Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Elections 2010 Kuelekea Uchaguzi mkuu CHADEMA Sept. 2009

Status
Not open for further replies.
Tuchukulie Juma ana mke lakini juma ni mhuni anachukuwa wake wengine na akatokezea Paulo huyu paulo kamwambia mke wa juma jinsi juma anavyofanya,paulo kaenda mbali mpaka kafanikisha mke wa juma kumshika juma ugoni.

Na baada ya tendo hilo paulo anaanza kumshawishi mke wa juma ,kwamba ili ngoma iwe droo ama malipizi naye atembee na paulo,paulo anajinadi yeye ni mtu mzuri kwa sababu amefanikisha kumsika ugoni bwana wake, hivyo yeye paulo ana mapenzi mema na anamtakia mambo mazuri sana mke wa juma hivyo anaomba mke wa juma ampe uroda.

JF huwa mafumbo hayasaidii, weka wazi kati ya mbowe na zitto nani kapata umaarufu kupitia kwa mwingine?? Siyo unazunguka mbali sina muda wa kuanza kujiuliza hasa unafumba nini.
 
JF huwa mafumbo hayasaidii, weka wazi kati ya mbowe na zitto nani kapata umaarufu kupitia kwa mwingine?? Siyo unazunguka mbali sina muda wa kuanza kujiuliza hasa unafumba nini.

Nani anafumba huo ni mfano.

Siku zote niko wazi Mbowe ndiyo kikwazo tangu enzi zile za Chacha,Huo ndio msimamo wangu.

Kama huelewi huo mfano ambao wewe umeuita fumbo ni CHADEMA Vs CCM.

Na saizi kwa mashabiki kweli Zitto usipotumia busara kuu kweli hili ndilo anguko lako maana wamesha ku corner pabaya.

1.Kama wamekuzuia kwa namna moja ama nyingine watakuwa wamekukata moli na wenda upiginaji wako utashuka , na ukiendelea kupigania demokrasia kwa kuishambulia ccm watu watakuhoji mbona ya ndani imekushinda ama lasivyo utakuwa mnafiki wa demokrasia.

2.Ukiamuwa kuhama chama watapata sababu ya kuthibitisha madai yao RA ka kukunua kaka kazi unayo.
 
Selous,

Nilikuwa nakuona una mawazo ya maana; yaani hii pumba hapo juu ni ya kwako kweli?

Kweli watu wakipenda hugeuka kuwa chongo na viziwi.

Zitto aligombea kwa hiari yake hata kama alishawishiwa na wanachama. Kwa Tanzania kila anayegombea anasema hivyo hivyo.

Hiyo yako hapo juu ni spinning!


Mkuu Bambumbile, nashawishika kuamini kiuwa hukumwelewa Selous ana maana gani. Tafadhali hebu rudia kumsoma tena ukirejea rejeo alilorejea ndo akato hii hoja.

tuendelee
 
Nafikiri tumetoa mawazo yetu ya kutosha kuhusu hili. Na nafikiri watu wameishiwana hoja mpya sasa wanaanza kutukanana, siyo busara bora msichangie. Mambo muhimu yaliyojitokeza ktk mjadala huu, wapo waliosema zitto angeruhusiwa tu agombee kwani ndo demokrasia, wapo wanaosema hakutakiwa kugombea kuwa alitakiwa avute subira kidogo kwani hana uzoefu, wapo waliotoa mawazo ya jumla kwa pande zote mbili, lakini wakionyesha wasi wasi wa uadilifu wa zitto hasa kuhusiana na issue ya DOWANS, na wakaonya kuwa huenda anatumiwa na CCM.

Hoja zilikuwa nzuri na nadhani CHADEMA wamepata cha kuweza kufanyia kazi. Masuala ya uchaga na nini, haya ni mambo ya kupuuzwa kwa sababu huwezi kumpata mtu/kiongozi yoyote asiye na kabila, hata mzanaki kama nyerere bado uzanaki ni kabila, kwa hiyo malumbano ya ukabila hayana nafasi hapa.

Sawa sawa Magezi hii summary nzuri, ila sasa na wewe mkuu utasemaje eti Mrema ndo alikuwa mpinzani wa kweli (labda)..huyo sidhani kama alishawahi kuwa mpinzani mkuu LOL
 
Waheshimiwa wanabodi
Naamini sasa kwamba siasa ni uhalalishaji wa mambo ya kihuni kwa kuendekeza uhafidhina na si fikra mbadala kama tulivyodhania wengi.

Nilitaka kurudisha kadi yangu ya CCM lakini sasa naifuta vumbi na naenda kulipia ada ya uanachama maana naona upinzani ni uwehu mtupu.

Kwa mtindo huu, huko tuendako ni ANGUKO la ANGUKO
 
Nilipinga sana Zitto kuwa mwenyekiti wa Chama, kwenye chama bwana huhitaji watu kama Zitto... Zitto anatakiwa kwenye utendaji sio kuwa mwenyekiti... in short ulikosea kaka... na kwa kweli nilivyofikiri imekuwa hivyo hivyo... Zitto Rungu la spika limekupitia mara nyingi sio kwa sababu ya hoja za kupinga bali... kushindwa kutumia maneno stahiki kwenye kutetea hoja... kwenye chama ndio ingekuwa ovyo zaidi.
 
Nilipinga sana Zitto kuwa mwenyekiti wa Chama, kwenye chama bwana huhitaji watu kama Zitto... Zitto anatakiwa kwenye utendaji sio kuwa mwenyekiti... in short ulikosea kaka... na kwa kweli nilivyofikiri imekuwa hivyo hivyo... Zitto Rungu la spika limekupitia mara nyingi sio kwa sababu ya hoja za kupinga bali... kushindwa kutumia maneno stahiki kwenye kutetea hoja... kwenye chama ndio ingekuwa ovyo zaidi.

Sasa hapa mkuu unataka kuhalalisha lipi?

Mimi binafsi ktk wanasiasa waliopo bado sijaona mkombonzi ,wenda tusubilie atakuja LAKINI sikbaliani na wewe kwa 100% yani ya kwamba mtu akiamuwa kugombea binafsi huwa anajiamini atafanya aliyopania kufanya ,hivyo wale wapiga kura ndio humpa kura zinazotosha ama kumpa zisizotosha.

Tatizo tunaloliona hapa Zitto wala hajapewa nafasi ya kupata kura ama kutopata ,wamemwacha hewani
 
CHADEMA kama ilivyo CCM na wao kumbe Mwenyekiti wao wa CHAMA-Taifa huwa hapingwi na yeyote yule kwenye sanduku la kura?a akijitokeza mtu kutaka kushindana na Mwenyekiti-Taifa kumbe wazee wanamuita kumtaka atoe jina?Hii ni aina ya demorasia ambayo akina Mnyika hapa kila siku wanajisifia?

Naam,hayo yamepita,ila ombi langu kwenu akina Mnyika,Slaa,Mbowe,Zitto,Mtei,Makani,Mdee na wengineo,kabla ya kuisha kikao chenu hiki hakikisheni mnarekebisha katiba yenu isomeke hivi "kwa kukinusuru chama na anguko,Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA HATAPINGWA na yeyote yule kwenye sanduku la kura"

CHADEMA kwangu mmejivunjia sana heshima kwa kuwa na mwongozo wa ki-CCM ambapo hadi leo kwenye demokrasia ya kweli duniani na nyie Kamati Kuu inapitisha jina moja tu la Mwenyekiti na Mkutano mkuu kazi yao ni kuthibitisha tu chaguo la kamati Kuu!

Kumbukeni kuwa CHADEMA mnatumia hela za walipa kodi mnazozipata kwa uwiano wa wabunge mlionao,na mimi kama mlipa kodi ninapinga kwa hela zetu kutumika kinyume na Demokrasia,ikiwezekana ili msiwe mnafuja hizi hela rekebisheni tena katiba ili Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa awe anateuliwa tu na "WAASISI"akina Mtei na awe anathibitishwa tu kwa njia ya SIMU na wajumbe wa mkutano mkuu!

CHADEMA you put me under tense dilemma,honestly and assuaredly I say to you my fellow JF's Greast thinkers;CHADEMA's moves to bowing to Zitto Kabwe so as to defend "Mboweism"character is totally UNDEMOCRATIC.
 
Hapa nilisema kuwa hawa ni mamluki tu copy & paste ya CCM ,ila kitu kimoja ambacho niliwashauri ,hawa akina Zitto wasiwe na papara ya kutaka uenyekiti waridhike na nafasi waliyokuwepo mpaka pale Mwenyekiti mwenyewe atakapoamua kuachia ngazi au kujiuzulu,na iwe mnapishana kiaina ,yaani katika safu kuu asitokeze mtu pua kutaka nafasi ya juu na hata akitokeza asiwemo katika ile safu kuu ya uongozi.

Maana Chama lazima kiwe na msimamo na viongozi wake walio katika nafasi kuu za juu kabisa ili kusitokee migongano kama tunavyoona ,kwa mfano Mwenyekiti agombee palepale makamu halikadhalika na katibu nae awanie nafasi yake ileile ,kama ni kupangwa au kupanguliwa, kilichojitokeza kwa CHADEMA nasema sio jambo zuri kabisa kwa Zitto kutaka kugombea nafasi hiyo ,kwani umri wake unamuwezesha kusubiri pale wakuu wenzake watakapofika wakati wa kuachia ngazi na kumkabidhi Chama.

Hizo ni hisia nzuri kabisa kwa Chama chenye viongozi wanaothaminiana na walio amua kukijenga Chama Chao , demokrasia itumike kwa walio nje ya uongozi na sio waliomo ndani ya uongozi wa ndani tena wa juu,hawa inawabidi watulize akili zao vilivyo kama tuonavyo katika uongozi wa CUF, nafasi za juu zinakuwa protected kwa wale waliomo ndani na zinakuwa open kwa walioko nje, natumai nimeeleweka.
 
Nilipinga sana Zitto kuwa mwenyekiti wa Chama, kwenye chama bwana huhitaji watu kama Zitto... Zitto anatakiwa kwenye utendaji sio kuwa mwenyekiti... in short ulikosea kaka... na kwa kweli nilivyofikiri imekuwa hivyo hivyo... Zitto Rungu la spika limekupitia mara nyingi sio kwa sababu ya hoja za kupinga bali... kushindwa kutumia maneno stahiki kwenye kutetea hoja... kwenye chama ndio ingekuwa ovyo zaidi.
..leo unakuja kusema Rungu la Spika lilikuwa sahihi dhidi ya Zitto...? simply bcz ametaka kugombea uenyekiti na Mbowe?....Wakati wa Mwanzo ulikuwa against spika...?

Unataka Utendaji gani afanye wakati Kichwa Hakifanyikazi sawa sawa?

Unaweza simamisha KIVULI wakati mti wake Umepinda?
 
Hapa nilisema kuwa hawa ni mamluki tu copy & paste ya CCM ,ila kitu kimoja ambacho niliwashauri ,hawa akina Zitto wasiwe na papara ya kutaka uenyekiti waridhike na nafasi waliyokuwepo mpaka pale Mwenyekiti mwenyewe atakapoamua kuachia ngazi au kujiuzulu,na iwe mnapishana kiaina ,yaani katika safu kuu asitokeze mtu pua kutaka nafasi ya juu na hata akitokeza asiwemo katika ile safu kuu ya uongozi.

Maana Chama lazima kiwe na msimamo na viongozi wake walio katika nafasi kuu za juu kabisa ili kusitokee migongano kama tunavyoona ,kwa mfano Mwenyekiti agombee palepale makamu halikadhalika na katibu nae awanie nafasi yake ileile ,kama ni kupangwa au kupanguliwa, kilichojitokeza kwa CHADEMA nasema sio jambo zuri kabisa kwa Zitto kutaka kugombea nafasi hiyo ,kwani umri wake unamuwezesha kusubiri pale wakuu wenzake watakapofika wakati wa kuachia ngazi na kumkabidhi Chama.

Hizo ni hisia nzuri kabisa kwa Chama chenye viongozi wanaothaminiana na walio amua kukijenga Chama Chao , demokrasia itumike kwa walio nje ya uongozi na sio waliomo ndani ya uongozi wa ndani tena wa juu,hawa inawabidi watulize akili zao vilivyo kama tuonavyo katika uongozi wa CUF, nafasi za juu zinakuwa protected kwa wale waliomo ndani na zinakuwa open kwa walioko nje, natumai nimeeleweka.

This is very low Mwiba...!!!
 
CUF na Wanyamwezi wapi na wapi?

Yule Lipumba kawekwa pale PICHA tu. Kwa Tabora anakotoka Picha Lipumba ni kwamba hakuna hata mbunge mmoja kutoka CUF. Hata mwenyewe hana ubunge. CUF ni Pemba na Maalim Seif Hamad , hiyo inajulikana kwa wote ila naona siyo wote.....
Ni kweli kabisa CUF sio Cha wanyamwezi na vilevile ikubalike sio Cha waPemba wala cha Seifu aidha si cha kidini ni Chama Cha Wananchi sasa kama wewe ni mwananchi wa inchi hii basi Chama chako ni CUF huna mbadala ,Chama ambacho kimevuka mitihani mikubwa tena ya kimataifa kutokana na mbinu za CCM.

Ajabu ni kuwa Chama Cha CUF kila kinapofanyiwa mizengwe huibuka na kuwa more aggressive against CCM ,kiasi cha kuifanya CCM isipate usingizi na katika mikutano yake ya ndani CCM inakiri kuwa tabu kubwa waliyonayo ni kuidhibiti CUF ,jambo ambalo linaonekana kuwashinda vibaya sana ,kwani kila wanapojiandaa na mechi ya CUF inabidi watumie kila walichonacho ,kuanzia usalama wa Taifa,polisi,majeshi ,vikosi vya SMZ na hata vikosi vya zimamoto navyo huingizwa kundini kupambana na CUF yaani inakuwa ni vita kamili,ni chama gani kilichofikia kuekewa mguu na CCM kiasi hicho ? Jawabu hakuna ,hivyo inataka utulize akili yenu vizuri sana mnapoitaja CUF ili uweze kupima na kupata jawabu kuwa CUF ipo makini kabisa katika kuendesha siasa hapa Tanzania.

Ukiangalia CUF imeweza kupita vikwazo vingi vikiwemo vinavyokihusu Chama chenyewe ndani ya utawala na imepita kwa ulaini kabisa ,vilevile utaona CUF imepewa majina kibao ,kama Chama cha wapemba,Chama cha kiislamu,Chama cha Mujahideen ,Chama Cha vurugu ,Chama cha wapenda uongozi ,Chama cha cha cha....! Lakini mote humo wamepuyanga na bado wanapeta na kama haitoshi hata kuzushiwa habari kuwa imeleta makontena ya mapanga na visu na wenye televisheni waliona Mkuu wa Polisi akisema uongo (Mahita) na still CUF haikuyumbishwa ,mbali na viongozi wengine kudondoka njiani lakini wapo na wanaendeleza msimamo wa kuing'oa CCM mpaka kieleweke. Na sasa hivi sina la kuwambia huko mikoani na vijijini kinakuja kama moto wa nyasi zilizochanganyika na msitu ,ni hatari tupu hasa kwa uhai wa CCM.
 
Nami napinga Zitto kuwa Mwenyekiti wa Chadema. Akili yangu inanituma kwamba ana mahusiano ya kiujanjaujanja na akina RA. Bila shaka RA angependa amrthi Mbowe.

Ukichunguza sana magazeti ya RA hasa Mtanzania na Rai utakuta yako upande wa Zitto. Jiulize kwa nini. Ipo sababu. Zitto asitubabaishe hapa.

Gazeti la leo la Mtanzania kwa mfano, ukurasa wa mbele limeandika kama vile tayari Zitto ni maarufu sana ndani ya Chadema kuliko Mbowe na kwamba katika uchaguzi angembwaga tu Mbowe. Gazeti hata lilidiriki kuandika matarajio ni kwamba uwiano wa kura ni Zitto 70% na Mbowe 30%.

Hii ina lengo lake. Kina RA walikuwa wametayarisha bahasha nene kwa wajumbe wapiga kura ili kumnyonga Mbowe katika uchaguzi.

Na sababu ipo, haihitaji PhD kujua. RA na Dr Slaa ni maadui wakubwa sana kwa mtandao wa mafisadi wa RA. EPA (Kagoda) imeibuliwa na akina Slaa, na bado wanakazania walioiba Kagoda wakamatwe na kushitakiwa.

Kina Slaa wamekuwa kero kwa akina RA na Zitto kazi yake, akiula uenyekiti, ni kumtimulia mbali Dr Slaa na “silaha” zake na kukifanya chama kisiwe kinafuatilia sana masuala ya ufisadi.

Wewe tazama tu akina RA walivyofanya kwa CUF, hadi kina profesa wameanza kuwatetea mafisadi.


 
Zitto huwa ana kawaida ya kuja kubalance habari hapa JF, ingependeza angefanya hivyo. Ni vyema akaeleza lengo lake la kugombea, na ikawaje akajitoa.
 
Nami napinga Zitto kuwa Mwenyekiti wa Chadema. Akili yangu inanituma kwamba ana mahusiano ya kiujanjaujanja na akina RA. Bila shaka RA angependa amrthi Mbowe.

Ukichunguza sana magazeti ya RA hasa Mtanzania na Rai utakuta yako upande wa Zitto. Jiulize kwa nini. Ipo sababu. Zitto asitubabaishe hapa.

Gazeti la leo la Mtanzania kwa mfano, ukurasa wa mbele limeandika kama vile tayari Zitto ni maarufu sana ndani ya Chadema kuliko Mbowe na kwamba katika uchaguzi angembwaga tu Mbowe. Gazeti hata lilidiriki kuandika matarajio ni kwamba uwiano wa kura ni Zitto 70% na Mbowe 30%.

Hii ina lengo lake. Kina RA walikuwa wametayarisha bahasha nene kwa wajumbe wapiga kura ili kumnyonga Mbowe katika uchaguzi.

Na sababu ipo, haihitaji PhD kujua. RA na Dr Slaa ni maadui wakubwa sana kwa mtandao wa mafisadi wa RA. EPA (Kagoda) imeibuliwa na akina Slaa, na bado wanakazania walioiba Kagoda wakamatwe na kushitakiwa.

Kina Slaa wamekuwa kero kwa akina RA na Zitto kazi yake, akiula uenyekiti, ni kumtimulia mbali Dr Slaa na “silaha” zake na kukifanya chama kisiwe kinafuatilia sana masuala ya ufisadi.

Wewe tazama tu akina RA walivyofanya kwa CUF, hadi kina profesa wameanza kuwatetea mafisadi.

Mimi nafikiri sasa huu mtindo wa kumhusisha RA na kila ufupi wetu wa kufikiri naona tuufanye umepitwa na wakati.

Haiwezekani Kabouru,Chacha,na sasa Zitto wote tuwaone wana matatizo na tusione tatizo la mtu mmoja anayekwaruzana nao yani Mbowe.
 
Ndugu wana JF na Watanzania kwa ujumla, hebu tujiulize ni vyama vingapi vya kisiasa hapa duniani wanaendesha uchaguzi wa nafasi ya mwenyekiti kwa mgombea zaidi ya mmoja??? Kama vipo ni vichache sana na tena tunajua asilimia kubwa ya vyama hivyo vinavyomeguga.

Si nia yangu ya kuvitaja hapa bali kila mmoja ajaribu kuangaza huku na kule katika kumbukumbu zake na afanye tathmini. Principally, ni kweli ingependeza sana kama pangekuwa na free competition. Lakini wanaogopa nini au kwa nini hawafanyi hivyo??

Hata Ulaya na Amerika ambako tunaamini ni wanzilishi wa demokrasia hii lakini bado katika hili vyama vingi vimeshindwa. Kwa hiyo sidhani kama ni busara kubwa kukilaumu sana CHADEMA, unless watu mnapenda kulaumu tu na hii itakuwa hasa kwa watu wasiopenda kuangalia mambo kwa mapana zaidi.

Nafikiri kinachoshuhudiwa hasa ni michuano ya watu mbali mbali katika vinyanganyiro vya uongozi na si kama unavyotaka tuamini. Mifano si ipo ya akina Obama na Hillry au wakati wa Blair na Brown.
 
CHADEMA kama ilivyo CCM na wao kumbe Mwenyekiti wao wa CHAMA-Taifa huwa hapingwi na yeyote yule kwenye sanduku la kura?a akijitokeza mtu kutaka kushindana na Mwenyekiti-Taifa kumbe wazee wanamuita kumtaka atoe jina?Hii ni aina ya demorasia ambayo akina Mnyika hapa kila siku wanajisifia?

Naam,hayo yamepita,ila ombi langu kwenu akina Mnyika,Slaa,Mbowe,Zitto,Mtei,Makani,Mdee na wengineo,kabla ya kuisha kikao chenu hiki hakikisheni mnarekebisha katiba yenu isomeke hivi "kwa kukinusuru chama na anguko,Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA HATAPINGWA na yeyote yule kwenye sanduku la kura"

CHADEMA kwangu mmejivunjia sana heshima kwa kuwa na mwongozo wa ki-CCM ambapo hadi leo kwenye demokrasia ya kweli duniani na nyie Kamati Kuu inapitisha jina moja tu la Mwenyekiti na Mkutano mkuu kazi yao ni kuthibitisha tu chaguo la kamati Kuu!

Kumbukeni kuwa CHADEMA mnatumia hela za walipa kodi mnazozipata kwa uwiano wa wabunge mlionao,na mimi kama mlipa kodi ninapinga kwa hela zetu kutumika kinyume na Demokrasia,ikiwezekana ili msiwe mnafuja hizi hela rekebisheni tena katiba ili Mwenyekiti wa CHADEMA-Taifa awe anateuliwa tu na "WAASISI"akina Mtei na awe anathibitishwa tu kwa njia ya SIMU na wajumbe wa mkutano mkuu!

CHADEMA you put me under tense dilemma,honestly and assuaredly I say to you my fellow JF's Greast thinkers;CHADEMA's moves to bowing to Zitto Kabwe so as to defend "Mboweism"character is totally UNDEMOCRATIC.
Mimi nadhani strategy aliyotumiya Mh Zitto ilikuwa muzuri sana. Ndani ya moyo wake (I am putting words in his mouth) Muheshimiwa Zitto aripochukuwa fomu za kungombeya uwongozi arikuwa anajalibu kusema kuwa CHADEMA inahitaji uwongozi wa namuna tofauti ili kupata mafanikiyo zaidi ya mafanikiyo yaliyopatikana chini ya uwongozi wa Mbowe. Na “nazani” angependeleya Dr. Slaa aongoze chama badala ya Mbowe kwasababu anaamini (na nakubaliyana naye) kuwa Slaa ana uwezo mkubwa zaidi wa kuongoza CHADEMA katika hatuwa chama kilipofika.

Zittor alipoingiza jina lake kwenye uchaguzi alikuwa anachokonowa tu lakini fall back position yake (ambayo mimi nadhani ndiyo preferred position) ilikuwa kumuweka Dr. Slaa kwenye uwongozi badala ya Mbowe. Sitashangaa kama hawa wawili hawakunong’onizana kuhusu suala hili kabula ya kuitosa kwenye kinyang’anyiro. Zittor nadhani alikujuwa atakataliwa na “wenye Chama” kwahiyo akajitayarisha kuomba yeye na Mbowe wasigombee na kumwacha njia wazi kwa Dr. Slaa.

Good try, lakini hiyo nayo imeshindikana, kwasababu CHADEMA ni chama cha familiya. Hiyo iko wazi kwa kila mutu, tusijidanganye. Hata wajaribu ku spin namuna gani huo utabaki kuwa ukweri. Labda solution ni kuigawa CHADEMA kwenye makundi mawili: CHADEMA-Family-Owned-Operation na CHADEMA-Real_National-Party, ambayo itaongozwa na Dr. Slaa. Hapo ndipo tutakapokuwa na opposition ya kweri. Munaonaje?
 
Naomba tuwe waangalifu tusitumiwe na yule mwovu (CCM). Habari hii ililetwa vibaya. Lengo lilikuwa lipi?

Zitto hajawahi kukatazwa kugombea. Kupewa presha ni sehemu ya demokrasia. Kukatazwa ndio kungekuwa udikteta. Kama tukiona kuna mwenzetu anachukua hatua ambazo tunadhani si za kuimarisha chama tusimpe presha abadilishe mawazo? Uamuzi wa mwisho ni wake.

CCM itatumia kila njia kujaribu kudhoofisha Chadema. Inakiogopo sana. Ila hapa JF tusikubali kutumiwa. Na wenzangu wana JF msikubali kila linaloandikwa hapa kwa haraka hivyo!

Kwangu mimi, nguvu ya Chadema inatokana na Dr. Slaa. Naamini si pandikizi la CCM yule. Na ni kiongozi dume kweli kweli. Atashughulikia haya mapigo ya adui kikamilifu (ana uzoefu wa kufanya hivyo).

Asikate mtu tamaa. Bado kutakuweko na jitihada nyingi za kukiangamiza Chadema, hasa kipindi hiki cha uchaguzi mkuu wa chama. Tusiyumbishwe kirahisi hivyo.
 
CUF na Wanyamwezi wapi na wapi?

Yule Lipumba kawekwa pale PICHA tu. Kwa Tabora anakotoka Picha Lipumba ni kwamba hakuna hata mbunge mmoja kutoka CUF. Hata mwenyewe hana ubunge. CUF ni Pemba na Maalim Seif Hamad , hiyo inajulikana kwa wote ila naona siyo wote.....

Sikonge guku, usiwe na wewe kama msambo ashilile ndago. Hivi inaingia akilini kweli CUF kupata 10% ya kura za urais bara na kushika nafasi yapili huku wasipate hata kiti kimoja cha ubunge bara?. Ule ulikuwa ni mkakati wa kuimaliza CUF isionekane ina nguvu bara. Tabora mjini ubunge alishinda Dr. Aziz CCM wakakwiba, Bukoba mjini alishinda Lwakatare, CCM wakakwiba na mifano mingi tu, hivi ni nani asiyejua kuwa CCM wanapanga matokeo ya uchaguzi kupitia tume yao ya Makame na Kiravu?.
 
Last edited:
Naomba tuwe waangalifu tusitumiwe na yule mwovu (CCM). Habari hii ililetwa vibaya. Lengo lilikuwa lipi?

Zitto hajawahi kukatazwa kugombea. Kupewa presha ni sehemu ya demokrasia. Kukatazwa ndio kungekuwa udikteta. Kama tukiona kuna mwenzetu anachukua hatua ambazo tunadhani si za kuimarisha chama tusimpe presha abadilishe mawazo? Uamuzi wa mwisho ni wake.

CCM itatumia kila njia kujaribu kudhoofisha Chadema. Inakiogopo sana. Ila hapa JF tusikubali kutumiwa. Na wenzangu wana JF msikubali kila linaloandikwa hapa kwa haraka hivyo!

Kwangu mimi, nguvu ya Chadema inatokana na Dr. Slaa. Naamini si pandikizi la CCM yule. Na ni kiongozi dume kweli kweli. Atashughulikia haya mapigo ya adui kikamilifu (ana uzoefu wa kufanya hivyo).

Asikate mtu tamaa. Bado kutakuweko na jitihada nyingi za kukiangamiza Chadema, hasa kipindi hiki cha uchaguzi mkuu wa chama. Tusiyumbishwe kirahisi hivyo.

Dr.Slaa mke wake anagombea ubunge 2010 kwa tiketi ya CCM anataka kumtoa Mary Nagu,jee ingekuwa Zitto mke wake ni CCM mngesemaje?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom