Kwani muda ukiisha kuna tatizo lipi? Si unanunuwa SIM card mpya na kuisajili hapo hapo?Wadau,Niko hapa maeneo ya mbagala mwanamtoti natoka kwenye pilika zangu,mpaka saa hizi naandika huu uzi ,saa moja na dakika hamsini na sita,Bado Kuna watu wamejazana katika vituo vya kusajilia laini za simu.
Mida mchache ujao tutasikiliza taarifa ya habari sijui,E-1 ataongeza muda Tena au ndo imetoka.
Hebu tuendelee kula mtori ,nyama tutazikuta chini.
Wenye updates za usajili watuletee kuitia uzi huu.
Cc,ziro iq.
Sent using Jamii Forums mobile app
Niko huku vijijini wakina mama wako na watoto mgongoniwakisajiriline na hakuna network. Ila sisi hatutalia na nida tutalia na tulio wapigia Kura watuongoze
Bure kabisa...huna akili kabisa wewe...
Ilikua na tatizo gani hio mkuu?Mimi nimesajili line zangu 3 kati ya 5 ninazomiliki. Moja hawa freelancer wameishindwa wameniambia niende HQ airtel
Kwa uelewa wangu mdogo Mh Rais alisema zoezi la kusajili laini kwa alama za vidole mwisho tarehe 20, hivo bas kufungwa kwa lain ambazo hazijasajiliwa zitafungwa tarehe January 21, 2020 saa 00:00 EAT.
unanunuwa = unanunuaKwani muda ukiisha kuna tatizo lipi? Si unanunuwa SIM card mpya na kuisajili hapo hapo?
Unaendeleaje huku Ni usajiri sio usajili yaani mateso matupu= wakisajili
Kiswahili ni lugha mama kwangu na sikusomea ujinga. Kumbuka hilo.
Mnazima kesho au keshokutwa? Mlisema mwisho tarehe 20/1/2020, sasa kwa nini mzime kesho badala ya keshokutwa?By Happiness Tesha, Mwananchi htesha@mwananchi.co.tz
Kigoma. Serikali ya Tanzania imesema itatumia hekima kuwasaidia wananchi walioshindwa kusajili laini za simu kwa sababu ya kukosa kitambulisho cha Taifa na namba licha ya kuanza mchakato wa kupata kitambulisho hicho.
Imesema wananchi hao taarifa zao zipo katika Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), huenda wamekosa kitambulisho au namba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wao.
Hayo yameelezwa leo Jumapili Januari 19, 2020 na naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Atashasta Nditiye katika mkutano wa ndani wa CCM mkoani Kigoma.
"Serikali itaona jinsi ya kutumia hekima kwa wananchi ambao taarifa zao zipo katika ofisi za Nida kuona namna ya kufanya lakini kwa wengine ambao hawajajaza fomu laini zao zitazimwa,” amesema Nditiye.
Amesema ambao laini zao zitazimwa ni wale waliosajili laini chache na kuacha nyingine licha ya kuwa na kitambulisho hicho.
Amebainisha kuwa usajili wa laini za simu ni endelevu licha ya baadhi ya wananchi kupuuza.
Kesho Jumatatu Januari 20, 2020 laini zote za simu ambazo hazijasajiliwa kwa alama za vidole zitazimwa. Ili uweze kusajili laini ni lazima uwe na kitambulisho cha Taifa au namba ya kitambulisho hicho.
Bibi naye chenga kumbe.......