KUELEKEA HATUA YA MAKUNDI CAFCC: Nazionea huruma sana St. Eloi Lupopo na US Monastir

ninosi

Senior Member
Joined
Jun 30, 2022
Posts
151
Reaction score
333
Matokeo ya mechi (In Aggregate) za playoff za kuwania hatua ya makundi za CAFCC katika msimu wa 2022/23 ni kama ifuatavyo:

Marumo Gallants 3-1 Al Ahli
Tripoli
CS Sfaxien 1-2 ASKO
St Eloi Lupopo 1-0 RC Kadiogo
Diables Noirs 6-2 La Passe
Al Akhdar 4-4 Plateau United
Club Africain 0-1 Yanga
Future 3-2 Primeiro Agosto
Real Bamako 4-2 Royal Leopards
SC Gagnoa 2-5 ASEC
Pyramids 3-1 AS Nigelec
Royal AM 0-3 TP Mazembe
USM Alger 1-0 Cape Town City
Motema Pembe 3-1 Flambeau du Centre
Al Nasr 1-6 Rivers United
RS Berkane 0-1 US Monastir
FAR Rabat 4-0 Djoliba

Baada ya kuangalia matokeo hayo (kwa jicho kali la kiuchambuzi) nazionea huruma sana timu zifuatazo:
1. St. Eloi Lupopo
2. US Monastir

Kwanini Nazionea Huruma:-
1. Hivi unakuwa vipi na furaha kuingia hatua ya makundi kwa aggregate ya goli 1-0 huku wenzako unaoenda kukutana nao wamemdunga mtu goli 6?

2. Natoa angalizo kwa mashabiki wa timu hizi 2 mjitahidi kujazana uwanja wa ndege leo kuwapokea mashujaa wenu maana yajayo yanasikitisha.
 
Us monastair kamtoa bingwa mtetezi Rs berkane siyo timu ya kubezwa hata kidogo

Japo najua umetumia sarcasm kuomock yanga lakn ukwel yanga imetushangaza zaidimetuvua nguo tuliamin watalambwa hamsa

Heshim kwenu yanga msibweteke Sasa kazeni walau mfike robo fainal tuongeze points za uwakilishi

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu hakuna sehemu nimeitaja Yanga
 
Yaan bongo cku hizi kila mtu mchambuzi wa mpira halafu ukiangalia alichochambua ni pumba tupu.Kuna mtu kaanza kushabikia mpira miaka ya hivi karibuni lkn na yeye ni mchambuzi
Kwanini mna hasira sana,mpira ni ushabiki haya wafanyayo ndio yanafanya mpira uwe hivi ulivyo.acheni watu washabikie.
 
We jamaa kumbe AKILI huna
 
St lupopo,shikya bintu,toka laurent kabila avenue, to estadio kibasa maliba
yelow and blue,tuko pamoja
 
Kuna katimu kamepata draw kwa tabu sana pale Singida. Kanaenda kuliabisha taifa huko kwenye makundi!
 
Watu wanaenda na mdundiko uwanja wa ndege kupokea kombe la kuingia makundi utawaambia nenee
 
Wazazi wanapaswa kuhakikisha watoto wananyonya vizuri na kula vyakula vyenye vitamin za kutosha ili kuepuka udumavu wa akili.
 
Nadhani unaongea kwa mafumbo, watu watafikiria unawasena Utopolo kumbe unamsema Makolo a.k.a Mikia ajiandae na vichapo vya aibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…