tarehe 23 natakiwa kusafiri tar 24 kwenda kijijini kwa ajili ya Xmas
Basi kujiongeza nikapata mchongo wa maembe huko Chanika Mvuti
Nikafanikiwa kupata 20 ya mkopo mahali.. Nikawa na 25 sasa.. Nikaenda zangu Mvuti
In short mpaka saa tatu usiku nilikuwa Buguruni na tenga langu la maembe nikiwa nimeshatumiq kama elfu 22 hivi gharama zote na matarajio ni kupata 45 hivi
Ugeni kwenye biashara jambo baya sana.. Nikaambiwa yale maembe yangu yanaweza kununuliwa kwa jumla elfu 25 tuu ama sivyo nikomae mwenyewe niuze mojamoja
Baada ya mabishano ya muda mrefu nikashindwa mimi inabidi nikubaliane nao
Sheshe likaja kwenye kuyamwaga chini yakaguliwe😭😭😭
1. Nilichomekewa maembe mabovu almost robo tenga
2. Waliweka majani mengi chini ya tenga..
Niliambulia Shilingi elfu 9000.tuu.
Hapo ndo unaweza kuanza kuwaza kwani Mungu yupo kwa ajili ya watu gani? So sad
 
Sinyanyuki niuweniπŸ˜‚
Hahaha kuna mila na desturi zina dharililisha utu wa mtu.

Yeye afanyacho huko Dar ni mambo yake binafsi, kwanini wao wadhani anao wajibu kuwaeleza wao, na eti lazima asimame wakati akijieleza?
 
Safi sana, huo ndio uwanaume.

Kuwa na mali nyingi haumpi mtu ufalme au mamlaka kudharilisha mwenzake.

Kaweka mguu chini , sinyanyuki niuweni.
Hahahha
Hahaha kuna mila na desturi zina dharililisha utu wa mtu.

Yeye afanyacho huko Dar ni mambo yake binafsi, kwanini wao wadhani anao wajibu kuwaeleza wao, na eti lazima asimame wakati akijieleza?
Ni changamoto.. Imagine kapambana pengine mwaka mzima na hata hiyo nauli ya kurudi home kakopa halafu anakutana na kitu moto😭
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚! Umenimbusha mwaka 2006 nikiwa nimejishikisha kibarua cha kufundisha shule moja Dar maarufu ya private ya wakatoliki. Basi, katika zungumza zungumza muda wa chai ikatokea hoja ya biashara ya kununua mbuzi mikoani na kuzileta Dar machinjioni Vingunguti na kuziuza kwa bei nzuri. Yaani mikoani mbuzi unamnunu elfu 5 hadi 8 lakini ukimfikisha Dar bei ni kuanzia 30 elfu hadi 60. Mwalimu mwenzetu kajaa mazima sijui hela alizitoa wapi kapakia lory. Kipindi hicho kilikuwa kipindi cha mvua daraja la Luvu likafurika magari hayapiti mbuzi kwa wiki mbuzi wengi wakadhoofu na kufa. Kwa ufupi hakuambualia hata senti na mwisho wa siku akawa haonekani kazini mpaka natoka pale sikuwahi kumuona!
Duh! Mwalimu alikula hasara ya Karne akaona iswe taabu akaamua kuacha na KAZI πŸ˜‚
 
2024, mwanangu alitegema kuoata mtoto bahati mbaya alizaliwa na mtoto bahati mbaya siku ya christmass.
Kwa upande wangu hii ni mbaya nilitegemea kuitwa babu..
Tunamshukuru Mungu.
 
Hahahha

Ni changamoto.. Imagine kapambana pengine mwaka mzima na hata hiyo nauli ya kurudi home kakopa halafu anakutana na kitu moto😭
Unajua hata kama mtu anataka kukusaidia usikubali akakudhalilisha. Kama nia yao ni kumsaidia, wampe huo msaada basi waanze upya, wamuulize matokeo mwakani.

Wao hawajajieleza wanafanya nini huko waliko, hakuna aliyewauliza. Mwamba kaenda nyumbani kama wao walivyokwenda, wafurahi, wasalimiane, hayo mengine waulizane private, na kila mtu aendelee kivyake.

Lakini haya mambo ya kupeana MIC halafu mtu anakwambia tuambie huko Dar es Salaam unafanya nini, sio poa kabisa.

Nimependa msimamo wake, Yani ni zile kwamba "maisha yangu ni yangu, nani kakwambia nataka kuwa kama wewe, hata kama una good life?"

Jamama mmoja nasema nyie mnao fanikiwa punguzeni ushauri, siyo kila mtu ana waona nyie ni wamaana, hivyo msidhani kila mtu anapenda kuwa kama nyie, au kufanya mfanyacho.

Ana maliza kwa kusema "To hell with your good life" Ukivaa suti ni mapenzi yako, mimi napenda jeans. Ukila kuku ni mapenzi yako mimi napenda matembele, your life your choice.

Hahaha ningekuwepo ninge mnunulia beer mshikaji, big up kwake.
 
Unajua hata kama mtu anataka kukusaidia usikubali akakudhalilisha. Kama nia yao ni kumsaidia, wampe huo msaada basi waanze upya, wamuulize matokeo mwakani.

Wao hawajajieleza wanafanya nini huko waliko, hakuna aliyewauliza. Mwamba kaenda nyumbani kama wao walivyokwenda, wafurahi, wasalimiane, hayo mengine waulizane private, na kila mtu aendelee kivyake.

Lakini haya mambo ya kupeana MIC halafu mtu anakwambia tuambie huko Dar es Salaam unafanya nini, sio poa kabisa.

Nimependa msimamo wake, Yani ni zile kwamba "maisha yangu ni yangu, nani kakwambia nataka kuwa kama wewe, hata kama una good life?"

Jamama mmoja nasema nyie mnao fanikiwa punguzeni ushauri, siyo kila mtu ana waona nyie ni wamaana, hivyo msidhani kila mtu anapenda kuwa kama nyie, au kufanya mfanyacho.

Ana maliza kwa kusema "To hell with your good life" Ukivaa suti ni mapenzi yako, mimi napenda jeans. Ukila kuku ni mapenzi yako mimi napenda matembele, your life your choice.

Hahaha ningekuwepo ninge mnunulia beer mshikaji, big up kwake.
Hahaha ningekuwepo ninge mnunulia beer mshikaji, big up kwake.πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
2024, mwanangu alitegema kuoata mtoto bahati mbaya alizaliwa na mtoto bahati mbaya siku ya christmass.
Kwa upande wangu hii ni mbaya nilitegemea kuitwa babu..
Tunamshukuru Mungu.
Pole sana sana
 
Chrismass ya Mwaka 1989 ilinikuta na pacha wangu vibaya sana. Tulikuwa tumemaliza Darasa la SABA na matokeo ni kuwa HATUKUCHAGULIWA kwenda sekondari.

Niliona ndo mwisho wa maisha maana kukosa kwenda seko ilikuwa ni kama Huna future tena. Hatukuwa na furaha kabisa na sikukuu haikuwa na maana tena.
 
Sasa ndonaelewa wazazi walikua wanapitia presha ya kiwango kipi pale sikukuu zinapokuja na ela hakuna nyumbani,tulikua tunajiliza tukikosa nguo za sikukuu ila sasa ndonaelewa wanangu wanaponigizama sikukuu imefika na sina ela
 
Back
Top Bottom