Kuachiwa Ndege Canada: Lissu, Fatma Karume na Membe muombeni radhi Profesa Kabudi

Kuachiwa Ndege Canada: Lissu, Fatma Karume na Membe muombeni radhi Profesa Kabudi

Ndugu zangu,

Takribani majuma mawili yaliyopita Waziri wa Mambo ya nje Prof.Palamaganda Kabudi aliutaarifu Umma kutokea Dodoma siku ambayo Rais Magufuli alikuwa na kazi ya kikatiba kuwaapisha mabalozi wetu.

Prof.Kabudi alimuelezea rais huku akieleza jinsi ambavyo wananchi wa Tanzania watauchukua ushindi dhidi ya kaburu Stein kwa mara nyingine baada ya ''kumcharaza'' katika mahakama ya Gauteng kule bondeni (Afrika ya kusini).

Aliyekuwa wa kwanza kubeza ni Ndugu Membe huku akiaminisha umma kuwa Prof.Kabudi hatafanikiwa, akishauri kuwa njia pekee ni kumuita mkulima Stein kwenye meza na ''kumlipa chake. Ajizi nyumba ya njaa naye Tundu Lissu na Fatuma Karume wakauvagaa mkenge huku akiwa hawana uzoefu wowote na mashauri katika korti ya kimataifa, walijaribu kuwaapooza wafuasi wao ambao walikuwa wenye hasira nyingi baada ya kushauriwa vibaya kujitoa uchaguzi wa serikali za mitaa.

Bila kuchelewa, wafuasi wa CHADEMA na wanasiasa hao wakaivagaa mitandao huku wakionesha dharau kwa Prof.Kabudi na Watanzania, wakisema Mkulima Stein ni ''kiboko'' wakiowanukuu Lissu,Fatuma na Membe.

Wanasheria wetu wazalendo walinyamaza kimya huku wakiandaa hoja za kumshinda ''Mkulima Stein'' kortini. Kwa hoja zilizotolewa kortini hatimaye siku mbili zilizopita Mahakama ya Canada iliipa Tanzania ushindi kwa mara nyingine tena huku ikiweka ''precedence'' kwa siku zijazo.

Nimalize tu kwa kusema, Hongereni wananchi wazalendo wa Tanzania, Mmeshinda tena!

Ni jambo jema sana ndege yetu kuachiwa maana hiyo ndege ilinunuliwa na kodi za watanzania na si za kiongozi yeyote hata huyo Kabudi.
Kwenye hiyo kesi kuna mambo mawili ya kuambiwa:

1: Kesi himefanyika ndani ya siku hizo na hukumu kutolewa? Je hiyo hukumu, tumeshinda/wamekubaliana kulipa au tumesamehewa?

2: tuambiwe kama tulishindwa hiyo kesi lakini kwa sabau tulikuwa na pesa, basi tukalipa.
 
Labda atadaiwa taratibu ...........
Leteni hati ya hukumu na cost za kesi acheni porojo.

Hati za hukumu za south africa na za canada ziko wapi? kwanini iwe siri wakati ni pesa za walipa kodi?

Mkulima kalipa garama za kesi? za kulala hotel za nyota 5 ujumbe wa kabudi South Na Canada?

Watanzania sio wajinga kiivyo.
Ili niwe mzalendo ni lazima,nisihoji,nisiulize chochote,unidaganye,basi nitakuwa nimeitendea nchi yangu vema

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tumelipa, tumesamehewa au tumeshinda kesi? Naomba majibu

Kama tumelipa nini maoni yako?? Na kama tumesamehewa ni nini maoni yako?? Na vipi kama tumeshinda wewe maoni yako ni yapi??
 
Kama tumelipa nini maoni yako?? Na kama tumesamehewa ni nini maoni yako?? Na vipi kama tumeshinda wewe maoni yako ni yapi??

Maoni ni Serikali iache Tabia ya kuharalisha dhuluma kutumia pesa nyingi kukwepa Deni badala ya kulipa Deni
 
Kamanda kwa hiyo kila mkono wako unapobonyeza keyboard kutukana unalipwa bei gani?

Sent using Jamii Forums mobile app

Kama wewe unalipwa na CCM kutengeneza propaganda mbalimbali zikiwemo za kuharalisha dhuluma haramu usifikiri wengine wanaokataa ujinga wenu nao wanalipwa chochote, kukataa ujinga siyo lazima kulipwa na mtu, anayelipwa ni yule anayeamua kutengeneza ujinga kama wewe unavyofanya mara nyingi humu mitandaoni.
 
Mzungu kalipwa kimya kimya kaombwa akae kimya maana kabudi anajua Siri ikivuja atakosa kujimwambafy kama kawaida yake
kwahiyo unataka kutuambia nini..awe amelipwa au hajalipwa inatuhusu nini au inakusaidiaje wewe kwa mfano....we jua imeachiwa inakuja kupiga kazi nchini basi...kama una hela utaipanda usafiri nayo unapotaka.ndege si yako..ndege ya watanzania...labda kama wewe sio mtanzania
 
Ndege haikuachiwa bure wamelipa ingawa profeselii wa Olijino comedy ndugu Kabudi kamuomba mkulima wa kizungu akae kimya atunze siri ili Kabudi apate kujimwambafy kuficha Aibu yao.
 
kwahiyo unataka kutuambia nini..awe amelipwa au amelipwa inatuhusu nini au inakusaidiaje wewe kwa mfano....we jua imeachiwa inakuja kupiga kazi nchini basi...kama una hela utaipanda usafiri nayo unapotaka

Kwani wewe mambo yote ya Nchi hii huwa yanakusaidia nini kwa mfano? Si kila kitu lazima kikuhusu au kisaidie chochote kwako, tunachokikataa ni kuharalisha dhuluma kuitia Aibu kubwa Taifa, dhuluma za kishamba ndizo wanazikataa wengi.
 
Dhuluma kwa mkulima wa kuzungu ndicho wengi hawakitaki kwani badala ya unafuu inatumika pesa nyingi kukwepa Deni, Yaani Deni limegeuka kuwa fursa ya wajanja wachache kupiga pesa kwa kisingizio kuwa wanapambana na mkulima kuokoa pesa ni aina fulani ya ufisadi wa kijanja
 
Back
Top Bottom