#COVID19 Kudhania janga la Covid 19 litakuwa mtaji wa kisiasa ni kufilisika kisiasa

#COVID19 Kudhania janga la Covid 19 litakuwa mtaji wa kisiasa ni kufilisika kisiasa

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Wana JF, hii kasumba ya wanasiasa wa upinzani kuwa wanasubiri majanga au kadhia flani itokee alafu wao wanufaike kisiasa ni kukosa busara za kisiasa.

Sasa hivi kila mwanasiasa wa upinzani amekomaa kuikosoa serikali ya Ccm bila hata kuwa na hoja zenye mashiko.

Mfano Mkuu wa nchi anaesema tutumie mask ambazo tunao uhakika wa usalama wake kiafya, hii imekuwa kama hoja kwa upinzani na wafuasi wake. Je, hii itawabeba?

Achana na hilo, bado wapinzani walitaka kupata kick ya kisiasa kutaka kuaminisha umma na jumuia ya kimataifa kuwa serikali haijachukua hatua madhubuti kupambana na jaga la covid 19. Jambo ambalo kiuhalisia sio kweli. Mlitaka hatua zipi zichukuliwe ili muone serikali inapambana na janga hili? Maana zipo taratibu za kupambana na haya majanga na ni lazima kiwango cha hatari kijulikane.

My take; Tusidhanie kuwa Covid 19 itakuwa mtaji wa kisiasa. Kama Watanzania tuonyeshe umoja kupambana na hili janga.
 
Nmesoma kichwa cha habari tu

Ila niamin nachokuambia, Ni MJINGA WA KIWANGO CHA LUMUMBA, ndio anaweza kutenganisha, corona na Siasa!

Kama sio mtaji wa Kisiasa, Kwann Jiwe alilitumia wakati wa Kampeni?

Ka sio mtaji wakisiasa, Jiulize kwann uko kwenye Mataifa ya watu, Viongozi wamepoteza nafasi zao za kuteuliwa upya, wengine wamejiuzulu kwa sababu ya corona?

Kama sio mtaji, jiulize kwann maDemos waliitumia ktk kumuagusha D.Trump?
 
Nmesoma kichwa cha habari tu

Ila niamin nachokuambia, Ni MJINGA WA KIWANGO CHA LUMUMBA, ndio anaweza kutenganisha, corona na Siasa !!!

Kama sio mtaji wa Kisiasa, Kwann Jiwe alilitumia wakati wa Kampeni?

Ka sio mtaji wakisiasa, Jiulize kwann uko kwenye Mataifa ya watu, Viongozi wamepoteza nafasi zao za kuteuliwa upya, wengine wamejiuzulu kwa sababu ya corona??

Kama sio mtaji, jiulize kwann maDemos waliitumia ktk kumuagusha D.Trump?
Utawabeba sasa?
 
Kwani upinzani ndio wameleta corona? Ndio wapingao uwepo wa corona? Ndio wapingao taifa kuchukua tahadhari dhidi ya corona?
 
Kiki ipi wakati ccm ndo iko mjengoni walishatwaa dola, na wanaendesha vita vya uchumi. Mbinu nyingi znatumika na unazijua.

Hakuna korona bali changamoto za ipumuaji. Data hazipo sababu korona haipo.

Barakoa ni imani haba.
Barakoa si salama nk.
Zipo dawa asili chanjo haiminiki.
Kwa akili zako nani anatumia siasa, au hujfikiria?
 
Kwanini mbumbumbu kama nyie huwaza siasa kwa kila kitu? Tunataka mtaji wa Kiafya kwenye Covid-19, nyie CCM mnataka maslahi ya kisiasa kwenye ugonjwa huu. Kwanini? Sisi tunataka tuhakikishie usalama wetu kiafya na siyo siasa zenu.
 
Kwani upinzani ndio wameleta corona? Ndio wapingao uwepo wa corona ? Ndio wapingao taifa kuchukua tahadhari dhidi ya corona ?
Hawa jamaa kila linalowashinda husingizia wapinzani. Nadhani unakumbuka huyu jamaa yao kwenye kampeni akifika eneo linalotawaliwa na kiongozi wa upinzani anasema "Hamna maendeleo hapa kwa sababu mlikosea kuchagua mpinzani". Jinga kweli hili jamaa
 
Achana na hilo, bado wapinzani walitaka kupata kick ya kisiasa kutaka kuaminisha umma na jumuia ya kimataifa kuwa serikali haijachukua hatua madhubuti kupambana na jaga la covid 19. Jambo ambalo kiuhalisia sio kweli. Mlitaka hatua zipi zichukuliwe ili muone serikali inapambana na janga hili? Maana zipo taratibu za kupambana na haya majanga na ni lazima kiwango cha hatari kijulikane.
Mleta mada, kufirisika ndio kufilisika?
Umekitathmini vyema ulichoandika?
Unajua upinzani ulionya yale mawazo 'hasi' kuhusu COVID wakapuuzwa?
Unajua yanayondelea kwa sasa baada ya kupuuza ile awamu ya kwanza?
Andika yako inaonyesha upeo wako wa kufikiri ni mdogo mno mno, ni bora ungekaa kimya kuficha ujinga wako.
 
Kwani corona ni uongo kama wa laptop za walimu?

Tatizo lenu mmeshindwa kuprove kuwepo au kutokuwepo kwa corona maana hivi ni virus, mkiwa mnataka kuandika jipeni muda kutafakari unachotaka kuandika!

Ndio maana watu wengi wamekimbia JamiiForums kwa ujinga wa watu kama nyinyi!
 
Back
Top Bottom