Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...

Elections 2015 Kuelekea 2015: Kama CCM Itamsimamisha Edward Lowassa...

Wanabodi,

Baada ya kumsikiliza kwa makini Waziri Mkuu "Mstaafu", Edward Lowassa katika two- series za kipindi cha Dakika 45 cha ITV, kwanza nimekubali sana huyu jamaa!, pili kama yeye ndiye angekuwa rais, ile 2005, Tanzania tusingefikia hapa tulipofikishwa sasa na utawala wa JK, ila kikubwa zaidi, (kama ni kweli afya yake sio mgogoro kama anavyodai yuko fit, japo he looks sick), CCM ikimsimamisha yeye kugombea urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, them matokeo ya urais kwa 2015, ni CCM tena!. Mkubali, mkatae!.

Hizi ni baadhi tuu ya sababu, kwanini CCM itashinda tena, endapo and only if itamsimamisha Lowassa!.

1. Uwezo wa Kupanga, Kusema, Kusimamia na Kutenda.
Viongozi karibu wote waliopo CCM, wana uwezo mkubwa sana kupanga wa kusema tuu, (Mkukuta, Mkumbita, Mkurabita, Mkuza, na sasa Dira 2025), lakini hawana uwezo wa kusimamia na kutenda!, mipango mingi iliyopangwa, inaishia kwenye maneno na vitendo sifuri!. Edward Lowassa sio msemaji, bali ni mtendaji, yeye sio mtu wa maneno mingi, ni mtu wa vitendo virefu, he is an action oriented man!.

Tulipopata uhuru miaka ya 60, maadui wetu wakuu watatu, walikuwa ni Elimu, Umasikini na Maradhi, na tulijiwekea misingi yetu mikuu minne ya maendeleo kuwa ili tuendelee, tulihitaji vitu vinne: Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora!. Kwenye hiyo misingi, tulisema Pesa sio msingi, pesa ni matokeo!, hili ndilol lililokuwa kosa pekee la Mwalimu, kutofautiana na misingi ya ukweli ya uchumi, kama ilivyofundishwa na Adam Smith (land, labor, capital na interpreneureship)!. Kwenye ile mising minne tulisahau capital!.

Watu tunao na ardhi ya kutosha, yenye rutuba, vyanzo lukuki vya maji, madini, maliasili etc etc tunazo. Tulikuwa na tatizo la siasa safi na uongozi bora, ndio maana nchi tulizopata nazo uhuru, wao wakiwa ni masikini wa kutupwa with nothing, kana Tiger nations, leo wako mbali!, sababu pekee iliyowafikisha wenzetu pale walipo, wakati sisi tunaendelea kupiga mark time ni Elimu!. Sisi tulitaja tuu kuwa Elimu ni adui, lakini we never invested because we had no capital. Nyerere aligombana na maprofesor wa uchumi, Kina Prof. Rweyemamu, wakajitimkia zao, akagombana na IMF, WB etc matokeo tunayajua!.

Lowassa na timu yake ya Boys II Men, walipoingia tuu madarakani, akafanya study tour ya tulioanza nao kwanini wao wamefanikiwa, wako mbali na sisi wametuacha nyuma sana!, akagundua wali invest kwenye elimu!. Akarudi akahamasisha kila kata iwe na shule ya sekondari ili kila Mtanzania apate kwanza elimu, mengine yote, yatafuatia!.

Baada ya kujiuzulu, serikali ya JK ikazi abandon zile shule za EL ili kumkomoa!. Jana alipozungumzia umuhimu wa kuwaelimisha kwanza watu wetu, amenigusa sana!. Tungekuwa tumeelimika, tusingeibiwa hivi madini yetu, tumeibiwa madini kwa sababu hatuna elimu ya madini, sasa tumegundua gesi,serikali inakimbilia kugawa vitalu kwa umiliki wa miaka 99 huku Watanzania hatuna hili wala lile kuhusu elimu ya gesi, kwa kifupi, hutujui lolote na tutaishia kuibiwa tena gesi yetu kwa kukosa elimu ya gesi!. EL ameshauri, lets invest kwenye elimu kwanza ili kuwa empower watu wetu kielimu ndipo tuingie kwenye ambitious projects kama za kilimo kwanza gesi etc!.

Kwa hili pekee, CCM ikimsimamisha EL, Tanzania itapata ukombozi wa kweli wa pili wa Mtanzania!.

Nimesema, CCM ikimsimamisha EL, 2015, itakuwa ni CCM tena, kwa sababu katika wapinzani wote, hakuna hata mgombea mmoja anayewa kusimama na Lowassa kwenye urais na bado akaambulia kura!, there is none, no one!.

Mwenye masikio na asikie!.

2. Dhambi Kubwa ya Lowassa ni Richmond Tuu!.

Najua wapinzani wa dhana ya ukweli, watakuja na hoja za dhambi kubwa ya Lowassa ni Richmond!, then time will tell, hiyo ni mizigo tuu ya watu, alijitolea kuibeba ili kwa kuteswa kwake, wao waokoke, wakati muafaka ukifika, hili litawekwa wazi na Watanzania mtawafahamu wenye zigo lao!. Wenye akili wameshang'amua ile metarmophosis process from Richmond -Dowans -Simbion na kwa msio jua, mkae mkijua Tanesco bado inailipa Simbion capacity charge ile ile ya dola 152 kama Richmond na Dowans, hivyo tumeruka majivu na kukanyaga moto, tumeruka maji na kukanyaga tope, na kwa usafi tumeruka nyasi, tukakanyaga ma..!.

3. CCM Haina zaidi ya EL na Upinzani hana wa Kushindana Nae!.

Wanabodi ni mimi niliwahi kusema, CCM imechokwa na Chadema Haijajipanga, baadae nikasema CCM imechokwa mpaka basi!, Baada ya Chadema kuanza kujipanga nikasema Chadema, Njia Nyeupe Ikulu, lakini sasa baada ya kumsikia Edward Lowassa, kama ni kweli CCM itamsimamisha, then, 2015, ni CCM tena, kinyume cha hapo, CCM ikimsimamisha mwingine yoyote, 2015, Chadema inachukuwa nchi kiulaini kama kumsukuma mlevi!.


Mwisho.

Namalizia kwa swali moja tuu, Jee CCM inaujasiri wa kuukubali huu ukweli mchungu wa kumsimamisha Edward Lowassa ili kuweza kujiokoa? au itaendeleza kiburi uongozi na jeuri ya uchama tawala kusubiria kifo cha mende huki inajiangalia kwa kutegemea itaendeleza uking'ang'anizi wake kwa kuamini this time pia itashinda tena kwa kuutumia uwongo ule ule, na mbinu zile zile za uchakachuaji ule ule, kwa kutegemea katiba mpya ita provide opportunities za aina ile ile ya miaka ya nyuma, kuwa ita endelea "to fool all the people all the times?!.

Asante.

Pasco.

NB. Japo Pasco wa JF sio mwanachama wa Chama chochote cha siasa, kwa CCM ni Pro Lowassa, kwa Chadema ni Pro ZZK na kwa CUF ni Pro-Jussa!.
[/QUOTE

2. Dhambi Kubwa ya Lowassa ni Richmond Tuu!. Nyerere!?
 
Mpaka sasa kuna kila dalili kuwa mgombea urais wa CCM 2015 huenda akawa Edward Lowassa kutokana na nguvu ya kisiasa aliyonayo ndani ya CCM kwa sasa hususani kwa wajumbe wengi wa vikao vikuu vya juu vya maamuzi ndani ya CCM(Kamati kuu, Halmashauri kuu na Mkutano Mkuu).
Wakati huo huo kama kuna jambo wanachama wa CHADEMA wangependa kuliona basi ni Lowassa kuwa mgombea urais wa CCM 2015.
Kwa sababu zifuatazo:

1/Moja ya hoja zilizoipa nguvu sana na Umaarufu mkubwa sana CHADEMA ni Vita dhidi ya Ufisadi, Lowassa ni mtu anaaminiwa kama fisadi zaidi kuwahi kutokea ndani ya CCM, hivyo kutaipa nguvu zaidi CHADEMA katika harakati zao.

2/Kumbukumbu isiyofutika ya kitendo cha Lowassa kujiuzuru uwaziri mkuu kutokana na kuhusika katika Ufisadi mkubwa wa mkataba tata wa kampuni ya kufua Umeme wa dharura(Richmond).

3/Vita ya kufa na kupona kati ya Lowassa dhidi ya makundi mengine ya wanaCCM wenzie wanaoutaka urais pia, ambao wamekuwa kila mara wakianikana baadhi ya maovu yao hadharani. Katika hili atakosa 'Support' muhimu kutoka kwa wanaCCM wengine 'muhimu' wanaomchukia.
Mkuu Tanganyika Tanu, pole sana, hii kitu yako imeunganishwa kwangu!. Ili kukutendea haki, nimeiweka kule juu kwenye main post.
Pasco.
 
Mkuu Pasco hata mimi nakuunga mkono kwa hizo hoja zako zenye mashiko na kweli tupu kwa mtanzania mwenye uchungu na mpenda maendeleo.

Unajua huyu bwana Lowasa vision yake katika suala la elimu ilikuwa nzuri sana, mwanzo alikuja na suala la kujenga shule nyingi za kata. Baadae alikuwa na lengo la kutatua shida ya walimu kwa kuwa majengo ya madarasa, nyumba za walimu na maabara tungelikuwa tumeshakamilisha kuvijenga.

Unajua hapa kinachowasumbua watu wengi kwa kukosa imani na huyu bwana Lowasa ni ile issue ya RICHMOND tu. Kwenye hili la Richmond hapa ni kama alitolewa kafara tu ili serikali isianguke. Na kwa kuwa huyu bwana ni mzalendo na mtiifu kwa serikali yake basi alikubali kutolewa kafara ili ainusuru serikali ya CCM.

Shime watanzania wapenda maendeleo tumpe nafasi huyu bwana Lowasa atufanyie hayo tunayoyaota kila kukicha.
Richmond ndio hiyo hiyo Kagoda, ndio hihi Simbion!. Wenye akili zao, wameisha jua ni nini kinaendelea!. Dodoki linasubiriwa tuu kwenda kusafishia ule uchafu wa bungeni!. Tena hoja utakapowasilishwa ile 2014!, utashuhudia wale wale walioishadidia Richmond, ndio hao hao utawashuhudia wakiisifia Simbion!.

Mimi nitamshamshauri kwanza Mwakiembe akiseme kile ambacho hakukisema kule kwenye tume yake, kisha EL atakomelea msumari wa mwisho kwenye jeneza la issue ya Richmond kuwa ilikufa ikazikwa hatimaye ikafufuka kama Simbion huku imetakasika!, hadi Obama na JK kuichezea muziki!.
P.
 
Pasco na njaa zake ni majanga tuliyonayo ndani ya jamii...Lowassa kuwa Rais????????????????? labda ahera ambako na Nchemba atakuwa Waziri mkuu
 
Laigwanan anawafuasi wengi, hawa akina pasco wote ni wafuasi, nilikuwa sijui.
Mkuu Mjuni Lwambo!, Pasco wa jf, sio mfuasi wa mtu yoyote, hana chama, hana upande na wala sio shabiki, ila anazungumza ukweli daima!. Wengi wanadhani jua linapochomoza Mashariki ile asubuhi, na kuzama Magharibi ile jioni, wengi wanadhani jua ndilo linalozunguka, hivyo huo ndio ukweli wao wanaouamini, ila ukweli halisi, ni jua limesimama hapo lilipo, ni dunia ndio inayozunguka!. Watu wanapenda kuushabikia ukweli wao lakini sio ukweli halisi!. Pasco wa jf, anasimama na ukweli halisi!. Subiria mpaka baada ya 2015 ndipo utawajua wafuasi halisi wa EL, mimi usinihesabu, kwa sababu kazi yangu ni kukupeni tuu ukweli halisi!.
P.
 
Pasco na njaa zake ni majanga tuliyonayo ndani ya jamii...Lowassa kuwa Rais????????????????? labda ahera ambako na Nchemba atakuwa Waziri mkuu
Mkuu Ngisi, hili la njaa, ni kweli!.. ila pia jifunze kusoma kwa kituo!. hAPA NAZUNGUMZIA Lowassa kuwa rais au nazungumzia CCM imsimamishe nani?!. Kumbe na wewe umeishaujua ukweli halisi kuwa mgombea atakayesimamishwa na CCM ndie lazima awe rais!?. Endelea kuniona janga, 2015 tutakumbushana!.
P.
 
Mkuu Ngisi, hili la njaa, ni kweli!.. ila pia jifunze kusoma kwa kituo!. hAPA NAZUNGUMZIA Lowassa kuwa rais au nazungumzia CCM imsimamishe nani?!. Kumbe na wewe umeishaujua ukweli halisi kuwa mgombea atakayesimamishwa na CCM ndie lazima awe rais!?. Endelea kuniona janga, 2015 tutakumbushana!.
P.
Pasco mzee wa njaa..
 
Last edited by a moderator:
"Heri wenye njaa na kiu ya haki, maana hao watashibishwa"-Nabii ...
Aisee Pasco,
Hebu nipigie pande nijiunge #Team Lowasa 2015" ili nami nijilie mema ya Nchi,
Tafadhali mkuu wangu.
Maana nami nina njaa kweli:help:
 
Last edited by a moderator:
Pasco, katika thread hii post yako ya awali umedai afya ya mzee EL inadorora. Labda ni nini kinamsibu?

Halafu zipo tetesi kuwa by 2015 mzee huyohuyo wa Monduli ataachia jimbo lake, na sasa vimeshaanza vikumbo chinichini kutafuta mrithi.

Hapa najaribu kunasibisha haya matukio na msimamo wako kihoja wa EL asimame kiti cha urais kupitia CCM.

Hebu nieleweshe kwa kadri uyajuavyo mambo.
 
Last edited by a moderator:
lowasa1.jpg


Hawa ndiyo wanakaopokezana vijiti.

Cc; Pasco,
Mkuu Ritz, huu ndio ukweli mchungu kwa wengi humu kuumeza!. Mimi sina mashaka kabisa na uwezo wa mpokeaji, natatizwa kidogo hali ya afya ya mpokeaji kijiti, if you look very closely with the "third eye", utaona fire in his eyes, and the fear is the weapon in his heart!.
Pasco.
 
Pasco, katika thread hii post yako ya awali umedai afya ya mzee EL inadorora. Labda ni nini kinamsibu?

Halafu zipo tetesi kuwa by 2015 mzee huyohuyo wa Monduli ataachia jimbo lake, na sasa vimeshaanza vikumbo chinichini kutafuta mrithi.

Hapa najaribu kunasibisha haya matukio na msimamo wako kihoja wa EL asimame kiti cha urais kupitia CCM.

Hebu nieleweshe kwa kadri uyajuavyo mambo.

Porojo za pasco.
 
Last edited by a moderator:
Aisee Pasco,
Hebu nipigie pande nijiunge #Team Lowasa 2015" ili nami nijilie mema ya Nchi,
Tafadhali mkuu wangu. Maana nami nina njaa kweli:help:
Mkuu Al Adawi, ingekuwa inaruhusiwa kujiapiza humu jf, ningeapa kwa Jina la Mungu aliye Juu!, WaLahi!
Pasco wa JF sio member wa Team EL!. Mimi kazi yangu ni kuandika ukweli tuu!.
Kama kwa kusema ukweli kunapelekea mimi kuonekana ndio team EL, then its ok with me!.
Watu wa ukweli, huwa hawatatizwi kabisa na hoja za wale watu ambao kazi yao ni kudhania tuu!.
P.
 
Bwa mdogo umeandika vizuri lowassa hotoshinda urais kwa sababu ya utendaji wake ni kwasababu ya hela yake na ccm kama hawatamchagua yeye basi ccm watapoteza 95% lowassa ananguvu kubwa ndani ya ccm kuliko unavyo fikiria
 
Pasco, katika thread hii post yako ya awali umedai afya ya mzee EL inadorora. Labda ni nini kinamsibu?

Halafu zipo tetesi kuwa by 2015 mzee huyohuyo wa Monduli ataachia jimbo lake, na sasa vimeshaanza vikumbo chinichini kutafuta mrithi.

Hapa najaribu kunasibisha haya matukio na msimamo wako kihoja wa EL asimame kiti cha urais kupitia CCM.

Hebu nieleweshe kwa kadri uyajuavyo mambo.
Mkuu Rock City, hii ni thread ya 2012 wakati EL alipozungumza ITV. Alisema yeye yuko fiti kabisa kwa lolote!. Nilichosema mimi humu, ni ukweli usiopinginga kuwa kwenye watu wote CCM iliyoo nao, EL the the one and only best option ya kuwapatia ushindi 2015, ila ninavyomuona mimi, kwa uonekano wake machoni, he is not fit!. He looks sick!.

Kwa vile he looks sick, lakini anasema yuko fit!, kwa kuujua ukweli huu, hivyo 2015, hatagombea sio urais wala sio ubunge!, atajipumzikia!. Kwa maoni yangu honestly, naamini hizi juhudi zote za kuonyesha kuutaka urais wa 2015, ni "sauti tuu ya mtu aliye nyikani", kunyoosha tuu mapito ya "yeye yuajaye!", ili kuzuia "mafisi!", "kunguru!" na "many'ang'au!" wasiisonge njia ya bwana!.

Naomba usiniulize hao "mafisi!", "kunguru!" na "many'ang'au!" ni akina nani, sambamba na "huyo yuajaye!".
Pasco.
 
Bwa mdogo umeandika vizuri lowassa hotoshinda urais kwa sababu ya utendaji wake ni kwasababu ya hela yake na ccm kama hawatamchagua yeye basi ccm watapoteza 95% lowassa ananguvu kubwa ndani ya ccm kuliko unavyo fikiria
Mkuu Cute, kumbe hata 2015 Watanzania watakwenda kumpigia kura mtu kwa sababu ya mihela yake!, na sio uwezo wake?!.

Kwa vile Lowassa ana nguvu kubwa ndani ya CCM kuliko ninavyofikiria, inaamani kwa uchaguzi wa 2015, mgombea mwenye nguvu kubwa ndani ya CCM ndie atakayekuwa rais wetu?!.

Nimekusikia!, mwenye masikio na asikie!".
P.
 
Porojo za pasco.
Hata dunia ilianza kwa porojo tuu! Hapo mwanzo, alikuwako Neno. Huyo. Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye. Nenoalikuwa Mungu.
Mungu katika uumbaji, alitumia porojo tuu "Mungu akasema, Na iwe mianga katika anga la mbingu ili itenge kati ya mchana na usiku; nayo iwe ndiyo dalili na majira na siku na miaka".

Ule msemo wa mdomo huumba, maana yake kauli huumba!. Mfano hapa nilipo, depending on my powers of will and the justification iliyopo juu yako, nikitamka kwa kauli unazoziita porojo kuwa "Wewe Matola Utakufa Usiku wa Leo!", amini usiamini Mkuu Matola kesho huamki!. Sina sababu ya kutamka hivi ili kuthibisha uwezo, bali sitamki kwa sababu bado tunakuhitaji humu jf!, kama unabisha, nibishie nitamke na kukupotezea jumla!. Kesho itapandishwa thread na Invicible "Tanzia Mwana JF Mwenzetu .....Ametutoka!".
Usicheze na kauli thabiti kwa kuziita porojo!.
Pasco
 
Mkuu Rock City, hii ni thread ya 2012 wakati EL alipozungumza ITV. Alisema yeye yuko fiti kabisa kwa lolote!. Nilichosema mimi humu, ni ukweli usiopinginga kuwa kwenye watu wote CCM iliyoo nao, EL the the one and only best option ya kuwapatia ushindi 2015, ila ninavyomuona mimi, kwa uonekano wake machoni, he is not fit!. He looks sick!.

Kwa vile he looks sick, lakini anasema yuko fit!, kwa kuujua ukweli huu, hivyo 2015, hatagombea sio urais wala sio ubunge!, atajipumzikia!. Kwa maoni yangu honestly, naamini hizi juhudi zote za kuonyesha kuutaka urais wa 2015, ni "sauti tuu ya mtu aliye nyikani", kunyoosha tuu mapito ya "yeye yuajaye!", ili kuzuia "mafisi!", "kunguru!" na "many'ang'au!" wasiisonge njia ya bwana!.

Naomba usiniulize hao "mafisi!", "kunguru!" na "many'ang'au!" ni akina nani, sambamba na "huyo yuajaye!".
Pasco.

Nimekupata vema Pasco, nimeelewa mantiki ya lugha uliyotumia.

PAMOJA.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom