Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Elections 2010 Kuelekea uchaguzi: Jeshi lawatisha wananchi

Uyo kamanda afaamu tu kuwa hata ndani ya jeshi wapinzani wamo na wamejaa tele ,humo ndani si wote wanaipendelea ccm ,bali wengi wao wanafahamu kwa undani ni nani mwizi na ambae anaewasababishia wanapomalizia muda wa kulitumikia jeshi wanarudi wakiwa wamechoka na hawana hata kiinua mgongo cha kuwasaidia muda wao wa uhai uliobakia ,ni wangapi walikwenda kupigana vita ya uganda hadi hii leo hawakupata malipo ,wakidai wanaambiwa walijitolea au wakamtafute nyerere ,ni bora mtumie busara katika kuutumikia umma huu wa WaTanzania ambao wameanza kufahamu kuwa nchi yao ni TAJIRI na hawana sababu ya kulala na njaa,kukosa matibabu kukosa mlo na mambo mengi tu.
 
Nimeona muda si mrefu BBC rais wa equador-korrea akiipata fresh toka kwa umma wenye uchungu na nchi yao. Yale inabidi yatokee hapa
 
Alianza yule mpiga ramli lakini wapi, akafuatia Makamba lakini wapi, akaja Kinana lakini wapi, vikaingia TBC na Daily News lakini wapi, kafuata mama Salma lakini wapi, kaingia mwana Ridhwani lakini wapi, zikaingia helicopta tatu lakini wapi, na sasa kapiga hodi mwanajeshi Shombo je tutegemee nini kitafuata, vifaru mitaani ? Juhudi zote hizi eti ni kuhakikisha Kikwete anaendela kubaki madarakani, come what may - kwa mbali naona yale ya Nicolae Ceausescu wa Romania au Mwai Kibaki wa Kenya yakiinyemelea Tanzania !
 
Na sintashangaa iwapo wazo la kumtaka Shimbo atoe tamko hilo lilitoka kwa Makamba!
 
If he is tired of peace, let him try wall. weare ready for that. kifua changu nimeshakiandaa kupokea risasi za JWTZ !
 
The problem with african leaders is that they don't learn from mistakes of leader in other countries. Hawa wanajeshi wakipewa bia za bure wanaridhika na hali ya maisha bila kujua kwamba wanatakiwa kuwa na maisha bora kuliko waliyo nayo. Hakika tunawatangazia wanajeshi tukiamua kupigana nao hawawezi kutushinda. Amani ya kweli hailindwi na mtutu wa bunduki, bali kwa haki kuonekan inatendeka. mbona huko Somalia Uganda na Burundi wameshindwa kuleta amai pamoja na mitutu yao ya bunduki?
 
Hehhe heheh wakaulize wenzao wa Equador yapo wapi maana prez yupo hosp kapigwa mabomu ya machozi na familia yake imepewa hifadhi kwa marafiki!
 
hivi hiyo kauli ya shombo aliruhusiwa na Mwamunyange kuitoa au yeye amekuwa msemaji wa majeshi? maana mkubwa kicheo jeshini ni Mwamunyange, asipotolea kitu kauli ni Msemaji wa Jeshi kwa niaba yake, we shombo chunga kauli zako usije ukaleta zogo bure lisilo na tija, kama wanao wameshindwa mkeo kashindwa kukushauri waulize wanao, au nduguzo , lazima katika familia yako kuna watu wana busara wanaweza kukushauri ni kauli gani utoe na ni wakati gani, sio kila kitu ni mtulinga tu. historia imeonyesha hivyo.
 
Hivi Jenerali Shombo alipata cheo kwa merit au ????
 
Hizi kauli za JWTZ zikijumlishwa na kauli za viongozi wa dini kudai
vyama vya siasa
tukielewa ni vya upinzani vikubali matokeo ni dhahiri ya kuwa wanajua uchaguzi huu hautakuwa wa huru na wa haki.

JK sasa hivi naye leo amevishutumu vyama vya upinzani kwa kile alichokiita kutishia kumwaga damu. Hakuna chama cho chote ambacho kimeahidi kusababisha umwagikaji wa damu. JK ninamwasa yeye aendelee na kampeni zake asije baadaye akaonekana alichochea vurugu kwa kauli zake hizi. Kule Rwanda watu wanafungwa na hata huku Mahakama ya kimataifa kwa kauli zao tu jinsi ikibainika zilichangia kuhamasisha vurugu na hizi za JK zinatosha kwa mahakama ya kimataifa kuzichunguza endapo huko mbeleni kweli anayoyataja yakajitokeza.

Njia rahisi ya kuondoa wasiwasi wa kuchakachuliwa matokeo ni NEC kurudisha utaratibu tunao ufahamu na uliozoeleka wa kuwaruhusu wapigakura kuweza kukaa mita 200 kutoka vituo vya kupiga kura.

Uwazi wa namna hii utaondoa mashaka ya mashushu kuzichakachua kura zetu kwa kutumia njaa ya mawakala kama mtaji wa kisiasa.

Bila ya kufanya hivyo kama vurugu zikitokea hakuna wa kumlaumu.

JWTZ ni vyema likajifunza yaliyotokea Kenya. Uchaguzi ni suala la kisiasa na kamwe
mtutu wa bunduki
hauwezi kuwa ni ufumbuzi naMnadhimu huyo Mkuu kujitokeza hadharani na kuongea matope basi ajue ameonyesha upeo mdogo alionao.
 
Sio tishio; ni kweli. Hawa jamaa wako tayari hata kuua kuhakikisha ushindi wa CCM. Kama kuna hatari kubwa inayoikabili Tanzania hivi sasa ni kikundi maalum cha wateule ndani ya CCM (na maswahiba zao) kuamua kulitumia JWTZ (ongeza Polisi, UwT, Takukuru, Uhamiaji, n.k.) kwa kazi zao chafu. Kuna taarifa za jeshi kutumika "kurekebisha" kura ndani ya masunduku katika chaguzi zilizopita. Hivyo, wanaelewa nini kinachoendelea na wanaanza kujiandaa mapema. Tumeona jinsi jeshi lilivyotumika katika wizi wa meremeta ambao hakuna aliye tayari kusema kitu. Hata Waziri Mkuu anaendelea kujiumauma hadi leo.

Kwa kifupi, jeshi letu limeondolewa toka kwenye hadhi yake ya zamani ya kupambana na waonezi wa nchi yetu (km Amin) na wa Waafrika wenzetu (enzi hizo: makaburu na wareno) na kuwa chombo cha mafisadi. Lina hatari ya kuwa kama jeshi la Mobutu: ukali na unyanyasaji wa raia ndani ya nchi huku mbele ya maadui wa nje likinywea kama kuku aliyelowa. Labda kupewa kazi ya kutimua vibaka kama walivyofanikiwa kufanya Comoro hivi majuzi. Sad! :sad:
 
Who the hell is Shimbo????????? mwambieni aende Mogadishu / Darfur / Afghanistan / Pakistan / Iraq kama mikono na akili inawasha sana. kule ndiyo hakuna amani kwa sasa na inahitajisha sana.

Umemsikia Jenerali wa Jeshi mwamnyange ameongea??? Hapana!!! je kwa nini???? anajua ukweli wa mambo na hali ngumu ya kiuchumi ya nchi na hata mafisadi kuongezeka na pia yeye ni mmoja ya wanajeshi wasomi... hivyo hawezi kubwatuka kaka huyu Shimbo aka shombo.

Tanzania hakuna vita wala nini kwa nini tusipinge matokeo wakati tunajua CCM watachachua.. Demokrasia iko wapi kama mambo hayaendi vizuri??? Kwa kifupi kama wanaona vipi wamwambie JK aachie ngazi kabla ya 31 Octoba. yaani ni kusema hatutaki wala hatuendekezi sera wala maoni wala mtazamo wa wagombea wala viongozi wa kifisadi wa CCM.

Huyo Shimbo anapiga debe ili akistaafu apewe Ukuu wa wilaya au mkoa au ubalozi... sasa anajua CCM ikishinda hivi vyeo vyote havipo hapo ndipo tumbua limapoingia Mchanga... Mzee kula jasho lako la halali..
mbele....

.


Naomba nikusahihishe msimuonee SHIMBO KAMA SHIMBO yeye ametumwa kuongea kutokana na nafasi yake jeshini....unatakiwa ujuwe kuwa nidhamu ya kijeshi hairuhusu shimbo kufanya jambo kubwa kama hili au jambo lolote linalohusu amri za mtiririko bila kupata maagizo ya MWAMUNYANGE......na mnatakiwa mjuwe mwamunyange ana report briefing daily kwa AMIRI JESHI MKUU na hangeweza kuagiza hili litangazwe bila kumuarifu AMIRI JESHI MKUU.......

.....HILI JAMBO LIMEJADILIWA NA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA WA TAIFA KWA KINA.....ni defensive mechanism ..ina maana hata wapinzani wakishinda TUME ITATANNGAZA NI CCM na MMESHAAMBIWA MSILETE FUJO.......VIFARU VINANOLEWA KUTANDA MITAANI KUWATISHA MKISHAIGA KURA MUENDE NYUMANI ..NA IKIBIDI AMRI YA KUTOTEMBEA OVYO BAADA YA SAA 12 ..ITAWEKWA ILI WATU WA KUIBA KURA WAIBE VIZURI.....MAJI YAMEZIDI UNGA ..NA KWA MARA YA KWANZA KWENYE NCHI HIII JESHI LA WANANCHI KUTOA STATEMENT WAKATI WA UCHAGUZI TENA IKITANGAZWA NA AFISA WAKE MKUU...
 
Ndugu wana JF nimeaangalia taarifa ya habari ya ITV saa mbili usiku leo Ijumaa Octoba mosi, ITV wameonyesha taarifa inayomwonyesha mnadhimu mkuu wa jeshi la wananchi Tanzania Lt. Gen Abdalahaman Shimbo akisema kuwa jeshi lipo tayari kuzuia umwagaji damu kwa kuwa eti kuna wagombea na vyama flani wamesema damu itamwagika wakati wa kutoa matokeo ya kura zotakazopigwa.


MY TAKE.


JWTZ wanaingiaje hapa, mbona hatujawahi sikia wakisema huko nyuma ambapo CCM imekuwa mstari wa mbele kuleta fujo
Hii inafanywa ili kuwatisha wananchi waogope na kukipigia kura ccm, kwa nini kila chombo cha dola kinajiisubmit kwa ccm na badala ya kufanya kazi kama wanavotakiwa?
 
Ni Aibu kwa Mnadhimu wa Mkuu wa Jeshi kuwa Boot liker wa Wanasiasa, Nimeshangaa kweli kweli kwa Serikali kuanza kutumia Jeshi kuwatisha wananchi
 
ccm ndio zao hizo, wanapanga kuiba kura maana wameshajua kuwa Kikwete atashindwa
 
Kama wanajeshi wanasema wanataka kuzuia fujo,we must take it at face value,tuamini kwamba they are sincere.
 
[FONT=Arial, sans-serif]Hii nimeipata sasa hivi
[/FONT]
[FONT=Arial, sans-serif]
[/FONT]
[FONT=Arial, sans-serif]Vyombo vya ulinzi na usalama nchini Tanzania vimewataka viongozi wa vyama vya siasa nchini kukubali matokeo ya uchaguzi mkuu yatakayotangazwa na tume ya taifa ya uchaguzi NEC na kutothubutu kupinga matokeo hayo na kusababisha vurugu.[/FONT]


[FONT=Arial, sans-serif]Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ Luteni Jenerali Abdurahmani Shimbo ametoa tamko hilo leo Jijini Dar-Es-Salaam kufuatia kuwepo kwa taarifa za vyama vya kisiasa kujiandaa kukataa matokeo yatakayotangazwa na tume ya uchaguzi. [/FONT]

[FONT=Arial, sans-serif]Luteni Jenerali Shimbo amesema vyombo vya usalama vimejipanga kukabiliana na hali yoyote ya vurugu ambayo itajitokeza na kuwaonya watu kutoshiriki katika vurugu zozote baada ya kutangazwa matokeo.[/FONT]



Huyu Shimbo nani kamwambia akiwa Jeshini ana ruhusa ya kuingilia mambo ya siasa? Hii inaonyesha kuwa kuna uwezekano mkubwa kwamba ana kadi ya CCM mfukoni, kinyume cha sheria, na kwamba anasubiri tu akistaafu ateuliwe Mkuu wa Mkoa au aende kugombea Ubunge huko kwao. Kama anataka cheo cha kisiasa aache kutafuta vya dezo au vya kushtukiza kwa kusubiri mpaka astaafu ndiyo aonyeshe kuwa siku zote akiwa jeshini alikuwa mwanachama wa CCM ijapokuwa sheria hairuhusu. Badala yake avue magwanda yake, aonyeshe kadi yake ya chama alichoko hadharani na kugombea au kuunga mkono wanachama wenzake.

Shimbo anaendekeza tabia mbovu iliyozoeleka ya baadhi ya Wanajeshi kujifanya mashujaa kwa kuonea na kupiga wananchi wasio na silaha. Kazi ya JWTZ siyo kupiga raia bali kulinda nchi dhidi ya mshambulizi kutoka nje ya nchi. Kazi ya kushughulikia vurugu za wananchi ni ya polisi, siyo ya JWTZ.
 
je tunawakumbuka hawa? Mejor gen Kombe, Brigadia Masese, Col Andrew Shija, nawalio baki waelewe hata kuwatetea mafisadi haiwahakikishi maisha yao ya baadae? Bodi gadi wa Jaji Mkuu , Dereva wa Msafara wa Sisiemu, nk nk, hivyo ni vizuri ukatubu dhambi zako na umwombe Mungu akukute ulisha upo tayari, na utakao waacha watu wawe tayari kuishi nao. Shimbo sijui umri wako uko wako, marafiki zako na wasifu wako, zaidi yakuwa CofS katika Jeshiletu la Tanzania, player your part kama mtanzania mwenye muono wa jana, leo na kesho, pare ni yetu sote.
 
Shimbo acha kuzeeka vibaya,wewe utapita ila tz haitapita kamwe,usikubali kutumiwa kwa viahadi vidogo kama vya kusomeshewa mtoto wako,kulindwa kwa cheo chako,usiwe msakatonge,watanzania si mabwege tena,kamwandae vizuri nyau wako ndipo uje tena kuwatishia watu
 
Back
Top Bottom