Uchaguzi 2020 Kuelekea Oktoba 28, 2020: Tundu Lissu atalisomba kundi la wasio na maamuzi kwa kishindo

Uchaguzi 2020 Kuelekea Oktoba 28, 2020: Tundu Lissu atalisomba kundi la wasio na maamuzi kwa kishindo

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Kwa mashambulizi haya ya Tundu Lissu kila siku anabomoa ngome ya mpinzani wake kwa matofali kadhaa. Kuna wale CCM damu na Chadema damu, hawa hata iweje kura zao hazibadiliki.

Kuna lile kundi linalokata shauri dakika za mwisho. Mara nyingi hawa ni watu wenye shughuli zao, wasomi, wakulima na wafanya biashara. Hawa husikilizia sera zenye tija kwa maisha yao, sera hizi ziwe Chauma, CCM au CHADEMA kama kuna tegenwoordig la ushindi huweka nguvu zao huko.

Kuna kila dalili za Tundu Lissu kulipia kundi la undecided group. Kuna mengi mtayasikia yanayomhusu mtu yule msiwe hata na hamu ya kulitazama bango lake.
 
Kuwapata hao undecided aende vijijini; siyo kupita mijini tu. Ubaya ni kwa vile huko vijijini, CHADEMA haina infrastructure kabisa. Kwa hiyo hawezi kwenda kwa sababu hakuna wa kutangza ujio wake.
 
Lissu ana roho ya Mungu ndani yake. Hana hata bango moja lakini mikutano yake inajaa mno. Sasa hivi habari zake zimesambaa nchi nzima mpaka vijijini kama moto wa kifuu cha nazi. Ni ajabu na kweli.
 
Baada ya Uchaguzi Mkuu tutarudi hapa kuwakumbusha maneno yenu!

Tundu Lissu hawezi kuwa Rais wa Tanzania 2020 labda CCM ya 2025 ambayo kutakuwa hakuna Rais anayetetea kiti chake na pia igawanyike makundi!
 
Itakuja awamu ya mtaa kwa mtaa kitanda kwa kitanda
Muda uko wapi mkuu... Mpaka sasa amepita majimbo mangapi na amefanya mikutano mingapi compare to opponent wake. Swala lilikuwa kuunda timu za kampeni zizunguke na sehemu zingine ufqnis mkubwa ungeonekana.

Changamoto wagombea majimboni wanahali mbaya hivyo kampeni hawafanyi. Anategemea kupata wabunge wangapi ili aunde serikali?
 
Kuwapata hao undecided aende vijijini; siyo kupita mijini tu. Ubaya ni kwa vile huko vijijini, CHADEMA haina infrastructure kabisa. Kwa hiyo hawezi kwenda kwa sababu hakuna wa kutangza ujio wake.

Ni muhimu tumuunge mkono mgombea huyu kwa kumsaidia kampeni za nyumba kwa nyumba na mtu kwa mtu tokea tulipo.

Multiplier effect hata ya member wa JF minus buku 7 si ndogo. Bado za wasomi, wafanya biashara, wafanyakazi nk. Wao na familia zao huyu mwenye mabango hadi maeneo kusiko na watu mbona njia nyeupe kuelekea Chatto?

Mikakati ya kulinda kura inapaswa kuwa thabiti haswa.
 
Kwa mashambulizi haya ya Tundu Lissu kila siku anabomoa ng’ombe ya mpinzani wake kwa matofali kadhaa. Kuna wale CCM damu na Chadema damu, hawa hata iweje kura zao hazibadiliki...

Sasa this is a sincere comment, niliamua sitapiga kura mwaka Huu, ila kwa hali hii nishatangaza nyumbani kwangu tunafanga Nyumba na kwenda kupiga kura wote!
 
Back
Top Bottom