Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

Ni mikoa iliyokaa kistrategia pia kwa kuwa ni rahisi kupata mashabiki wa nchi jirani nyingi kwa gharama nafuu kiusafiri. Ni rahisi kuifikia Mwanza kwa mashabiki kutoka Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi, Kongo DRC (upande wa Kaskazini Magharibi na hata baadhi ya maeneo ya Tanganyika Province), Sudani ya Kusini. Kadhalika ni rahisi kwa mashabiki kutoka Zambia, Malawi, Kongo DRC Mashariki, Zimbabwe, Msumbiji, Namibia, Botswana, na hata Afrika Kusini.
 
Imagine Zambia akifuzu ,Mbeya itafurika Mashabiki wao lakini huko Dodoma sijui Arusha ni upuuzi
 
Arusha ni mji bora na uliondelea kuliko mwanza. na ni mji wenye infrastructures bora kuliko Mwanza na mbeya combined.
Mimi nilitamani iwe Arusha, Dar na Zanzibar. Hiyo mikoa mingine imekaa kushoto.
 
Arusha ni mji bora na uliondelea kuliko mwanza. na ni mji wenye infrastructures bora kuliko Mwanza na mbeya combined.
Mimi nilitamani iwe Arusha, Dar na Zanzibar. Hiyo mikoa mingine imekaa kushoto.
Unadhani miundombinu unayoita Bora huko Arusha ilishushuka na mvua? Ni upendeleo ule ule wa kuchukua pesa zetu kwenda kujenga huko.

Kuna siku tutaikomesha hii tabia.By the way baada ya Afcon uwanja utabakia pambo,wavuta bangi na mpira wapi na wapi?

Mwisho Kwa Sasa wanaweza Jenga ila hata wa watu 20,000 Kwa Arusha ingewafaa.

Sisi tunataka viwanja vikubwa vya watu kuanzia 30,000-50,000 maana tuna mashabiki wenye wazimu wa soka na tuma Vijana wenye vipajo vya michezo.Tunahitaji viwanja sio Kwa Ajili ya Afcon Bali michezo.
 
Kwanza kuna watu kutoka corners nyingine za Africa hawajawahi kuliona Ziwa Victoria, hii ingekuwa fursa kwao. Ingawa Arusha nayo inafaa kwa kuwa kuna vivutio wa watalii vingi.

Tatizo la Arusha nawahurumia wageni. Ule mji hauna adabu kabisa:umejaa wahuni, wasela mavi, wavuta bangi na wezi kama wote. A typically hooligan place! Wageni wetu wanaenda kuibiwa, kujeruhiwa, kupigwa vidole sehemu nyeti, kubakwa,n.k. MJI WA HOVYO SANA ULE!
 
Game nyingi sana za maana zimechezwa Arusha, na ule mji umeandaa mashindano na events kubwa za kimataifa na watu wake wamekuwa wenyeji wa matukio mengi sana ya kimataifa na mji ule unaweza hata sasa hivi kupokea wageni wengi wa caliber ya juu.
Msifananishe Arusha na mwanza, hayo ni mambo ya humu jamiiforums siyo kiuhalisia.
 
Umeongea ukweli mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…