Kubenea awaonya wanaopiga ramli kuhusu hatima yake CHADEMA, azungumzia Virusi vya Corona

Kubenea awaonya wanaopiga ramli kuhusu hatima yake CHADEMA, azungumzia Virusi vya Corona

Tunakuunga mkono mh kubenea hamia chama chochote Achana na hao wapiga majungu wa ufipa
Nani alimshauri kukuunga na cdm? Ni wewe? Kama sio wewe, mbona unadandia kazi ya aliyemshauri na kumshawishi mwanzoni!
Unajidanganya Sana ukisaidiana na bulicheka wako hapo lumumba kuwa mnaweza kumnunua kiuongozi yeyote wa upinzani Ila mnasahau kuwa nao Wana akili kubwa kwani wanaotoka chama kikubwa kinachotishia uhai wa ccm!
Polepole a.k.a bulicheka alitweet Jana kuwa kubenea angetangaza kuhamia ccm leo! Natakiwa na hayatakuwa!
Mshauri huyo Dr uchwara aandae nondo za kuwashawishi wananchi juu ya miradi hewa isiyokamilika ambayo imewatia umaskini wa miaka 50 iliyopita! Kinyume chake jiandaeni kuwa wapinzani!
 
Haya ni matumizi mabaya ya fedha za misaada. Watu wa Mungu wamejitoa kusaidia mapambano dhidi ya Corona matokeo yake vifaa walivyotoa bure vinauzwa fedha anapewa Polepole kulipa madeni ya Lumumba Bk7!

Sent using Jamii Forums mobile app
Mzee Vuta nikuvute alimuibua polepole ndio kakopa pesa za kuwalipa vijiposho vyao! Waliaibika na kupigika mno hapo Kati!
 
Kubenea Ndani ya chadema umekuwa kama punching bag, kila kiongozi anakutukana na mtandaoni wame mobilize vijana kukutukana

Hawa Chadema ni watu wasio na shukran wala heshima

Chadema walikutumia Wewe kuanika ajenda zao sasa wanakutukana

Kupitia gazeti la mwanahalisi ambalo lilikuwa linaongozwa kwa kusomwa Nchini uliripoti kila hotuba za Chadema

Kila tukio la Chadema uliliandika leo hii wanakuona taka taka hii ni kweli jamani? Mimi nakasirika sana

Kupitia hoja za Chadema uliingia matatizoni na mafisadi ukamwagiwa tindikali almanusura uwe kipofu serkali ikakutibia

Bado kupitia hoja za Chadema, gazeti lako lilifungiwa hadi ukaingia kwenye madeni makubwa

Hawa ambao wakutukana leo hasa mitandaoni tukiwafatilia 2007 walikuwa hawaijui hata Chadema, walikuwa hata hawajui mwenye Chadema ni nani?

ati leo Ndio wanakuona Wewe mbaya kwa lipi?

Nikiikumbuka Chadema ya dr slaa ilyoheshimika nikiifananisha na hii ya kina mdee nagundua Chadema ina dhambi nyingi inatakiwa itubu kwa dr. Slaa

Kubenea waachie chama acha kutishwa na watu wasio jitambua

Ondoka Chadema Achana na vyama vya watu

Akufukuzay...
Msaliti anaweza akaondoka tu, aondoke taasisi imara hazifi kwa kuwa misingi yake haijajengwa juu ya dola bali kwenye mioyo ya wananchi.
 
Daaah! Asante kwa udadafuzi mzuri nakutufumbulia mengi ambayo wengi hatukuyajua juu ya EL&SK.

Lakini pia kwa mbaaali hivi, naona unajaribu kumchimba biti SK nae asiwatupe kama komu alivowafanya.

But pamoja na biti lote, anything can happen. Namkubali SK, so, stay tuned and mark my words

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nakufuatilia uzuri ndugu Mshana, endelea kumwaga nondo.
Kumekucha tena tuendelee
Kama inavyofahamika wazi kuwa EL alikuwa na kiu kubwa ya kuwa rais wa Jamhuri na kwa vyovyote waliunda umoja yeye na JK way back 1995 ili mmojawao awe akiwa raisi basi mwingine awe makamu ama Waziri mkuu.. Aliyetibua hii mission alikuwa hayati Mwalimu Nyerere.. Lakini tukirudi nyuma zaidi miaka ile ya 80 mwishoni kipindi cha mzee Mwinyi wakati huo Mzee Malecela akiwa na nguvu kubwa pia naye alishaonesha nia ya dhati ya kuutaka urais... Kama kwa EL tu aliyetibua mipango yote alikuwa Mwalimu Nyerere mchonga meno
Malecela alikuwa kajijenga mno ndani ya ccm kuanzia chini mpaka juu.. Wajumbe wote wa mikoani na wilayani walikuwa team yake.. Tunatambua dhima ya wakuu wa wilaya na mikoa.. Hawa ndio wasimamizi wa kamati za ulinzi na usalama.. Na ripoti zote za kila siku walikuwa wanaziwasilisha kwa Waziri mkuu... Malecela pia alishawahi kuwa Waziri mkuu
Mbinu za Malecela ndio zilikuja kuwa mbinu za EL.. Ni kama alikopi na kupest na kumbuka Malecela alishawahi kuwa boss wake..... Nia ya dhati ya Kukaa magogoni haikuwahi kuwatoka vijana wawili machachari almaarufu kama BOYS II MEN.. Jakaya na Lowassa.. Waliendelea kujiwekeza na hatimaye 2005 JK akawa rais na kumteua Lowassa rafiki wa siku nyingi kuwa Waziri mkuu
Mambo yalikuwa ok mwanzoni lakini uchapakazi wake ulianza kuwatia shaka wengi. Alikuwa na kila elements za hayati Edward Moringe Sokoine wajina wake.. Hili liliwatisha wengi... Taratibu waziri mkuu akawa maarufu kuliko boss wake
Mpango wa wananchi uliovumbuliwa na Waziri mkuu EL wa kuchangia elimu kwa hiari ulikuwa na matokeo chanya ya kutisha.
Ndipo hapa JK akatonywa kuwa ukimuachia huyu 2010 hutoboi atakutoa.. Hii pesa ya UJENZI wa madarasa na kuchangia elimu account zake zilikuwa chini ya PM.. Kwahiyo alikuwa na madaraka nazo kwa asilimia mia.. Ikaonekana wazi anaweza kutumia mwanya huo kujikita zaidi na kukusanya pesa kwa ajili ya uchaguzi 2010

Ni hapa sasa watu kama SK walihitajika kwa nguvu mno.. Hasa kwenye propaganda na kujiwekeza kwenye kukubalika na kuwabana wengine... EL angekuwa na uchaguzi wa watu wengine wenye UTHUBUTU
Kulikuwa na Mchungaji Mtikila RIP wa Liberty desk lakini huyu alikuwa keshaharibu na akawa hatabiriki wala kuaminika na tayari akawa na chama cha SIASA
Kulikuwa na Mrema lakini naye alikuwa na nia kama ya EL na tayari alikuwa keshamalizwa na kitengo alipokimbilia NCCR-MAGEUZI
Kulikuwa na waandishi na wanasiasa wengi lakini akachagua the most potential one.. Na hapa SL akalamba dume
Kama tunakumbuka Mwanahalisi liliripoti ishu ya Richmond kwa namna ya kumkinga EL
Habari ni ndefu lakini SK aliendelea kuwa bega kwa bega na EL na baadae wakafanikiwa kujipenyeza CHADEMA kupitia Dr. Slaa.. CHADEMA ikawa juu lakini nyuma yake kulikuwa na mkono wa EL hasa kwenye connection na kitengo

Mambo yalipoharibika kabisa CCM EL alikimbilia CHADEMA ili akatimize ndoto yake.. Lakini ujio wake haukumfurahisha hata kidogo Dr. Slaa kwakuwa kama EL angefanikiwa kuwa rais thamani ya Dr Slaa ingeshuka sana kwakuwa connection yake sasa ina connect yenyewe... Yaliyofuatia yote yanajulikana
SK amekuwa kiungo muhimu sana kwenye siasa za upinzani hasa CHADEMA na EL na Slaa.. Amefaidika pia.. Ametengeneza na kujenga jina lake ana mchango wake mkubwa tu.. Ndio maana nikahoji kama anaweza kuvaa uso wa mbuzi na kumuua nyani... Bahati nzuri amekuwa na tafakuri kuu

Jr[emoji769]
 
Nyie ufipa hamna madhara Kwenye siasa endeleeni kula mbege
Nani alimshauri kukuunga na cdm? Ni wewe? Kama sio wewe, mbona unadandia kazi ya aliyemshauri na kumshawishi mwanzoni!
Unajidanganya Sana ukisaidiana na bulicheka wako hapo lumumba kuwa mnaweza kumnunua kiuongozi yeyote wa upinzani Ila mnasahau kuwa nao Wana akili kubwa kwani wanaotoka chama kikubwa kinachotishia uhai wa ccm!
Polepole a.k.a bulicheka alitweet Jana kuwa kubenea angetangaza kuhamia ccm leo! Natakiwa na hayatakuwa!
Mshauri huyo Dr uchwara aandae nondo za kuwashawishi wananchi juu ya miradi hewa isiyokamilika ambayo imewatia umaskini wa miaka 50 iliyopita! Kinyume chake jiandaeni kuwa wapinzani!
 
Mods uzi wa Mshana Jr ni muhimu sana ungeachwa peke yake kwenye jukwaa la siasa, mmefanya makosa kuunganisha huku.
 
Moderator please hebu kuweni na tafakuri jamani
Hizi ni nyuzi mbili tofauti
1. Ni uzi wa kubenea kutoa taarifa yake
2. Ni uchambuzi wangu kumhusu Kubenea
Kamwe huwezi kuziunganisha hizi nyuzi mbili kuwa moja hakuna mahusiano kabisa
JamiiForums

Jr[emoji769]
 
Uzi wangu unarudi way back 2007 na ukielezea mambo mengi mengine.. Uzi wa pili ni kubenea press conference kujibu mtanziko uliopo kuhusu yeye kuondoka CHADEMA.. Bado sioni uhusiano kabisa hapa
Moderator
jamiiforum

Jr[emoji769]
 
Back
Top Bottom