Tetesi: Kuelekea Mkutano Mkuu wa CCM: Mbunge, Wajumbe na Katibu wa Mikoa wa Upinzani kujiunga CCM

Tetesi: Kuelekea Mkutano Mkuu wa CCM: Mbunge, Wajumbe na Katibu wa Mikoa wa Upinzani kujiunga CCM

TandaleOne

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2010
Posts
1,644
Reaction score
709
Kuelekea Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaotarajia kufanyika tarehe 23th July 2016 mjini Dodoma, tayari zipo taarifa za kuaminika juu ya Viongozi wakubwa wa Vyama vya Upinzani kuazimia kujiunga na CCM katika siku hiyo.

Taarifa iliyotufikia inamtaja Mbunge mmoja maarufu wa CHADEMA ambae mpaka jana alikuwa anamaliza mazungumzo ya mwisho na viongozi waandamizi wa CCM juu ya utaratibu wa mapokezi yake na hatma yake kisiasa.

Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Pia yupo Mgombea Uenyekiti wa BAVICHA na mgombea Ubunge wa Moja ya Majimbo ya Kaskazini. Pamoja nao yupo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, pamoja na Makatibu kadhaa wa Mikoa wa Chama cha ACT.

Ukiachilia mbali Viongozi hao wa wapinzani ambao idadi yao kwa ujumla inakaribia 18, wapo waliokuwa wa CCM na wakahama na kumfuata LOWASSA upinzani, Viongozi hao nao wameendelea kubembeleza ili waweze kupokelewa tena ndani ya CCM. Watatu kati yao tayari wako Dodoma wakiongozwa na aliyekuwa "Mtoto na Msiri" wa Lowassa ambae pia alikuwa ni KATIBU wa CCM Wilaya ya Monduli.

Wakati Viongozi hao wakijiandaa kujiunga na CCM, maandalizi ya Mkutano Mkuu yameendelea kukamilika na kufikia hatua nzuri, ambapo jana Katibu Mkuu wa CCM alikagua hatua ya maandalizi na kujiridhisha kuwa Mkutano Mkuu utakuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kukamilika kwa maandalizi ya Mkutano huo kwa sehemu kubwa.
 
Kuelekea Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaotarajia kufanyika tarehe 23th July 2016 mjini Dodoma, tayari zipo taarifa za kuaminika juu ya Viongozi wakubwa wa Vyama vya Upinzani kuazimia kujiunga na CCM katika siku hiyo.

Taarifa iliyotufikia inamtaja Mbunge mmoja maarufu wa CHADEMA ambae mpaka jana alikuwa anamaliza mazungumzo ya mwisho na viongozi waandamizi wa CCM juu ya utaratibu wa mapokezi yake na hatma yake kisiasa.

Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Pia yupo Mgombea Uenyekiti wa BAVICHA na mgombea Ubunge wa Moja ya Majimbo ya Kaskazini. Pamoja nao yupo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, pamoja na Makatibu kadhaa wa Mikoa wa Chama cha ACT.

Ukiachilia mbali Viongozi hao wa wapinzani ambao idadi yao kwa ujumla inakaribia 18, wapo waliokuwa wa CCM na wakahama na kumfuata LOWASSA upinzani, Viongozi hao nao wameendelea kubembeleza ili waweze kupokelewa tena ndani ya CCM. Watatu kati yao tayari wako Dodoma wakiongozwa na aliyekuwa "Mtoto na Msiri" wa Lowassa ambae pia alikuwa ni KATIBU wa CCM Wilaya ya Monduli.

Wakati Viongozi hao wakijiandaa kujiunga na CCM, maandalizi ya Mkutano Mkuu yameendelea kukamilika na kufikia hatua nzuri, ambapo jana Katibu Mkuu wa CCM alikagua hatua ya maandalizi na kujiridhisha kuwa Mkutano Mkuu utakuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kukamilika kwa maandalizi ya Mkutano huo kwa sehemu kubwa.
Wakati ccm wakitalajia kuwapokea hao 18 tarehe 23/7 ....tarehe 25 upinzani utapokea vigogo kutoka ccm 180 ...hii inaitwa kampa , kampa tena ...
 
Weka majina yao hapa acha porojo.
Uenyekiti wenyewe mnataka kutoana naona mnazuga na taarifa za uzushi
 
Lkn kwasababu nchi yetu ni ya kidemokrasia iliyokandamizwa naona wametumia uhuru wao lkn wakumbuke yakuwa UDC udas na uded zimeisha kwasasa
 
Kuelekea Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaotarajia kufanyika tarehe 23th July 2016 mjini Dodoma, tayari zipo taarifa za kuaminika juu ya Viongozi wakubwa wa Vyama vya Upinzani kuazimia kujiunga na CCM katika siku hiyo.

Taarifa iliyotufikia inamtaja Mbunge mmoja maarufu wa CHADEMA ambae mpaka jana alikuwa anamaliza mazungumzo ya mwisho na viongozi waandamizi wa CCM juu ya utaratibu wa mapokezi yake na hatma yake kisiasa.

Wengine ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Pia yupo Mgombea Uenyekiti wa BAVICHA na mgombea Ubunge wa Moja ya Majimbo ya Kaskazini. Pamoja nao yupo aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, pamoja na Makatibu kadhaa wa Mikoa wa Chama cha ACT.

Ukiachilia mbali Viongozi hao wa wapinzani ambao idadi yao kwa ujumla inakaribia 18, wapo waliokuwa wa CCM na wakahama na kumfuata LOWASSA upinzani, Viongozi hao nao wameendelea kubembeleza ili waweze kupokelewa tena ndani ya CCM. Watatu kati yao tayari wako Dodoma wakiongozwa na aliyekuwa "Mtoto na Msiri" wa Lowassa ambae pia alikuwa ni KATIBU wa CCM Wilaya ya Monduli.

Wakati Viongozi hao wakijiandaa kujiunga na CCM, maandalizi ya Mkutano Mkuu yameendelea kukamilika na kufikia hatua nzuri, ambapo jana Katibu Mkuu wa CCM alikagua hatua ya maandalizi na kujiridhisha kuwa Mkutano Mkuu utakuwa wa mafanikio makubwa kutokana na kukamilika kwa maandalizi ya Mkutano huo kwa sehemu kubwa.
Huu ni uongo una uzushi! Tetesi halafu uthibitisha mmana ake nini? Hivi unafikiri JJ Mnyika hata kama kuna mambo hayafurahii Chadema unafikiri anapelekwa na bongo za CCM?
 
Siasa za namna hii zinalipa lakini ni hatari sana kwa maisha yaliyobakia ya mhusika pamoja na familia yake.
Nimemfuatilia kiongozi mmoja Kenya ambaye 'anawasumbua' ODM mara kuja kusikia kapewa mtaji mkuwa na kununuliwa nyumba katika kitongoji aghali cha Karen kama fadhili ya kuwasaliti wenzie. Sasa unajiuliza maisha yake kweli yatakuwa halisi kama hao wakazi wa Karen au ndio mambo ya 'kufoji cheti ili upate kazi'!?
Nimecheka sana....eti wanafanya maongezi..naona mnapanga alipwe shilingi ngap......
 
Back
Top Bottom