Kuachiwa Ndege Canada: Lissu, Fatma Karume na Membe muombeni radhi Profesa Kabudi

Kuachiwa Ndege Canada: Lissu, Fatma Karume na Membe muombeni radhi Profesa Kabudi

Wakudadavuwa

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2016
Posts
17,506
Reaction score
16,003
Ndugu zangu,

Takribani majuma mawili yaliyopita Waziri wa Mambo ya nje Prof.Palamaganda Kabudi aliutaarifu Umma kutokea Dodoma siku ambayo Rais Magufuli alikuwa na kazi ya kikatiba kuwaapisha mabalozi wetu.

Prof.Kabudi alimuelezea rais huku akieleza jinsi ambavyo wananchi wa Tanzania watauchukua ushindi dhidi ya kaburu Stein kwa mara nyingine baada ya ''kumcharaza'' katika mahakama ya Gauteng kule bondeni (Afrika ya kusini).

Aliyekuwa wa kwanza kubeza ni Ndugu Membe huku akiaminisha umma kuwa Prof.Kabudi hatafanikiwa, akishauri kuwa njia pekee ni kumuita mkulima Stein kwenye meza na ''kumlipa chake. Ajizi nyumba ya njaa naye Tundu Lissu na Fatuma Karume wakauvagaa mkenge huku akiwa hawana uzoefu wowote na mashauri katika korti ya kimataifa, walijaribu kuwaapooza wafuasi wao ambao walikuwa wenye hasira nyingi baada ya kushauriwa vibaya kujitoa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Bila kuchelewa, wafuasi wa CHADEMA na wanasiasa hao wakaivagaa mitandao huku wakionesha dharau kwa Prof.Kabudi na Watanzania, wakisema Mkulima Stein ni ''kiboko'' wakiowanukuu Lissu,Fatuma na Membe.

Wanasheria wetu wazalendo walinyamaza kimya huku wakiandaa hoja za kumshinda ''Mkulima Stein'' kortini. Kwa hoja zilizotolewa kortini hatimaye siku mbili zilizopita Mahakama ya Canada iliipa Tanzania ushindi kwa mara nyingine tena huku ikiweka ''precedence'' kwa siku zijazo.

Nimalize tu kwa kusema, Hongereni wananchi wazalendo wa Tanzania, Mmeshinda tena!
 
Leteni hati ya hukumu na cost za kesi acheni porojo.

Hati za hukumu za south africa na za canada ziko wapi? kwanini iwe siri wakati ni pesa za walipa kodi?

Mkulima kalipa garama za kesi? za kulala hotel za nyota 5 ujumbe wa kabudi South Na Canada?

Watanzania sio wajinga kiivyo.
 
counting-cash-gif-4.gif

Mkulima akizihesabu na kuzihakikisha huko Canada
 
Acha kuyumba na biti za mpiga sumari wewe cheza tuni yako! Ulikwina siku zote hizo usiuandike huu ushuzi wako hapa? Yaani mmelipa kimyakimya Kisha mnataka kutuimbisha mmeshinda kesi! Weka hukumu hapa tuione Kama hujanikimbia! Yaani hii praise team inampotosha sana Magu! Hebu awaweke Kando kwanza ili ajisikilize mwenyewe! Wakudadavua, sahau viti maalumu msimu ujao!
 
Back
Top Bottom