Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

Kubagua Mwanza na Mbeya AFCON haikubaliki

Wewe si ndio tukipindea viongozi unaleta uzwazwa...

CCM kirumba wa Mwanza ni uwanja mzuri ila umeachwa umeenda kuchukuliwa wa Arusha wenye kuhitaji ukarabati mwingi, wakati CCM kirumba ilikuwa ni pesa kidogo tu uwanja unakaa shikopa
Mkuu huko Arusha unaenda kujengwa uwanja mpya na kama kuna ukarabati wa uwanja uliopo basi ni kwaajili ya mazoezi tu
 
Hii tabia ya kubagua Mikoa ya Mbeya na Mwanza kwenye mambo ya Maendeleo naona imeanza kukita mizizi.

Wakati mikoa mingine ikipendelewa sie Mwanza na Mbeya tumekuwa wahanga wa kutengwa na Kubaguliwa kwenye masuala mbalimbali ya kimaendeleo licha ya kuwa tunastahili kwa vigezo na sio kwa kuonewa huruma.

Haiwezekani na haiingii akilini eti kubagua miji hii maarufu kwa wanamichezo na badala yake wakaipendelea miji isiyo na mashabiki wala wanamichezo ya Arusha na Dodoma.

Nasisitiza tunadai haki yetu na sio favour kwa sababu zifuatazo;

Mwanza
  • Mikoa wa pili kuchangia Pato la Taifa GDP baada ya Dar.
  • Jiji la Pili kuwa na population kubwa baada ya Dar.
  • Jiji la 3 Kuchangia Mapato ya Kikodi.
  • Uwepo wa mashabiki wa kutosha na wanamichezo.

Mbeya
  • Mikoa wa 3 kuchangia Pato la Taifa nyuma ya Dar na Mwanza.
  • Jiji la 6 Kwa idadi ya watu Tanzania.
  • Jiji la 2 Kwa Wanamichezo wengi kama timu za NBC&Championship.
  • Pamoja na mtoto Wetu Songwe ni Mkoa wa 4 Kwa mapato ya Kikodi.
View attachment 2766225
Kwa vigezo hivyo pekee tunastahili kupata kitu sio kwa upendeleo bali kwa haki.

Habari za kusema hakuna hoteli au miundombinu ya kisasa na blaa blaa kama hizo zinatokana na Serikali hii ya ccm kuchukua pesa na jasho letu kwenda kujenga Mikoa mingine kama Arusha, Dodoma, Tanga, Dar nk.

Ni aidha Serikali ianze ujenzi wa viwanja vya Kisasa kwenye miji yetu kutufuta machozi na sio lazima kwa ajili ya AFCON bali kutupa heshima yetu kwenye michezo au tumwage mboga 2025.

Hali hii haivumiliki na haikubaliki, ni wakati wa watu wa Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini kufanya jambo la kujitambua mwaka 2025 endapo wataziba maskio.

Ni bora kumwaga mboga sio kwa sababu tunawakubali Wapinzani bali ni kwa nia ya kukomoana kwamba tukose wote, tumechoka kutengwa na tabia hii ikiendelea ipo siku tutagawana fito.
View attachment 2766050View attachment 2766051View attachment 2766052

Angalizo: Haya ni maoni na mtizamo binafsi, yasichukuliwe kama uchochezi.Nachokonoa mada Kwa maslahi mapana ya Nchi hii na watu wa Mbeya na Mwanza.
Watu wenu wanakula milungura ya waarab unadhani nini kitafanyika tena huko?!!
 
Kote ni Tanzania ndugu.Punguza jazba hii siyo AFCON ya mwisho wakati mwingine tukipata nafasi ya kuandaa hiyo miji uliyotaja pengine nayo ikapata nafasi hiyo ya kujengewa viwanja tena Kwa wakati huo vikawa ni vikubwa na vizuri kuliko vya Sasa
 
Kote ni Tanzania ndugu.Punguza jazba hii siyo AFCON ya mwisho wakati mwingine tukipata nafasi ya kuandaa hiyo miji uliyotaja pengine nayo ikapata nafasi hiyo ya kujengewa viwanja tena Kwa wakati huo vikawa ni vikubwa na vizuri kuliko vya Sasa
Ubaguzi hauko tuu Afcon Bali kwenye nyanja nyingine nyingi tuu za Maendeleo
 
Enzi za mwamba alisema atakenga Chato uwanja kama wa Lupaso. Ikishindikana mtajengewa 2070 wakati tunashiriki kombe la Dunia.
 
Hii tabia ya kubagua Mikoa ya Mbeya na Mwanza kwenye mambo ya Maendeleo naona imeanza kukita mizizi.

Wakati mikoa mingine ikipendelewa sie Mwanza na Mbeya tumekuwa wahanga wa kutengwa na Kubaguliwa kwenye masuala mbalimbali ya kimaendeleo licha ya kuwa tunastahili kwa vigezo na sio kwa kuonewa huruma.

Haiwezekani na haiingii akilini eti kubagua miji hii maarufu kwa wanamichezo na badala yake wakaipendelea miji isiyo na mashabiki wala wanamichezo ya Arusha na Dodoma.

Nasisitiza tunadai haki yetu na sio favour kwa sababu zifuatazo;

Mwanza
  • Mikoa wa pili kuchangia Pato la Taifa GDP baada ya Dar.
  • Jiji la Pili kuwa na population kubwa baada ya Dar.
  • Jiji la 3 Kuchangia Mapato ya Kikodi.
  • Uwepo wa mashabiki wa kutosha na wanamichezo.

Mbeya
  • Mikoa wa 3 kuchangia Pato la Taifa nyuma ya Dar na Mwanza.
  • Jiji la 6 Kwa idadi ya watu Tanzania.
  • Jiji la 2 Kwa Wanamichezo wengi kama timu za NBC&Championship.
  • Pamoja na mtoto Wetu Songwe ni Mkoa wa 4 Kwa mapato ya Kikodi.
View attachment 2766225
Kwa vigezo hivyo pekee tunastahili kupata kitu sio kwa upendeleo bali kwa haki.

Habari za kusema hakuna hoteli au miundombinu ya kisasa na blaa blaa kama hizo zinatokana na Serikali hii ya ccm kuchukua pesa na jasho letu kwenda kujenga Mikoa mingine kama Arusha, Dodoma, Tanga, Dar nk.

Ni aidha Serikali ianze ujenzi wa viwanja vya Kisasa kwenye miji yetu kutufuta machozi na sio lazima kwa ajili ya AFCON bali kutupa heshima yetu kwenye michezo au tumwage mboga 2025.

Hali hii haivumiliki na haikubaliki, ni wakati wa watu wa Kanda ya Ziwa na Nyanda za Juu Kusini kufanya jambo la kujitambua mwaka 2025 endapo wataziba maskio.

Ni bora kumwaga mboga sio kwa sababu tunawakubali Wapinzani bali ni kwa nia ya kukomoana kwamba tukose wote, tumechoka kutengwa na tabia hii ikiendelea ipo siku tutagawana fito.
View attachment 2766050View attachment 2766051View attachment 2766052

Angalizo: Haya ni maoni na mtizamo binafsi, yasichukuliwe kama uchochezi.Nachokonoa mada Kwa maslahi mapana ya Nchi hii na watu wa Mbeya na Mwanza.
JPM alikuwa wa Kanda ya Ziwa, miradi mingi ilitekelezwa huko mpaka viwanja vya ndege ambavyo havina matumizi kwa sasa. Mbeya mna Spika( kiongozi wa mhimili) na Mbeya ina miradi mingi ya ujenzi inaendelea kwa sasa. Hivyo kwa kutulia. Dar ndio mbabe wa mapato hapa nchini, utalii tuwaachie Kanda ya Kaskazini. Hivyo kaa kwa kutulia kabisa.

Sent from my SM-A6050 using JamiiForums mobile app
 
Hakuna mkoa zaidi ya dar na Arusha unaoipa serikali mapato ya kujiendesha na maendeleo.
Tofauti kati ya Dar na Arusha ni kwamba Arusha inaizidi Dar kwa mapato ya NGO foreign exchange ambayo inachangia serikali kuwa na uwezo wa kufanya miradi na kununa madawa, machinery etc...

Kwa hiyo , wewe waambie hao watu wengine lakini mimi najua by data kwamba Arusha ni mkoa muhimu sana kwa Tanzania na haupati miradi proportional to its revenue collection.
Panga pangua mwanza haikufaa hata kupata Airport kubwa kuliko Arusha, haifai hata kuinvest ni hasara tupu. There will never be tax collected in Mwanza kupita Arusha hata serikali ikisema sasa hatuwekezi Arusha.
Uwanja siyo wa mpira tu, uwanja ule unaweza ku-host track meets (mashindano ya riadha), mashindano ya majeshi ya dunia na Africa, mashindano ya walemavu etc.. na Arusha bado ikahimili ugeni wake.
Tanzania hakuna mkoa wa kuulinganisha na dar, mikoa iliyobaki imeachwa na dar karibu kwa kila kitu
 
Back
Top Bottom