Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

Kuelekea laini za simu zisizosajiliwa kuzimwa; Ushauri wa namna bora ya kufanya ili kutovunja sheria za nchi

jukumu la matumizi ya laini anabeba aliyesajili kwa vidole endapo umeruhusu kidole chako kusajilia mtu unahusika na jinsi lain itakuvyotumika
 
Serikali inatakiwa kuhakikisha NIDA wana maliza zoezi lakutoa namba kwa wananchi walio jiandikisha kwanza ndio waje na huompango wa kufungia line.

Watu kwa mamilioni wamekwama NIDA alafu unawafungia line manayake nini, raiya unaowaongoza kwanini kuwatia umaskini, unafaidika na nini?.

Mwananchi akishindwa kumtumia mzaziwake kikongwe kijijini hela ya dawa alafu mzazi akapoteza maisha kwasababu ya kukosa huduma wewe kiongozi unapata faida gani?.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watanzania tunapenda kutesana sisi kwa sisi ndio furaha yetu wengine ndio hupata nafasi ya kumtafuna mwenzake kipesa.dhambi ya kudhulumu nyumba za watu nakuzifanya NHC mungu hatotuacha salama kizazi na kizazi vitateseka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hujapitia vyombo vya habari kabla ya bandiko lako mkuu?
Screenshot_2020-01-18-19-43-16.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pointi yenye mashiko hapo ni hilo la Vijana kusajili kiholela.

Hayo mengine ni matakwa tu ya teknolojia, na hatuna uchaguzi zaidi ya kuenda nayo sambamba.

Sasa tu usichanganye changamoto zenu za miundo mbinu, kipato duni cha Wananchi wenu kutaka kukwepa mabadiliko..usisahau hizo teknolojia karibu zote hatuna asili nazo, sisi ni watumiaji tu.

Ni ajabu kama unataka bado tuwe na sauti juu ya kitu tusicho na asili nacho.

Mfano mzuri tu ni kama hivi Microsoft walivyotangaza tangu tar 14 ni wisho wa ku support window 7, kwa hiyo kwa ushauri wako au Watu wa kaliba yako unaona Microsoft wanasumbua? ni juu yako Mzee baba ku upgrade Window yako au la, wewe ndio upime hasara na faida sio wao tena.
 
Mara simu fake sijui iliishia wapi, tukapata hasara, ivi kweli raia mimi ntajuaje hii ni fake au sio, kwanini Serikali kupitia TBS isizuie zisiingie, kiukweli Serikali ndo inarudisha nyuma Maendeleo ya wananchi
Kwakweli anaeumia ni mwananchi,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata pale mwananchi anaponyanyaswa na serikali yake bila hatia kazi yako ww nikujikomba kwa jiwe ili upate mlo!
Nani kalalamika hapa kwamba ana namba ya NIDA na ameshindwa kusajiri?

Hata hivyo, wakati wewe unasifu na kuabudu watawala walio kosa hekima, ukidhani mnawakomoa wapinzani,
ndg zako huko kijijini wanasota na NIDA na hawajafanikiwa kupata hata namba na ni miongoni mwa watakaofungiwa line zao.

Sent using Jamii Forums mobile app

Wezi 2tawakamata tu,,kama na wewe mmojawapo pole sana,,,Coz kuna wapumbavu na mahanisi wasiopenda kufanya kazi za halali na ku2mia kivuli cha tigo pesa, halopesa n.k kuwaibia watanzania pesa zao kwenye account,,,tutawakamata tu mbwa hao.
 
Bado sijaelewa kukataliwa kwa kitambulisho hiki muhimu sana kinachotumika kwenye jambo sensitive la Kupata viongozi wa nchi kwenye kusajili line za simu inatokana na nini .

Kulikuwa na uvumi wa kuandikishwa hata wageni kwenye uchaguzi mkuu 2015 ili kusaidia CCM. Je, ni kweli kwamba wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2015 kuna maelfu ya wageni walisajiliwa ili kupiga kura za kuiokoa CCM na sasa serikali inawaogopa? line za simu zina umuhimu gani kushinda uchaguzi wa nchi?

Naomba mwenye uelewa wa hili anifafanulie
 
Mtu mmoja anamiliki line tatu mpaka nne na wengine mpaka sita kwa hiyo huenda hao wanaomiliki line nyingi wameamua kuzipunguza japo hii haiondoi ukweli kuwa wananchi wananyanyaswa kwa vile NIDA wameshindwa kazi yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom